Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Lakini pia wakuu, ngoja tujaribu kuchambua sababu za msingi zilizowafanya CCM warudishe utaratibu huu.Ikumbukwe utaratibu huu kauanzisha Julius na si kama wanavyodai waungwana hapa eti wakati wa Julius haukuwepo,huo ni uongo...tena wakati huo ulikuwa mkubwa na mgumu kuliko sasa kwani moja ya kazi za balozi zetu nje ilikuwa ni kuratibu mashina na matawi haya ya CCM nje waliko,so walichofanya CCM kwasasa ni kuyaanzisha upya lakini kwa stail ya kuyatoa ofisi za ubalozi na kuya weka kwa wanachama wenyewe...ni kama ilivyo dini,hivi leo waislamu au wakristo au wapagani wakikutana na kuunda umoja wao wa mahali flani kosa lao nini?? njia bora ni wale wa dini nyingine waanzishe yao nao,badala ya kupondana.Mbona wenye Umoja wa dini flani hatusemi kama wanawagawa watz nje???

THIONG'O

Nakuunga mkono kabisa, hii ndio hoja ya kujadili hapa bodini.

Nasikitika kusema wanabodi wanapoteza muda kupinga mambo ambayo hawana uwezo wa kuyazuia. Kama CCM wamefungua matawi hiyo ni juu yao. Sisi cha kufanya ni kuhakikisha hakuna ufisadi unaofanya chini ya miavuli ya haya matawi huku ughaibuni.

Halmashauri Kuu ya CCM imeamua Chama kiwe na matawi nje ya Tanzania. Hivyo hili linafanyika na linaendelea kufanyika. Hebu tujadili namna ya kukabiliana na ufisadi kwenye haya matawi madala ya kupoteza muda kupinga mambo ambayo wenye Chama chao wameamua kufanya kwa faida ya Chama chao.
 
Thiongo,

Usipotoshe watu hapa, wengine tumeishi nje miaka mingi kabla hata ya kuanza kwa vyama vingi. Hakukuwa na matawi ya CCM nje ya nchi.

Haikuwahi kutokea kiongozi wa nchi anakuja kukutana na wana CCM tu nje ya nchi.

Kila sehemu kwenye Watanzania tulikuwa tunapeperusha bendera ya Tanzania.

Ni nje wapi huko munakokusema ambako kulikuwa na matawi ya CCM?

Chama kilikuwa kinashika hatamu na kweli ilikuwa lazima balozi awe mwana CCM lakini balozi zilikuwa hazibagui Watanzania kwa vyama vya siasa.


Mkuu hili lifanyie utafiti kwanza kabla hujapingana na Thiong'o. Vyama vingi vimeanzishwa 1995 Nyerere aliondoka madarakani 1985 sasa hebu rudi nyuma zaidi ya hiyo 1992.

Aidha inabidi uelewe sio kila jambo lililo halali ni nobel. Makosa ya hayo matawi ya vyama vya siasa ni kuvunja umoja wa Watanzania ambao ulikuwepo miaka ya nyuma.

Umoja huo wa Watanzani uliokuwepo kabla awi la CCM halijaazishwa Februry/March 2007 ni upi? Pia, hebu tuambie umoja huo umeadhirika namna gani tangu Februry/March 2007 baada ya CCM London kuanzishwa.


Katika siasa na sheria motive ni kitu muhimu sana. Hata kama jambo ni halali lakini motive yake ni mbaya, hilo jambo haliendelei kuwa halali.

Kuna watu hapa wako tayari kwenda mikutano ya CCM kwasababu watapata nafasi ya kuonana na viongozi wa juu TZ, lakini watu hao hao wanakuambia kuhudhuria mikutano ya Watanzania wote ni kupoteza muda. Hakuna maslahi huko.

In future ukiwa na viongozi kama hao unategemea nini?

Sasa hao watu wanafanikiwa kwa sababu mtu kama wewe na wengine wenye mawazo kama yako hawajitokezi huko kwenye mikutano kuwapinga wasiwe viongozi. Na kama unaona huwezi kwenda kwenye mikutano kwa sababu wewe sio CCM basi kwa nini usiwaachie wana CCM wachague viongozi wao wanaowaona wanafaa. Kama huyu kiongozi ukimuona hafai katika chaguzi za ngazi za juu una uhuru wa kupigia kura mgombea wa Chama kingine.

Mimi naamini bila CCM imara Taifa letu liko mashakani na nina imani hapa UK kuna watu wanaweza kwenda kujiunga na CCM na kubadilisha mambo kwa nfasi zao kama ambavyo Mbunge Anne Kilango au Dr Mwakyembe wamefanya mpaka sasa.
 



Mkuu hili lifanyie utafiti kwanza kabla hujapingana na Thiong'o. Vyama vingi vimeanzishwa 1995 Nyerere aliondoka madarakani 1985 sasa hebu rudi nyuma zaidi ya hiyo 1992.



Umoja huo wa Watanzani uliokuwepo kabla awi la CCM halijaazishwa Februry/March 2007 ni upi? Pia, hebu tuambie umoja huo umeadhirika namna gani tangu Februry/March 2007 baada ya CCM London kuanzishwa.


Sasa hao watu wanafanikiwa kwa sababu mtu kama wewe na wengine wenye mawazo kama yako hawajitokezi huko kwenye mikutano kuwapinga wasiwe viongozi. Na kama unaona huwezi kwenda kwenye mikutano kwa sababu wewe sio CCM basi kwa nini usiwaachie wana CCM wachague viongozi wao wanaowaona wanafaa. Kama huyu kiongozi ukimuona hafai katika chaguzi za ngazi za juu una uhuru wa kupigia kura mgombea wa Chama kingine.

Mimi naamini bila CCM imara Taifa letu liko mashakani na nina imani hapa UK kuna watu wanaweza kwenda kujiunga na CCM na kubadilisha mambo kwa nfasi zao kama ambavyo Mbunge Anne Kilango au Dr Mwakyembe wamefanya mpaka sasa.

Yebo Yebo,

Uhuru wangu hauishii kwenye kupiga kura, ni pamoja na haya tunayopinga sasa. Process ya kupata kiongozi wa taifa ni ndefu mmno, kama unavyojua garbage in garbage out. Ni muhimu kupinga yale ninayoyaona hayafai mapema kabla hata ya kufika huko kwenye uchaguzi. Hayaishii hapa, tutawapinga hata hiyo 2010, ndio maana ni muhimu kukusanya dossiers zao.

Tumeona madhara ya hawa watu ambao wako tayari kutumia kila njia ili kujijengea mazingira ya kutwaa uongozi Tanzania. Nyerere alisema ogopa mtu anayekimbilia Ikulu kwa njia zote, wengine tunasema ogopa watu ambao wako tayari kutumia njia zozote kupata ubunge Tanzania.

Kuhusu umoja, tatizo la watu wengi ni kuangalia mazingira waliyopo tu. UK kuna matatizo mengi kabla hata ya matawi ya CCM kuanzishwa. Kuanza kwa hayo matawi kunazidisha kubomoka kwa haraka kwa umoja ambao Nyerere alitumia nguvu zote kutuhakikisha tunakuwa nao. Wengine tumeishi nchi nyingi zaidi ya UK, hasa Europe, kwasababu wao mara nyingi wanakuwa wachache kuna umoja mkubwa na mafanikio kuliko hapa UK.

Nani kakuambia sihudhurii mikutano ya Watanzania UK? Nilichosema sitahudhuria ni hiyo mikutano ya CCM nje ya nchi.

Kuhusu matawi ya CCM nje ya nchi, labda wewe na huyo Thiongo ndio leteni
ushahidi. Huko nyuma nimewahi kuwa kiongozi wa vyama vya wanafunzi hapa Europe, hakuna mahali popote hata kwenye historia ya hivyo vyama panapoonyesha wananchi wa nje walikuwa na matawi ya vyama au walikuwa wanaweka UCCM mbele. Chama kilikuwa kinashika hatamu na ili uje nje ilikuwa lazima uwe mwana CCM lakini hapo ndio ulikuwa mwisho wake, ukifika nje wote tulikuwa Watanzania.

