Vitu sita ambavyo si viumbe vya Mungu

Vitu sita ambavyo si viumbe vya Mungu

Unajuaje kwamba mungu yupo na mawazo yake hayachunguziki kweli, na kwamba hii si story tu ambayo imetungwa na watu waliotaka kuuelezea ulimwengu ambao hawauelewi?

Nimeuliza swali, kwa nini mungu mwenye ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati ana uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Ukiniambia mawazo yake hayachunguziki kimsingi unaniambia unaamini katika mungu usiyemuelewa na ambaye hawezi kueleweka.

Na kama unaamini katika mungu ambaye humuelewi na wala haeleweki, utajuaje kwamba yupo na si hadithi tu?
KWANZA,kupitia maandiko yanaeleza ukuu wa MUNGU ambao biblia niliyo soma inasema MUNGU ni roho,yeye hakuumbwa,yuko mahali popote.Sasa biblia inasema YEYE NI ROHO,scientist wanasema SUPERNATURAL POWER,natural power ambayo hawajaweza kuiprove kwa namna yoyote ndo mana wanashia hapo,,,,SASA kuishia hapo tu biblia pia imesema kuwa HACHUNGUZIKI,ALFA NA OMEGA,maana yake kama tumeshindwa kusema zaidi kuhusu SUPERNATURAL POWER maana yake HACHUNGUZIKI...
PILI,Maandiko yenyewe yanasema kuwa MUNGU kila alicho umba akaona nichema sana akavibariki hasa viumbe hai akasema MKAZAE,MKAONGEZEKE,mkaijaze nchi,,,,,LAKINI VIUMBE KAMA MARAIKA,MWANADAMU,viliumbwa tofauti na viumbe wengine,au vitu vingine,kwani VILIWEKEWA "WILLING"Viliwekewa kuchagua,kuamua,KUTAWALA VINGINE,hata vikapewa maarifa,,,,TULIPEWA UHURU,SASA magonjwa,njaa,na vita chanzo chake ni SHETANI,NA MWANADAMU MWENYEWE JINSI ALIVYO TUMIA AKILI,AU WILLING YAKE KAMA WEWE "KIRANGA",,,,MUNGU anao uwezo wa kuviondoa vitu vilivyo sababishwa na willing ya mwanadamu na shetani,LAKINI Maandiko husema ameruhusu tu viwepo,hata YESU akasema shetani amepewa nafasi ya kuwapepeta ngano,,,,MUNGU alitaka aone utii,KAMA LEO UTAPEWA MADARAKA MAKUBWA,JE utayatumiaje?????SASA AKILI YAKO KIRANGA NDIO INATAKA IKUUE,IKUPOTEZE,MUULIZE NIETCHZECK
TATU,unasema MUNGU nisie muelewa,kumbuka mungu ni roho,nao wamwabudie inawapasa kumwabudu katika roho na kweli,UKITAFSIRI VITU VYA ROHONI NA AKILI your lost,wewe unatumia akili hiyo ndogo MUNGU aliyokupa KUFIKIRIA VITU VYA ROHONI,,,ndo mana humwelewi MUNGU.BIBLIA INASEMA onja uone,,,,umetumia akili yako vya kutosha NJOO ROHONI UONE,na ukiwa bado na maswali sitakukatalia......WELCOME BROTHER
 
Unajuaje kwamba mungu yupo na mawazo yake hayachunguziki kweli, na kwamba hii si story tu ambayo imetungwa na watu waliotaka kuuelezea ulimwengu ambao hawauelewi?

Nimeuliza swali, kwa nini mungu mwenye ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati ana uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Ukiniambia mawazo yake hayachunguziki kimsingi unaniambia unaamini katika mungu usiyemuelewa na ambaye hawezi kueleweka.

Na kama unaamini katika mungu ambaye humuelewi na wala haeleweki, utajuaje kwamba yupo na si hadithi tu?
Mungu ktk maamuzi yake hakosei...na anafanya analotaka yeye.
 
