Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Sijui kama hili ni tatizo la uelewa wangu binafsi au kuna kitu kisicho cha kawaida. Nimeshuhudia katika siku za karibuni kuibuka kwa matangazo ya sherehe za sherehe za kuzaliwa CCM ktk nchi mbalimbali, hasa UK na leo tena Marekani. Si lengo langu kuwakosoa watu ambao ni wanachama wa chama chochote, lakini najiuliza ndio vipaumbele kweli vya watanzania walioko nje ya nchi? kukaa kusherehekea kuzaliwa ccm? Ni kwamba wanaipongeza na kuitakia maisha mema, kwa yote mazuri yanayofanyika au?Tena watu wanapongezana kula na kunywa bure, analipa nani gharama? anayelipa kama ni mtu binafsi ana ajenda gani? tuwe wakweli kuna matatizo ya msingi kabisa yanayowakabili watanzania, na wenzetu waliopo nje ya nchi, tulidhani wangetumia muda wao kuona namna gani ya kusaidia mawazo kuliko kupoteza muda kuanzisha matawi ya chama. Ni maoni yangu tu I stand to be corrected.
Ushahidi:

sherehe za kuzliwa CCM marekani
CHAMA CHA MAPINDUZI
TAWI LA MAREKANI
Linapenda kuwakaribisha Wanachama,
Wakereketwa na Watanzania wote popote pale mlipo
katika sherehe za kuadhimisha miaka 32ya
kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Zitakazofanyika
Houston - Texas,
siku ya Jumamosi tarehe 07 mwezi wa 02 saa Mbili kamili usiku,
katika ukumbi wa Safari.
Kwa maelezo zaidi wasiliana na;
Zainab Janguo: 832 206 6277
Miraji Malewa: 832 741 4452
Michael Ndejembi. 713 384 4567.
Wote mnakaribishwa: Vinywaji, Vyakula na muziki bure!

Zainab Janguo,
Katibu Mwenezi,
CCM-Marekani.
 
Hivi sheria za nchi ambazo matawi ya CCM yamefunguliwa zinaruhusu vyama vya siasa ya nchi nyingine kuwa na matawi katika nchi zao!? Sasa naona Watanzania nchi za nje badala ya kuwa na umoja watakuwa wanatenganishwa na vyama hawa CCM, wale CUF na hawa CHADEMA!!! Sijui nchi yetu inaenda wapi!!! Ni bora nchi husika zipige marufuku haya matawi ya CCM katika nchi zao. Imagine kama wahutu na watusi wanaoishi Tanzania waanzishe vyama vyao vya siasa na kisha kutokana na uadui mkubwa kati yao miaka nenda miaka rudi wanapigana na kuuana katika ardhi ya Tanzania, je serikali ya Tanzania italivumilia hili?
 
Last edited:
Hivi sheria za nchi ambazo matawi ya CCM yamefunguliwa zinaruhusu vyama vya siasa ya nchi nyingine kuwa na matawi katika nchi zao!? Sasa naona Watanzania nchi za nje badala ya kuwa na umoja watakuwa wanatenganishwa na vyama hawa CCM, wale CUF na hawa CHADEMA!!! Sijui nchi yetu inaenda wapi!!! Ni bora nchi husika zipige marufuku haya matawi ya CCM katika nchi zao.

Huo ni uwoga wa mawazo. Kila mtu yuko huru kufanya jambo analotaka ili mradi havunji sheria za nchi husika. Kama wewe unataka kufanya sanaa nje ya Tanzania hukatazwi, kama unapenda siasa na unataka kushiriki ruksa. Namba ya watanzania wanaoishi nje ya nchi sasa hivi ni kubwa na mahitaji yanaongezeka. Kama unaipenda Chadema, CUF, TLP ruksa kujiunga na kujadili yale unayoyaona yana manufaa kwa chama chako na nchi yako pia.

Kumbuka CCM ni chama kama vilivyo vyama vingine vya siasa hapa Tanzania, kina wanachama, wakereketwa na wapenzi wake. Nina wapongeza sana CCM kwa kuonesha mshikamano hata wanapokuwa nje ya nchi.
 
