Vita Kali ndani ya CHADEMA

Vita Kali ndani ya CHADEMA

Wana JF,

Nimesoma majibu ya wanajambo kwa hoja iliyotolewa kuhusiana na uzushi wa maisha ya Dkt. Slaa. Mimi binafsi nilijua haya masuala ya uzushi yatatokea kwani ndio umekua utamaduni wetu kisiasa hapa tanzania. Yalitokea kwa Kambona, Bibi Titi na baade akina Mrema. Slaa, Zitto, Mbowe, Mnyika etc hawatapona katika siasa hizi za kipuuzi kabisa.

Mambo haya yaliyoandikwa juu ya Dr. Slaa ni uzushi ambao hata haiingilii akilini kwa mtu mwenye akili kuanza kujibu. Unajibu nini jamani?

Sisi CHADEMA tunaongoza kama timu. Hatuna la kuoneana kijicho kuhusiana na umaarufu wa yeyote. Kazi ambazo viongozi wetu wanafanya ni kwa niaba ya nchi na ili kuiweka nchi yetu pazuri tunaimarisha chama chetu.

Dkt. Slaa aliacha Upadre kwa taratibu zote za kanisa katoliki na kupewa kibali kutoka Vatican. Wanaosema kafukuzwa, kirahisi tu hawajui wasemacho.

Dkt. Slaa mpaka hapa tunapozungumza ni mjumbe wa bodi ya Tanzania League of the Blind. Pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya CCBRT. Kama aliiba huko angekuwa amefukuzwa!

Mimi ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, mahusiano ya Dkt. Slaa na Lazaro Masay ni mzuri mno na hakuna dalili zozote ati kuwa Dkt. Slaa kachukua mkewe nk.

Ninavyojua mimi Dkt. Slaa hana ambition za Urais. Honest person doing his work. Mbona watu wanaweweseka sana na Urais ujao? Maana kitu hii inazuka sana, mtu akifanya kazi yake, anataka Urais........ mchecheto huu ni wa nini?

Mimi nadhani tuangalie masuala ya msingi zaidi yanayohusu nchi yetu..... Ufisadi unamong'onyoa taifa letu. Juhudi za kuchafua viongozi wa upinzani haziaidii kuliendeleza taifa letu
 
Mkuu Zitto shukurani kwa kuja na kuweka hapa issue. Ni kweli wana JF wengi walijua huu ni mchezo wa kucahfuana tuu. Kazeni but kupambana na ufisadi kwa maendeleo ya taifa letu. Nimesoma maelezo ya Mwinyi kwenye siku ya Nyerere anasema suala la ruswa na ufisadi halina chama hili ni swala la kitaifa kwa masilahi ya Taifa.
 
Ngoja kwanza nianze na wewe Mtoto wa Mkulima, ulianza kwa kusema umetumiwa kwenye mail, lakini post yako ya mwisho unayojifanya kucheka saaaana, jinsi watu wanavyojadili inanitia mashaka.

Kwamba, huenda habari hizi hujatumiwa kwenye mail kama unavyodai, either kuna mtu amekuinfluence kuyaleta au wewe mwenyewe una lako jambo!

Tukienda kwenye hoja yenyewe,
Kuna hoja saba ninazoziona pale,
1. Hana nyumba Karatu, analala kwa rafiki yake, Hapa
wanataka kutuambia kuwa kutojenga nyumba jimboni ni dhambi?"ingawa hatuna uhakika kama kweli hana nyumba" Kosa lake nini! kutojenga nyumba au kulala kwa rafiki yake? Siwaelewi hapa.

2. Kuoa: Unamkumbuka yule askofu wa Zambia? Hili huwa ni jambo linaloisumbua Kanisa la RC siku zote. Paulo anasema kama huwezi kukaa kama mimi basi kaoe, ndo maana aliamua kutoka kwenye Upadre akaamua kuwa muumini wa kawaida baada ya kuona kuwa karama ya useja imemshinda. Kiserikali, Hata Clinton hakuondolewa kwenye uraisi baada ya kufumaniwa akiwa na Monica Lewinsk tena ikulu.

Kama mtu ana marafiki wa kike wengi lakini anachapa kazi yenye tija kitaifa, Anafaa kutuongoza. Hukuwahi kusikia tuhuma kuwa hata Kikwete kabla hajawa Rais alikuwa na mademu wengi sinza na mpaka kibaha huko? Lakini hatumuhukumu kwa hilo, kama kuna tatizo ni hili la kushindwa kuleta Maisha Bora aliyoahidi, na badala yake kupaisha uchumi wao peke yao watawala.

3. Ugonjwa mkubwa, ndo ugonjwa gani huo? Kuumwa ni Tuhuma inayotaka jibu?

4. Kama alikula pesa za Vilema, ashtakiwe, polisi wako wapi?
5. Ana mpango wa kuhamia ujerumani: Hapa mnajichanganya ndugu zangu; Unasema ana mpango wa kugombea uraisi kitu kinachowaogofya kina Mbowe eti na Zito{na zito anataka upresida?}, utamwogopaje mtu ambaye karibu ataihama nchi? Atatawala nchi kutokea Ujerumani?

6.Usalama wa Taifa, Hebu nielewesheni vizuri, kama mtu ni mwajiriwa wa usalama wa Taifa, akipewa malipo anapangiwa na Matumizi? Matumizi wanayoruhusiwa kufanya watu wa usalama wa Taifa ni yapi?

7. Ana nyaraka za Kughushi; Hapa watoa shutuma ndo mmechemsha kabisa, Mkataba wa Buzwagi mlibahatika kuuona ni wa kughushi ule? Nani kakanusha kuwa huo mkataba si wenyewe! Ulisikia hata mmoja akitoa sauti? Kama ni hivyo kwa nini una mashaka na nyaraka zingine alizo nazo? Kama kaghushi kina karamagi wameshindwa nini kufungua kesi mpaka leo?

Mara nyingi mtuhumiwa anapaswa kutoa majibu kwa mtu fulani aliyemtuhumu, Sasa basi ni mtu yupi huyo aliyetoa hizi Tuhuma? Ajitokeze ili Hata mtuhumiwa mwenyewe Slaa ajue anamjibu nani kwa wale wanaotaka aseme mwenyewe!

Naomba kutoa Hoja!
 
Tumeshaona mengi humu JF. Mambo yakiwa mazito serikali inatuma watu wake kuja ku divert attention. Tumewaona akina Tafiti, Mvumbuzi ambao wanakuja kwa sababu maalumu wakimaliza kazi yao wanapotea. Sasa upuuzi kama huu kwa mtu mwenye akili zake unategemea aamini. Kama hizo data walikuwa nazo CCM wangezitumia kumnyang'anya ubunge? Wasituletee za kuleta hapa.
 
Inasikitisha sana kuona Watanzania sasa wanaamua kutumia ufuska kama silaha ya kuwaangamiza watu wenye akili,wazalendo.Mbona Viongozi kibao ni mafuska,wanajaza watoto kibao Dodoma wanapohudhuria vikao vya Bunge?Kuna watoto wa wabunge kila kona ya mji wa Dodoma,na wabunge karibu wote wana nyumba ndogo si chini ya mbili.........Mimi naona ufuska ni maisha binafsi ya mtu,wala hatitakiwi kujua kwa sababu haitusaidii.
Pia kama mtu ni fuska,ekesha anatekeleza wajibu wake,hiyo sisi tusijali,kwani tunapoteza muda kujadili mambo hayana msingi,ufuska ni wa kwake,sisi inatuhusu nini?Mwacheni azidi kufichua wazandiki na mafisadi,ufuska wake tuiachie familia yake.

Hizi tuhuma za Mauaji ni utumbo mtupu,mtu hawezi kuua akaachwa hata siku moja,walau tungesikia kesi,ikarindima mahakamani,akaachiwa huru kwa kukosa vithibitisho,hatujawahi kusikia hilo.Kwa hiyo huu ni uwongo mweupe,tena mweupe pe!!!

Hao watu wanaojiita mapadri,wote ni mafuska,nani kakwambieni kwamba mwanaume rijali anaweza kukaa mwaka bila ......a?Hiyo kitu haipo,ndo maana wale wanaokosa kabisa wanaamua hata kubaka,mshasikia mapadri wengine hata wanawalawiti watoto,hakuna upadri wala nini,tunadanganyana...Hiyo ndo tabia ya mapadri.Ila kuthibitisha ndo inakuwa ngumu.Sote tunajua padri aliyejifanya mdhamini wa binti mmoja kule Arusha,matokeo yake akawa anafanya mapenzi na binti wa watu,baadaye akamjaza mimba,akampeleka kwenye hospitali mbovu kumtoa mimba,matokeo yake akafa.....na acha ajabu ma padre wenzake walimficha kwenye nyumba za parokia,huu ndo upadri?

Kwa hiyo kwa mapadri kuwa na mahawara ni jambo ambalo tunalijua na hatuna haja ya kuletewa huu utumbo,eti Dr.Slaa alikuwa na hawara...hiyo ni kawaida.

Kwa hiyo the whole story is dismissed liminely!!!!
 
1.Kweli kaka, lakini ajibu mwenyewe wewe nani? wewe ni Katibu Mutasi/mwenezi wake? Hivi si ninyi mlizaja JF kuwajadili akina marehemu na Suzy,,, seuse huyo kiongozi mtukuka wa Chama kitakatifu... waliosikiliza hotuba za nyerere kipindi hiki cha maadhimisho ya kifo chacke aligusia ufuska,,, at mpaka wa kunyang'anya watu wake zao?

2.TUHUMA za kula fedha za walemavu nazo ni personal,


3.Waleteni wajibu wenyewe, acheni unazi hapa,,, hamuisaini nchi,,, inaonyesha mnapenda madaraka kama CCM tu,,, nilidhani ninyi wazuri lakini naanza kuwa na masharaka..,


sasa kama ulitaka ajibu mwenyewe kwa nini umeileta hapa? huna namba yake ya simu, au mawasiliano. tuna haki ya kureason out profoundly and come with the initial decison.

Pia Kada mpinzani anasema tusubiri tu tutaona yakitokea. kwamba the future will tell, sasa kama anaamini kuwa tusubiri future, kwa nini ameleta hii thread sasa hivi. kwa nini hakusubiri future ikatell. yes the future will tell that all spoken over him were allegations.
 
Pamoja na kumshukur Mh. Zitto kwa maelezo yake safi dhidi ya madai haya ya kipuuzi ambayo yana kila dalili za mchezo mchafu wa CCM, mie ningependa kuongezea kwa yafuatayo:

1: Hata kama kuna mgongano au husuda ndani ya Chadema, hayo hayawezi kulinganishwa na mgongano na chuki iliyopo wazi ndani ya CCM kiasi cha kusababisha baadhi ya watu walioshikilia uongozi wa juu wa kiutendaji ndani ya chama hicho kutupwa na kuonekana hawafai. Hapa nazungumzia kuanguka au kuangushwa kisiasa kwa Bw. Mangula ambaye alikuwa mtendani mkuu wa chama hiki cha Mafisadi lakini hii leo anaonekana hafai hata kuwa mjumbe wa NEC. Nani atasahau kampeni za chuki za wanamtandao dhidi ya Dr. Salim Ahmed Salim katika kinyang'anyiro cha urais in 2005? Kama ni chuki za kisiasa, CCM ndio chimbuko lake.

2: Hata kama Dr. Slaa anakabiliwa na kashfa zote hizo dhidi ya character yake, kwamba yeye aliasi kanisa katiloki, kwamba anachukulia watu wake zao, swala hilo haliwezi kubadilisha ukweli kwamba amekua jasiri na hajawaasi wananchi wa Tanzania ilipokuja suala la kuanika uozo na ufisadi unaofanywa na viongozi wa CCM na serikali yake kwa wananchi wa Tanzania. Tuhuma za ufisadi bado zipo palepale na inabidi zijibiwe sio kwa kujaribu kumchafua Dr. Slaa, bali kwa kufanya uchunguzi wa kina na kuwashtaki wale wote waliohusika wakianziwa na Mkapa, Mama Mkapa, Bilali na wengine wote.
 
Mapambano ya kifikira, kiitikadi na Uchumi yanahitaji Dhamira ya Uhakika,malengo na mikakati thabiti na endelevu ili kufikia Ushindi na Mafanikio.
 
Kama taarifa hizi tungezipata kabla Dr Slaa hajaweka bayana juu ya UFISADI ambao sisi wananchi ndiyo waathirika wakubwa kwa kiasi fulani ningeweza kudanganyika lakini kwa kuwa baada ya nyati kujeruhiwa huparamia hata miti ninadharau asilimia 100%.

Aliyoyasema Dr Slaa ni kwa maslahi ya taifa lakini vijituhuma hivyo shauri yake yeye maana kuna sheria akishikwa ugoni sheria zipo. Kashfa nyingine hazina msingi kabisa kuhusu kufumaniwa au kufanya ngono, Checkbob Ditopile aliwahi kufanya ufuska na mke wa mtu na akatamka bayana kwamba mwanamke mwenyewe alijipendekeza, na hakuna lolote lililotokea zaidi ya kuandikwa magazetini naye kushabikia.

