Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Nina sikia kuwa wanaofungua matawi hayo wengi wao ni wale wasio kwenda shule, siamini kama uko unahenya na PHD yako au Masters yako unao muda huo wa kufanya hivyo.
Mantiki ya kufungua matawi ya vyama vya siasa nje ya nchi ni ipi?,nadhani hili tuliachie opportunists.
Nchini uingereza nasikia pia kuwa majority ya wanachama wa vyama vya kisiasa huko ni watu waliojiunguza(waliokana utanzania/wakimbizi wa kiuchumi).Sasa watu wajinsi hiyo ni wakuamini kweli?.
Tusubiri tuone mwisho wake.Ushauri wangu kwa wale wanaopiga kitabu kipigeni sana siku moja kitalipa(siku zina fanana lakini hazilingani).

Unasikia tu, huna uhakika na hata unachokiandika hapa. Hebu basi kama unaelewa maana ya usomi fanya utafiti, then uje na facts. vinginevyo mchango wako bado unaonekana kuwa hauna hoja yeyote.
 
Kwanza huyo anayekwenda kufungua hayo matawi na wanaokwenda kwenye sherehe za ufunguzi wa matawi ya ughaibuni ni watu wasio na shughuli za kufanya. Mimi sielewi inakuaje mtu unakwenda kusikiliza porojo za ccm ambazo ni hizo hizo tangu 1977.

Ni kujipanga na kupangilia mambo yako. kila jambo linawezekana ikiwa tu una nia na unapangilia mambo yako vizuri
 
Kwanza huyo anayekwenda kufungua hayo matawi na wanaokwenda kwenye sherehe za ufunguzi wa matawi ya ughaibuni ni watu wasio na shughuli za kufanya. Mimi sielewi inakuaje mtu unakwenda kusikiliza porojo za ccm ambazo ni hizo hizo tangu 1977.


Kazi bado tunayo...hawa wanasoma, wanafanya kazi ama wamejilipua?

IMG_1067.JPG



Susan Mzee katibu wa ccm Tawi kuu la london akikabidhi wa kwa viongozi wa shina picha Ya mwenyekiti wa CCM (Michuzi Blog)
 
i am not a fan of matawi but i guess its good to attend to pass time..im sure after the photos kulikuwa na drinks nakadhalika and meeting new people...nothing more to it.
 
i am not a fan of matawi but i guess its good to attend to pass time..im sure after the photos kulikuwa na drinks nakadhalika and meeting new people...nothing more to it.

Mkuu why don't you go to pubs....to meet new people and ad lib drinks.....jamaa hawana lolote wamelost wanatafuta mataulo...
 
matawi yatatapakaa dunia nzima kuanzia Uk, Dc, Kansas na Houston.
Uk yanongozwa na Maaja na mumewe kumuenzi Jk na vibaraka wengine wasiojua kwanini wapo ulaya.
DC wanasubiria kunasa misafara ya mkulu.
Kansas Deo anahangaika na maisha.
Houston Yupo mtoto wa ndugu yake mzee Ndejembi.Haya matawi hayana chochote zaidi ya watoto wa CCM B kujitangaza.
 
.........Siku hizi naona matawi mengi ya CCM yanafunguliwa huko ughaibuni, lakini mwenzenu sielewi malengo yake haswa ni nini? Je kama taifa linapata faida gani kutokana na hayo matawi ya chama cha siasa nje ya nchi?

Mwenzenu najiuliza hivi kwa sababu sijajua bado kama nchi nyingine hapa duniani nao wana utaratibu wa kufungua matawi ya vyama vyao tawala nje ya nchi zao?

Hapa Tanzania wapo raia wa nchi mbali mbali wanaishi hapa, lakini sijasikia kama wamefungua matawi ya vyama vyao vya siasa hapa nchini.

Lengo haswa ni nini hadi CCM inafungua matawi huko ughaibuni?Mie huwa najiuliza sababu ya ufunguzi wa hayo matawi sipati jibu...........hivyo nimeamua kuleta hapa labda nitapata majibu.
 
teh tehe,teh, te.. tee..eeeh!!
wana hela hao,kwani hukumsikia msekwa alivyosema - wao wana mbinu za kushinda.
pretty,usichoke ndo nchi yako hii kila siku hawa jamaa wanawaza jambo jipya ila kuwachimba bit wanasiasa wenzao wenye hela kidogo - ila ipo washa washa litapita miilini mwao ndipo watakapolia na kuiacha nchi safi na yenye afya.
 
hiyo ni made in Tanzania only...
yote yanayotokea Tanzania ,mengi ni made in TZ only..
huyaoni nchi zingine....
 
hiyo ni made in Tanzania only...
yote yanayotokea Tanzania ,mengi ni made in TZ only..
huyaoni nchi zingine....

.........Kumbe ni Tanzania tu ndio wanaojua siasa ya kufungua matawi ya chama hadi nchi za watu, ndio maana nataka kujua nia yao haswa ni nini?
 
.........Kumbe ni Tanzania tu ndio wanaojua siasa ya kufungua matawi ya chama hadi nchi za watu, ndio maana nataka kujua nia yao haswa ni nini?

