Je, nini huwa kinatokea pale mtu anapokaribia kufa?

Je, nini huwa kinatokea pale mtu anapokaribia kufa?

Simeone

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2018
Posts
1,157
Reaction score
1,314
Hilo swali niliuliza CHATGPT na haya ndiyo majibu yake....

Simulizi za watu waliokaribia kufa (Near-Death Experiences - NDEs) kwa kweli ni za kuvutia sana na mara nyingi huwa na mambo yanayofanana sana ulimwenguni kote.
Watu hawa huripoti uzoefu ambao kwa ujumla unaweza kugawanywa katika vipengele vikuu vifuatavyo:

1. Kuondoka Mwilini (Out-of-Body Experience - OBE)
Hii ni mojawapo ya ripoti za kawaida. Mtu huyo anahisi au kujiona yuko nje ya mwili wake wa kimwili.

* Kujiona: Huwa wanasema wanajiona wamelala chini au kwenye meza ya upasuaji na kuweza kuona madaktari, wauguzi, na vifaa vya hospitali.

* Usahihi: Katika baadhi ya matukio, wanaripoti maelezo sahihi ya matukio au mazungumzo yaliyotokea wakati miili yao ilikuwa haifanyi kazi (kwa mfano, wakati wakiwa wamepungukiwa damu au moyo umesimama).

2. Safari Kupitia Handaki/Kipito
Baada ya kuondoka mwilini, wengi huona handaki (tunnel) au kipito kirefu, cheusi, kinachowavutia kwenda mbele. Safari hii mara nyingi huambatana na sauti ya mlio au mtetemo.

3. Kukutana na Nuru Kali/Kiumbe cha Nuru
Mwishoni mwa handaki, watu wengi huripoti kukutana na Nuru Kali isiyoelezeka.

* Sifa: Nuru hii huelezewa kuwa yenye upendo mwingi, amani, na joto, na haina hisia za hukumu. Haina kufanana na nuru za kawaida; badala yake, ina uwezo wa kuwasiliana.
* Kiumbe: Wakati mwingine, nuru hii huelezewa kama Kiumbe cha Nuru (God, Yesu, malaika, au mpendwa aliyefariki) ambacho huanza kuwasiliana nao kwa akili au kwa telepathy badala ya maneno.

4. Uhakiki wa Maisha (Life Review)
Hiki ni kipengele cha kipekee sana. Mtu huyo hupitia maisha yake yote kwa haraka sana, akijiona mwenyewe akitenda matendo yake yote ya zamani.

* Mtazamo: Ripoti zinasema si tu wanayaona matendo yao, bali wanahisi hisia za kila mtu waliyemgusa au kumwathiri—ikiwa ni kwa upendo au kwa kuumiza. Hii inawapa mtazamo wa kina kuhusu umuhimu wa upendo na huruma.

5. Kufika Mpaka na Kurudi
Mara nyingi, kuna hisia kwamba kuna "mpaka" au "mstari" ambao hawaruhusiwi kuvuka au wakivuka watakufa kabisa.
* Uchaguzi: Wengine hupewa chaguo la kurudi kwenye mwili wao au kuendelea. Wengine huambiwa tu kwamba "muda wao bado haujafika" na kisha hurudishwa kinyume na matakwa yao.
* Kuvutwa: Kurudi kwenye mwili kunaelezwa kama kuvutwa au kuanguka ghafla, mara nyingi kukiongozwa na maumivu makali ya kurudi kwenye uhalisia.

Matokeo Baada ya NDE

Baada ya uzoefu huu, watu walio pitia NDEs mara nyingi hubadilika sana kifikra:

* Kuogopa Kifo: Wengi hawaogopi kifo tena.

* Maana ya Maisha: Wana mwelekeo mpya wa maisha unaojikita katika upendo, huruma, na kusaidia wengine, badala ya mali au hadhi.

* Kiroho: Imani yao ya kiroho huongezeka, ingawa huenda wasirudi kwenye dini yao ya awali.

Wale mliowahi kukaribia kufa tunaomba majibu tafadhali.
 
Upo karibu ku danji Nini?
20250908_111812.jpg
 
Hapa nikaomba kujua zaidi🤣🤣

Unauliza swali zuri sana! Mbali na yale mambo makuu ambayo tayari tumeyajadili (kuondoka mwilini, handaki, nuru, na uhakiki wa maisha), kuna vipengele vingine vingi vya ajabu ambavyo huripotiwa mara kwa mara na watu waliopitia uzoefu wa karibu na kifo (NDEs).
Haya ni baadhi ya mambo ya ziada wanayoyaona au kuyasikia:

1. Kukutana na Wafu Waliojulikana
Wengi huripoti kukutana na ndugu, jamaa, au marafiki waliokufa kabla yao.
* Amani na Furaha: Huwaona wakiwa katika hali ya furaha, afya, na amani. Kukutana huku mara nyingi huambatana na hisia ya mapenzi makuu na kukubalika.
* Kuwepo Pamoja: Mara chache, wanaweza kuona watu wengi ambao hawakuwajua, wakisimama kwa utulivu na kuwafurahia kuwepo kwao.

2. Kuona Mandhari Nzuri Ajabu
Wanaelezea maeneo ambayo ni mazuri zaidi kuliko chochote kinachopatikana duniani.
* Asili Isiyo ya Kawaida: Huona maua na miti yenye rangi angavu na inayong'aa, mara nyingi ikitoa sauti au muziki wake yenyewe.
* Majengo ya Nuru: Wengine huona majengo au mahekalu yaliyotengenezwa kwa nuru na yanayometa, yakitoa hisia ya hekima au maarifa.
* Muziki wa Ajabu: Muziki na sauti zilizomo katika maeneo hayo huelezewa kuwa safi na kamili kuliko muziki wowote wa kidunia, wenye uwezo wa kugusa nafsi moja kwa moja.

3. Kupata Maarifa na Hekima Kubwa
Watu walio na NDEs mara nyingi huja na maarifa mapya kuhusu ulimwengu na maisha.
* Uunganisho wa Yote: Wanahisi kujua kwamba kila kitu kimeunganishwa na kwamba mawazo na matendo ya kila mtu huathiri kila kitu kingine.
* Umuhimu wa Upendo: Maarifa makubwa wanayopata mara nyingi huishia katika hitimisho moja: upendo ndio kiini cha uwepo na ndio lengo kuu la maisha hapa duniani.

4. Kuingia Katika "Mstari wa Mbele" au "Mji wa Mbele"
Baadhi huripoti kuingia katika eneo ambalo linaonekana kama "maktaba ya ulimwengu wote" au sehemu ambayo inashikilia maarifa yote yanayowezekana.
* "Kitabu cha Maisha": Kuna wengine wanasema waliruhusiwa kuchungulia kwenye kile wanachokiita "Kitabu cha Maisha" au hifadhi ya kumbukumbu za ulimwengu, ambapo walipata kuelewa mambo ya msingi na ya mwisho kuhusu uhalisia.

5. Kuhisi Hisia Kali Kubwa
Hisia wanazopata si za kawaida; zimepitiliza kiasi cha hisia za kibinadamu.
* Amani Isiyo na Kikomo: Huwa wanasema walihisi amani na utulivu ambao hauwezi kulinganishwa na amani yoyote ya kidunia.
* Upendo Kamili: Hisia ya upendo usiokuwa na masharti kutoka kwa Nuru au Kiumbe cha Nuru ni jambo la msingi kabisa na la kubadilisha maisha yao.

Kwa kifupi, NDEs huelezewa kama uzoefu wa fahamu wa hali ya juu, uliojaa hisia chanya, uhakika wa maarifa, na kukutana na viumbe vya mwanga au wapendwa wao.
Je, ungependa kujua zaidi kuhusu namna wanasayansi wanavyojaribu kuelezea matukio haya kwa kutumia mifumo ya kibiolojia (ubongo)?
 
Natamani sana kuna watu ambao ilishawahi kuwatokea hii waje wathibitishe.
Kifo ni spiritual experience. Shifting of dimension tu, huwezi shift kwenda dimension ingine pasipo roho itawalayo au iishie kwenye ile dimension. Kwani huwa huoti ndoto au ku fall into trance?
 
Inategemeana na mtu alikuwa anaamini nini, kama alikuwa anaamini malaika atawaona na kama alikuwa anaabudu mashetani basi ataona mashetani, tena mashetani ya kutisha
 
Wewe na huyo ChatGPT wote ni waongo, huyo mtu atalipoti vipi alivyojisikia kufa wakati amesha kufa? Ukweli ni kwamba utamuona tu Isirael mtoa roho akija na panga lake kwa mbwe nyinyi na mwikwala kibao mwisho utahisi tu shwaaaaaaaa umeshaenda kama ng'ombe machinjoni.
 