Waziri Masilingi na ile kashfa ya changudoa wakati yeye ni waziri wa mambo ya katiba na utawala bora, tulitegemea angevuliwa madaraka yake kinyume chake akazidi kupewa majukumu zaidi, kwa ujumla kuhusu hilo kwetu sisi Watanzania ni wachache sana wako katika usafi wa kweli. Wabunge wengi wawapo Dodoma pamoja na kukaa vitini na kupata usingizi wa pono wakishatoka humo kwenye jengo kazi yao kubwa ni hiyo hiyo.

Mama Terry kama tunamkumbuka aliwahi kuhoji kuhusu tabia ya wabunge kuendekeza ngono na machangudoa wa OHIO. Aliitwa pale Dodoma kujieleza yule mama hadi leo alimeza sponchi sauti yake haisikiki tena hadi leo kilichotaka kumpata anakijua yeye mwenyewe. Tujaribu kuangalia kati ya tuhuma za Dr Slaa dhidi ya mafisadi na hizi za ufuska wake zipi zina uzito.

Tatizo lililopo hapa kama tungepiga kura kwa swali hili mafisadi wengi watampinga Dr Slaa kwa kisingizio anaweza kulala na wake zao, lakini wake za hao mafisadi kwa kuwa wanajiamini watapiga kura kulaani ufisadi wa waume za aliouanika Dr Slaa dhidi ya hao mafisadi, Watanzania amkeni piganieni suala la msingi hayo ya Dr Slaa ni CHANGA LA MACHO HILO.
 
Huyu Mtoto wa Mkulima ameileta humu katika JF ili aone watu tusivyo wanafiki kwa maslahi ya taifa.
Huyu Dr Thlaa siyo Slaa alikuwa Padre sawa baadaye akaoa lakini je baada ya kuoa aliishi wapi na Mkewe? Maana unasema hana nyumba kule Karatu HAPO UMEDANGANYA
Kutokana na kudanganya hili nina hakika WEWE AGENT WA MAFISADI
JAMBOFORUM NI KWA AJILI YA WANAJAMII WAADILIFU WASIOSEMA KWA KUJIPENDEKEZA KAMA WEWE
 
Tumewaona akina Tafiti,


1. Jamaaa finally nimefahamishwa rasmi kuwa ni mjomba/mpwa wa RO, kwa nikaelewa kumbe ndio maana 2+2=4,

2. kuhusu hiii habari ya Slaaa nilifahamishwa toka juzi kuwa ipo mahali lakini sikuamini, mpaka nilipoiona leo hapa JF, anyway bado ninai-diggest kabla sijatoa kauli yangu, na pia ninataka kugusa base ili kujua ukweli uko wapi na pumba zilipo, na inahusika vipi na taifa kwa ujumla,

Ni jana tu nilikutana na mtu anyemjua sana Dr. Slaa, akanifahamisha kuwa mkuu ana degree tatu, ikiwa ni pamoja na PHD, na jinsi alivyo na kichwa kizima, na jinsi Karamagi anavyoogopa kwenda naye mahakamani, maana hiyo bongo nzima inaeleweka kuwa haitakuja tokea,

Anyway, siasa ni mchezo mchafu sana, unaochezwa na watu wachache wachafu, hoja hujibiwa kwa hoja, ni vyema tukachambua ukweli uko wapi na pumba ziko wapi, tukijibu kirahisi rahisi tutawapa wenye nia mbaya na taifa njia ya kutushusha wote kwenye level yao kama ambavyo tayari nimeanza kuona kwenye hii ishu, hakuna haraka, pole pole tutazipata zote mchele na pumba zilizpo, na tutajua ni nani yuko behind hii kitu, kama ni kweli au uongo,

Isipokuwa tu one thing sihitaji kutafuta ukweli wake, kwamba eti hii habari imetengenezwa na Freeman, that is pure NONESENSE, Zitto simfahamu vizuri, lakini I know Free, NO WAY anaweza kupika this NONESENSE,

Halafu another thing, hiii inafanana sana na zile za Salim na uarabu na uhizbu, na Sumaye na rushwa, I mean it is very close, anyway tuta-dig mpaka tujue FACTS na PUMBA.

