Vita Kali ndani ya CHADEMA

Sisi tunazingatia mambo ya public interest, si mambo ya mtu binafsi. Mbona Clinton alikuwa fuska na aliongoza nchi ya Marekani vizuri kuliko hata Bush?
 
Kweli tuna kazi kubwa kufikia malengo ktk mchakato huu wa kima pambano ya kifikra. Mapambano yaliyojikita ktk kutazama upande mmoja tu kwa ukosoaji.

Dr Slaa ni mwanachama hapa JF kama alivyo Zitto, kwa mtaji huo basi Mh. Zitto nadhani itakuwa ni jambo la busara kama utawasiliana na bosi wako Slaa ili aje atimize wajibu wake kama mwana JF kuweka wazi haya masuala.

Kinachoonekana hapa ni kutolewa majibu myepesi kutoka kwenye maswali magumu kama kawaida yetu jambo lipohusu maadili ya viongozi wa upinzani hususan Chadema.

Labda niseme tu kuwa suala hapa sio source ya hiyo document, suala ni contents zilizomo ndani ya Doc, badala ya kujadili contents tuna mnashambulia alie leta hilo doc na wengine wana enda mbali na conclude kuwa ni njama za CCM. Mbona lilipoletwa Doc la BOT na la Maliasili yote (hayakuwa na source bayana) tulishabikia na kuanza kujadili na ndio imepelekea leo tuna "list of shame" Nani kati yetu ali hoji chanzo cha BOT Doc? Lakini ukirudi na kuangali kwa makini source zake ni hizi hizi za ki-anonymous na tupo willing kujadili kwa kina. Vipi leo hili la Slaa tunapatwa na kigugumizi?

Kwa mwendo huu soon JF tutakuwa/tushakuwa wasanii kuliko hao tuwao wapiga vita
 
Kweli tuna kazi kubwa kufikia malengo ktk mchakato huu wa kima pambano ya kifikra. Mapambano yaliyojikita ktk kutazama upande mmoja tu kwa ukosoaji.

Dr Slaa ni mwanachama hapa JF kama alivyo Zitto, kwa mtaji huo basi Mh. Zitto nadhani itakuwa ni jambo la busara kama utawasiliana na bosi wako Slaa ili aje atimize wajibu wake kama mwana JF kuweka wazi haya masuala.

Kinachoonekana hapa ni kutolewa majibu myepesi kutoka kwenye maswali magumu kama kawaida yetu jambo lipohusu maadili ya viongozi wa upinzani hususan Chadema.

Labda niseme tu kuwa suala hapa sio source ya hiyo document, suala ni contents zilizomo ndani ya Doc, badala ya kujadili contents tuna mnashambulia alie leta hilo doc na wengine wana enda mbali na conclude kuwa ni njama za CCM. Mbona lilipoletwa Doc la BOT na la Maliasili yote (hayakuwa na source bayana) tulishabikia na kuanza kujadili na ndio imepelekea leo tuna "list of shame" Nani kati yetu ali hoji chanzo cha BOT Doc? Lakini ukirudi na kuangali kwa makini source zake ni hizi hizi za ki-anonymous na tupo willing kujadili kwa kina. Vipi leo hili la Slaa tunapatwa na kigugumizi?

Kwa mwendo huu soon JF tutakuwa/tushakuwa wasanii kuliko hao tuwao wapiga vita


Masatu, heshima mbele.

Naomba unisahihishe uelewa wangu kuhusu hoja yako hapo juu...

Unasema tuzipe uzito sawa hii habari za maisha binafsi ya Dr Slaa kama zile tuhuma walizotoa dhidi ya BOT, Buzwagi na Maliasili.

Mhe Masatu kwa kutumia busara zako zote hivyo ndivyo unavyomaanisha kwa sababu tu (kwa mtazamo wako) vyanzo vya tuhuma hizi vinafanana?
 
Kwa mwendo huu hatufiki popote,labda muanzishe mada nyingine ya kujadili viongozi wetu.kwa tanzania mtu kuwa na vimada au watoto wa nje ya ndoa hayana nafasi ktk uongozi wa nchi.tukitaka iwehivyo basi hatutakuwa na kiongozi hata mmoja.hivi tukimjadili slaa na familia yake nchi itanufaika vipi au tunapeleka ujumbe gani kwa jamii,zaidi ya kuchekwa.
Naomba hii kitu ipelekwe kwenye udaku watu wakachangie huko ndio mahala pake.
 
Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwiiiii hahahahahhahhahahahhaaaaaaaaaaaaaaa!

WAKUU LEO NIMECHEKA SANA MAANA SIJAWAHI KULETA POSTY HAPA IKAPATA WACHANGIAJI WENGI NA KWA KASI YA KUTISHA KAMA HII. NAKUMBUKA KUNA MCHANGIAJI ALIWAHI KULALAMIKA HAPA KUWA KILA AKILETA MADA WATU HAWACHANGII! DUH SINA MBAVU HAKIKA INGEKUWA MADA KAMA ZINAZOLETWA HAPA ZA MAMBO YA UCHUMI NA NYINGINE AMBAZO WANACHANGIA WATU WACHACHE KAMA KICHUJUU, ES NA MKANDARA BASI TUNGEKUWA TUNATISHA SANA. POWA WAKUU ENDELEENI KUKATA ISSUE.
:rolleyes:

Mtoto wa mkulima. Michango ya JF katika hii post, ukiisoma vizuri utaona dhahiri kuwa haijadili maisha ya Dr.Slaa. Wajumbe wengi hapa wamepinga uchafu unaonezwa na CCM dhidi ya watanzania wanaotetea maslahi ya nchi (uchumi).

Wajumbe wanapinga huu uchafu unaonenezwa na CCM kwa ajili ya kuvunja nguvu za watanzania wanaotetea maslahi ya wanyonge. Sasa kama wewe unaona watu wanamjadili Dr.Slaa, hiyo ni haki yako ya kidemokrasia.

Kwa hivi, ukitaka kusema hii mada si ya kiuchumi, nashindwa kukuelewa. Mada za kiuchumi si lazima zilenge katika majadiliano ya ujenzi wa barabara, shule na zahanati.

Naomba kuwasilisha.
 
...hao Ze comedy wameshageuka TOT sasa,njaa na ujinga kitu kibaya sana na wamesahau washabiki wao wengi wao ni wale wanaozomea mafisadi na wadhulumiwa,umaarufu na pesa zao ni hao hao walalahoi wanaowashangilia na kulipa kuona show zao lakini leo wanajifanya ndio wasaidizi wa mafisadi...wamesahau watanzania wa leo sio miaka ile ya chama kushika hatamu na wameelimika,ngoja waanze kuzomewa nao ndio watatia akili
 
Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwi Kwi kwi kwi kwiiiii hahahahahhahhahahahhaaaaaaaaaaaaaaa!

WAKUU LEO NIMECHEKA SANA MAANA SIJAWAHI KULETA POSTY HAPA IKAPATA WACHANGIAJI WENGI
:rolleyes:

ahaaaa...

kumbe nia yako ni kupata wachangiaji wengi kwenye post yako..

nia sio kujadili yanayohusu taifa letu hapa JF, kwako nia ni kupata wachangiaji wengi!...

Ulivyocheka basi ikasaidia kwenye mkataba mbovu wa Buzwagi?
 
Hakuna kitu, mtu mwenye akili timamu atasoma hiyo message na kutupa,
Ni hao hao wajanja wachache wanaoiba pesa za watanzania kisha wanazitumia pesa hizo kuwadanganya na kufanya kampeni kama hiyo hapo juu,

Je mabilioni yanayopotea, Watanzania wanaokufa kila siku kwa magonjwa yanayoweza tibika ndio kusema ghalama yao ndio huo upuuzi hapo juu?
 
Ndugu zangu, kwanza nawapongeza kwa dhati wale wote waliojitokeza kupinga uchafu huu wa kutojibu hoja kwa kujibu kwa vioja. Ni lazima tuweke kanuni ambayo si rahisi kuivunja katika kujenga hoja amasivyo itakuwa ni yale kwa kiswahili tunayaita "kuzunguka mbuyu"!

Katika mapambano haya ya kifikra silaha zote zinaruhusiwa na zinakaribishwa, ni mapambano ambayo hatima yake ni ushindi wa utawala wa sheria, demokrasia, usawa, na nafasi sawa kwa watu wote katika Taifa letu. Kuna watu ambao hawako tayari kuona hilo linatokea ingawa mbele ya hadhara wanaimba pambio za sifa zake.

Na hii ni mojawapo ya sababu zinazotufanya wengine tuweke mbali kwa muda majina yetu ili tuweze kujenga hoja pasipo kuleta maisha yetu binafsi hadharani kwani tunafahamu kuwa watawala wakishindwa hoja wao huleta kejeli na tuhuma zisizo na msingi. Askofu Ncube wa Zimbabwe alipokuwa anapiga kelele sana dhidi ya utawala wa Zimbabwe, mashushushu wakamseti up na mke wa kiongozi mmoja wa kanisa na kumkuta katika "compromising position" (KLH Exclusive pictures ziko kule HAPA.

Na huko tunakokwenda tuhuma za nani alivaa nguo gani alipoenda kulala na nani alikula na nani na watoto wao walilala wapi zitaendelea kutolewa katika kuzima uzito wa hoja.

Jambo nashukuru ni kuwa wengi tumegundua kuwa yeyote aliyeleta hoja hizi ana kusudio la kuchafua mjadala. Kwa vile wao watawala wamekuja na huu mtindo kuwa wao wanaheshimu utawala wa sheria sana na ya kuwa mwenye kutoa tuhuma basi aende mahakamani, wakati umefika kama wanatuhuma za ubadhirifu au uvunjaji wa sheria uliofanywa na Dr. Slaa au kiongozi yoyote yule basi waende mahakamani! Si wao wanasema Mahakamani ndiko haki inawezekana kupatikana?

Vinginevyo, tutaendelea bila kutishwa, kubabaishwa, au kwa namna yoyote ile kufanywa duni katika kuzungumza mustakabali wa Taifa letu. Binafsi sina muda wa mambo binafsi ambayo hayahusiani na kazi na utumishi wa mtu na hayavunji sheria. Dito alipofumaniwa na mke wa mtu mbona alizawadiwa Ukuu wa Mkoa na hawakusema kuwa inamfanya mtu mbaya? Kwani Karamagi mke wake kamtoa wapi? .. mkijua hili wenzenu wanajua lile.. huo ni mfano tu..!!!

Siasa ni fani yangu na wakitaka kuleta mchezo mchafu, wajue kwamba binafsi sina mpinzani!!! Ukianza kuchezea matope kuwarushia wengine, na wewe yanakuchafua!
 
Kweli tuna kazi kubwa kufikia malengo ktk mchakato huu wa kima pambano ya kifikra. Mapambano yaliyojikita ktk kutazama upande mmoja tu kwa ukosoaji.

Dr Slaa ni mwanachama hapa JF kama alivyo Zitto, kwa mtaji huo basi Mh. Zitto nadhani itakuwa ni jambo la busara kama utawasiliana na bosi wako Slaa ili aje atimize wajibu wake kama mwana JF kuweka wazi haya masuala.

Hana wajibu huo na hana deni hilo! Hakuna mwana JF anayetakiwa kulazimishwa kuja hapa kusema lolote au kukatazwa kusema lolote!

Kinachoonekana hapa ni kutolewa majibu myepesi kutoka kwenye maswali magumu kama kawaida yetu jambo lipohusu maadili ya viongozi wa upinzani hususan Chadema.

Majibu mepesi ya hoja gani, na maswali magumu yapi, maana kilichoelezwa hapo siyo maswali ni "wasifu" wa mtu, sasa maswali yanatoka wapi, nani alilala na nani, na alipolala alivaa nguo gani ni maswali tunayotakiwa kujadili hapa? Fulani alishiriki katika mauaji ya fulani ni swali la msingi lakini si kuna vyombo vya usalama kwanini wasiende mahakamani kama wanavyowataka watu wengine wafanye zinapotolewa tuhuma za kiuhalifu?


[quoteLabda niseme tu kuwa suala hapa sio source ya hiyo document, suala ni contents zilizomo ndani ya Doc, badala ya kujadili contents tuna mnashambulia alie leta hilo doc na wengine wana enda mbali na conclude kuwa ni njama za CCM. Mbona lilipoletwa Doc la BOT na la Maliasili yote (hayakuwa na source bayana) tulishabikia na kuanza kujadili na ndio imepelekea leo tuna "list of shame" Nani kati yetu ali hoji chanzo cha BOT Doc? Lakini ukirudi na kuangali kwa makini source zake ni hizi hizi za ki-anonymous na tupo willing kujadili kwa kina. Vipi leo hili la Slaa tunapatwa na kigugumizi? [/quote]

Hakuna mtu mwenye kigugumizi! Wenye kigugumizi ni wale ambao wanagwaya kuzungumzia Buzwagi na Karamagi, Richmond na Dowans n.k na badala yake wanatutaka tuzungumzie maadili ya kitandani ya watu wenye akili zao timamu! Kama kuna mtu anatuhuma kuwa Dr. Slaa au kiongozi yoyote amebaka au kufanya kitendo cha kihalifu hiyo ni hoja inayojadilika na hakuna anayeogopwa! Lakini Fulani kala uroda mke wa fulani.. kweli mnataka tugeuze kibao hicho kwa CCM? au viongozi walioko madarakani?..

Kwa mwendo huu soon JF tutakuwa/tushakuwa wasanii kuliko hao tuwao wapiga vita

Hilo ndilo tatizo, nani kakuambia JF tuko hapa kupiga vita watu? Binafsi sina muda wa kupiga vita watu, lakini nitatumia hadi pumzi yangu ya mwisho kuliamsha taifa kuwakataa viongozi wasioweka maslahi ya Taifa mbele, wababaishaji, na ambao wako tayari kufanya lolote ili kung'ang'ania madarakani. Na hilo sina ninayempenda. Akiwa CCM nitawasema, akiwa Chadema, TLP, au CUF tutawasema na tutaonesha rangi zao halisi! Hata hivyo kama ni suala la nani amelalia kitanda cha nani wakati anakula nchi na kuchota mali ya umma, miye nitaangalia hilo kula mali ya umma kuliko kitanda alicholalia!
 
... binafsi sikuwa na chama chochote lakini kwa kuwa hapa forum kulikuwa na bias on one side, ... so they made me ccm since that day ....

Kada.....

Wanaccm hatuhitaji watu kama wewe kutuwakilisha hapa maana unaaibisa chama kwa arguments zako za kitoto....

ccm itakuwa bora kama wachache waovu wakitolewa kwa njia zinazofaa... huwezi kutetea kila kiovu ndani ya ccm na kisha unafurahia kujitangaza hapa kuwa wewe ni ccm.....

Hata mimi nimepingana na namna wapinzani walivyolichukulia suala la ufisadi wa watu wachache na kulifanya la wanaccm wote ila sitafikia hatua ya kulinganisha baadhi ya tuhuma zilizotajwa na hii email...

kama mulidhani kwa kutoa hii email mnaisadia ccm basi mjue maanzidi kkuaibisha chama.... endelea kutokuwa na chama.. utoto kama wa hii email ni chini ya wanaccm ambao baadhi yetu tuna heshima na tunajiheshimu!
 
Nyani.. its a long story... lakini imehusisha kuuma na kupuliza.. nadhani ukigoogle kidogo utapata story nzima.
 
Hii issue ya Slaa mbona ni old news!! its true that alipigwa chini upadri na its true kuwa alifumaniwa millenium hii but what ever the case ni kuwa amewasha moto sheli(petrol station) ya CCM na wanamtafuta and i feel sorry for their lousy strategies to frame him...chase those crazy baldheads CCM's...mwafrika wa kike dada nimekukubali, you have in your replies, Slaaa oyeee, Chadema oyeee, and down with Chama Cha Mafisadi
 
Nyani mbona yapo mengi kama ni kuongelea mambo ya wanawake? sema sisi hatutaki kuingia personal tu,

Tunaelewa kuhusu mke wa DC Mongela na ilivyokuwa.
Tunaelewa kuhusu Vicky Kamata pia (mtu mwingine sio Buzwagi).

Ila sio issue hizo kwetu. Issue ni Taifa jamani. Chonde chonde kuleni mbakizie vijukuu jamani, mali hata ukilimbikiza UTAKUFA na kuziacha zikiliwa na husiowapenda!
 
Nyani mbona yapo mengi kama ni kuongelea mambo ya wanawake? sema sisi hatutaki kuingia personal tu,

Tunaelewa kuhusu mke wa DC Mongela na ilivyokuwa.
Tunaelewa kuhusu Vicky Kamata pia (mtu mwingine sio Buzwagi).