Huo ni uwoga wa mawazo. Kila mtu yuko huru kufanya jambo analotaka ili mradi havunji sheria za nchi husika. Kama wewe unataka kufanya sanaa nje ya Tanzania hukatazwi, kama unapenda siasa na unataka kushiriki ruksa. Namba ya watanzania wanaoishi nje ya nchi sasa hivi ni kubwa na mahitaji yanaongezeka. Kama unaipenda Chadema, CUF, TLP ruksa kujiunga na kujadili yale unayoyaona yana manufaa kwa chama chako na nchi yako pia.

Kumbuka CCM ni chama kama vilivyo vyama vingine vya siasa hapa Tanzania, kina wanachama, wakereketwa na wapenzi wake. Nina wapongeza sana CCM kwa kuonesha mshikamano hata wanapokuwa nje ya nchi.

Kufanya sanaa na kuanzisha vyama vya siasa katika nchi za watu ni vitu viwili tofauti. Sijasikia nchi yoyote duniani ina matawi ya vyama vya siasa katika nchi za magharibi UK, US n.k. Na kwa nini wanang'ang'ania kufungua matawi nchi za magharibi!!!? Kwanini wasifungue matawi Kenya, Uganda, Zambia, SA n.k.? Kulikoni? Mbona wakati wa Nyerere hakufungua matawi ya TANU na CCM nchi za magharibi wala majirani zetu!? Kulikoni mpaka awamu ya nne ishabikie hili la kufungua matawi nchi za magharibi?
 
Kufanya sanaa na kuanzisha vyama vya siasa katika nchi za watu ni vitu viwili tofauti. Sijasikia nchi yoyote duniani ina matawi ya vyama vya siasa katika nchi za magharibi UK, US n.k. Na kwa nini wanang'ang'ania kufungua matawi nchi za magharibi!!!? Kwanini wasifungue matawi Kenya, Uganda, Zambia, SA n.k.? Kulikoni? Mbona wakati wa Nyerere hakufungua matawi ya TANU na CCM nchi za magharibi!? Kulikoni mpaka awamu ya nne ishabukie hili la kufungua matawi nchi za magharibi?

CCM haifungui matawi popote pale, ila wanachama ndiyo wanaofungua matawi. Utaratibu ni kwamba mahali popote ambapo pana wanachama wa CCM wasiopungua 50, basi tawi linaweza kuanzishwa. Kwa mantiki hiyo basi pale wanachama walipofikisha idadi ndiyo matawi yameweza kuanzishwa. Kwa taarifa yako matawi ya vyama vya siasa katika nchi za Ulaya na Amerika yanaruhusiwa kwani kuna sheria na taratibu za uanzishwaji na uwepo wake. Mahali kama Amerika wote tunajua Demokrasia ni kongwe.
 

CCM haifungui matawi popote pale, ila wanachama ndiyo wanaofungua matawi. Utaratibu ni kwamba mahali popote ambapo pana wanachama wa CCM wasiopungua 50, basi tawi linaweza kuanzishwa. Kwa mantiki hiyo basi pale wanachama walipofikisha idadi ndiyo matawi yameweza kuanzishwa. Kwa taarifa yako matawi ya vyama vya siasa katika nchi za Ulaya na Amerika yanaruhusiwa kwani kuna sheria na taratibu za uanzishwaji na uwepo wake. Mahali kama Amerika wote tunajua Demokrasia ni kongwe.

Demokrasi ya Marekani ni kongwe lakini hata 'marafiki' wao wa karibu Wayahudi hatujasikia wakifungua matawi ya vyama vyao vya siasa Marekani. Waingereza pia hawana matawi ya vyama vyao vya siasa katika mji wowote ule wa Marekani lakini CCM wamekuwa wa kwanza kufanya hivyo sijui wanawania nini hasa. Itakuwa ni aibu ya hali ya juu kwa nchi yetu pale ambapo vyombo vya habari vya dunia vitakapotangaza "Watanzania wa vyama viwili tofauti vya siasa wapigana Uingereza au Marekani"

Hii katiba uliyonukuu hapo ni kuhusu ndani ya Tanzania na siyo katika nchi za watu.
 

CCM haifungui matawi popote pale, ila wanachama ndiyo wanaofungua matawi. Utaratibu ni kwamba mahali popote ambapo pana wanachama wa CCM wasiopungua 50, basi tawi linaweza kuanzishwa. Kwa mantiki hiyo basi pale wanachama walipofikisha idadi ndiyo matawi yameweza kuanzishwa. Kwa taarifa yako matawi ya vyama vya siasa katika nchi za Ulaya na Amerika yanaruhusiwa kwani kuna sheria na taratibu za uanzishwaji na uwepo wake. Mahali kama Amerika wote tunajua Demokrasia ni kongwe.

"Chama cha siasa ni mjumuiko wa hiyari wa watu wenye lengo moja ya kutwaa uongozi wa nchi au kuongoza nchi" -Hakuna tofauti kati ya CCM na WANACCM, unaposema chama hakifungui matawi ila wanachama inaonesha ni jinsi gani usivyojua unalolisema zaidi ya ubishi wa kiasa ulioambatana na half knowledge. Hakuna mantiki wala Sababu zozote za msingi zinazomfanya mkimbizi kufungua Tawi la Chama cha siasa katika nchi ambayo hawezi kuchukua madaraka ya dola zaidi ya kuwa na nia ya ukombozi ukombozi wa nchi yake ambayo anaufanya kwenye nchi rafiki.

Sasa tukirudi Tanzania ni nchi huru ambayo haihitaji ukombozi wowote zaidi ya ufisadi unaoendelea. Kitendo cha kufungua matawi ni ishara tosha kuwa lengo lenu ni kujiweka karibu na watawala(aka kujipendekeza) mkiwa na fikra kuwa mnaweza kupata upendeleo wa nafasi fulani nyumbani toka kwa watawala kwa kuwa mna exposure dhana ambayo ni mfu na yenye lengo la kifisadi na interest binafsi wala si za chama chenu wala nchi yenu.

Ingekuwa na maana zaidi kama matawi hayo yangekuwa na agenda ya kuwekeza nyumbani na kuanzisha ajira mpya kwa watanzania walio masikini wasio na ajira nyumbani kwa kutumia nafasi mlizonazo huko ughaibuni ( Na hili halihitaji kuwa na chama cha siasa zaidi ya kuwa na charity au NGO).

Usiniambie kuwa wewe una mapenzi na chama fulani kwa sababu tu unakipenda, huo utakuwa uwongo usio na kipimo kwani malengo ya chama cha siasa si kukusanyana na kula na kunywa bali ni kuchukua dola ya nchi au kuendelea kuongoza.

Mwisho kabisa ni kwamba matawi haya ni matawi ya kisaliti kwa nchi kwani yana hiden agendas za kifisadi za kutwa nafasi za ulaji badala ya kutumia nafasi zenu za kuwa nje ya nchi kusaidia maendeleo nyumbani japo hata kwa kuanzisha vitega uchumi nyumbani na kukuza uchumi.
 
"Chama cha siasa ni mjumuiko wa hiyari wa watu wenye lengo moja ya kutwaa uongozi wa nchi au kuongoza nchi" -Hakuna tofauti kati ya CCM na WANACCM, unaposema chama hakifungui matawi ila wanachama inaonesha ni jinsi gani usivyojua unalolisema zaidi ya ubishi wa kiasa ulioambatana na half knowledge.

Hapa ndugu yangu umedandia hukuwa kwenye picha kamili. CCM kama chama hakiagizi wapi matawi yafunguliwe, isipokuwa wanachama ndiyo wanaoamua wapi tawi lifunguliwe na hii ni kwa mujibu wa taratibu ambazo nimezitaja hapo awali. Fuatilia thread kwa makini kabla hujakurupuka.

Hakuna mantiki wala Sababu zozote za msingi zinazomfanya mkimbizi kufungua Tawi la Chama cha siasa katika nchi ambayo hawezi kuchukua madaraka ya dola zaidi ya kuwa na nia ya ukombozi ukombozi wa nchi yake ambayo anaufanya kwenye nchi rafiki.

Nadhani swali lako litakupa jibu mwenyewe pale utakapo toa tafsiri ya neno 'Mkimbizi'.

Sasa tukirudi Tanzania ni nchi huru ambayo haihitaji ukombozi wowote zaidi ya ufisadi unaoendelea. Kitendo cha kufungua matawi ni ishara tosha kuwa lengo lenu ni kujiweka karibu na watawala(aka kujipendekeza) mkiwa na fikra kuwa mnaweza kupata upendeleo wa nafasi fulani nyumbani toka kwa watawala kwa kuwa mna exposure dhana ambayo ni mfu na yenye lengo la kifisadi na interest binafsi wala si za chama chenu wala nchi yenu.

Maelezo yako hapo juu ni dhana, hayana ukweli na uhakika wa namna yeyote, sina haja ya kuyajadili in any way ni kupoteza wakati.