Ukiangalia haya mambo ya vyama, washabiki wakubwa ni watu waliokuja nje miaka ya 2000. Ni matokeo ya mgawanyiko wa Watanzania huko nyumbani na wanauleta hata Ulaya. Huko nyuma umoja wa Watanzania nje ya nchi ulikuwa muhimu sana, hakukuwa na mawasiliano ya kuaminika na nyumbani, hakukuwa na JF, hata kuongea na nyumbani ilikuwa shida. Mshikamo ilikuwa ni kitu muhimu mno kwa Watanzania na ndio maana mpaka leo watu waliokuja siku nyingi nje ya nchi wanaheshimu umoja wa Watanzania kuliko waliokuja miaka ya karibuni.

Huko tunakokwenda na kadri Watanzania wanavyozidi kuwa wengi nje ya nchi, hata ukabila utaanza kukua na tutaishia kuwa kama Wakenya tu. Usipozuia jambo moja, mengine huzaliwa.
 
Yebo Yebo,

Kuhusu umoja, tatizo la watu wengi ni kuangalia mazingira waliyopo tu. UK kuna matatizo mengi kabla hata ya matawi ya CCM kuanzishwa. Kuanza kwa hayo matawi kunazidisha kubomoka kwa haraka kwa umoja ambao Nyerere alitumia nguvu zote kutuhakikisha tunakuwa nao. Wengine tumeishi nchi nyingi zaidi ya UK, hasa Europe, kwasababu wao mara nyingi wanakuwa wachache kuna umoja mkubwa na mafanikio kuliko hapa UK.

Nani kakuambia sihudhurii mikutano ya Watanzania UK? Nilichosema sitahudhuria ni hiyo mikutano ya CCM nje ya nchi.

Sijakutuhumu uhudhurii mikutano ya Watanzania UK. Nilichoandika kiko wazi kinaeleweka, nimezungumzia mikutano ya CCM UK.

Kuhusu matawi ya CCM nje ya nchi, labda wewe na huyo Thiongo ndio leteni ushahidi.

Mimi naunga mkono haya matawi kuwepo, yawe ya CCM, Chadema, Cuf n.k

Ni wewe Mtanzania uliyesema na bado unaendelea kusema kuwa Matawi ya CCM yaliyoanzishwa February/March 2007 yamevunja umoja wa Watanzania uliokuwepo kabla ya hapo; hii statement yako ndio naomba ulete ushahidi. Mimi naamini hizi ni hisia zako ambazo hazina misingi yoyote ya facts.

Ukiangalia haya mambo ya vyama, washabiki wakubwa ni watu waliokuja nje miaka ya 2000. Ni matokeo ya mgawanyiko wa Watanzania huko nyumbani na wanauleta hata Ulaya.

Kweli Mtanzania, unathubutu kusema kule nyumbani leo Watanzania tumegawanyika kwa sababu za kisiasa??!!!

Hawa waliokuja miaka ya 2000 ndio kundi kubwa la kupeleka chachu ya mabadiliko Tanzania, mtu kama umekaa ulaya zaidi ya miaka 15 mfululizo sitegemei kama utakuwa karibu sana siasa za Tanzania unless ufanye juhudi za ziada (au uwe karibu na safu ya viongozi).

Pia kumbuka ni kati ya 2003 na 2006 ndipo CCM walibadili katiba ili kuruhusu rasmi matawi ya chama chao nje ya nchi. Baada ya muda ndipo tutaweza kujua ukweli halisi (kwa ushahidi) kama haya matawi ni faida kwetu Watanzania wa ngambo. Lakini kupinga kitu kwa hisia peke yake haitoshi.

Huko nyuma umoja wa Watanzania nje ya nchi ulikuwa muhimu sana, hakukuwa na mawasiliano ya kuaminika na nyumbani, hakukuwa na JF, hata kuongea na nyumbani ilikuwa shida. Mshikamo ilikuwa ni kitu muhimu mno kwa Watanzania na ndio maana mpaka leo watu waliokuja siku nyingi nje ya nchi wanaheshimu umoja wa Watanzania kuliko waliokuja miaka ya karibuni.


Sasa kama kuna hilo kundi kubwa linaloheshimu umoja wa Watanzania kwa nguvu hiyo unayotaka tuamini hapa forum; kwa nini basi Tanzania Association UK inalegalega?

Nimesema huko nyuma kuwa kulegalega kwa Tanzania Association UK kumechangia kwa kiwango kikubwa kushamiri kwa CCM London. Hoja yangu hii hujasema kama unapingana nayo au unaiunga mkono.

Huko tunakokwenda na kadri Watanzania wanavyozidi kuwa wengi nje ya nchi, hata ukabila utaanza kukua na tutaishia kuwa kama Wakenya tu. Usipozuia jambo moja, mengine huzaliwa.

Watanzania waliopo Tanzania wapo zaidi ya mil 36, mfumo wa vyama vingi Tanzania vimeanzishwa 1992 (miaka 16 iliyopita). Nikuulize swali Mtanzania. Je, unaweza leo kusema kwa hoja zenye mashiko kuwa vyama vya siasa vimeleta Ukabila uliopo Kenya nchini Tanzania?

Natumai hoja zangu unazielewa vema; mimi naheshimu mawazo yako, ila ninaona yanaendeshwa na hisia badala ya facts.
 
Yebo Yebo,

Kwanza kuamini kwamba waliokaa nje miaka mingi hawaelewi yanayoendelea Tanzania naona hauko sahihi. Mimi niko Europe karibu miaka 18 sasa, ninaelewa mambo yanayoendelea TZ labda kuliko watu wengi hata baadhi walioko TZ na siko karibu na kiongozi yeyote na wala sina haja ya kuwa karibu na kiongozi yeyote. Mafanikio yangu yanatokana na yatatokana na kuchakarika na sio vinginevyo. Naamini pia kuna watu wengi mno ambao wako kama mimi. Kama ni mwanachama wa Tanzanet basi unajua kule kuna Watanzania wengi sana wanaojua na wanashiriki na mambo ya Tanzania labda kuliko kundi kubwa la watu walioko TZ.

Sipingi matawi ya CCM kwasababu yanaanzishwa UK, napinga kwasababu ya effect yake kwenye mshikamo wa Wsatanzania popote pale duniani. Leo mmeanza nyie UK, kesho hayo matawi yatajaa kila sehemu hata mahali ambako effect yake itakuwa kubwa zaidi. Matatizo ya UK kama nilivyosema ni makubwa zaidi na kuanzishwa kwahayo matawi ni sababu moja tu katika sababu kibao. Kwenye nchi zingine hasa Europe mambo ni tofauti ukilinganisha na UK.

Matatizo ya UK ni matokeo ya ubinafsi na pia kuwa na watu wengi London ambao
wanaona TA kama chombo cha kufanikisha mambo binafsi. Kwasasa kuna jumuia nyingi tu za Watanzania mikoani. Tulijitahidi tulivyoweza mwaka jana kuzuia
matapeli wasichukue TA, lakini bahati mbaya tulishindwa na sasa hata mliokuwa mashabiki wa hao matapeli mnaanza kuona ukweli wake. Bahati mbaya it is too late. Labda mpaka uchaguzi mwingine.

Sijasema mahali popote kwamba vyama vya siasa vimeleta ukabila. Nilichosema
ni kwamba kwasasa Tanzania ukabila unarudi, matokeo yake muda sio mrefu hata huku Ulaya tutaanza kuona madhara ya ukabila. Wakati wengine tunaondoka TZ siasa ilikuwa sio issue TZ, lakini sasa ni issue. Dini pia ilikuwa sio issue lakini sasa ni issue, ukabila ulikuwa sio issue lakini sasa ni issue.

Usipoziba ufa utajenga ukuta.

Ninaheshimu demokrasia na uhuru wa mtu kufanya anachoona kinamfaa. Sitaenda kuwapiga ngumi wanaofungua matawi nje, tutapambana kwa hoja humu humu JF na hata huko nyumbani. K,ama unaona kufungua matawi ya CCM Ulaya ni bora zaidi, endelea na wengine tutaendelea kupinga. Only time will tell kati yetu
nani yuko sahihi.

Sidhani kama kuna kuelemishana hapa tena na wacha tukubali kutofautiana na kuendelea na mijadala mingine. Huu mchango wangu wa mwisho juu ya hili.
 
Yebo Yebo,

Kwanza kuamini kwamba waliokaa nje miaka mingi hawaelewi yanayoendelea Tanzania naona hauko sahihi. Mimi niko Europe karibu miaka 18 sasa, ninaelewa mambo yanayoendelea TZ labda kuliko watu wengi hata baadhi walioko TZ na siko karibu na kiongozi yeyote na wala sina haja ya kuwa karibu na kiongozi yeyote. Mafanikio yangu yanatokana na yatatokana na kuchakarika na sio vinginevyo. Naamini pia kuna watu wengi mno ambao wako kama mimi. Kama ni mwanachama wa Tanzanet basi unajua kule kuna Watanzania wengi sana wanaojua na wanashiriki na mambo ya Tanzania labda kuliko kundi kubwa la watu walioko TZ.


Sikuwa na nia ya kudharau mtu yoyote nimejaribu kuweka umakini kwenye hiyo kauli, nasikitika hukuilewa kama nilivyodhamiria.

Kitu kimoja cha muhimu nikiseme, ni kuwa the FACT kuwa upo hapa tunafanya huu mjadala ni ushahidi tosha kuwa unafanya "juhudi za ziada" kujua siasa ya nchi yetu inaelekea wapi.

Sidhani kama kuna kuelemishana hapa tena na wacha tukubali kutofautiana na kuendelea na mijadala mingine. Huu mchango wangu wa mwisho juu ya hili.

Naheshimu uamuzi wako, nakubali kutofautiana na wewe kwenye hili. Shukrani kwa kushiriki mjadala bila jazba na kubaki kwenye hoja.
 
CCM READING/LONDON ndio huyu bibie SUSAN ndani ya KHANGA

KWA MTAJI HUU SITOSHANGAA AKIWA MBUNGE


gse_multipart59264.jpg
 
CCM READING/LONDON ndio huyu bibie SUSAN ndani ya KHANGA

KWA MTAJI HUU SITOSHANGAA AKIWA MBUNGE


gse_multipart59264.jpg

GT,

Hii ngoma vipi, na tusio wanachama tunaruhusiwa kujiunga? Mtu unaweza kuchukua kadi bila kujijua kwi kwi kwi!!!!

Kitila, huyo dada mwingine unamtakia nini?
 
ndugu zangu kumbukeni matawi ya CCM UK ni mradi wa mume wa balozi si mnajua ni baba wa nyumbani kwa hiyo kuweni makini maana na yeye anatafuta jinsi ya kula kupitia CCM kwa kujifanya mlezi wa matawi wakati alikua hana hata card hadi mkewe alipo pewa hicho cheo
 
ndugu zangu kumbukeni matawi ya CCM UK ni mradi wa mume wa balozi si mnajua ni baba wa nyumbani kwa hiyo kuweni makini maana na yeye anatafuta jinsi ya kula kupitia CCM kwa kujifanya mlezi wa matawi wakati alikua hana hata card hadi mkewe alipo pewa hicho cheo

mradi kwa maana gani ?
kumuingiza kipato au kama kijiwe cha kupiga zogo ?
 
GT,

Hii ngoma vipi, na tusio wanachama tunaruhusiwa kujiunga? Mtu unaweza kuchukua kadi bila kujijua kwi kwi kwi!!!!

Actually unajua mimi nilikuwa sina mpango na mambo ya CCM lakini nadhani its not a bad idea kujoin kama mambo yenyewe ndio haya

sema kuna taizo dogo...

SUSAN ni mke wa mtu! sasa sheikh huoni kama hapo utakuwa unafanya dhambi kwa kuwa na nia hiyo ilionayo?
 

Actually unajua mimi nilikuwa sina mpango na mambo ya CCM lakini nadhani its not a bad idea kujoin kama mambo yenyewe ndio haya

sema kuna taizo dogo...

SUSAN ni mke wa mtu! sasa sheikh huoni kama hapo utakuwa unafanya dhambi kwa kuwa na nia hiyo ilionayo?

GT,

Hivi kucheza ngoma na mke wa mtu ni dhambi? Sikujua hilo maana hata biblia haijasema hivyo.

Kama hao wawili wanavyocheza kwani kuna dhambi hapo?
 
@ GT.....mmmmh, dhambi nyingine ni bora kama zitatafutiwa njia ya kusameheka tu !!!!..... na kwa ijumaa kama hii, wimbo huu nimeukumbuka..
[media]http://www.youtube.com/watch?v=YnFC9jS7968[/media]
 
hao wanaofungua matawi ya CCM huko hebu waulizeni ndicho kilichowapeleka huko?
na mbona walishindwa kufungua wakiwa hapa?
mi naona niwakumbushe kale ka msemo ka wahenga walisema "haikufaa rangi je itafaa chokaa?"
 
Ndugu wana JF
Kwa mara nyingine tena tumekutana kujadili mustakabali wa utanzania na uzalendo wetu!Kwa wale ambao tumeshawahi kukutana kwenye mijadala mbali mbali ni wazi kuwa wote tunafahamiana kimisimamo pale inapokuja kwenye hoja ambazo tulishawahi kuzijadili.Mara baada ya kashfa za ufisadi kuibuka..watanzania tulioko nje tulishtushwa mno!Pengine niseme wengi wetu..unless proven otherwise!Nevertheless mimi ni muumini mkubwa wa utaifa!Mimi ni mtanzania kwanza..then mwanachama wa chama flani(ingawa hata hivyo sina chama)Ningependa kuwa na chama ambacho ni "independent"Mwanakijiji ebu angalia kama kuna uwezekano wa kuanzisha "Independent and Progressive Party"Chama ambacho kitaibua kizazi kipya chenye mawazo ya utaifa kwanza kabla ya uanachama..jambo ambalo kwa kusema kweli linapeleka migawanyo!
Ndg wana jf:
Ningependa kuweka wazi kwamba nimesoma every single post kwenye mada hii na mawazo na maoni yangu yaeleke kwa waheshmiwa MTANZANIA pamoja na GEEQUE.Ni kweli tupu kama inavyoelekea Mh Geeque anavyo imply kwamba LITAKUWA NI JAMBO LISILOVUMILIKA NA WALA KUELEWEKA HATA CHEMBE NA MTANZANIA HALISI YEYOTE..KWAMBA UFUNGUZI WA MATAWI HAYO HUKO UK NA KWINGINEKO HAKUTAKUWA NA NIA YA KULETA MABDILKO HUKO KWENYE CHAMA CHAO NA SERIKALINI KWA UJUMLA!Niliwahi kuanzisha thread huko nyuma ambayo nilkuwa nikiwapa changamoto watanzania kuwa serikali ishinikizwe ili justice i prevail!Ni wazi kama inavyoeleweka kuwa wana jf tulipiga kelele!Ila nilishangazwa na wananchi wenyewe ambao wanaelekea wameuchapa usingizi wa kifrika za kidemokrasia!Nimekuwa nikiweka wazi kuwa..wapinzani waendelee kuota ndoto za Ikulu kama hawatapigani katiba mpya!Na ndio maana sikutaka kukurupuka na kuanza kutoa tuhuma za ni kwanini hivi vyama vinaanzishwa huku unyamwezini!Sababu ya kwanza ni ile imani kuwa labda hiki kizazi kipya cha wasomi walioko nje ya nchi kimeamua kuinusuru nchi kwa namna moja ama nyingine..lakini kwa namna ambayo wachangiaji wengine ambao hoja zao zinaelekea kuwa nzito tunakuwa na MASHAKA MAKUBWA MNO KWASABABU KWENYE HOTUBA ZA VIONGOZI HAO INASEMEKANA HATA HAWAGUSII WALA KULAANI UFISADI!SASA HIVYO VYAMA NI VYA KUSAIDIA ZIRUDISHWE NA UWAJIBIKAJI NDANI YA CCM NA VIONGOZI WAKE WA SERIKALI AMA NI NAMNA YA KUZIKINGA?Najiuliza sasa lakini bado nashindwa kupata jibu na kama walivyosema wachangiaji wengine..time will definetly be the last resolution!"Kufungua kwao matawi hakutapewa lawama zozote zile kama wao ni wale PROGRESSIVE CCM"Kwa maana kwamba "MASLAHI YA TAIFA NI MBELE KWANZA" Ili litawawezesha kujenga CCM mpya itakayoleta mabadilko ya kikweli!Naelewa wazi kabisa kuwa kuna wana CCM wengi tu ambao hawakufurahishwa na pi hawafurahii yale mambo ya kiufisadiufisadi!Na mimi mwenyewe huwa najiuliza..je kuna watanzania ambao bado wana ujasiri wa "kuwa upande wa haki"hata kama hakuna faida?Kwamba hata kama wananchi walio wengi ambao hawana ufahamu wa kutosha na ambao ni masikini wa kutupwa bado wataipigia kura CCM....JE KUNA ATAKAYE KUWA UPANDE WAO REGADLESS?!KUWAONEA HURUMA NA KUJARIBU AT LEAST KUWAPELEKEA HUDUMA MUHIMU ZA JAMII? Honestly mimi bado najiuliza sana tu..sometimes i even wonder if we actually need multiparty system yet!Kwasababu ni wazi kuwa west walipotushinikiza tufuate mkumbo wa siasa zao...tuzikumbatia kwa style ya "FULLL KUJIACHIA" KUTATULETEA MADHARA NA SI VINGINEVYO!WENZETU WALIAMUA KUZIKUMBATIA HIZO POLITICS KWASABABU ZINAENDANA NA LEVEL YAO WALIYOFIKIA YA MAENDELEO YA KIJAMII NA KIUCHUMI!Sasa tunapotaka kuzi adopt hizo politics ni sawa na kuibeza ile falsafa ya social hierachy!Falsafa ambayo inaweka wazi kuwa watu hawawezi kufikiria beyond the "just the means" to get some food if they're actually starving!Ni saikolojia hiyo..taka tusitake!Sasa mara nyingi viongozi huwa wanasema they're following the people's wish..kama wananchi wengi wananona mabo ni poa tu..then kwanini CCM na viongozi wao wasione the same?
Usahuri wangu kwa wenye vyama;
1)Kwa wale wote walio nje ya nchi..kama mnafungua vyama bila kuonyesha kuwa nia yenu ni kuleta mabadiliko ndani ya CCM ili kuwasaidia wananchi na kutokomeza ufisadi..then migawanyo anayodai Mtanzania haitaweza kuepukwa..kwani ni wazi kuwa watanzania wengi walioko nje wlikasirishwa kupita kiasi na kashfa za ufisadi(narudia kuwa i still assume ni wote walioguswa na ufisadi unless proven otherwise)
2)Kwa upinzani;
Kama ningekuwa nyie ningegundua ukweli ulio wazi kwamba bila mabadilko ya katiba ambayo yatavibana vyama vya kisiasa na kufutilia mbali itikadi before uzalendo..then mtaula wa chuya na ni time wasting!This is my honest advice..Huwezi kutaka kupigania matawi ya juu wakati yale ya chini yenyewe bado hamuyawezi!Sasa hawa ndugu zetu walioko nje ya nchi wanaziona siasa za bongo..at the same time wanataka wa utilize elimu yao kwenye maendeleo ya nchi..sasa watathubutu vipi kujiunga na upinzani wakati waathrika wenyewe(wananchi)hawautaki?MH
Ndugu wana jf mjadala ndio kwanza umeanza na nina ahidi kushiriki kikamilifu na kwa moyo mmoja!Kama nilivyosema hapo awali..nakubaliana na Mtanzania na geeque na wao wameshasema mengi tu na hivyo kuwa na haya machache kwa sasa.God Bless Tanzania God Bless Africa!
 
Back
Top Bottom