Ila sio issue hizo kwetu. Issue ni Taifa jamani. Chonde chonde kuleni mbakizie vijukuu jamani, mali hata ukilimbikiza UTAKUFA na kuziacha zikiliwa na husiowapenda!

Nakubaliana na nyie wote kuwa mambo binafsi, yasiyo ya kihalifu, yasiyokiuka maadili na miiko ya kazi au nafasi ashikiliayo mtu katika jamii, yasiyohujumu uchumi au taifa kwa namna yoyote ile, katika haya mapambano ya kifikra, hayana nafasi hata kidogo.

Tuendelee kukata ishus....
 
Nyani mbona yapo mengi kama ni kuongelea mambo ya wanawake? sema sisi hatutaki kuingia personal tu,

Tunaelewa kuhusu mke wa DC Mongela na ilivyokuwa.
Tunaelewa kuhusu Vicky Kamata pia (mtu mwingine sio Buzwagi).

Ila sio issue hizo kwetu. Issue ni Taifa jamani. Chonde chonde kuleni mbakizie vijukuu jamani, mali hata ukilimbikiza UTAKUFA na kuziacha zikiliwa na husiowapenda!

Fikira Duni...

ingawa tumetofautiana nawe kabla lakini katika hili nakubaliana nawe kuwa mambo yakianza kwenda personal the main issue at stake hapa itapotea....

kuna mengi sana yanajulikana kuhusu wake, waume, na watoto wa watu... ila muda ukichukuliwa kuanza kuyajadili hayo ... iptl, buzwagi, kiwira, richmonduli,nk wataendelea kujichukulia mabilioni huku walala hoi wakifa kama nzi vijijini kwa kukosa madawa hospitalini!
 
Jamani tungepewa ushahidi ama wa vyeti vya watoto wanaodaiwa wa Slaa, ama hati ya nyumba ya Ujerumani, ama uhusika wa Slaa katika kifo cha mume wa mwanamama wa Ujerumani na mengine ya namna hiyo nadhani ingependeza zaidi, tungejadili kwa mapana na marefu sana.
Bila hivyo, habari hii itabaki kuwa ni hoax na propaganda za sisiemu kutaka kumchafua Slaa pasipo hoja zenye akili.
Kama Zitto upo mtandaoni tunaomba utupe ishu kidogo juu ya tuhuma hizi, kuwa huna uhusiano mzri na Slaa.
 
...Kama Zitto upo mtandaoni tunaomba utupe ishu kidogo juu ya tuhuma hizi, kuwa huna uhusiano mzri na Slaa.

Mtupori.... Zitto anafaa kupigania ili mikataba ya Bulyanhulu na Geita nayo ikapatikana na ikajadiliwa kama Mkjj alivyoshauri badala ya kurudia kujibu ambacho ameshajibu hapa tayari....

Nia ya walioanzisha hii mada ni kuwatoa watu kwenye point ya kusikiliza muziki wa Richmonduli uliowekwa hapa jana na wakuu ili wasikilize kelele za TOT ...

wameshachemsha maana hii kitu imebackfire big time..
 
we Kicha maji, hii kitu mbona iko kwenye thred ya Eid,
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=6150&page=6[/QUOTE]

Hata kama imetoka wapi, 'busara' zako zilipaswa kukusaidia kutambua 'nia mbaya' iliyomo; ungepima uzito wa hoja na kuona mahali inakofaa kupelekwa. Wewe umeona ni veme uilete hapa kulisha watu 'sumu ya kina Rostam!' Ndiyo maana wanaoelewa mambo yanayofanyika gizani wamefanya haraka kukuuliza kama 'umetumwa,' maana wameshatumwa wengi kabla yako, lakini wametumia hekima pevu. Si ajabu hao waliokuuliza ndio wanaojua vema asili ya 'sumu' hiyo. Haya mashambulizi unayopata hapa yanaonyesha kwamba kama ungekuwa barabarani ungezomewa kama mawaziri wa Kikwete. Wewe unzomewa halafu unashangilia kwamba wachangiaji wamekuwa wengi? Wassira alipozomewa akasema ameshangiliwa! Kumbe wewe unaweza kuokota chochote kuleta hapa? Labda umejifunza.
 
Back
Top Bottom