Ingekuwa na maana zaidi kama matawi hayo yangekuwa na agenda ya kuwekeza nyumbani na kuanzisha ajira mpya kwa watanzania walio masikini wasio na ajira nyumbani kwa kutumia nafasi mlizonazo huko ughaibuni ( Na hili halihitaji kuwa na chama cha siasa zaidi ya kuwa na charity au NGO).

Hayo ni mawazo yako binafsi, lakini kila mtu yuko huru kufanya jambo lile analolipenda ili mradi havunji sheria za mahali husika. Kama unapenda kucheza mpira 'ruksa' kama unapenda kujirusha 'ruksa' na kama unapenda kushiriki siasa hujakatazwa, tafuta namna unayoona itakufaa.

Usiniambie kuwa wewe una mapenzi na chama fulani kwa sababu tu unakipenda, huo utakuwa uwongo usio na kipimo kwani malengo ya chama cha siasa si kukusanyana na kula na kunywa bali ni kuchukua dola ya nchi au kuendelea kuongoza.

Again hii ni dhana isiyokuwa na hata mwelekeo, CCM tayari wanaendesha serikali, hiyo ya kuchukua nchi inatoka wapi? hawa CCM wanajiimarisha. Ninaandika haya kwa makusudi kabisa ili baadhi ya wale wachangiaji ambao hawataki kusikia kwenye masikio yao jambo lolote zuri kwa CCM, wasikie na ikibidi wajifunze yale mazuri toka kwa CCM siasa si uadui. Believe me kuna mengi ya kujifuunza kutoka kwa CCM ili kuimarisha upande wa pili wa upinzani.

Mwisho kabisa ni kwamba matawi haya ni matawi ya kisaliti kwa nchi kwani yana hiden agendas za kifisadi za kutwa nafasi za ulaji badala ya kutumia nafasi zenu za kuwa nje ya nchi kusaidia maendeleo nyumbani japo hata kwa kuanzisha vitega uchumi nyumbani na kukuza uchumi.

Hizi dhana zako zitakufanya usiweze kupambanua mambo kwa uhalisia wake. Waache wanaCCM na chama chao watekeleze yale waliyojipangia kuyatekeleza, waache wazidi kushikamana na kukiimarisha chama chao, lakini maoni yako watayapokea.


Pamoja na maelezo yako marefu yasiyoelewa nini maana ya demokrasia ni kwamba CCM ina wanachama, wakereketwa na wapenzi. Huwezi kuwapangia nini cha kufanya kwa kushiriki siasa ni jambo moja na kujishughulisha na harakati zingine kama kuwekeza nyumbani ni suala jingine ambalo si la kiitikadi. For your information ni kwamba CCM ndiyo wanazidi kujiimarisha wakati wengine wanazidi kupoteza muda wa kulalamika. Wake up!
 
Demokrasi ya Marekani ni kongwe lakini hata 'marafiki' wao wa karibu Wayahudi hatujasikia wakifungua matawi ya vyama vyao vya siasa Marekani. Waingereza pia hawana matawi ya vyama vyao vya siasa katika mji wowote ule wa Marekani lakini CCM wamekuwa wa kwanza kufanya hivyo sijui wanawania nini hasa. Itakuwa ni aibu ya hali ya juu kwa nchi yetu pale ambapo vyombo vya habari vya dunia vitakapotangaza "Watanzania wa vyama viwili tofauti vya siasa wapigana Uingereza au Marekani"

Hii katiba uliyonukuu hapo ni kuhusu ndani ya Tanzania na siyo katika nchi za watu.

Watanzania tuwe wabunifu ili tuweze kuendelea, tutumie fursa zilizopo kujenga nchi yetu na wala si vinginevyo. Kama mataifa mengine unayoyataja hayajafanya hivyo, je unataka kuhalalisha kuwa hiyo ni sababu ya msingi watanzania wasifanye hivyo? Si lazima maamuzi yatakayofanywa na watanzania ni lazima yawe tegemezi au kuiga kutoka kwa wengine.

Ninarudia tena na tena, siasa si uadui, kutofautiana kiitikadi si ugomvi. Ni vema kabisa watanzania popote pale walipo wakashiriki katika shughuli zanchi yao bila ya kujali umbali waliopo kutoka nyumbani. Kuishi nje ya Tanzania haina maana umeondolewa haki zako za kushiriki katika shughuli za kijamii. Kila mtu mmoja mmoja au kikundi waangalie ni kwa namna gani wanaweza kushiriki katika shughuli za kijamii.
 
