Yuko Mungu anayejibu Maombi

Yuko Mungu anayejibu Maombi

Mwl Mwakujonga

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2023
Posts
362
Reaction score
712
Miaka 7 iliyopita nipitia katika changamoto kubwa ya mahusiano yangu na Mungu.

Katika kipindi hicho chote Mungu alikuwa mwaminifu katika maisha yangu , mambo mengi ambayo hata sikuyaomba Mungu alinifanyia kwa upendo

Maisha yalikuwa mazuri katika upande wa familia, watoto, uchumi nk kwa kweli Mungu alikuwa ni mwema sana na hata leo nasema tena Mungu ni mwema.

Katika miaka hiyo yote jambo 1 ambalo nilikuwa namwomba Mungu hakuweza kunijibu, ombi hilo moja lilikuwa la muhimu sana kwangu kuliko maombi yote ambayo nimemwomba Mungu anifanyie

Ombi hilo lilianza mwaka 2019 nilianza kuomba Mungu juu ya jambo hilo, mwanzoni ili kuwa ni sehemu ya maombi yangu kwa Mungu.

Mwaka 2020 niliendelea kupeleka ombi kwa Mungu juu ya hitaji langu kwake kama kawaida pasipo kuchoka

Mwaka 2021 maombi yaliendelea na mkakati wa kufanya maombi ulibadilika

Mwaka 2022 maombi yalibadilika yakawa kilio, badala ya kuomba nikawa namlilia Mungu

Mwaka 2023 jambo lile likawa kama deni kwa Mungu, nikaanza kusoma tena biblia namkumbusha Mungu juu ya shuhuda mbalimbali alizofanya juu ya watumishi wake , maombi ya mifungo yakaanza na kwa kweli maombi yalikuwa mengi

Mwaka 2024 nikaanza kuwasilikisha na baadhi ya marafiki zangu ili tuweze kuomba kwa pamoja juu ya jambo langu,maombi ya kufunga tatu kavu na mifungo mirefu kuanza

Mwaka 2024 ndio mwaka ambao maombi ya siku 40 nilianza kuomba kwa ajili ya Mungu kunikubuka juu ya ombi langu

Mwaka 2025 nguvu za maombi zilipungua imani kwa Mungu ilipata pancha kidogo kidogo nikaona kama Mungu amenisahau lakini sikujua yale ambao wengine wanaomba usiku kucha Mungu alinipa hata bila kuomba kwa kweli sikuona wema wa Mungu katika mengi zaidi ya lile moja ambalo sikupata

Mwaka 2026 Mungu alinifuta machozi akanijaria ombi langu la miaka 7, kwa kweli siku majibu yalipopatikana nilifurahi sana lakini sio sana hile ambayo labda nikapata mwaka 1 au 2 iliyopita, nilipopata nikajikuta sehemu kubwa ya uhusiano wangu na Mungu umepungua kiu yangu ikawa sio tena kile nilichopata kiu yangu ikawa juu ya uhusiano wangu na Mungu

Mara nyingi tunapokuwa tuna uhitaji tunapokuwa tunaomba kwa ajili ya uitaji wetu na inafika mahali katika kuomba badala ya kujenga uhusiano wetu na Mungu tunajenga uhusiano wetu na vitu ambavyo Mungu anatupa

Ibrahimu alipopewa Isaka akasahau uhusiano wake na Mungu, Mungu akamwomba Isaka, sio kwamba Mungu alimtaka isaka hapana Mungu alitaka Moyo wake Ibrahimu

Ni kweli tunamwitaji Mungu sana kujibu maombi yetu, lakini katika kumsubiri Mungu tusije kutenda dhambi.

Kuna mtu amasema kama Mungu hajajibu maombi yangu basi hakuna Mungu, ile Mungu kutokujibu ombi lako hakuondoi ukuu wake wa Uungu

Kumbuka ukiona maombi yako yanachelewa ujue pia ni mpango wa Mungu, Mungu hajawai luchelewa wala kuwai siku zote yuko ontime

Mungu anajibu maombi, ila ni kwa wakati wake sio kwa wakati wako sio kwa wakati wetu Mungu ni Mungu tu na hatabakia kuwa Mungu.
 
Kuna mtu amasema kama Mungu hajajibu maombi yangu basi hakuna Mungu, ile Mungu kutokujibu ombi lako hakuondoi ukuu wake wa Uungu
 
Ikiwa sipo hapa duniani
Mali zangu zote msimamizi mkuu ni mtume Boniface Mwamposa akishirikiana na
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom