ARIGATO GOZAIMASHITA
New Member
- Oct 17, 2018
- 3
- 1
Ndugu mteja,
Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?
Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.
Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:
- Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
- Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.
Karibu
Vodacom Tanzania
Ni kweli. Hata Mimi nina shida hiyo hiyo. Maelezo mengi na pamoja na kusikiliza, sijabahatika kukutana na hiyo ya kuongea na muhudumu. No vema watueleze huduma hiyo inapatikana menu gani, au wameifuta?Mm nataka kuongea na customer care leo ni siku ya nne nikipiga namba 100 naona maelezo mengi
Kweli kabisa tunashindwa kuongea Na watoa huduma kwa wateja kulikonii??Hivi kweli kabisa Vodacom hamtaki tuongee na watoa huduma kwa wateja... Maana hatuwapi ama hatupati hicho kipengele cha kuongea na mtoa huduma kwa wateja... Ukipiga 100
Voda wanazngua sanaHivi kweli kabisa Vodacom hamtaki tuongee na watoa huduma kwa wateja... Maana hatuwapi ama hatupati hicho kipengele cha kuongea na mtoa huduma kwa wateja... Ukipiga 100
Mnamo tarehe 12 Sept.2018 nilituma pesa kutoka ktk account yangu ya M-Pesa 500,000/= Tsh(Laki 5) kwenda bank ya DTB(Through CELLULANT Tanzania Ltd),sms ya malipo nikaipokea tarehe 13 sept.2018.Cha kushangaza kwenye account ya DTB pesa haikuingia.Nilipiga simu huduma kwa mteja bila mafanikio,kwa bahati mbaya siku hio hio nilitakiwa kusafiri nje ya nchi hivyo nikaondoka na kumwachia mdogo wangu afanye follow up.Alivyowasiliana na vodacom wakamwambia aende Bank ,kwenda bank wakamwambia hakuna pesa iliyoingia,akawapigia tena voda,ila cha ajabu voda hawajafanya chochote na mpaka sasa pesa haijaingia kwenye account.Tafadhali sana Vodacom ninaomba mshughulikie tatizo langu,nimeattach image ya muamala.
Mkuu hao ni wezi waliokubuhu,nashangaa serikali inawaangalia tu wanavyotuibiaVodacom nimefanya malipo kwenye kampuni fulani, mlichelewa kunipa sms, niliipata kwesho yake, mmekiri kuwa ni kosa lenu, ila ni mwezi sasa mnanizungusha. Nashukuru.
Voda mnaudhi mpk leo hii mwiko mm kuweka salio kweny simu yangu labda mpesa tu na nmeacha kununua bundle za data .mnabundle chache mno jamna ipeni thaman hela ya mtanzania mnponipa mb 1 hivi mm nnaifanyia nn hiyo mb moja ,usiweke vocha kweny simu yako ukaiacha hata kwa dk tano zinatosha kukata hata simu ikiwa imezimwa mnakata huu kama sio wizi ni nn nikapiga sim hudum kwa wateja three times wakasema imetumika kweny data chakushangaza cm yangu ilizima had nkaanza kujiuliza .mna majibu marahisi hamtoi maelezo mazuri huduma kwa wateja ipo ilimradi na nyie muwe nayo ila binafsi sion faida yake.Ndugu mteja,
Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?
Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.
Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:
- Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
- Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.
Karibu
Vodacom Tanzania
Kuna wizi mkubwa kwa fedha za salio za wateja unaoendelea sasa hivi katika mtandao wa Vodacom.
Kwa vile hili si jungu bali ukweli nimisha report wizi huo katika kitengo cha malalamiko TCRA kwa hatua zaidi.
Nimeweka salio la Tsha 10,000 mchana wa leo kwa Mpesa ref Y23SY687 na baada ya muda mfupi nikakuta salio langu la maongezi ni sifuri.
Nikanunua vocha na kutumiwa tshs 10,000 na hela yote imekatwa tena.
Wateja wa Vodacom jihadharini, kuna mwizi kaingia mtandaoni Vodacom
UPDATE
=====
VODACOM wamefanya ustaarabu wa kunipigia baada ya kuona detail ya transaction hapo juu, na kuiona kwenye mtandao wa Jamiiforums.
Kimsingi wameapologise kwa mtafaruku uliotokea lakini wamenieleza nifike ofisini kwao kuona aian ya simu ninyotumia isije ikawa data apps ziko wazi.
Na kweli baada ya maongezi ya kuchunguza, mobile data setting ilikuwa ON, na mimeizima sasa.
Hata hivyo ni vema nitaenda kupata maelezo ya kuyeyuka kwa salio langu , karibu 20,000, kwa siku moja.
Wanabodi mtajulishwa inawezekana kuna wenye tatizo kama langu.
UPDATE
=====
Nimeonana na waheshimiwa sana wa Customer Care pale Block 4 Mlimani City.
Cha kusikitisha ni wao kushindwa kuchukua malalamiko yangu na kuyafanyia kazi, na hii ni licha ya kuwaelewesha kuwa hili tukio nalijawahi kunitokea na hii kuwa ni mara ya kwanza.
Hawa jamaa wa Customer Care ni kama mabalozi waliopewa jukumu la kusafisha kampuni ya VODACOM hata kama inanuka kwa wizi uliodhahiri.
Kitu ambacho hawajui ni kuwa nilifanya due diligence kupitia wafanyakazi ndani ya VODACOM walionidhihirishia kuwa kuna wafanyakazi wasio waaminifu ambao wana access na personal security settings za wateja.
Na wafanyakazi hao huwa "wapiga kishenzi" fedha za wateja.
Kwa kifupi mtu wa Customer Care ameshindwa kuniconvince na maelezo yake ya upotevu wa Tshs 20,000 katika mtandao wa VODACOM.