Mungu ktk maamuzi yake hakosei...na anafanya analotaka yeye.
Sijasema amekosea. Sijasema hafanyi analotaka yeye.

Hujajibu swali lililoulizwa, ulilojibu kama lipo, halijaulizwa.

Rudia kusoma halafu jibu lililoulizwa. Kama huna jibu unaruhusiwa kusema hujui.
 
Ukitaka haya mambo yasikusumbue we amini hivi..
NATURE IS THE SUPREME POWER ABOVE ALL. IS THE INDEPENDENT POWER THAT GOVERNS EACH AND EVERY THING ON ITS OWN WAY..
Below nature there are 2 sides Good and Bad.
Good ones are coming from GOD
Bad ones are coming from Satan
*********Over********
 
Kwa mtazamo wangu wewe ndiye hujielewi zaidi yake.Hivi hadi leo nyie watu mpo ?,mnaoamini kwamba et mungu(kama yupo)alimtuma mwana wake wa pekee sijui yesu aje kutukomboa?,so what?.Hakuna hata logic katika jambo hilo ni kitu ambacho hakina maana.Who is yes after all? Aisee
ni upumbavu na hapo kwa yesu ndio wanaharibu kabisa.kisha wanaona vyakwao ndio bora.eti vifungu kwani hivi sio vifungu.
 
Mungu na shetani, mwenye nguvu ni Mungu. Mungu alimuamuru shetani asimuue Ayubu akatii.. inamaana alijua nguvu za MUNGU
Vipi Babu yako? hajatii.... afu tena Sikia... hizo Hadithi za Kijinga sio issue maana hiyo convensation between Mungu na Shetani waeza sema nani huyo aliyewasikia... au kuna mtu alitega kinasa sauti? au cctv footage ilinasa huo ubishani? Na kama Nguvu ni utii pekee hiyo ni kali... so Mimi nikikuambia uendelee kuchat humu jf na wewe ukaendelea so mimi nina nguvu kuliko wewe? what kind of mifano ya kucompare
 
Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao magonjwa yanawezekana kuwepo wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao magonjwa hayawezekani?
Mungu huyo huyo anao uwezo wa kumfanya kila mtu akawa Tajiri kwanini kuna Maskini??? Mungu ana uwezo wa kuifanya dunia kuwa na Amani kusiwe na vita wala mauwaji kwanini yapo? ukipata majibu ya hayo utapata na jibu kuhusu maradhi anao uwezo wa kufanya mengi yasiwepo lakin yapo kwa ajili ya Mitihani kwetu. Mungu ameumba ardhi safi isiyo na maradhi bali sisi watumiaji wa hiyo ardhi ndio tumejiletea maradhi mengi.
 
Ukinitatulia contradiction hii nitaanza kukusikiliza kwa ku entertain uwepo wa mungu.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

This is a logical contradiction that needs to be resolved by logic.

Huhitaji kutoa picha ya mungu au fingerprints zake.

Logic tu.

Unaweza kutatua swali hili?
Vitu vingine vinamajibu rahisi lkn watu wanasumbuka cjui nn.
Ukisema kwa nini Mungu asingeumba ulimwengu usio na dhambi wakti yy ndo anamamlaka yote unakosea.
Ukisoma Yeremia 29:11 mungu anasema mipango yake nikutuwazia mema wakati wote. Mwanzo kabisa Mungu aliumba Ulimwengu ulio perfect usio na dhambi ambamo aliishi Adam na Hawa. Ila kuna siri moja kubwa Mungu alimuumbia Adam na Hawa.....UWEZO WA KUJICHAGULIA MEMA NA MABAYA.... na tunaona Hawa alitumia uwezo huu akachagua kusikiliza nyoka na ikaletea maasi kwa kizazi chake chote. Pia Lucifer alitumia huu uwezo na akaasi mbinguni akiwa na malaika zake. Hta leo kila mtu ana hii nguvu bado.
Waweza kuniuliza ni kwa nini Mungu asingeondoa hii nguvu ya uhuru wakujichagualia mema na mabaya na akatuwekea moja tuu yakuchagua mema ili tusitende dhambi tena?
Jibu la swali hili linapatikana Warumi 9.
Mfinyanzi anapoandaa udongo kwa kutengeneza chombo huwa anatengeneza chombo akiwa na makusudi maalum na akizingatia matumizi ya chombo hicho.
Anaweza akatengeneza cha kikombe,chungu,kinu na kadhilika...huo ni uamuzi wake. Pia anaweza akatengeneza kingine kwa ajili ya matumizi yakawaida na kingine kwa matumizi ya kifalme. Je hicho chombo kina mamlaka gano ya kumuuliza mfinyanzi kwa nini umenitengeneza hivi?
Wanadamu ni kazi ya ifinyanzi ya Mungu....wew ni nani na unamamlaka gani kumuuliza Mungu kwa nini ameumba ulimwengu jinsi ulivyo na akaweka hiyo nguvu ya kujiamulia(willing power) ndani yetu????
 