N.D.E aliipata Shangazi yangu baada ya kupata Ajali .. (Aligongwa na Baiskeli) alikuw afe.

Baada ya fahamu kumrudia (akiwa ICU) alisimulia same scenario ya watu wengine wanayopitia N.D.E

Yeye yake ilikuwa tofauti kdg sana, aliitwa sehemu aende.. akaangalia nyuma.. akagoma kwenda na kurudi nyuma. (Inavyosemekana, kama angekubali kwenda basi alikuwa Afe).

Ni siku nyingi sana.. ntamtafuta nimuulize zaidi...
 
Wewe na huyo ChatGPT wote ni waongo, huyo mtu atalipoti vipi alivyojisikia kufa wakati amesha kufa? Ukweli ni kwamba utamuona tu Isirael mtoa roho akija na panga lake kwa mbwe nyinyi na mwikwala kibao mwisho utahisi tu shwaaaaaaaa umeshaenda kama ng'ombe machinjoni.
Mkuu umesoma vizuri lakini?
Siyo kwamba mtu alikufa yaani alikaribia kufa mfano kupata ajali mbaya pia kuhusu kusimulia...baada ya kupata fahamu huwa wanaeleza matukio yaliyokuwa yakiendelea mfano wanasimulia madaktari walivyokuwa wanafanya.
 
Inategemeana na mtu alikuwa anaamini nini, kama alikuwa anaamini malaika atawaona na kama alikuwa anaabudu mashetani basi ataona mashetani, tena mashetani ya kutisha
Hakuna vitu kama hivyo, hizi stories zimeletwa na watu wa dini kabla ya hapo hakukuwai kuwa na hizi stories za kusadikika.

Mtu yeyote anapokufa anapitia hatua ambayo angepitia muovu au mtenda mema, hizo habari zenu za kuona malaika na mashetani ni uzushi umeletwa ambao hauna ushahidi, vile vile huwezi kuleta masimulizi ya mahala ambapo hakuna mtu amewai kwenda akarudi, hivyo stories zenu zinabaki kama ngonjera za kusimulia watoto muda uende.

Dini zimeleta hofu kwa watu kuofia hata kwa kitu ambacho ni asili hakihusiani na mambo ya kutishana wala hizo hukumu zenu na Mbingu za mchongo.

Anayesema ukifa unaenda mbinguni sijui jehanamu muulize anaushahidi upi? Kama hajaanza kusema kasikia kwa fulani au kaona imeandikwa mahala fulani, why asilete ushahidi aliouna yeye kama yeye?.

Hakuna aliyewai kufa akarudi, hayupo na hatowai kuwepo, kiuhalisia hata hawa mnaowaona wamezinduka mkidai walikufa, kiuhalisia walipitia tu kitendo cha baiolojia ambapo Ubongo unakuwa active lakini mapigo ya moyo yanasimama kwa zaidi ya saa72,

Madactari wanaelewa hili, ndiomana kuna mashine za kushitua mapigo ya moyo ili mtu huyu aamke, ikishindikana kama akili(ubongo) bado uko active mtu huyu lazima ataamka tu hata zipite siku5, kwa maana hakufa bali alikuwa ktk DEEP SLEEP PARALYZE.

Tutafute maarifa tuache kuupa uongo kipaumbele hata kwa mambo mepesi
 
Mkuu umesoma vizuri lakini?
Siyo kwamba mtu alikufa yaani alikaribia kufa mfano kupata ajali mbaya pia kuhusu kusimulia...baada ya kupata fahamu huwa wanaeleza matukio yaliyokuwa yakiendelea mfano wanasimulia madaktari walivyokuwa wanafanya.
Hao hawakufa na hawakupitia kitendo cha kufa bali sehemu ya akili ambayo haihusiani na matendo ya hiari huamka the same way akili inavyoamshwa na wale wafanya meditation mwili unakuwa ktk paralyse lkn akili kupitia milango ya fahamu ya ndani(Nafsi) ambayo haiutegemei mwili kuhisi, huwa active na kuona kila litendekalo ktk mazingira yanayouzunguka mwili.

Kitendo hiki ni kawaida mwili ukiwa ktk shida za kiufahamu, au usingizi, au mawazo mazito na hakihusiani na kifo, hili watu wa meditation wanalijua ni kawaida, wanaoshituka ni hawa wasiojua lolote kuhusu sayansi ya akili na utambuzi wa akili ya kina, mngekuwa mnafundishwa haya mambo msingekuwa mnashituka mkiyaona au kuyasikia.

The same way afanyaye meditation kwa mara ya kwanza hupitia mshituko ule ule anaoupitia mtu aliye ktk paralyse ya kimwili baada ya ugonjwa/accident kwa maana hajui ni nini kinafanyika, hakuna muujiza hapo.

Narudia tena, hakuna anayeweza kushuhudia mambo ya huko kifoni maana hakuna aliyewai kufa akafufuka hayupo, hao mnaosema walikufa ni UONGO walikuwa ktk Deep sleep huku akili zao zikipitia matendo ambayo wafanya tahajudi, meditation na yoga hupitia.
 
Wewe na huyo ChatGPT wote ni waongo, huyo mtu atalipoti vipi alivyojisikia kufa wakati amesha kufa? Ukweli ni kwamba utamuona tu Isirael mtoa roho akija na panga lake kwa mbwe nyinyi na mwikwala kibao mwisho utahisi tu shwaaaaaaaa umeshaenda kama ng'ombe machinjoni.​
Huo ukweli wewe umeujuaje ?
 
N.D.E aliipata Shangazi yangu baada ya kupata Ajali .. (Aligongwa na Baiskeli) alikuw afe.

Baada ya fahamu kumrudia (akiwa ICU) alisimulia same scenario ya watu wengine wanayopitia N.D.E

Yeye yake ilikuwa tofauti kdg sana, aliitwa sehemu aende.. akaangalia nyuma.. akagoma kwenda na kurudi nyuma. (Inavyosemekana, kama angekubali kwenda basi alikuwa Afe).

Ni siku nyingi sana.. ntamtafuta nimuulize zaidi...
Hata wewe hapa ukijaribu kufanya meditation utayapitia hayo aliyoyapitia huyo ndugu yako.

Kifo kinapotokea huwa hakuna excuse ni lazima ufe either unataka au hutaki maana hiyo huwa ni nguvu ya asili ambayo inatambua uwepo wako duniani kwa siku na saa ambazo lazima uzikamilishe na zinapokamilika ni lazima tu ufe iwe kwa ajali au hata mafua lazima yakuondoshe,

Hayo mambo ya kuitwa na kuona watu sijui mambo gani ni yakawaida na mara nyingi ni viumbe wa sanaa(pepo wa giza) ambao ndio hawa hawa huwapa maono wale wanaojiita wachungaji au wale wanaosema walipelekwa kuzimu na mbinguni kumbe ni michezo ya hawa viumbe wenye uwezo wa kuteka akili na kuionesha maono yoyote ili mtu huyu baada ya akili Yake ya kimwili kuamka akayasimulie haya mambo ambayo kiuhalisia ni uongo na uzishi.

Nikazie tena, mtu yoyote anayefanya meditation anaelewa hili jambo unapofungua mlango wa fahamu wa mwili wako na nafsi yako automatic unakuwa ktk ulimwengu wa mwili na nafsi kwa wakati mmoja ambapo lazima utakuwa na uwezo wa kuona/kuhisi uwepo wa viumbe wengine ambao ndio hao huishawishi nafsi yako kubaki ktk makazi hayo ili ziutawale mwili wako kama vile wanavyotawaliwa watu wenye pepo,

Zoezi hili likifanikiwa mtu huyu anakuwa kapagawa na pepo lakini hafi bali anapoamka huamka akiwa tayari anamilikiwa na pepo, na zoezi hili halihusiani na kifo wala pepo hao hawana uwezo wa kukutoa uhai.

Mambo haya hamuwezi kufundishwa ktk hizo dini zenu maana yako BEYOND ufahamu wa watu waliofungwa na mafundisho ya kidini.
 
Hata wewe hapa ukijaribu kufanya meditation utayapitia hayo aliyoyapitia huyo ndugu yako.

Kifo kinapotokea huwa hakuna excuse ni lazima ufe either unataka au hutaki maana hiyo huwa ni nguvu ya asili ambayo inatambua uwepo wako duniani kwa siku na saa ambazo lazima uzikamilishe na zinapokamilika ni lazima tu ufe iwe kwa ajali au hata mafua lazima yakuondoshe,

Hayo mambo ya kuitwa na kuona watu sijui mambo gani ni yakawaida na mara nyingi ni viumbe wa sanaa(pepo wa giza) ambao ndio hawa hawa huwapa maono wale wanaojiita wachungaji au wale wanaosema walipelekwa kuzimu na mbinguni kumbe ni michezo ya hawa viumbe wenye uwezo wa kuteka akili na kuionesha maono yoyote ili mtu huyu baada ya akili Yake ya kimwili kuamka akayasimulie haya mambo ambayo kiuhalisia ni uongo na uzishi.

Nikazie tena, mtu yoyote anayefanya meditation anaelewa hili jambo unapofungua mlango wa fahamu wa mwili wako na nafsi yako automatic unakuwa ktk ulimwengu wa mwili na nafsi kwa wakati mmoja ambapo lazima utakuwa na uwezo wa kuona/kuhisi uwepo wa viumbe wengine ambao ndio hao huishawishi nafsi yako kubaki ktk makazi hayo ili ziutawale mwili wako kama vile wanavyotawaliwa watu wenye pepo,

Zoezi hili likifanikiwa mtu huyu anakuwa kapagawa na pepo lakini hafi bali anapoamka huamka akiwa tayari anamilikiwa na pepo, na zoezi hili halihusiani na kifo wala pepo hao hawana uwezo wa kukutoa uhai.

Mambo haya hamuwezi kufundishwa ktk hizo dini zenu maana yako BEYOND ufahamu wa watu waliofungwa na mafundisho ya kidini.
Je hata hao watu wa mediation na wao hupata maumivu makali wakati wa kurudi katika mwili wao?
 
Hakuna vitu kama hivyo, hizi stories zimeletwa na watu wa dini kabla ya hapo hakukuwai kuwa na hizi stories za kusadikika.

Mtu yeyote anapokufa anapitia hatua ambayo angepitia muovu au mtenda mema, hizo habari zenu za kuona malaika na mashetani ni uzushi umeletwa ambao hauna ushahidi, vile vile huwezi kuleta masimulizi ya mahala ambapo hakuna mtu amewai kwenda akarudi, hivyo stories zenu zinabaki kama ngonjera za kusimulia watoto muda uende.

Dini zimeleta hofu kwa watu kuofia hata kwa kitu ambacho ni asili hakihusiani na mambo ya kutishana wala hizo hukumu zenu na Mbingu za mchongo.

Anayesema ukifa unaenda mbinguni sijui jehanamu muulize anaushahidi upi? Kama hajaanza kusema kasikia kwa fulani au kaona imeandikwa mahala fulani, why asilete ushahidi aliouna yeye kama yeye?.

Hakuna aliyewai kufa akarudi, hayupo na hatowai kuwepo, kiuhalisia hata hawa mnaowaona wamezinduka mkidai walikufa, kiuhalisia walipitia tu kitendo cha baiolojia ambapo Ubongo unakuwa active lakini mapigo ya moyo yanasimama kwa zaidi ya saa72,

Madactari wanaelewa hili, ndiomana kuna mashine za kushitua mapigo ya moyo ili mtu huyu aamke, ikishindikana kama akili(ubongo) bado uko active mtu huyu lazima ataamka tu hata zipite siku5, kwa maana hakufa bali alikuwa ktk DEEP SLEEP PARALYZE.

Tutafute maarifa tuache kuupa uongo kipaumbele hata kwa mambo mepesi
subiri lissu akirudi tumuulize
 
Binadamu wanapokufa huenda kuzimu. Na kuzimu ni sehemu ya giza ila ni ndani ya ulimwengu huu tunaoishi lakini hapo ni total darkness. Wanaofanya meditations kutoka nje ya mwili at the first ni lazima ulione giza. Ulimwengu wa nje ya roho ni giza but am not sure.
 
Mkuu umesoma vizuri lakini?
Siyo kwamba mtu alikufa yaani alikaribia kufa mfano kupata ajali mbaya pia kuhusu kusimulia...baada ya kupata fahamu huwa wanaeleza matukio yaliyokuwa yakiendelea mfano wanasimulia madaktari walivyokuwa wanafanya.
Sasa hizo ni ndoto za kuzimia siyo kufa.
 
Back
Top Bottom