Wachawi wamemchukua mwanangu

Wachawi wamemchukua mwanangu

namuunga mkono diamond kwa kumkinga mwanae dhidi ya uchawi, haya mambo yapo kabisa, na hakuna namna ya kumkinga mtoto zaidi ya njia za kitamaduni. wazazi wetu walitulinda na wao walilindwa. tusijifanye wazungu na kuona aibu. tutakuwa tunawazalia wachawi
 
Pole sana!
ila hofu yangu ni moja! ku deal na mchawi lzm utumie uchawi pia vinginevyo butimba itakuhusu! nenda kiafrika zaidi anza na ramri ukimjua nawe mrushie kombora mgawane maumivu!
 
Pole sana Ndg yangu. Hakika inauma sana. Sasa kiapo cha kisasi, kisasi utarudisha kwa nani nawe humfahamu aletenda hayo?
 
Pole sana ndugu hata mimi nilishapatwa na janga kama lako. Hilo tatizo lililosababisha mauti ya mwanao nitatizo analopata wakati anazaliwa na nadiliki kusema ni uzembe wa wakunga.

Hii inatokana na njia ya mzazi kuwa ndogo(ila sio ya kufanyiwa upasuaji) kwahiyo wakati mama anajifungua inatakiwa mkunga amsaidie kumvuta mtoto badala ya kuachwa akasukuma mwenyewe.

Akiachwa mzazi kusukuma mtoto peke yake itasababisha atumie mda mrefu kujifungua huku mtoto anatoka amebanwa mwili na ni kwasababu viungo havijakomaa itasababisha damu ivilie ndani kichwani, puani mdomoni hata kifuani .

kwa kifupi wakunga wengi ama hawajui au makusudi husababisha vifo vya wachanga wengi wakati wa kujifungua.

Mungu akupe subira na nguvu.
 
Sihitaji kukuelewa kwa Sasa umechanganyikiwa saana Japo kwa imani yangu tena ya mbinguni naamini ni kweli uchawi upo licha kufanikiwa au kutofanikiwa kwa uchawi ni jambo lililo mkononi mwa Muumba MUHIMU :Ishi maisha ya Imani na jua lililo kufika lisingekufika ila ni ili ujaribiwe
 
Pole sana mkuu @Counseller. Wachawi ni washenzi sana. Mkuu wangu ninakuomba kama ukimpata mganga wa kuweza kusitisha roho ya huyo mchawi basi tuwasiliane PM nimpate maana kuna ndugu yangu tatizo kubwa sana. Dawa ya moto ni moto si maji. Liwalo na liwe. Kama hayajakufika huwezi kuwaza kama mimi Zogwale hapa.
 
Mimi ninaamini asilimia mia moja kwa maelezo uliyotoa ni kweli kalogwa sasa hakuna namna pambana nao nawewe uwauwe kwa njia hiyo hiyo waliyotumia kumtoa uhai mwanao ila usijaribu kushika panga utafungwa na adui yako atakumalizia ukiwa jela angalia
 
Mama alimuacha peke yake? Kwa nn hukuenda kupima akitobolewa na nini? Km je paka alitaka kumla? Jmn usirukie upande mmoja tu na kutoa conclusion.

Pole sana!
 
Kwako na kwa baadhi ya wana Jf pia.
...Mtoto anapozaliwa hususani hospitalini, kile chumba za kujifungua huwa kunakuwapo na wachawi wengi sana. Ni ngumu kuwaona ktk macho ya nyama ila ni wapo mule. Wakiwa mule ndani huwa wanakuja chukua vitu vifuatavyo
1. Damu inayotoka kwa mmama anayejifungua, damu ndio kinywaji cha majini na wachawi. Pia mda mwingine huwa wanabatiza kupitia damu za watu, hii ni stage ya juu ktk uchawi.
2. Vitovu vya watoto, vitovu vya watoto huwa vinatumika hususani ktk mauaji, ushawahi kusikia mtu anaumwa ghafla anakonda kama anaumwa UKIMWI kisha akafa, yaani hachukui hata wiki mbili? Basi hiyo ni moja ya shughuli za kitovu cha mtoto, ni KUUA. Kitovu pia kinaweza kutumika kuhifadhia uchawi, kitovu pamoja na malango ya uzazi. Kama wachawi wanataka kumpa mtoto mikoba na kumwandaa mapema huwa wanafanya hiki kitu.
3. Nyota ya mtoto, mtoto tangu akiwa tumboni mwa mamaye mchawi anaweza tambua nyota ya mtoto.
4. DAMU (Hii ndo MBAYA ZAIDI) Damu ni uhai wa mtu yaani ndio nafsi kamili ya mtu. Wanapochukua damu ya mtu ina maana Uhai kamili wa mtoto upo kwao, yule mtoto anaweza akalelewa kuzimu au na kituo cha wachawi na ninyi watu kwenye jamii msijue. Watoto wanaochukuliwa damu na wachawi tangu wakiwa wadogo wakifika miaka ya 16 na kuendelea huwa wanakuwa wachawi ktk kiwango cha hali ya juu sana, na kadri siku zinavyozidi kwenda ndo anavyozidi kupanda kiwango. Na kama mtoto huyo amechukuliwa damu akiwa anazaliwa na kulelewa kuzimu, akafika miaka flani hivi huwa wanapotea kabisa jamii au huwa wanakufa ktk hali isiyoleweka. Kinachotokea hapo ni kumchukua huyo mtoto moja kwa moja. Watoto hawa huitwa JINI JIWE (Yaani ameunganishwa na ufalme wa majini tangu akiwa tumboni mwa mama yake). Inawezekana mama yake akawa anajua au asijue.

Vipo vitu vingi sana watoto wetu wanapozaliwa kama hawana kinga ya Mungu mambo hayo hutokea.

TURUDI KWENYE MADA.

Ukiona kifo chochote cha ghafla, inawezakana ni kweli ni mapenzi ya Mungu ama ni ya Ibilisi. Wachawi huwa wanatumia mbinu flani ktk kuua na inawezakana kwa mtoto wako ikawa ni hivyo.
Huwa wanatuma Jini kwa huyo mtoto, lile jini likishamwingia huyo mlengwa wachawi wanakuja kumchukua yule mtoto halisi ambae ni wa kwako kisha wao wanaacha lile jini. Kwahiyo kwa macho ya kibinadamu unaona ni mtu ila sio mtu. Na Jini hilo sharti ni kuishi SIKU 7 TUU. Likiendeleza hapo mnaweza mkagundua mabadiliko ndani ya mtoto, anaweza akakataa vitu vya kawaida na hata maumbile yake yakabadilika. Ama hilo jini linaweza kuishi zaidi ili kuwadhoofisha na kuwanyanyasa ndugu wanaoishi na huyo mtu. Kwahiyo kama ni mipango ya Ibilisi basi tambua yule hakuwa mtoto ila lilikuwa ni hilo jini ambalo lilipaswa kukaa ndani ya siku 7 tuu ili kuonesha mauti kwa mtoto. Na kikawaida mtu ukishachukuliwa nafsi yako, akija Mtumishi wa Mungu kukuombea, anaweza kuirejesha nafsi ya huyo mtu. Hata kama madaktari wakisema huyo mtu kafa ila kama hajafa kwa mapenzi ya Mungu ila ni nafsi tu imechukuliwa basi uhai wa huyo mtu waweza kurudi.

Kwahiyo kama ni nguvu za zimemuondoa mwanao basi tambua mlichozika sio mtu, ndo maana unaambiwa hata mtu akichukuliwa msukule huwa hawaziki mtu.

***USHAURI WANGU KWAKO***
Mpe Yesu maisha yako, hakuna njia mbadala wa kupambana na mchawi mbali na YESU. Usiende kwa Mganga maana Mganga ndie mchawi mwenyewe. Sitaweza kueleza sana juu ya hili kwa Post ila amini nikuambiacho.
Sababu kubwa ya wewe hayo yote kukutokea ni kutokumpa Yesu maisha yako, Mkuu OKOKA na usimame kweli kweli kwenye wokovu. Shetani hajawahi kumshinda Mungu, hao waganga nao ni wafuasi wa shetani ndani ya dunia hii.
Karibu ndani ya Yesu, ukiingia ktk vita hii na wachawi pasipo Yesu utakuja kujijutia tuu.
Amina.
 
Pole sana ndugu yangu;
Napenda kusema tu kwamba, ukianza kwenda kwa waganga wa kienyeji (ambao wengi ni wachawi) utajikuta unaendelea na mahudhurio mpaka pesa zako zitakapoisha kabisa. Hakuna watu wabaya hapa duniani kama waganga wa kienyeji, mimi nilishapata maruweruwe kazini, kun watu wakanipush niende kwa waganga( wao walisema wataalam) Nilichoambiwa huko ni kwamba rafiki yangu kipenzi kabisa ndo ananiroga eti ananionea wivu nimemzidi maendeleo.

Niliona ni upumbavu kabisa maana kwa huduma hiyo tu nililiwa 230,000/- (laki mbili na elf thelathini), kilichofuata ITV, nilifuta ratiba zote za za waganga na nilitangaza la mgambo kwa wote waliokuwa wananishauri uganga, nikaamua kujiendea kanisani maana nilijilaumu afadhali ile 230 ningenunua kreti zacastle lager nikajifungia ndani mpaka ziishe. ukienda huko wanawezakukuambia either mke wako, mama yako, mama mkwe wako au jirani au ndugu yako ndokamroga kwakuwa tu wanajua umejiandaa kupokea taarifa za uchawi.


Nakushauri, u move on, achana na haya mambo kabisa.
 
Duh pole sana mkuu.mungu akutie nguvu kwa wakati mgumu ulionao
 
Mimi ninaamini asilimia mia moja kwa maelezo uliyotoa ni kweli kalogwa sasa hakuna namna pambana nao nawewe uwauwe kwa njia hiyo hiyo waliyotumia kumtoa uhai mwanao ila usijaribu kushika panga utafungwa na adui yako atakumalizia ukiwa jela angalia
Unaweza ukaona ni rahisi sana kupambana na mchawi kupitia waganga, usipoangalia hata wewe unaweza ukaja ukawa mchawi.
Neno la Mungu ndio silaha pekee ya kupambana na mchawi. Vita ya kichawi ni mbaya saaaana. Inakuja kugharimu mpaka watoto wako na kizazi chako.
 
Pole saana..! Huko sukumaland kwa akina 'nyoka a makengeza' kunatisha
 
pole sana mkuu but usingezika mapema maana mmh! kuna dalili ya maiti kuwa mgomba...
 
Back
Top Bottom