Agizo hili walipewa wana wa Israel kipindi kile cha sheria/torati, waliambiwa kuwa mwanamke asiichi pia kuna andiko linasema asionekane mchawi kwako/mbele yako. Swali la kwanza la kujiuliza, waliwatambuaje wachawi wakati wao walikuwa wakitembea sana kimwili na sio kiroho kama Kanisa la sasa lilivyo kupitia Roho Mtakatifu? Ukweli ni kwamba walikuwa wakiwatambua wachawi kupitia makuhani, kumbuka kipindi kile Roho hakuachiliwa kwa kila mshirika kama sasa hivi ilivyo. Roho alikuwa anapatikana kupitia makuhani na manabii. Na uchawi huwa unajulikana kwa jinsi ya rohoni (kwa wale ambao wanajua vita vya rohoni watakuwa wananielewa) sasa wale makuhani/manabii na waonaji wakishatambua watu flani ni wachawi walikuwa wanahukumiwa vifo maana ndivyo sheria ya Mussa ilivyoamuru, na sio Mussa ndo alipendekeza hivi, hapana ila ni Mungu.
Swali lingine la kujiuliza ni kwanini awe mwanamke na sio mwanamme mchawi?
Mwanamke ni chombo dhaifu kama maandiko yanavyotuelezea na hata ktk jamii inaonekana hivyo ila Mkuu labda nikwambie tu kuwa MWANAMKE AKISHAKUWA MCHAWI ANAKUWA NI MBAYA KULIKO HATA JAMBAZI. Mwanamke mchawi ni katili sana. Na Mwanamke anatumika sana kumdondosha mwanamme. Kumbuka Ajenda ya Shetani ni kunyanyasa binadamu, unaweza ukawa na ela ila ukawa ni mlevi au fisadi. Kupitia mwanamke mwanamke mchawi shetani anaweza akakuingiza ktk maagano/mikataba au akakuingizia maroho machafu sana na akakuharibia maisha yako ambayo hautakuja kuiona ile mbingu ambayo Mungu ameiandaa kwa ajili yetu wanadamu.
Niongezee kidogo tu kwa kusema kuwa, Mwanamke mchawi ni ngumu kuuacha uchawi au kuundoa ndo maana unaambiwa usimuache akaishi. Mwanamke mchawi yoyote yule huwa uchawi wake upo ktk malango ya uzazi wa mwanamke na kwa mwanaume yapo kichwani. Mwanaume ni mwepesi kuondoa uchawi wake sababu upo kichwani, wachawi wa kiume ni wepesi kuibiwa uchawi wao sababu upo kichwani ila mwanamke ni ngumu kuiba uchawi wake sababu upo ktk malango ya siri. Kwahiyo wanaume wengi hawatakiwi kukabidhiwa uchawi sababu hawadumu nao na raha ya uchawi ni kukaa nao kwa mda mrefu sana, na unapokabidhiwa huo uchawi unashauriwa uutunze na kuulinda. Kumbuka uchawi unapikwa na kuuzwa na mtu huwa anapewa uchawi kutoka kwa falme flani au falme husika na atakuwa anatumika kichawi ndani ya hiyo falme. Kwahiyo hizo falme zikimpa mtu mchawi na kisha kuibiwa wanaona wameingia hasara kubwa sana ndo maana wanawapenda zaidi wanawake sababu ni ngumu kuiba uchawi wao na kisha mwanamke ni katili sana na anaweza akamuangusha mwanamme.
******Naomba niishie hapa, nimechoka kutype mkuu, utansamehe ktk hili******