Zogwale
JF-Expert Member
- Jul 10, 2008
- 15,295
- 10,957
Mkuu dolevaby pole sana. Aise kisa chako kimenishtua. Ila hakika mchawi si mtu kabisa wa kukenulia meno. Ukimuweza ni kummaliza tu kiishe. Ninaamini umeshapona tatizo lako. Ila mimi nina fundo ni lazima nilipize kisasi, ila ninatafiti ili nimpate fundi haswa ambaye akitenga tu anamaliza. Niko tayari kusafiri hata kama ni mbali kiasi gani ili mradi tu nihakikishe atafanikisha tu. Siwezi kusema mengi ila kuna mateso sana wanafanyiwa hasa watoto ambao hawana hatia kabisa.Ndg yangu Zogwale sijui imani yako niipi ila kama una huyo ndg yako anataabishwa na wachawi or Mizimu sikushauri ushindane na mchawi Kichawi hutaweza.....Tambua kwamba wachawi hadi wanakufanyia majanga....huwa wanatoa makafara makubwa nailia ujinasue lazima ujue kafara aliyotumia ili ulipe hiyo Gharama then ndio ujue namna yakujinasua sio..Ishu ndogo km inavyofikiriwa kuna watu wamewekeza kwa shetani above 100% acha kabisa nakupa mfano wangu Mimi kuna MTU aliniharibia maisha Kafara aliyotumia alichukua.. sehemu za SIRI za wanawake wawili....ndio aliniapizi nazo sasa niambie utawezaje kulipa fidia ya Kafara kama hiyo ukienda kwa mganga japokuwa atajua kinachokutesa lkn hatakwambia namna yakujinasua ataishia kula Pesa yako tu....Ingawa sijui imani yako lkn....muamini MUNGU wakweli waganga ni Mawakala wa Shetani watakutesa sana
Last edited by a moderator: