Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,185
- 64
Kukimbilia kufungua mashina ya CCM huku mkiongoza kuwamwagia misifa viongozi wa CCM ambao kila mtu anajua ni incompetent na Corrupt ni kuishiwa hoja ambazo zingeweza kuongoza kujenga taifa letu. Hivi inaingia akilini kweli wakati huu ambao Taifa liko katika wakati mgumu kutokana na viongozi wengi waliotoka CCM ambao wanaongoza kwa ubadhirifu wa mali za umma na rasilimali za nchi, baada ya kukaripia uchafu huu unaoendelea, nyinyi mnaongoza kuwamwagia sifa hawa mafisadi. Ilitegemewa kwamba wasomi kama nyinyi ndio mngekuwa mstari wa mbele katika mapigano ya kuleta haki na kumaliza rushwa hatimaye kuingoza nchi katika kuiletea maendeleo ya kiuchumi. Lakini leo hii ndio kwanza mnajiunga na MAFISADI na kuzidi kuwafanya waone kuwa hata wasomi wanawakubali katika ujambazi wao wanaoufanya nchini mwetu. MNABOA, MNANUKA NA MNATIA AIBU.
Good job Geeque,
mazee naona wamekuboa hadi basi tu! Utakuta watu mambo muhimu ya nchi wako kimya na kusifia ufisadi day in day out. Inaonekana wengine hata kuwa na redio ya internet ni makosa! Kwi kwi kwi yaani kuna watu wanataka kuwe na radio uhuru na RTD pekee ili kumwaga propaganda za Kingunge na wezi wenzake! grrrrrrrrr