Vizuizi vya chip vya Marekani dhidi ya China ni sawa na "kutangaza vita" dhidi ya mnyororo wa ugavi wa bidhaa husika duniani

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG211287007531.jpg


Serikali ya Marekani imesema inafikiria kuongeza muda wa vizuizi vya uuzaji nje wa bidhaa za chip kwa China vilivyoanza mwezi Oktoba mwaka jana, ikiwa ni juhudi zaidi za kudhoofisha maendeleo ya sekta ya akili bandia ya China. Gazeti la "the New York Times" limechapisha makala ikisema hatua hii ni kitendo cha vita.



Tangu wakati wa utawala rais Donald Trump, Marekani imekuwa ikitumia "usalama wa taifa" kama kisingizio cha kudhibiti na kuzuia sekta ya teknolojia ya China. Leo kisingizio kama hicho hakionekani sana, lakini Marekani haifichi fikra na nia mbaya ya umwamba—“China haipaswi kupiga hatua katika nyanja fulani muhimu za kiteknolojia, na nyanja hizi ndizo zinazochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya siku za usoni.” Hayo yamesemwa na mtafiti mwandamizi wa jopo la washauri bingwa la The Center for a New American Security (CNAS) Emily Kilcrease na aliyekuwa ofisa wa biashara wa serikali ya Marekani.



Ni kweli kwamba karibu chip zinazotumiwa na China kuendesha mipango na taasisi za kisasa zote zimetumia teknolojia ya Marekani. Kwa hiyo, vizuizi vya chip vya raundi kwa raundi vya Marekani vilileta changamoto kubwa dhidi ya sekta za uchumi na teknolojia nchini China. Lakini wakati huo huo, uamuzi wa Marekani wa kuchukua hatua ya upande mmoja pia ni mchezo wa kamari wa kidiplomasia, sio tu kuchezea kamari maslahi ya Wamarekani wenyewe, lakini pia ni sawa na kutangaza vita dhidi ya usalama wa mnyororo wa ugavi wa bidhaa husika duniani.



Hivi karibuni, maofisa wakuu watendaji wa makampuni matatu makubwa ya Marekani ya Intel, Qualcomm, na Nvidia walikutana na maofisa mbalimbali waandamizi wa serikali ya Marekani, akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje Antony Blinken, na kupinga kuongeza vizuizi dhidi ya China. Mwaka jana China bara iliagiza bidhaa za semiconductor zenye thamani ya takriban dola bilioni 180 kutoka Marekani, karibu theluthi moja ya jumla ya bidhaa hizo zilizouzwa duniani. Vikwazo vya serikali ya Marekani vitadhoofisha uwezo wa China wa kununua chip za Marekani, jambo ambalo sio litaathiri mapato ya makampuni ya Marekani, lakini kwa hakika litaharibu uwekezaji mkubwa wa serikali ya Marekani katika sekta ya chip, na hatimaye kudhoofisha nguvu ya ushindani ya sekta ya semiconductor ya Marekani duniani. Muhimu zaidi, ikiwa hatua hizi za vikwazo vya Marekani dhidi ya China zitashindwa, zitakuwa na athari za kushangaza za kuhimiza maendeleo ya teknolojia ya China, na matokeo ambayo Marekani inajaribu kuyaepuka yatatokea mapema zaidi.



Sio tu vita vya teknolojia vilivyoanzishwa na Marekani dhidi ya China vimeathiri maslahi ya makampuni ya Marekani, bali pia vitahatarisha usalama wa mnyororo wa ugavi na uzalishaji duniani kote. Leo sekta ya semiconductor ndio msingi wa sekta ya uzalishaji viwandani duniani, na hatua 300 katika tasnia ya semiconductor duniani zinakamilishwa na kampuni kutoka nchi na sehemu mbalimbali. China ni soko kubwa zaidi la kibiashara la semiconductor, na kudhoofisha uwezo wake wa uzalishaji na ununuzi wa bidhaa hizo bila shaka kutaathiri tasnia ya semiconductor duniani na kuwa na athari mbaya kwa uchumi wa nchi nyingi. Hii sio tu itaongeza kiwango cha ukosefu wa ajira zinazohusika, lakini pia itadhuru maslahi ya wateja.



Hivi karibuni China ilitangaza kudhibiti uuzaji nje kwenye madini ya gallium na germanium, raslimali muhimu kwa uzalishaji wa semiconductor, baada ya Marekani kuchukua hatua mfululizo dhidi ya China. China ni mzalishaji mkubwa zaidi wa madini hayo duniani, na zaidi yake ya madini hayo yanayotumiwa nchini Marekani yanaagizwa kutoka China. Hii inaikumbusha Marekani kwamba China inachukua nafasi muhimu katika mnyororo wa ugavi wa semiconductor duniani, na jaribio lolote la kuidhibiti na kukandamiza China litadhuru mnyororo wa ugavi duniani, na inaelekea kushindwa na hatimaye itajidhuru yenyewe.
 
Back
Top Bottom