Sijasema amekosea. Sijasema hafanyi analotaka yeye.

Hujajibu swali lililoulizwa, ulilojibu kama lipo, halijaulizwa.

Rudia kusoma halafu jibu lililoulizwa. Kama huna jibu unaruhusiwa kusema hujui.
Kiranga hilo ni jibu tosha ...
 
Sijasema amekosea. Sijasema hafanyi analotaka yeye.

Hujajibu swali lililoulizwa, ulilojibu kama lipo, halijaulizwa.

Rudia kusoma halafu jibu lililoulizwa. Kama huna jibu unaruhusiwa kusema hujui.
Ok ni hivi mungu kaumba ulimwengu wenye mabaya na mazuri kwa mwanadamu na majini ..hii ni kama mtihani kwao na atakaye faulu au atakaye mfata atakayo muumba basi atapata ulimwengu wa mazuri milele(peponi)..alafu usijisahau kuwa huu ulimwengu sio kwa ajili ya binaadamu pekee kwa sababu viumbe wengine kama wanyama na malaika mimea na kadhalika wao wanaulimwengu mmoja tuu wa mazuri ...na mungu kafanya haya yoote kwa matakwa yake kama muumba mfalme wetu na katika anayoyafanya hakosei...LIFE SPAN YA MTANZANIA NI 45 YEAR
 
Mungu huyo huyo anao uwezo wa kumfanya kila mtu akawa Tajiri kwanini kuna Maskini??? Mungu ana uwezo wa kuifanya dunia kuwa na Amani kusiwe na vita wala mauwaji kwanini yapo? ukipata majibu ya hayo utapata na jibu kuhusu maradhi anao uwezo wa kufanya mengi yasiwepo lakin yapo kwa ajili ya Mitihani kwetu. Mungu ameumba ardhi safi isiyo na maradhi bali sisi watumiaji wa hiyo ardhi ndio tumejiletea maradhi mengi.
Hujaelewa swali.

Unasema mungu ameumba ardhi safi bali sisi watumiaji wa hiyo ardhi ndio tumejiletea maradhi.

Nauliza hivi, pale mungu alipokuwa anaanza kupanga kuumba ulimwengu, kabla hajaumba kiumbe chochote, alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya/ maradhi yoyote hayawezekani kufanyika.

Angeweza kuumba ulimwengu ambao wewe huwezi kufanya mabaya wala kupata ugonjwa kama usivyoweza kurudi nyuma katika muda uende mwaka 1982.

Kwa nini hakuumba ulimwengu huo na kaumba huu ambao mabaya yanawezekana?

Ukisema sis ndio tumejiletea maradhi, unakuwa hujajibu swali la kwamba, ili sisi tujiletee maradhi inabidi tuwe katika ulimwengu ambao maradhi yanawezekana kuwepo.

Kama mungu angeumba ulimwengu ambao maradhi hayawezekani kuwepo, tusingeweza kupata maradhi, kama ambavyo hatuwezi kurudi nyuma katika muda.

Umelewa swali langu sasa?
 
Vitu vingine vinamajibu rahisi lkn watu wanasumbuka cjui nn.
Ukisema kwa nini Mungu asingeumba ulimwengu usio na dhambi wakti yy ndo anamamlaka yote unakosea.
Ukisoma Yeremia 29:11 mungu anasema mipango yake nikutuwazia mema wakati wote. Mwanzo kabisa Mungu aliumba Ulimwengu ulio perfect usio na dhambi ambamo aliishi Adam na Hawa. Ila kuna siri moja kubwa Mungu alimuumbia Adam na Hawa.....UWEZO WA KUJICHAGULIA MEMA NA MABAYA.... na tunaona Hawa alitumia uwezo huu akachagua kusikiliza nyoka na ikaletea maasi kwa kizazi chake chote. Pia Lucifer alitumia huu uwezo na akaasi mbinguni akiwa na malaika zake. Hta leo kila mtu ana hii nguvu bado.
Waweza kuniuliza ni kwa nini Mungu asingeondoa hii nguvu ya uhuru wakujichagualia mema na mabaya na akatuwekea moja tuu yakuchagua mema ili tusitende dhambi tena?
Jibu la swali hili linapatikana Warumi 9.
Mfinyanzi anapoandaa udongo kwa kutengeneza chombo huwa anatengeneza chombo akiwa na makusudi maalum na akizingatia matumizi ya chombo hicho.
Anaweza akatengeneza cha kikombe,chungu,kinu na kadhilika...huo ni uamuzi wake. Pia anaweza akatengeneza kingine kwa ajili ya matumizi yakawaida na kingine kwa matumizi ya kifalme. Je hicho chombo kina mamlaka gano ya kumuuliza mfinyanzi kwa nini umenitengeneza hivi?
Wanadamu ni kazi ya ifinyanzi ya Mungu....wew ni nani na unamamlaka gani kumuuliza Mungu kwa nini ameumba ulimwengu jinsi ulivyo na akaweka hiyo nguvu ya kujiamulia(willing power) ndani yetu????
Utasemaje mwanzo kabisa mungu aliumba ulimwengu perfect, halafu baadaye hiyo perfection ikatoweka?

Ulimwengu ambao perfection inaweza kuondoka si perfect.

Kwa nini mungu hakuumba ulimwengu ambao perfection haiwezi kuondoka?

Alitaka ila akashindwa?

Kama alishindwa ni kweli anaweza yote?

Au aliweza hakutaka?

Kama hakutaka tu, ni kweli ana upendo wote?
 
Kiranga hilo ni jibu tosha ...
Lipi ni jibu tosha?

Nikiuliza, kwa nini baba kavaa suti leo, mtu akinijibu "baba anavaa anavyotaka, ana uamuzi wote kuhusu nguo anazovaa" hilo jibu limejibu swali langu?

Hilo si jibu la swali langu, hilo ni jibu la swali linguine, swali hilo ni "Nani anamuamulia baba nguo za kuvaa".

Sijauliza nani anamuamulia mungu, nimeuliza kwa nini kaamua hivyo.

Kwa swali la baba kuvaa suti, jibu linaweza kuwa "amevaa suti kwa sababu anaenda kwenye sherehe" au "amevaa suti kwa sababu ana interview ya kazi" au "sijui kwa nini amevaa suti leo"

Usilazimishe kukwepa kutoa jibu kuwe ni jibu.

Mtu anayesema mungu anaamua vyovyote, hajajibu swali la kwa nini mungu kaamua hivi na si vile.
 
Ok ni hivi mungu kaumba ulimwengu wenye mabaya na mazuri kwa mwanadamu na majini ..hii ni kama mtihani kwao na atakaye faulu au atakaye mfata atakayo muumba basi atapata ulimwengu wa mazuri milele(peponi)..alafu usijisahau kuwa huu ulimwengu sio kwa ajili ya binaadamu pekee kwa sababu viumbe wengine kama wanyama na malaika mimea na kadhalika wao wanaulimwengu mmoja tuu wa mazuri ...na mungu kafanya haya yoote kwa matakwa yake kama muumba mfalme wetu na katika anayoyafanya hakosei...LIFE SPAN YA MTANZANIA NI 45 YEAR
Kwa nini mungu ahitaji mtihani?

