Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Hapa watapata wanachama wengi tu.

Si unajua mitoto yote ya Mafisadi ipo hapa?

Shule haiendi kazi yao kubwa ni kuangusha Birth Day, BBQ, Ulabu na kujifanya Buzy kwenye kila Misiba hata kama aliyekufa ni rafiki wa rafiki yake kutoka Ghana au Nigeria.

ulichokisema ni cha ukweli kabisa tena kweli tupu
 
Nguruwe hata kama utampaka lip stik bado atakuwa ni nguruwe tu
 
Kama super power USA inaporomoka what a hell is SISIEMU? Kuna mitaifa kama China India zinakuja juu na ULAYA wakaogopa wakaungana lakini its use less kwani hii mitaifa ya China na India wanadamu wengi waishi humu na nguvu kazi kubwa iko huko na wafanya kazi kweli kweli!

Kwa hiyo sasa watapa tapa na dawa ni kudhibiti fedha kutoka BOT nk. ili washindwe kufanya kampeni za kifisadi wanaume family sijui na sasa wataweka wanawake family 2010
 
Kama sirkali inaongozwa na sisi emu....Then sirkali ni ccm na viongozi wake wakija huku ni ccm bado...Yani ni ccm na ni sirkali hapo hapo...Ni sirkali ya EPA.
Hatuwezi kuwachagulia watanzania ni maisha ya aina gani wanataka....Kama wanataka pilao shida ikwapi?
Na kama watoto wao wanataka kandambili pia wapi shida?
Wa USA na kwingineko nao wadai ulabu...Ndio maisha hayo...Kula kwa mwendo wa mbere.
Wananchi itabidi wavumilie tu...Kwasababu sisi ni masikini sana...Hivyo wananchi wafunge mkanda....Na nina imani ccm haitafanya makosa.
Kwanza hata EPA haikuwa makosa ni UNAFIKI TU wa hao wanaojiita wapinzani!
Njaa KALI...Sasa wao wanataka zaidi ya pilao...Nani awape?
 
Hawa watu wa UK na Asia wanaofungua haya mashina ya CCM wanaboa kweli. I'll put em on blast this coming sunday. I just can't stand them grrrrrrrrrr.

AAAAAAAAAAAAARGHHHHHHHHHH...hawa watu wa USA wanaboa kweli na mashina yao ya CCM.........I'll put 'em on a mix tape this x-mas!! LOL!!
 
Nzoka ni muhimu kuyaheshimu maamuzi ya wananchi hata kama hatuyapendi.
Wananchi waliandamana kumuunga mkono Mh Rais mara baada ya hotuba yake...Sasa kutaka sisi tupingane na wananchi na viongozi wao wanao wapenda ni sawa na uhaini ama kutaka kuleta machafuko.
Hawa watu hawana shida...Acha wafungue matawi kwasababu sirkali ni ccm na ccm ni sirkali....Sasa hata kama wakifunguwa matawi a sirkali...ccm si ndio hio hiyo sirkali?
Upinzani nafasi kubwa waliyoipata msimu huu ni tume ya madini aliyowekwa Zitto.
Sana sana ni hadi urudi ccm kama Kaburu,Marandu na Masumbuko....Nje ya hapo ni HASARA!
Huyu Hasara naye ni member mzuri tu ila alishafungiwa hapa....
 
Nzoka ni muhimu kuyaheshimu maamuzi ya wananchi hata kama hatuyapendi.
Wananchi waliandamana kumuunga mkono Mh Rais mara baada ya hotuba yake...Sasa kutaka sisi tupingane na wananchi na viongozi wao wanao wapenda ni sawa na uhaini ama kutaka kuleta machafuko.
Hawa watu hawana shida...Acha wafungue matawi kwasababu sirkali ni ccm na ccm ni sirkali....Sasa hata kama wakifunguwa matawi a sirkali...ccm si ndio hio hiyo sirkali?
Upinzani nafasi kubwa waliyoipata msimu huu ni tume ya madini aliyowekwa Zitto.
Sana sana ni hadi urudi ccm kama Kaburu,Marandu na Masumbuko....Nje ya hapo ni HASARA!
Huyu Hasara naye ni member mzuri tu ila alishafungiwa hapa....

jmushi, I could care less about that stuff. Namtania tu GQ, the fact now they are knocking into the USA.......I thought u guys were wiser/smarter than us wabeba ze maboksiz.
 
jmushi, I could care less about that stuff. Namtania tu GQ, the fact now they are knocking into the USA.......I thought u guys were wiser/smarter than us wabeba ze maboksiz.

Mimi binafsi simo humo...Ila mtima nyongo siwaonei wala nini...Kwanza waanze mageuzi huko bongo.
Kama hao wasomi wa huko bongo ndio EPA...Na wananchi wanawapenda...Sasa sisi upinzani nje ya nchi wa kazi gani?
Na kama ni kuwa wise..Basi hao walioko bungeni ndio wa kuwapigia kelele....Tena muwakwide mashati kabisa!
Kuwalaumu watanzania wa USA kwa kufungua matawi ili na wao wafaidi EPA ni uonevu wa hali ya juu!
Mbona Zitto yeye aliachiwa ulaji wa kamati ya madini?
Upinzani na ufe!
 
Ukitaka mambo yako yanyooke, jiunge na CCM. Vibaka wa CCM wanaweza wakaanzisha matawi kuepuka kuchomwa moto. Maalbino wafungue tawi la CCM wasichunwe ngozi na kuuawa. Machangudoa waanzishe tawi la CCM na mambo yao yatawanyokea (UWMDCCM). Wapida Debe wa Daladala wanasubiri nini kuwa Umoja wa Wapiga Debe wa CCM (UWDDCCM) wasibughudhiwe na askari. Umoja wa Wapika Gongo wa CCM (UWGCCM) bila shaka utatafutiwa mitambo ya kisasa badala ya kukamatwa. Tawi la CCM la Wasambaji wa Dawa za Kulevya litakua tishio kwa wapinzani (UWDKCCM). Magaidi nao hawatabaki nyuma kuanzisha bonge la tawi and the list goes on and on and on........
 
Kila kitu haramu ni halali ndani ya ccm...Cha muhimu tujenge Taifa letu na tuachane na kupingana ambako kunapoteza muda wa wananchi na ruzuku ambazo ni pesa za kodi.
Wananchi wahahakikishe wanawachaguwa viongozi wa kweli.
Mrema na yeye arudi ccm tu.
Hakuna haja tena ya kupoteza muda,pesa,rsilimali na kumwaga damu kama ilivyotokea kwa Wangwe....Sisi sote ni ndugu moja na upinzani ni ushetani wa mkoloni ili aweze kurudi kwa kuwatumia mamluki wake...Huku wakiwa na lugha nzuri na vitendo hewa na unafiki juu!
Ukabila haukuwa kwenye levele iliyoko kabla sijaondoka bongo...Nilirudi hapo nikagunduwa kuwa direction tunayochukuwa ni mbovu!
Tupiganie kwanza mambo ya absolute advantage na opportunity costs....Tuwape wananchi ELIMU na UHURU upiganiwe....Baada ya hapo ni sisi tutakuwa tunawanyima wazungu na waarabu na wahindi visa.
Kwanza wahindi nao hovyo sana tu.
Waafrika....Mchina na muhindi....Wanaenda matawi ya juu...Mwafrika awe makini kwani hatutaki tena kutumika kama ngazi ya hawa mashetani...Muhindi utajiri nao si anatoa Afrika tu kama mzungu na sasa mchina...Mwarabu naye ananyemelea ili kuziba pumzi mzungu....Lakini wao ndio wametufikisha hapa tulipo...AFRIKA....THIS IS YOUR TIME.
Tuanze kuviweka vyama vingi kando na tupiganie maslahi ya AFRIKA.
KWANINI TUSIANZISHE CHAMA KIMOJA CHENYE ITIKADI MOJA YA AFRIKA?
YANI ILE AFRIKA KABLA YA COLONIALISM....
 
hakuna ubaya wowote wa kufungua matawi nje ya nchi ya chama chochote kama hakuna uvunjaji wa sheria!
 
hakuna ubaya wowote wa kufungua matawi nje ya nchi ya chama chochote kama hakuna uvunjaji wa sheria!

I agree with you. Ni vizuri watanzania tukakuza uhuru wa mawazo kwani hiyo ndiyo njia pekee itakayosaidia kuwapatia uelewa watanzania walio wengi. Kama watanzania wanaoshi nje kwa utashi wao wataka kujihusisha na siasa kwa namna wao wenyewe wanaona inafaa, waachwe wafanye hivyo.
 
Nimekuwa nikijiuliza sana je kunani kwenye Chama cha mapinduzi mpaka kuanza harakati za kufungua matawi ya chama chake nje ya nchi, ninaamini kwamba watanzania walioko nje hawajaruhusiwa kupiga kura, hivyo kama unataka kushiriki kwenye siasa ni lazima urudi tanzania wakati wa uchaguzi ndipo utaweza piga kura. Swali jingine ni kwamba gharama za uendeshaji tawi ni za juu sana nje ya nchi haswa kwenye nchi za ulaya na marekani ya kaskazini.

Je haya ni matawi ya CCM ama ni mbinu za kifisadi kuibia fedha za umma kwa mgongo wa CCM.

Kimtazomo kinachofanyika ni kukusanya watoto na jamaa za mafisadi ilikuweza kuridhishwa ufisadi. Matawi mengi yanayoazishwa yanaanzishwa na watoto wa vigogo au wa ndugu au jamaa waliopo madaraka kwa ahadi ya kutumiwa fedha kwa mgongo wa chama au kupewa tenda za serikali kwa mgongo wa mwenzetu au kupatiwa kazi.

Hii sumu inayopandikizwa ni sumu mbaya sana, ukiangalia kuanzia uingereza na marekani safu ya matawi haya ni utapeli, wizi, hujuma na uzandiki. Wanatumia fedha za serikali kufanyia mambo ya chama, wanatumia vyeo vya serikali kufanyia mambo ya chama wanatumia fedha za wananchi kulelea watoto wao na jamaa zao kwa kutumia jina la chama.

Badala ya watanzania kuungana kitaifa CCM inabomoa hilo nje ya Tanzania na kuanzisha imani za chama. Viongozi wa serikali wakitembea nchi za nje badala ya kukutana na watanzania wa kada mbalimbali eti wanakutana na viongozi wa ccm kwenye matawi ya nje kweli tutafika.

Wapo watanzania wengi nje ya tanzania wasomi, wataalamu mbalimbali, wafanyabiashara,nk lakini haya yote ndani ya serkali ya ccm hayaonekani wanaleta siasa mpaka kwenye mambo muhimu ya maendeleo ya nchi.
hawa viongozi wa matawi ya CCM wataisaidia nini nchi?
Badala ya kutengeneza network ya watu wanaohitajika kwa maendeleo ya nchi inatengenezwa network ya ufisadi.
Rejea upatikanaji wa GIRE wa Richmind.

Imefikia wakati watu hawaamini wanaweza fanya biashara, kazi, au kutumia ujuzi wao tanzania bila kuwa CCM na hii inaletwa na kasumba na vitisho vinavyoenezwa na CCM na serikali yake dhidi ya wananchi wake.Ijulikane wazi kwamba sio kila mwananchi lazima awe mwanasiasa au na chama cha siasa.

Tusipo ziba ufa tutajenga nyumba.
 
Je haya ni matawi ya CCM ama ni mbinu za kifisadi kuibia fedha za umma kwa mgongo wa CCM.

- Jamani jamani mweee mweee mweee, yaani wananchi wa Tanzania, watuwawazima na akili zao timamu, wako majuu wameamua kuanzisha matawi ya CCM, eti hilo nalo ni tatizo la CCM? Wooooi! I am lost!

- Mkuu hivi vyama na matawi vinaanzishwa na mamluki wananchi wenzetu wenye tamaa ya ukubwa na kujikomba kwa viongozi wa juu wanapokwenda kutembelea majuu, mimi enzi zangu za ubaharia sikuona baharia akianzisha tawi la CCM, mind you mabaharia wengi walikuwa na elimu ya kawaida, sasa iweje wasomi tena wa kubobea kujiingiza kwenye haya mambo ya kufungua matawi ya CCM tena Ulaya?

Haya ya kwenda kuanzisha matawi ya CCM ulaya sina uhakika ni nini hasa, lakini one thing I know ni kwamba sio ishu ya CCM kama chama cha siasa!
 
...Mkuu hivi vyama na matawi vinaanzishwa na mamluki wananchi wenzetu wenye tamaa ya ukubwa na kujikomba kwa viongozi wa juu wanapokwenda kutembelea majuu, mimi enzi zangu za ubaharia sikuona baharia akianzisha tawi la CCM, mind you mabaharia wengi walikuwa na elimu ya kawaida, sasa iweje wasomi tena wa kubobea kujiingiza kwenye haya mambo ya kufungua matawi ya CCM?
Kinepinepi, ukweli ni kuwa 'mentality' ya Watanzania imeshaaribiwa na kasumba ya kuona Siasa ndio njia rahisi ya kupata mafanikio, karibu kila Mtanzania sasa hivi anatamani kuwa mwanasiasa; tujiulize kwa nini?

Enzi za Mwalimu mwanasiasa alionekana mtu wa kawaida kwasababu kipato chake kilikuwa sawa na kipato cha Mtanzania wa kawaida. Watanzania walipenda na kujivunia kazi zao na wengi ungewaambia waache kazi zao waende kwenye siasa wangekataa. Leo mambo yamegeuka kwa sababu wanasiasa wamejiongezea ujira usioendana na kipato halisi cha Mtanzania wa kawaida na pia kisichowiana na jasho. Leo hii unaweza kuchagua mwanasiasa kuwa mbunge, akakusanya pesa bila ya kufanya kitu chochote jimboni kwake kisha akatumia 'surplus' aliyokusanya kuwaadaa wananchi wamchague tena. Hii ndio 'mentality' tuliyojipandikisha Watanzania kwa kuhacha 'loopholes' nyingi katika 'laws' na 'bylaws' zetu.

Hawa wenzetu wanasumbuliwa na hako kamentality lakini 'this time' tunapaswa tuwakemee vikali. Kama alivyosema FMES, hawana lolote zaidi ya kujikomba kwa viangozi wa nchi kwa lengo la kuukwaa uanasiasa. Usishangae kama kitaingia chama kingine madarakani vijitawi hivyo vikapukutika vyote au kujibadili na kuwa matawi ya chama hicho. Hawana nia njema na Tanzania kwa sababu Watanzania walio nje ya Nchi wanahitaji kuungana kusaidia Wananchi masikini pasipo kujali 'affiliation' zao na vyama vya siasa. Unapoanzisha tawi la CCM nje ya nchi ni wazi unawatenga wale wasio waumini wa chama hicho na haiwezekani kuwashawishi wachangie maendeleo ya nyumbani maana nguvu ya ushawishi umeshaipunguza! Sasa wanachotaka hasa ni nini??

Siku za nyuma Watanzania nje ya nchi walikuwa na vyama visivyo na uchama wowote, hii ya kuanzisha matawi ya chama naona ni stahili mpya ya kuvivunja vyama hivyo, sasa tunakwenda wapi? Tuwakemee vikali sana hawa walafi wanaojipendekeza kwa viongozi, kama wanataka siasa warudi nyumbani wakagombee; tunachohitaji nje ya nchi ni umoja wa Watanzania wote kwa maendeleo ya nchi na sio kujigawa kivyama.
 
Mimi mtazamo wangu unarejea katika ule usemi usemao 'kila jambo na wakati wake' au maarufu kama ambavyo Mzee Ali Hassan Mwinyi alipenda kusema 'kila zama na kitabu chake'

Mimi ni muumini mzuri wa Uhuru wa kujieleza na pia demokrasia, sioni sababu ya kuwabana watu kimawazo wasiwe huru pale walipo.

Tanzania iliyokuwepo 1960s ni tofauti na ile ya 1970s, 1990s na hata hii ya 2000s. Na Tanzania hiyo pia itaendelea kubadilika kadri siku zinavyokwenda mbele.

Mabadiliko ya makubwa yaliyotokea duniani katika nyanja ya mawasiliano, imebadilisha mtazamo wa dunia hii iliyokuwanayo miongo kadhaa iliyopita. Jambo hili basi limeongeza mahitaji ya binadamu kwa kiwango kikubwa takribani katika jambo linalomgusa katika maisha yake. Kwa hiyo basi, kasi ya mabadiliko sasa na huko tunakoelekea ni kubwa sana na hakuna ambaye ataweza kutabiri ni jinsi gani ya kuipunguza. Na kadri siku zinavyokwenda Dunia inazidi kuwa ndogo kama kijiji.

Shinikizo la mabadiliko hayo na kuifanya dunia kuonekana kama Kijiji hayataitenga siasa na wanasiasa, kwahiyo kinachotokea ni jambo la kawaida linalokwenda na wakati uliopo. Hao unaowaita watanzania, ninahakika kuwa idadi yao leo hii waliopo nje ya nchi ni kubwa kuliko wale waliokuwa katika miaka ya 1990 na hii idadi itaendelea kukua kadri siku zinavyokwenda. Kwahiyo kwa vile community ya watanzania inazidi kukua basi na mahitaji miongoni mwao yanaongezeka, ikiwa ni pamoja na kushiriki siasa kitu ambacho ni utashi wa mtu binafsi na ni haki yake kufanya hivyo.

Ninaamini kuwa umoja wa watanzania hautaghubikwa na maneno ya kinafiki kuwa sisi watanzania ni wamoja kama utakomaa kukataza mtu mwingine asitumie uhuru wake wa kushiriki katika jambo ambalo analipenda ili mradi hajavunja sheria. Hakuna mahali ambapo mtanzania yeyote ambaye amekatazwa kushiriki siasa akiwa nje ya nchi. Hakuna mtazania yeyote ambaye amekatazwa asioe/kuolewa na mtu ambaye si mtanzania eti kwa kufanya hivyo atakuwa haleti umoja wa watanzania, la hasha, tujioneshe vile tulivyo hata kama tuko nje ya nchi na tu-test hiyo dhana kwamba kwa kushiriki siasa nje ya nchi kutaleta utengano miongoni mwa watanzania. Na kama kuna mtu anafikiria kuwa siasa ni eneo la kutengana basi hayuko sawa na haelewi ni nini maana ya siasa.

Ni vema tuwaone watanzania wakiwa na mawazo tofauti kwa maendeleo yao na Tanzania kwa ujumla.

'Kila jambo na wakati wake' au 'kila zama na kitabu chake'
 
Back
Top Bottom