Ahsante Wakuu!
 
hivi ni wapi vile katika hiyo makala or whatever inasema ni ccm ndio wameandika ? kama hamna, then shut your computers people ! acheni kuongea vitu msivyoweka kuproove. endeleeni na kampeni zenu kuipaka mavi ccm !

kuhusu list ya mafisadi ( slaa akiwemo namba 12 ) nakubaliana nayo, lakini mnapata wapi hii mentality ya mtu anapokosoa wapinzani mnamuita ccm ?? sielewi bado hii kitu !

kada, heshima mkuu,
unasahau upande wa pili wa coin! mtu anapokuwa against(anapokosoa) CCM, anaitwa mpinzani(katumwa na).

Hapa inamaanisha kuna makundi mawili
CCM na UPINZANI, hivyo unapokuwa against na one group automatically utakuwa the opposite group, japokuwa not necessary to be true.
 
Waheshmiwa,

Ninaomba tukijadili hili tuweke pembeni vitu ambavyo ni personal, tu concetrate kwenye kujadili taifa.

Hilo tu
 
Hivi wanaposema Doc. amekula pesa za walemavu wanataka kutuambia nini? Wapuuzi hawa wanafikiri JF hatuna akili. Mapesa wanayoyala kila siku mchanamchana bila hata kujificha tena mabilioni ya TZShs. Kweli SISIEM wameshatudharau sana waTZ!!! Doc. anajaribu kuongelea maslahi ya Taifa wao wanatuletea story za primary school. Nafikiri Mtoto wa Mkulima na Kilitime wametumwa kama akina Tafiti, Mvumbuzi, Mgongo x 2 au wanatoka kwenye familia hizohizo za MAFISADI!!!!
 
Hivi wanaposema Doc. amekula pesa za walemavu wanataka kutuambia nini? Wapuuzi hawa wanafikiri JF hatuna akili. Mapesa wanayoyala kila siku mchanamchana bila hata kujificha tena mabilioni ya TZShs. Kweli SISIEM wameshatudharau sana waTZ!!! Doc. anajaribu kuongelea maslahi ya Taifa wao wanatuletea story za primary school. Nafikiri Mtoto wa Mkulima na Kilitime wametumwa kama akina Tafiti, Mvumbuzi, Mgongo x 2 au wanatoka kwenye familia hizohizo za MAFISADI!!!!

Kweli wewe Mr. Zero unafikiria kila mtu ni mtu wa kutumwa? Mwkjj, FES wanasema walishaiona hii issue au kuisikia toka jana. Issue ipo inazunguka kwa mitandao watu tumeinasa tumeileta hapa. Toa poinnt nyingine za msingi kwani sikueleza iko kwa e mail? Mkjj hakusema aliiona jana kwenye thread ya Eidi?
 
watu hapa wanataka asubuhi, mchana na jioni zijae threads za bot, muungwana, ccm, ra, el, nchimbi, mafisadi, na vinginevyo, SAWA HATUPINGI ! LAKINI inakuwaje zinapokuja thread kama hizi watu mnachonga sana ? yaani hamuoni tu forum ilivyo bias kwa kubase upande mmoja ? sina maana ya kusema mengi wakuu, lakini hapa kila mtu ana akili timamu hivyo nadhani mtaelewa !

just take this issue lightly and you'll overcome it people ! ilikuja thread ya mbowe kutafuna pesa, ikanisababisha nifungiwe, sasa imekuja hii tena naona longlongo kibaoooooo. vipi wanachama ?

tukateni ishu, wapinzani ipo siku watashika madarakani ( angalau sio hivi karibuni ) hivyo lazima tuanze kuwaangalia mafisadi wa ccm na wa upinzani vile vile, lakini watu wameng'ang'ania ccm weee utafikiri ccm watatawala milele ! damn.... people.

kama tunadhani ipo siku wapinzani watashika madaraka ( which they have alreadystarted ) basi sioni baya lolote kuwazungumzia, lakini kama mtaongelea ccm tu peke yake, thats not fair ! ndio maana ya kuwa politician, acha watu wakujadili binafsi na sera zako, kama hamtaki tuwaongelee hawa watu nashauri they need a career change au vyama vya upinzani vibadirishwe vile vilabu vya soka !


