Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Tawi la India nadhani ni kampeni za Nape katika kuja kukamata madaraka ya UVCCM

Mie sioni kosa kwa watu kujiunga na CCM ila suala la kuwa na matawi huko nje ni njia ya ulaji tu!

tuipige vita tabia hii
 
Wakuu,heshima kwenu.......
Maneno mengi hapa kama vile twajifurahisha tu, mtu mmoja aliwahi kusema...hasira hata iwe kali vipi,haiwezi kuivisha chakula...maneno haya hata kama makali vipi hayawezi kuwazuiya CCM kufungua matawi nje..na ukiona asiyekutaka analalamika kwa wewe kufanya jambo ujue hilo jema kwako na umemshika pabaya mbaya wako....KWANINI KUANDIKIA MATE NA WINO UPO?BEN NA WENZAKO FUNGUENI MATAWI INDIA HATA CHINI YA MWAMVULI WA MUUNGANIKO WA VYAMA VITANO MNAVYOSHIRIKIANA..NA WENGINE KOTE WALIPO KAMA MNAWEZA FUNGUENI MTOE SERA MBADALA BADALA YA KULALAMIKA TU HAPA JF...
Wacha ninywe maji,ntaleta stori ya mbweha wa tano waliofungwa mikia yao pamoja ukawashwa moto mikiani wakaambiwa kimbieni.....mhhhhhhhhhhhhhhh!!!!!!!!
 
Tawi la India nadhani ni kampeni za Nape katika kuja kukamata madaraka ya UVCCM

Mie sioni kosa kwa watu kujiunga na CCM ila suala la kuwa na matawi huko nje ni njia ya ulaji tu!

tuipige vita tabia hii

Ndugu yangu Gembe na wengine wote wanaodai ni ULAJI hebu tuelezeni kwa uwazi na mifano ulaji gani huu/huo???
Swala la Nape kwamba wadai ni kampeni kutaka UVCCM,nani kati ya walio India ni mpiga kura kwenye mkutano wa UVCCM na je wengine nchi zingine wanataka UV gani?? Tujenge hoja sio vioja...
 
Naona ni kweli mwafrika wa kike hawa watu wanataka tusikilize Radio Uhuru na RTD pekee watupe propaganda zao. Bora hizi radio zetu uchwara lakini zinawafikia wengi katika nchi mbalimbali duniani kwa sababu tunajaribu kwenda sambamba na maendeleo ya teknolojia kuliko wao hata tovuti ya Ikulu inawshinda kutengeneza.

Mazee Geeque,

Hatimaye umesikia kilio changu na kuweka bolingo .... GOOD job!

Bongo radio ... the best radio on the web! radio uhuru walie tu!

Visit www.bongoradio.com

Thanks!
 



Sio kila mtu anaweza kuja hapa forum, Tanzanet na kwingineko kutoa michango.

Wao ni wanasiasa, majukwaa yao sio humu ni kule mitaani na majukwaani kuomba kura na kuahidi maendeleo kwa kila Mtanzania.

Nashindwa kuelewa mkuu kwa nini hutaki kuthamini na kuheshimu fani za watu wengine?

Yebo Yebo,

Unataka niamini utapeli na misheni mjini? Utajipima uongozi kwa wanachama 20? Si afadhali hata Tanzanet au TA vyombo ambavyo japo vina wanachama wengi?

Nimekaa Nje miaka mingi na Watanzania tulikuwa tunaongoza kwa mshikamano
lakini sasa yanaanza mambo ya vyama, tutaishia kuwa kama Wakenya tu. Huyu CCM, yule CUF nk.

Hakuna anayemkataza mtu kuwa mwanachama wa chama lakini kuanza kufungua matawi nje ni ulaji tu ambao kwa mtu yeyote mwenye lengo la kusaidia jamii hawezi kuhangaika nayo.
 
Ndugu yangu Gembe na wengine wote wanaodai ni ULAJI hebu tuelezeni kwa uwazi na mifano ulaji gani huu/huo???
Swala la Nape kwamba wadai ni kampeni kutaka UVCCM,nani kati ya walio India ni mpiga kura kwenye mkutano wa UVCCM na je wengine nchi zingine wanataka UV gani?? Tujenge hoja sio vioja...

Kama huelewi, wenzako wanachotengeneza ni CV. Ni sawa na wale wenye Ph.D fake. Hata wao wanajua ni fake ila wanachotaka ni hiyo Dr. kwenye CV.

Ukiandika ulikuwa Mwenyekiti wa CCM London, kwa mtu wa kule Musoma anaweza kuamini wewe ni mkali kweli kweli, kumbe hakuna kitu na ulikuwa na wanachama 10.

Soma CV ya Nape wakati anagombea UVCCM labda ndio utaelewa maana yake.
 
Wakuu,heshima kwenu.......
Maneno mengi hapa kama vile twajifurahisha tu, mtu mmoja aliwahi kusema...hasira hata iwe kali vipi,haiwezi kuivisha chakula...maneno haya hata kama makali vipi hayawezi kuwazuiya CCM kufungua matawi nje..na ukiona asiyekutaka analalamika kwa wewe kufanya jambo ujue hilo jema kwako na umemshika pabaya mbaya wako....KWANINI KUANDIKIA MATE NA WINO UPO?BEN NA WENZAKO FUNGUENI MATAWI INDIA HATA CHINI YA MWAMVULI WA MUUNGANIKO WA VYAMA VITANO MNAVYOSHIRIKIANA..NA WENGINE KOTE WALIPO KAMA MNAWEZA FUNGUENI MTOE SERA MBADALA BADALA YA KULALAMIKA TU HAPA JF...
Wacha ninywe maji,ntaleta stori ya mbweha wa tano waliofungwa mikia yao pamoja ukawashwa moto mikiani wakaambiwa kimbieni.....mhhhhhhhhhhhhhhh!!!!!!!!

Watu tunalalamika kuhusu ufisadi kwahiyo UFISADI NI JAMBO JEMA KWA MAFISADI?

Labda ni kweli na ndio maana wengine nao wanakimbilia huko ili waendelee kutuibia.
 
Yebo Yebo,

Unataka niamini utapeli na misheni mjini? Utajipima uongozi kwa wanachama 20? Si afadhali hata Tanzanet au TA vyombo ambavyo japo vina wanachama wengi?

Nimekaa Nje miaka mingi na Watanzania tulikuwa tunaongoza kwa mshikamano lakini sasa yanaanza mambo ya vyama, tutaishia kuwa kama Wakenya tu. Huyu CCM, yule CUF nk.

Hakuna anayemkataza mtu kuwa mwanachama wa chama lakini kuanza kufungua matawi nje ni ulaji tu ambao kwa mtu yeyote mwenye lengo la kusaidia jamii hawezi kuhangaika nayo.


Kama sio kulegalega kwa hiyo TA pengine leo kusingekuwa na CCM London....

Sitaki kukushawishi; ila naona unahitaji kuhudhuria hiyo mikutano ya CCM London ujionee mwenyewe idadi ya wanachama walionao. Sina la zaidi mkuu
 



Kama sio kulegalega kwa hiyo TA pengine leo kusingekuwa na CCM London....

Sitaki kukushawishi; ila naona unahitaji kuhudhuria hiyo mikutano ya CCM London ujionee mwenyewe idadi ya wanachama walionao. Sina la zaidi mkuu

Siku nikitaka nitajiunga na CCM lakini sio Ulaya. Hata siku moja hutaniona kwenye hiyo mikutano ya CCM.

Wengi wa hao wanachama wa CCM, hawakuhudhuria mikutano ya TA, lakini wakahudhuria mkutano wa CCM na JK.
 
Mtanzania, hapa umeonesha jambo moja muhimu sana hasa kwa Watanzania walioko Ughaibuni; je Ibara ile ya 15 inafanya kazi hata huku kwamba CCM inakuwa juu ya jumuiya ya Watanzania wote na jambo lolote litakalohatarisha maslahi ya wana CCM hata kama linaweza kunufaisha Watanzania wote laweza kupingwa na wana CCM ili kukilinda chama chao.

Itakuwaje kama wana CCM wanakuwa ni wengi zaidi (kitu ambacho siwezi kushangaa) na wanakuwa very loyal to their party na wale ambao sio wana CCM wanajikuta ni minority?

Inakuwaje basi unapotokea mkutano wa Watanzania ambao watu wakija over 2/3 ni wana CCM pia?

Hapa umezua maswali ya msingi...
 
Yebo Yebo,

Unataka niamini utapeli na misheni mjini? Utajipima uongozi kwa wanachama 20? Si afadhali hata Tanzanet au TA vyombo ambavyo japo vina wanachama wengi?