Last edited:
Pamoja na maelezo yako marefu yasiyoelewa nini maana ya demokrasia ni kwamba CCM ina wanachama, wakereketwa na wapenzi. Huwezi kuwapangia nini cha kufanya kwa kushiriki siasa ni jambo moja na kujishughulisha na harakati zingine kama kuwekeza nyumbani ni suala jingine ambalo si la kiitikadi. For your information ni kwamba CCM ndiyo wanazidi kujiimarisha wakati wengine wanazidi kupoteza muda wa kulalamika. Wake up!

Ukweli utabaki kama ukweli kuwa matawi yenu huko nje ya Tanzania ni gimmick na hayana Maslahi zaidi ya interest binafsi zenu ninyi wenye ndoto za kupenyezwa serikalini kwa upendeleo ambao kwa Tanzania ya sasa hamna mtakachopata zaidi ya kupiga picha na viongozi wanapokuja tembelea ughaibuni na kuziweka kwenye blog for show up basi.
 
Ukweli utabaki kama ukweli kuwa matawi yenu huko nje ya Tanzania ni gimmick na hayana Maslahi zaidi ya interest binafsi zenu ninyi wenye ndoto za kupenyezwa serikalini kwa upendeleo ambao kwa Tanzania ya sasa hamna mtakachopata zaidi ya kupiga picha na viongozi wanapokuja tembelea ughaibuni na kuziweka kwenye blog for show up basi.

Dhana potofu hiyo, as I told you before CCM wanajipanga, kama hutaki kusikia hayo mimi ndiyo furaha yangu kwani ninaelewa kuwa kuna baadhi ya watu hawataki kujifunza kwa kupata ukweli kutoka upande wa pili. Nitaendelea kuchangia hasa yale ambayo wengine hawataki kuyasikia, nina hakika mwisho wa siku ita-sink mu-kichwa na kwenda pamoja.
 
- Jamani jamani mweee mweee mweee, yaani wananchi wa Tanzania, watuwawazima na akili zao timamu, wako majuu wameamua kuanzisha matawi ya CCM, eti hilo nalo ni tatizo la CCM? Wooooi! I am lost!

- Mkuu hivi vyama na matawi vinaanzishwa na mamluki wananchi wenzetu wenye tamaa ya ukubwa na kujikomba kwa viongozi wa juu wanapokwenda kutembelea majuu, mimi enzi zangu za ubaharia sikuona baharia akianzisha tawi la CCM, mind you mabaharia wengi walikuwa na elimu ya kawaida, sasa iweje wasomi tena wa kubobea kujiingiza kwenye haya mambo ya kufungua matawi ya CCM tena Ulaya?

Haya ya kwenda kuanzisha matawi ya CCM ulaya sina uhakika ni nini hasa, lakini one thing I know ni kwamba sio ishu ya CCM kama chama cha siasa!


Mkuu, heshima mbele.

Inaeleweka hapa kuwa hukubaliani na uamuzi wa baadhi ya wana ccm kufungua matawi nje ya Tanzania. Ila sioni kwa nini unataka kuitoa CCM kwenye hili wakati ambapo yana idhini ya Kamati Kuu. Katiba yao inasema wazi kuhusu haya matawi?

Kwa faida ya wana Jf wengine, kifungu kutoka kwenye katiba ya ccm kinasema hizi:-

FUNGU LA II
VIKAO VYA TAWI


31. (1) Kutakuwa na aina nne za Matawi ya CCM
kama ifuatavyo:-

(a) Matawi ambayo yameundwa vijijini ambayo yataitwa Matawi ya Vijijini.

(b) Matawi ambayo yameundwa katika maeneo wanayoishi watu mijini
ambayo yataitwa Matawi ya Mitaani.

(c) Matawi maalum ambayo yameundwa kwenye Ofisi za CCM, Taasisi za CCM,
na Taasisi nyingine zinazoongozwa na CCM.

(d) Matawi ambayo yameundwa nje ya nchi yenye wana-CCM wengi wanaoishi katika sehemu mbalimbali za nchi hiyo na ambao wana Mashina yao. Matawi haya yatafunguliwa kwa idhini ya Kamati Kuu.

(2) Tawi litafunguliwa tu iwapo mahali hapo panapohusika kuna Wanachama
wasiopungua hamsini na wasiozidi mia sita.


Waacheni wana CCM wafanye kama ambavyo katiba ya chama chao inawaruhusu na ili mradi hawavunji sheria za nchi waliyopo.
 
Mkuu, heshima mbele.

Inaeleweka hapa kuwa hukubaliani na uamuzi wa baadhi ya wana ccm kufungua matawi nje ya Tanzania. Ila sioni kwa nini unataka kuitoa CCM kwenye hili wakati ambapo yana idhini ya Kamati Kuu. Katiba yao inasema wazi kuhusu haya matawi?

Kwa faida ya wana Jf wengine, kifungu kutoka kwenye katiba ya ccm kinasema hizi:-

FUNGU LA II
VIKAO VYA TAWI


31. (1) Kutakuwa na aina nne za Matawi ya CCM
kama ifuatavyo:-

(a) Matawi ambayo yameundwa vijijini ambayo yataitwa Matawi ya Vijijini.

(b) Matawi ambayo yameundwa katika maeneo wanayoishi watu mijini
ambayo yataitwa Matawi ya Mitaani.

(c) Matawi maalum ambayo yameundwa kwenye Ofisi za CCM, Taasisi za CCM,
na Taasisi nyingine zinazoongozwa na CCM.

(d) Matawi ambayo yameundwa nje ya nchi yenye wana-CCM wengi wanaoishi katika sehemu mbalimbali za nchi hiyo na ambao wana Mashina yao. Matawi haya yatafunguliwa kwa idhini ya Kamati Kuu.

(2) Tawi litafunguliwa tu iwapo mahali hapo panapohusika kuna Wanachama
wasiopungua hamsini na wasiozidi mia sita.


Waacheni wana CCM wafanye kama ambavyo katiba ya chama chao inawaruhusu na ili mradi hawavunji sheria za nchi waliyopo.

Yebo Yebo,
Ahsante mkuu kwa ufafanuzi
 
Watanzania tuwe wabunifu ili tuweze kuendelea
Pls tell me you're kidding, kuanzisha tawi ni ubunifu? Ubunifu wa kujenga mazingira gani ya kumsaidia Mtanzania masikini? Tawi la chama cha siasa ni kwa lengo la kutwaa madaraka katika sehemu husika [period]. Sasa ubunifu gani unaoongelea wewe? CCM inampango wa kuongoza mji wa London?
...tutumie fursa zilizopo kujenga nchi yetu na wala si vinginevyo.
oooh, so mmeamua kutumia fursa kuwagawa Watanzania kivyama hata nje ya nchi? Hii ndio fursa ya kibunifu unayoongelea? Ubunifu ambao unakupunguzia ushawishi sehemu na mahali ambapo 'political practive' haina tija? Tufikiri mara mbili...
 
Watanzania tuwe wabunifu ili tuweze kuendelea, tutumie fursa zilizopo kujenga nchi yetu na wala si vinginevyo. Kama mataifa mengine unayoyataja hayajafanya hivyo, je unataka kuhalalisha kuwa hiyo ni sababu ya msingi watanzania wasifanye hivyo? Si lazima maamuzi yatakayofanywa na watanzania ni lazima yawe tegemezi au kuiga kutoka kwa wengine.

Ninarudia tena na tena, siasa si uadui, kutofautiana kiitikadi si ugomvi. Ni vema kabisa watanzania popote pale walipo wakashiriki katika shughuli zanchi yao bila ya kujali umbali waliopo kutoka nyumbani. Kuishi nje ya Tanzania haina maana umeondolewa haki zako za kushiriki katika shughuli za kijamii. Kila mtu mmoja mmoja au kikundi waangalie ni kwa namna gani wanaweza kushiriki katika shughuli za kijamii.

Hakuna ubunifu wowote kufungua matawi ya CCM katika nchi za Watu. CCM na serikali haioni umuhimu wa kuruhusu dual citizenship wakati huo huo inataka kufungua matawi yake nchi za nje ambako Watanzania wengine wameshakuwa raia wa nchi hizo, huu ni undumilakuwili!!!! Hatujaona Wacanada au Wamexico ambao wako wengi Marekani kuliko Watanzania kufungua matawi ya vyama vya siasa vya nchi zao ndani ya Marekani. Hatujaona Wamarekani ambao wako wengi Uingereza kuliko Watanzania wakifungua matawi ya vyama vyao (Republicans na Democrats) huko Uingereza.