Kada na Mtoto wa Mkulima,

Mna akili za kitoto, hivyo pelekeni utoto wenu mahali pake, siyo hapa. Watu wanaoweza kufikiri vizuri wanajua mnakotaka kutuelekezana kutuondoa kwenye hoja za msingi. Hata kama mmeuokota uchafu huu jalalani, nlidhani hili ni dampo linalofaa kwa uchafu huu? Mnatarajia tuwaamini? Hivi mnadhani Watanzania hawajui mbinu chafu zinazofanywa na wahusika kutuondoa kwenye mjadala wa kitaifa? Yote haya yanaonyesha utoto wa wapika majungu na wanapropaganda wa ccm, na wenao wanaookota lolote na kusambaza (kama hawa ulionao hapa).

Nimeanza kuamini baadhi yenu humu ni wauaji kabisa, kama hamtambui uzito wa hoja za Dr. Slaa, nan mnabaki kuona kwamba njia pekee ya kuzikabili ni kujadili udhaifu wake...Hata kama tungependa kumjadili Dr. Slaa, hatufanyi hivyo hadi tumalizane na hoja ya msingi. Ni utoto pia kufikiri Dr. Slaa anatoao tuhuma ili apate urais, na kwamba anawakera kina Mbowe na Zitto. Hii ni thinking ya aina Rostam na Lowassa na mashoga wao...naona na baadhi yenu mmeamua kuwa kwenye kundi hilo.

Mnapoteza muda, Watanzania waleo hawadanganyiki kirahisi.
 
kada, heshima mkuu,
unasahau upande wa pili wa coin! mtu anapokuwa against(anapokosoa) CCM, anaitwa mpinzani(katumwa na).

Hapa inamaanisha kuna makundi mawili
CCM na UPINZANI, hivyo unapokuwa against na one group automatically utakuwa the opposite group, japokuwa not necessary to be true.

Kasana,

Baadhi yetu hatuandiki kwa kuwa vitu vimebandikwa hapa, bali kwa sababu tunaishi na hao wanaoyatunga haya, tunajua mipango yao, na tunshangaa inevuja mpaka hapa. Watu wasiojua kinachoendelea, wanaosubiri kuletewa na kusoma hapa ndio wanaodakia na kupokea na kukubali kila lnalorushwa hapa. Tanzania imeharibika mno, maana walio na madaraka wanafanya mambo ya kihuni na ya kitoto, ambayo kwa mujibu wa vyeo walivyo navyo hawapaswi kujihusisha nayo. Bahati mbaya ndio hao waheshimiwa na watukufu wetu...

Tunasema hivyo kwa kuwa tunajua propaganda zao na sasa tumechoshwa nazo. Hatuandiki hapa ktafuta umaarufu au kuonewa huruma na mtu bali kusafisha takataka katika akili za Watanzania zilizochafuliwa kwa muda mrefu, na zilizovamiwa kwa kasi ya ajabu sasa, hasa zile za watu wasio kuwa informed! kama na wewe ni mmojawapo, kanzia leo anza maisha mapya ya kujua kinachoendelea nchini mwetu bila kusubiri kujulishwa hapa JF forum.
 
Tuhuma alizozimwaga hadharani Slaa na timu yake ziliwatoa machozi wale wote wenye mapenzi mema na nchi yao.

Katika tuhuma hizo hakugusa maisha binafsi ya yeyote katika ile 'list of shame' Huku ndio kukomaa kisiasa na dalili za uungwana. Sasa Mtanzania gani mzalendo atatoa machozi eti kwa kuwa Slaa aliacha Upadre na kuoa?alifumaniwa? au ujinga mwingine uliotajwa? HAKUNA,kwa sababu hayo Sio sababu ya kukosa kwake maisha bora anayopaswa kuyapata.

Njama hizi za kuchafuana kwa kulenga maisha binafsi ndio zile za kimtandaotandao. Salim anazijua,Sumaye anazijua na ndio maana aliapa pale Airport kuwa safari hii hatakubali kuchafuliwa kijinga tena (atafanyaje na yeye si hatujui). Funzo ni kuwa hawa jamaa wamezoea mbinu chafu katika kufunika mambo ya msingi yasijadiliwe. Hata hivyo sasa basi. Slaa awe vyovyote vile,wao wanapaswa watujibu yale maswali yetu (maana sio ya Slaa pekee) na wahusika wawajibishwe kulingana na sheria.

Keki hii TANZANIA ni ya wote sio wachache,lazima tuigawane kwa uwiano unaostahili kwa kila mtu. Na ujingaujinga sasa hatutaki vinginevyo huu uungwana wetu utafikia mwisho.
 
Back
Top Bottom