We unashangaa hayo...
sisi ndo nchi pekee duniani,waziri
anaacha shughuli zake halafu eti
anakwenda kwenye sherehe ya kumpa
bendera mrembo wa miss takataka n.k....

yapo mengi ,nikiyaorodhesha hapa utachoka...
 
teh tehe,teh, te.. tee..eeeh!!
wana hela hao,kwani hukumsikia msekwa alivyosema - wao wana mbinu za kushinda.
pretty,usichoke ndo nchi yako hii kila siku hawa jamaa wanawaza jambo jipya ila kuwachimba bit wanasiasa wenzao wenye hela kidogo - ila ipo washa washa litapita miilini mwao ndipo watakapolia na kuiacha nchi safi na yenye afya.

.........Hizo pesa si wanazipata kwa watoa kodi au? Mangapi tunashindwa kufanya hapa kwetu halafu wakatumie pesa za walipa kodi kwa kufungua matawi yasio na umuhimu wowote huko ughaibuni?
 
Lengo haswa ni nini hadi CCM inafungua matawi huko ughaibuni?Mie huwa najiuliza sababu ya ufunguzi wa hayo matawi sipati jibu...........hivyo nimeamua kuleta hapa labda nitapata majibu.

Pretty.. kwanza nadhani kuna majibu ya kisiasa na majibu ya kimkakati. La kisiasa ni kuwa CCM inafanya hivyo kwa sababu inaweza na kwa sababu Chama kinajijenga zaidi. Kwa upande wa mkakati ni kuwa kwa mtu yeyote ambaye anataka kufanikiwa huko mbeleni (kisiasa, kiuchumi na vinginevyo) ni muhimu kuchagua upande unaoshinda.

Wakati mwingine nafikiria hata yawezekana ni bora kurudisha chama kimoja tu ili kila mtu awe anaingia kwenye chama halafu tukijaza fomu za kuomba kazi, n.k tujaze kuwa "tulipitia UVCCM" au tumewahi kuwa viongozi wa chama mahali fulani. It comes na ujiko fulani.

Lakini upande mwingine inawezekana kabisa wananchi hawa wanamapenzi ya kweli ya CCM na wameshindwa kujizuia kutoyaonesha mapenzi hayo na wameamua kufanya hivyo. Kama hili ni kweli basi ni matatizo ya upinzani kutojitahidi kupata wanachama hadi nje ya nchi au matatizo ya mashabiki wa vyama vya upinzani na wenyewe kutojiunganisha na kuanzisha matawi yao huko waliko.

Tatizo litakuja pale ambapo vyama vya upinnzani navyo vitaanza kuanzisha amtawi kama hapo London n.k na matokeo yakawa ni mgawanyiko wa Watanzania. Ndio maana sisi wengine huku US tuko sensitive kweli na mambo haya ya kuanzisha matawi ya vyama hapa.
 
hiyo ni made in Tanzania only...
yote yanayotokea Tanzania ,mengi ni made in TZ only..
huyaoni nchi zingine....

Japo naafikiana nawe kuwa kuna mengi yanapatikana au kutengenezwa Tanzania pekee,hili la vyama vya siasa kidogo naomba kufanya marekebisho kidogo.Kwa hapa UK,kuna organisations mbili za Wamarekani: Democrats Abroad UK (Democrats Abroad is the overseas branch of the U.S. Democratic Party,kwa mujibu wa tovuti yao) na Republicans Abroad (mobilizes the support of Americans overseas to support Republican candidates in US elections,according to tovuti yao).

Baada ya ufafanuzi huo,naomba kutamka bayana kuwa kwa mtizamo wangu ufunguzi wa matawi ya CCM huku nje unasukumwa zaidi na kujikomba,ndoto za madaraka,njaa plus frustrations za kusaka/kukosa makaratasi.
 
CCM wanataka kujenga siasa za Monopoly kila mahali walipo waTanzania.
 
kwa haraka haraka ngoja nijibu hoja:
Wengi wanaojiunga na mavyama haya ooopss ccm .......wengi wao box limeshawashinda I mean maisha huku yamewapindia sasa pa kukimbilia ni huko kwenye chama....Mtu na akili yako timamu ujiunge na haya mavyama ughaibuni ili upate nini??????wanatafuta pa kuegama wafanye ufisadi huku ughaibuni.
Wajanja wote huwakuti kwenye huu upuuzi wa politiki or sijui diaspora...maana huko ujinga miiingi hamna jipya.
 
Hata walioko Italy wamefungua !Lakini kama kuna mtu anajua mambo ya Italy,especially ya immigrant wa kiafrika walioko huko,tuliotembea tunajua .
CCM itakuja kuadhirika na watu hawa ,wengi wana history mbaya.
 
Mimi kwa maoni yangu ni kujibaraguza tu wanakuja na idea ya Watanzania waaanzishe association zao kitu ambacho mimi nakiafiki kabisa halafu association ikishasimama wanakuja na idea ya kuunda matawi ya chama. Sehemu nyingi wameligomea hili la kufungua matawi ya CCM kama ilivyo katika baadhi ya nchi za Europe. Matawi haya badala ya kusaidia kuwaunganisha Watanzania mara nyingi yanakuwa yanawatenga maana wengi hawaprndi CCM kutokana na utendaji wake mbovu kama chama twawala.
 
Ni njia mojawapo mbadala ya kuweza kupata keki na kufanya ufisadi kirahisi mara warudipo nyumbani kwao.
 
Back
Top Bottom