Mtanzania
Sio kama nakutusi kwa hayo maneno niliweka ili nieleweke vizuri sasa wewe unamoja na unalalamika, ijapokuwa umekubali sasa more deposit unayoweka low monthly repayment itakavyokuwa sasa wewe hutaki kweli kuwa na hiyo investment property na kuepuka na hayo mabox
Si unajua mabox yanaababisha mtindio wa ubongo
wewe hiyo moja tuu unalalamika sasa mwenzio analipa tatu au zaidi na bado anaisaidia CCM na mwaka jana alidhamini Umoja Cup na timu ya mpira ya Reading walishinda hilo kombe
Mkora,
Unakoenda ni nje ya mada. Mimi nilikuwa naelezea tu kwamba kuwa na nyumba tatu haina maana mtu ni tajiri. Kama ana utajiri mwingine sawa, wala mimi
huyo mtu simfahamu kwahiyo suala la tajiri au sio tajiri hapa halikuwa muhimu. Rudia tena ujumbe wangu wa mwanzo.
Kama ni kujadili juu ya investment ipi inafaa, hapo ni topic nyingine na
bahati nzuri ujuzi wangu mwingine ni juu ya mambo kama hayo.
Kuna watu wengi tu wana investments mbalimbali na pia wana suppot projects mbalimbali hasa TZ. Wengi wao ni wabeba mabox kama sisi wengine hapa na bado
bongo zao zinafanya kazi vizuri kabisa. Hakuna haja ya kutangaza hapa mtu
anamiliki nini na anasaidia nini, maana kutoa ni moyo na wala sio utajiri. Pia hakuna haja ya kudharau kazi ya mtu. Ni bora kuwa mbeba box kuliko kuiba pesa za watu maskini. Au kuliko kushiriki kwenye ufisadi ili tu upate pesa za haraka. Hakuna haja kabisa ya kujisikia vibaya kuwa mbeba box, ni kazi halali.
Wala hata mimi sijalalamika kuhusu nyumba ninayokaa na badala yake nimekuambia ukweli kwamba nilipata mkopo asilimia 100. Ningetaka mbwembwe
ningesema nilitoa deposit asilimia 20. Ukweli kwa anayejua maisha ya UK, wengi hata kwa walio na nyumba zaidi ya moja, wanatumia hiyo hiyo kati ya 90% na 100% loans.
UK inaendeshwa na mikopo, huwezi kuamini. Hata watu wanaotanua, ukienda ndani utakuta mikopo imetumika. Tanzania tunakwama kwasababu ili ufanye kitu chochote lazima uwe na pesa, uwe tajiri, wakati huku majuu wala sio lazima kabisa.
Baadhi ya Watanzania vijana ukikutana nao, wanafikiri ni tajiri. lakini mimi huwa sioni aibu kuwaambia ukweli kwamba hapa system ndio tajiri na ndio maana hata raia wao wanatanua. Ukienda kwa mtu mmoja mmoja, ni madeni matupu.