Nimekaa Nje miaka mingi na Watanzania tulikuwa tunaongoza kwa mshikamano
lakini sasa yanaanza mambo ya vyama, tutaishia kuwa kama Wakenya tu. Huyu CCM, yule CUF nk.

Hakuna anayemkataza mtu kuwa mwanachama wa chama lakini kuanza kufungua matawi nje ni ulaji tu ambao kwa mtu yeyote mwenye lengo la kusaidia jamii hawezi kuhangaika nayo.

Kwa maneno haya nakubaliana nawe kabisa .CCM kuweka matawi nje and then the same people wanakuwa viongozi wa Umoja wa Watanzania na vingozi wa CCM inaleta mgawanyiko na tunakuwa Taifa la watu walio changanyikiwa .JK anaenda London watu wanamuona anaenda ki CCM na watanzania wengine wanakaa mbali .Balozi anapo amua kufanya kazi za CCM openly sijui anataka wasio na vyama waende wapi .Mwalimu angaliyafanya haya Tanzania leo tusingalikuwa hapa JF kwa umoja huu , bali tungalikuwa kama Kenya .CCM wanatugawa nasi tuna shangilia jamani amkeni .Ukiwa kiongozi wa CCM basi jiondoe uongozi kwenye umoja wa Watanzania .
 
Kwa maneno haya nakubaliana nawe kabisa .CCM kuweka matawi nje and then the same people wanakuwa viongozi wa Umoja wa Watanzania na vingozi wa CCM inaleta mgawanyiko na tunakuwa Taifa la watu walio changanyikiwa .JK anaenda London watu wanamuona anaenda ki CCM na watanzania wengine wanakaa mbali .Balozi anapo amua kufanya kazi za CCM openly sijui anataka wasio na vyama waende wapi .Mwalimu angaliyafanya haya Tanzania leo tusingalikuwa hapa JF kwa umoja huu , bali tungalikuwa kama Kenya .CCM wanatugawa nasi tuna shangilia jamani amkeni .Ukiwa kiongozi wa CCM basi jiondoe uongozi kwenye umoja wa Watanzania .

Amen...Hapa ndo tatizo lilipo!!
 
Yebo Yebo,

Unataka niamini utapeli na misheni mjini? Utajipima uongozi kwa wanachama 20? Si afadhali hata Tanzanet au TA vyombo ambavyo japo vina wanachama wengi?

Nimekaa Nje miaka mingi na Watanzania tulikuwa tunaongoza kwa mshikamano
lakini sasa yanaanza mambo ya vyama, tutaishia kuwa kama Wakenya tu. Huyu CCM, yule CUF nk.

Hakuna anayemkataza mtu kuwa mwanachama wa chama lakini kuanza kufungua matawi nje ni ulaji tu ambao kwa mtu yeyote mwenye lengo la kusaidia jamii hawezi kuhangaika nayo.
Hili ndio nimekuwa nalisema wakati wote kuhusiana na hawa wapambe wa CCM wanapoamua kuendelea kuanzisha haya mashina yao.Inajulikana kabisa ni haki yao kuwa wanachama wa chama chochote na hakuna anayepinga kuhusiana na hili lakini suala linalogomba hapa ni Judgement na nia yao ya kuanzisha haya matawi. Ina maana hawa watu hawaelewi uchafu wote unaofanywa na CCM mpaka wao kuamua kuvutiwa na kuzidi kufungua matawi huku ughaibuni. Sijawasikia hata siku moja wakitoa matamko ya kulaani ufisadi unaofanywa na wananchama wenzao kwa sababu siku zote kazi yao kubwa ni kukenua midomo na kupiga vigelegele na kushangilia kidumu chama cha Majambazi bila ya kuhoji muelekeo wa chama au matendo ya viongozi wengi wa juu wa CCM. Unajua wengi tunategemea watu ambao wameenda shule na kupata exposure wawe hawaangalii au kufanya maamuzi ya juu juu bila ya kutafakari kwa kina.
 


Je haya matawi yanayofunguliwa ughaibuni yana malengo gani? Ni jinsi gani wanachama wake wanaweza kushiriki katika siasa nyumbani?.

Mkuu,

Malengo ya kuanzishwa kwa matawi haya mpaka sasa hayajulikani ingawa unaweza kuhisi kwamba labda ni namna ya kutaka kuwadhibiti watanzania walio nje au kuwapa nafasi ya wale wenye nia , kuingia katika mfumo wa "vicious circles" ambazo kwa sasa zimetapakaa hadi ughaibuni.

Kwangu mimi naona wazo la kuanzishwa kwa matawi haya kumelenga mtazamo wa kisiasa wa Marekani ambapo ukiangalia vizuri utaona chama cha siasa cha Democrat kina wanachama waishio nje ya Marekani wapatao 20,000 na walimpa kura Barack Obama asilimia 65 na asilimia 72 kwa wale wa Asia-Pasific. Kwa uelewa zaidi tembelea website ya "Democrats Abroad"

Kwa hio wazo hili sio baya ingawa inaonekana CCM imewahi na kwa sasa wapo mbali. Vyama vingine kama Chadema na CUF nao wana uwezo wa kufanya hivi bila matatizo yoyote ingawa inabidi ijulikane rasmi katika nchi husika kama Uingereza.

Lakini pia mimi napinga kuanzishwa wakati huu tena kwa kasi ya ajabu na itabidi wale wote waliomo humo wahojiwe na wapiga kura wajinga waliko vijijini Tanzania ambao huweza kudanganywa kwa mipira kutoka Ulaya na suala zima la takrima kutoka Ughaibuni.

Unajua kuna watu wameishi muda mrefu nje ya Tanzania kama nchini Uingereza na wasifanye kitu chichote cha maana kule nyumbani lakini wameona ni kheri wajibanze ndani ya CCM na huu ni ujinga wa hali ya juu.



Kwa maoni yangu naona kwamba kuanza kuwepo kwa matawi ya vyama vya kisiasa ughaibuni kutaanza kuleta mgawanyiko kwa Watanzania waishio huku. Hata siku moja sijawahi kusikia au kuona kama kuna matawi ya Republicams, Democrats, Labour, Conservatives, CDU au Forza Italia katika nchi zingine! Au huu ni mtindo mpya wa siasa za kimataifa ambao unahamishia siasa za ndani ya nchi, kwenda nchi zingine? Ikumbukwe kuwa, nauliza tu.

Hapa mkuu sidhani kama kutakuwa na mgawanyiko wowote ule ikiwa wewe utaendelea kuwa "neutral" kama mimi na masuala haya na kuangalia wengine wakishiriki kudanganyana na kuhujumu nchi kwa mgongo wa wapiga kura.

Kama wewe ni sawa na mimi tuna kazi zetu na tunajua tuna majukumu gani, kifamilia na kijamii basi itakuwa ni budi kusaidia jamii nyumbani kwa njia mbalimbali bila kuhitaji "publicity" na unaweza kulaza hata bomba za maji pale Kisiju Pwani na watu wakakushukuru ingawa mbunge wa pale atawaza unamezea mate nafasi yake.

Kuhusu vyama vya siasa ulivyovitaja ni kwa mfumo wa Marekani ndio wanafanya hivyo kama nilivyoeleza hapo juu ingawa wao wanajumuisha wamarekani wote waishio nje katika nchi tofauti kwa ujumla bila kuwa na matawi mengine ndani ya nchi hizo kama wafanyavyo CCM.

Na hili la siasa za kimataifa. Tanzania haiwezi na haijawahi kuhamisha siasa zake za kudanganya watu nje ya mipaka yake isipokuwa "slogan" yake ya kwamba Amani na Utulivu, huku watu wakihujumu nchi ndio inaonekana ina nguvu.

Mwisho, ni kuhusu baadhi ya wale waliomo humo CCM. Wengi wao ni wale ambao kwa miaka nenda rudi wamekuwa wakisika kukosoa mambo mengi yanayorudisha nyuma maendeleo ya nchi yetu. Sasa hii labda itakuwa ni nafasi kwa kuhakikisha wanatekeleza kile kitu mabadiliko ambayo wanataka yawepo nchini Tanzania.
 
Lunyungu,

Unalolisema "nadhani" ndilo lililokuwa nia ya wajanja wachache wakati Tawi la London linaanzishwa lakini; ila kwa sasa ninavyojua mimi hakuna mfanyabiashara anayefadhili chama tawi la London kwa hela nyingi kuliko wanachama. Nimedadisi kwa karibu nikagundua kuwa asilimia kubwa Tawi linaendeshwa na wanachama wa kawaida kama mimi na wewe..sasa hawa ndugu zetu wana nia gani; time will tell.




Mkuu Heshima yako,

Unatoa tuhuma hewani bila kujua kuwa huku tupo ughaibuni. Hapa una hoja unauliza kama ilivyo. Unaposema rent ya ofisi ya Shina North London inalipwa na chama; una ushahidi wowote? Maneno yako sio tu kwamba yanalenga kuleta mfarakano kati ya mwenye Cafe na Viongozi wa shina bali pia inaonyesha ni jinsi gani usivyotaka kupata data za uhakika. Hiyo ofisi sana sana itwakuwa inatumiwa kwa sababu mwenye Cafe amejitolea itumiwe na Chama. Kama nilivyosema hapo awali chama (UK) kinaendeshwa na wanachama, mwenye senti za kutoa anatoa, mwenye petroli za kwenda kufungua mashina anatoa, mwenye printer ya rangi ya kuprint nyaraka za chama anatoa n.k

Hakuna mjomba anayefadhili chama kama ambavyo mnataka wanabodi hapa waamini; na iwapo atatokea na kuonekana ana malengo yake binafsi basi mimi kama mwanabodi hapa nitakuwa na wajibu wa kuwaambieni ukweli; kwa sasa fungueni akili wekeni maswali na hoja zenye mashiko za kwa nini haya matawi yawepo huku ughaibuni.

Jamani tusidanganyane hapa. Tumeona ya RA na JK na pesa chafu za kampeni. Hivi huyu mwenye CAFE ni tajiri sana kuweza kulipia jengo la ofisi ya CCM UK? Je, analipa kodi yake bila ubadhirifu? Maana hapa tunayo SOCA kama haya mambo ni kweli itabidi tuwaeleze wenyewe wayachunguze isije ikawa pesa ya walipa kodi wa UK ndio inafadhili UFISADI wa CCM kwa kutumia mgongo wa WTZ au vice versa.

Kwa maisha ya UK na wengi wa WTZ ambao ni wanafunzi au wabeba mabox watakuwa very lucky kupata £20 kwa saa, Je kama wanapata chini ya hapo hiyo pesa nyingine inatoka wapi? Je, hii sio pesa ya walipa kodi wa Tanzania ambayo inachezewa?

Yebo2 hebu tupe ufafanuzi mkuu.
 
Mwenye CAFE Anajiweza kama sikosei hadi mwaka 2003 alikuwa na nyumba tatu UK
Moja ipo karibu sana na uwanja wa manchester city
Ila ni bahili sana
 
Kama huelewi, wenzako wanachotengeneza ni CV. Ni sawa na wale wenye Ph.D fake. Hata wao wanajua ni fake ila wanachotaka ni hiyo Dr. kwenye CV.

Ukiandika ulikuwa Mwenyekiti wa CCM London, kwa mtu wa kule Musoma anaweza kuamini wewe ni mkali kweli kweli, kumbe hakuna kitu na ulikuwa na wanachama 10.

Soma CV ya Nape wakati anagombea UVCCM labda ndio utaelewa maana yake.
Mkuu hebu niambie kosa lao hasa nini? kama nikutengeneza cv kwa njia halali za kufanya kazi ya chama chao na ikaonekana na kutambuliwa kosa lao nini???Nikama mtu anasoma apate labda degree ili agombee urais kama ndio kigezo kilichowekwa kosa lake nini hasa??Kama kuna mtu anadhani hana sifa ni bora kwenda kushindana kwa wananchi kuwaeleza kwamba huyu hatoshi badala ya kumsema anapojitafutia cv yake.
Idadi hapa siyo hoja,kimsingi mi ningedhani 'quality' ndo hoja hapa.Maana ni ukweli kuwa kuongoza watu 50 wasio na elimu huwezi linganisha na hata 10 waliosoma na kupata exposure,mitazamo yao tofauti,so sidhani kama hii ni hoja.
Nimesoma tena na tena cv ya Nape akigombea uvccm toka alipoomba UNEC mara ya kwanza 2002,ameeleza alichokifanyia mchama chake tena toka akiwa chipukizi mwaka 1989,sasa sijui kama hili tatizo lake nini? Naamini wapiga kura pamoja na kwamba sio wote wanauelewa tusiwadharau watz kiasi hichi,naamini pengine sera mbadala hazijaelezwa kwao wakazielewa,hapa ndipo penye tatizo na ndo maana kuwatoa ccm ni kazi kubwa....
 
Lakini pia wakuu, ngoja tujaribu kuchambua sababu za msingi zilizowafanya CCM warudishe utaratibu huu.Ikumbukwe utaratibu huu kauanzisha Julius na si kama wanavyodai waungwana hapa eti wakati wa Julius haukuwepo,huo ni uongo...tena wakati huo ulikuwa mkubwa na mgumu kuliko sasa kwani moja ya kazi za balozi zetu nje ilikuwa ni kuratibu mashina na matawi haya ya CCM nje waliko,so walichofanya CCM kwasasa ni kuyaanzisha upya lakini kwa stail ya kuyatoa ofisi za ubalozi na kuya weka kwa wanachama wenyewe...ni kama ilivyo dini,hivi leo waislamu au wakristo au wapagani wakikutana na kuunda umoja wao wa mahali flani kosa lao nini?? njia bora ni wale wa dini nyingine waanzishe yao nao,badala ya kupondana.Mbona wenye Umoja wa dini flani hatusemi kama wanawagawa watz nje???
 
Mwenye CAFE Anajiweza kama sikosei hadi mwaka 2003 alikuwa na nyumba tatu UK
Moja ipo karibu sana na uwanja wa manchester city
Ila ni bahili sana

Kuwa na nyumba tatu UK wala haina maana mtu ana pesa. Mortgage miaka ya nyuma ilikuwa rahisi sana kama unataka kununua nyumba kwa ajili ya kupangisha (buy to let).

Kuna watu nawajua labda wanapata mshahara kidogo sana lakini wana nyumba zaidi ya moja. Hiyo ni investment. Inaweza kufanikiwa lakini pia inaweza ku burst kama ambavyo watu wengi sasa wanakumbwa na hii credit crunch.

Simfahamu jamaa, hivyo anaweza kuwa na pesa lakini wengi ninaowajua hasa Wahindi, nyumba hizo ni investment kwa kutumia mortgage na wala sio kwamba wana mapesa mengi.
 
Lakini pia wakuu, ngoja tujaribu kuchambua sababu za msingi zilizowafanya CCM warudishe utaratibu huu.Ikumbukwe utaratibu huu kauanzisha Julius na si kama wanavyodai waungwana hapa eti wakati wa Julius haukuwepo,huo ni uongo...tena wakati huo ulikuwa mkubwa na mgumu kuliko sasa kwani moja ya kazi za balozi zetu nje ilikuwa ni kuratibu mashina na matawi haya ya CCM nje waliko,so walichofanya CCM kwasasa ni kuyaanzisha upya lakini kwa stail ya kuyatoa ofisi za ubalozi na kuya weka kwa wanachama wenyewe...ni kama ilivyo dini,hivi leo waislamu au wakristo au wapagani wakikutana na kuunda umoja wao wa mahali flani kosa lao nini?? njia bora ni wale wa dini nyingine waanzishe yao nao,badala ya kupondana.Mbona wenye Umoja wa dini flani hatusemi kama wanawagawa watz nje???

Thiongo,

Usipotoshe watu hapa, wengine tumeishi nje miaka mingi kabla hata ya kuanza kwa vyama vingi. Hakukuwa na matawi ya CCM nje ya nchi.

Haikuwahi kutokea kiongozi wa nchi anakuja kukutana na wana CCM tu nje ya nchi.

Kila sehemu kwenye Watanzania tulikuwa tunapeperusha bendera ya Tanzania.

Ni nje wapi huko munakokusema ambako kulikuwa na matawi ya CCM?

Chama kilikuwa kinashika hatamu na kweli ilikuwa lazima balozi awe mwana CCM
lakini balozi zilikuwa hazibagui Watanzania kwa vyama vya siasa.

Aidha inabidi uelewe sio kila jambo lililo halali ni nobel. Makosa ya hayo matawi ya vyama vya siasa ni kuvunja umoja wa Watanzania ambao ulikuwepo miaka ya nyuma.

Katika siasa na sheria motive ni kitu muhimu sana. Hata kama jambo ni halali lakini motive yake ni mbaya, hilo jambo haliendelei kuwa halali.

Kuna watu hapa wako tayari kwenda mikutano ya CCM kwasababu watapata nafasi ya kuonana na viongozi wa juu TZ, lakini watu hao hao wanakuambia kuhudhuria mikutano ya Watanzania wote ni kupoteza muda. Hakuna maslahi huko.

In future ukiwa na viongozi kama hao unategemea nini?
 
Back
Top Bottom