Watanzania wanaoishi nchi za nje kama wanataka kujiingiza katika mambo ya siasa basi wajiunge na vyama vya huko waliko na siyo kubeba siasa za Tanzania na kuzipeleka huko. Imagine nchi kama Marekani ambayo ina wahamiaji kutoka kila kona ya dunia ikiruhusu wahamiaji wafungue matawi ya vyama vya siasa vya huko wanakutoka, si itakuwa vurugu mechi ya hali ya juu!!!? hivi vyama vyao viwili tu nanga inapaa sasa fikiria na vyama vingine toka kila kona ya dunia.

Na wamarekani kamwe hawatakubali upumbavu huu wa wahamiaji toka nchi nyingine kuruhusiwa kufungua matawi ya vyama vyao vya siasa toka makwao. Jibu lao litakuwa kwamba kama unataka kuishi Marekani na kujishughulisha na siasa basi chagua vyama kimoja kati ya vyama vyao na siyo kuleta vyama toka utokako vinginevyo rudi kwenu ukajishughulishe na siasa za kwenu. Haya matawi hayana muda mrefu wenye nchi zao wakigundua tu basi watayashushia nyundo mara moja.
 
Pls tell me you're kidding, kuanzisha tawi ni ubunifu? Ubunifu wa kujenga mazingira gani ya kumsaidia Mtanzania masikini? Tawi la chama cha siasa ni kwa lengo la kutwaa madaraka katika sehemu husika [period]. Sasa ubunifu gani unaoongelea wewe? CCM inampango wa kuongoza mji wa London?

oooh, so mmeamua kutumia fursa kuwagawa Watanzania kivyama hata nje ya nchi? Hii ndio fursa ya kibunifu unayoongelea? Ubunifu ambao unakupunguzia ushawishi sehemu na mahali ambapo 'political practive' haina tija? Tufikiri mara mbili...


Niliposema kuwa...Watanzania tuwe wabunifu ili tuweze kuendelea......tutumie fursa zilizopo kujenga nchi yetu na wala si vinginevyo...ni ushauri, kama unaona kuwa hatutakiwi kuwa wabunifu, basi hayo ni mawazo yako, nitayaheshimu nikielewa kuwa umeyatoa ukiwa na akili timamu.

Watanzania wataendelea kubaki kuwa watanzania wakati wote, wakiwa na dini zao tofauti, wakiwa na makabila yao tofauti, wakiwa na misimamo yao tofauti ya kiitikadi nk. Ni vema watanzania wakaonekana hivyo kulikoni kujifanya wanafiki kwa kusema kuwa hatutofautiani ilihali si kweli. Umoja wetu unajengwa kwa kuzingatia utaifa wetu na wala si Imani za kidi, ukabila, itikadi za kisiasa nk.
 
Unless you stop personalizing the unconsciousness and generalizing that comes from myths and glorification without sacredness an purity, you will get to understand the CCMs and their their used praises.
"FUTURE BELONGS TO THOSE WHO BELIEVE IN THEIR DREAMS"Eleanor Roosevelt.
 
Nina sikia kuwa wanaofungua matawi hayo wengi wao ni wale wasio kwenda shule, siamini kama uko unahenya na PHD yako au Masters yako unao muda huo wa kufanya hivyo.
Mantiki ya kufungua matawi ya vyama vya siasa nje ya nchi ni ipi?,nadhani hili tuliachie opportunists.
Nchini uingereza nasikia pia kuwa majority ya wanachama wa vyama vya kisiasa huko ni watu waliojiunguza(waliokana utanzania/wakimbizi wa kiuchumi).Sasa watu wajinsi hiyo ni wakuamini kweli?.
Tusubiri tuone mwisho wake.Ushauri wangu kwa wale wanaopiga kitabu kipigeni sana siku moja kitalipa(siku zina fanana lakini hazilingani).
 
Kwanza huyo anayekwenda kufungua hayo matawi na wanaokwenda kwenye sherehe za ufunguzi wa matawi ya ughaibuni ni watu wasio na shughuli za kufanya. Mimi sielewi inakuaje mtu unakwenda kusikiliza porojo za ccm ambazo ni hizo hizo tangu 1977.
 
Back
Top Bottom