Mwalimu anapotoa mtihani ni kwa sababu hana uwezo wa kujua yote, mtihani unamsaidia kujua mwanafunzi anaelewa nini.

Mungu mwenye ujuzi wote anahitaji mtihani kwa nini?
 
Kwa nini mungu ahitaji mtihani?

Mwalimu anapotoa mtihani ni kwa sababu hana uwezo wa kujua yote, mtihani unamsaidia kujua mwanafunzi anaelewa nini.

Mungu mwenye ujuzi wote anahitaji mtihani kwa nini?
Anatoa mtihani kama hekima ili kesho akikuchapa usilalamike kuwa umeonewa..ujijue kuwa wewe kweli umefeli wenzio wamefahulu mtihani huo huo so ni kama reference.
 
Anatoa mtihani kama hekima ili kesho akikuchapa usilalamike kuwa umeonewa..ujijue kuwa wewe kweli umefeli wenzio wamefahulu mtihani huo huo so ni kama reference.
Kwa nini atoe mtihani na kuhitaji kuchapa wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hakuna kukosea (kukosea hakuwezekani) na hivyo hakuna haja ya mtihani wala mtu kuhukumiwa?
 
Kwa nini atoe mtihani na kuhitaji kuchapa wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hakuna kukosea (kukosea hakuwezekani) na hivyo hakuna haja ya mtihani wala mtu kuhukumiwa?
Sijui kwanini baba leo kaamua kuvaa koti..may be ni mapenzi yake ila ninachokumbuka kuwa baba huwa hakosei katika mavazi yake.
 
Sijui kwanini baba leo kaamua kuvaa koti..may be ni mapenzi yake ila ninachokumbuka kuwa baba huwa hakosei katika mavazi yake.
Kama hujui kwa nini baba kavaa koti, huwezi kujua kama hakosei.

Utajuaje hakosei wakati hujui kwa nini kavaa koti?

Kama hujui kwa nini mungu kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati angeweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani, humjui huyu mungu.

Humuelewi.

Na unaweza kuwa unaamini mungu ambaye katungwa tu na watu, kiuhalisi hayupo.

Kwa sababu hujaweza kutatua a major contradiction.

Kwa nini mungu mwenye ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
 
Kama hujui kwa nini baba kavaa koti, huwezi kujua kama hakosei.

Utajuaje hakosei wakati hujui kwa nini kavaa koti?

Kama hujui kwa nini mungu kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati angeweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani, humjui huyu mungu.

Humuelewi.

Na unaweza kuwa unaamini mungu ambaye katungwa tu na watu, kiuhalisi hayupo.

Kwa sababu hujaweza kutatua a major contradiction.

Kwa nini mungu mwenye ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
Sababu ya mungu kuumba ulimwengu inajulikana ....ila hilo swali la kusema kwanini kaumba ulimwengu wa aina mbili wa mabaya na mazuri haliyakuwa anaweza kuuumba wa mazuri tuu..hili swali lipo beyond sana kaka
 
Sababu ya mungu kuumba ulimwengu inajulikana ....ila hilo swali la kusema kwanini kaumba ulimwengu wa aina mbili wa mabaya na mazuri haliyakuwa anaweza kuuumba wa mazuri tuu..hili swali lipo beyond sana kaka
Unaliona lipo beyond kwa sababu mungu huyo hayupo.

Swali lina expose contradiction.

Mungu huyo mnayemsema (mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote) angekuwepo, ulimwengu ambao mabaya yanawezekana usingekuwepo. Asingeuruhusu.

Ulimwengu unaowezekana mabaya upo. Ndio huu tunaoishi.

Kwa hiyo, mungu huyo hayupo. Katungwa na watu tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom