Visiwa na nchi zinazopakana na bahari zaingiwa na taharuki baada ya Japan kumwaga majitaka yenye sumu ya nyuklia baharini

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111451285478.jpg


Hivi majuzi Japan ilianza kuyaachilia maji taka yanayotoka kwenye kituo cha nyuklia cha Fukushima na kuyamwaga kwenye baharini ya Pasifiki, licha ya kwamba nchi zake nyingi jirani zilionesha wasiwasi mkubwa juu ya hatua hii, na hata kupinga kitendo hicho. Japan inadai kwamba eti maji haya yametibiwa na kisayansi hayana matatizo kwa viumbe vya baharini endapo yatamwagwa, lakini hakuna uhakika wa mia kwa mia kwamba hayataleta madhara kwa afya za watu na viumbe wa baharini.

Tetemeko la ardhi na tsunami mbaya la mwaka 2011 lililotokea nchini Japan lilisababisha maji ndani ya kinu cha nyuklia cha Fukushima kuchafuliwa na vitu vyenye mionzi mingi. Tangu wakati huo, maji mapya yamekuwa yakiingizwa ndani ili kupoza uchafu wa mafuta kwenye mitambo, huku maji ya ardhini na ya mvua yakivuja na kuingia ndani na kusababisha maji machafu yenye mionzi zaidi.

Hii ni hatari kubwa sana kwa nchi jirani za Japan na hata nchi nyingine duniani hasa nchi za visiwa na zile zinazopakana na bahari. Kwa sisi watu ambao tunatoka visiwani, na kutegemea kwa kiasi kikubwa uchumi wa buluu, ndio tunaopata uchungu mkubwa na kujua madhara ya kitendo kama hiki. Kama kweli maji haya yametibiwa na hayana madhara, Je, kwanini wasitafute njia mbadala ya kumwaga maji haya humohumo ndani ya Japan, badala ya kumwaga baharini na kuzifanya nchi nyingi kuwa na taharuki? Hili ni suala ambalo lilihitaji mashauriano ya kina kabla ya utekelezaji wake.

Kwa mawazo yangu naona ingekuwa bora kama wangetafuta maeneo maalumu humohumo nchini Japan, kama vile mashamba na kumwaga maji haya, ama kama wanataka kumwaga baharini basi angalau wangeunda tume inayoshirikisha nchi jirani na kushauriana kwa pamoja nini cha kufanya, na sio tu kutoa uamuzi wa upande mmoja kwenye suala kubwa kama hili ambalo litaathiri nchi nyingi zaidi.

Tunafahamu kuwa bahari ina mawimbi, na mawimbi yanatembea na kufika mbali sana, wasiwasi wetu mkubwa ni kwamba maji taka haya yakifika hadi kwenye bahari ya Hindi mathalan kufika hadi kwenye bahari inayozunguka Visiwa vya Zanzibar, itakuwa maafa makubwa kwani uchumi wa Zanzibar unategemea zaidi bahari kuliko chochote kile. Kwa maana hiyo hii itakuwa ni sawa na kulemeza visiwa hivi katika kipindi ambacho nchi nyingi duniani zinaungana ili kupata maendeleo ya pamoja.

Kwa Zanzibar uchumi wa Buluu ama uchumi wa bahari unafungamanisha kwa pamoja na sekta za uvuvi, ufugaji samaki, ujenzi wa viwanda vya samaki, ukulima wa mwani, uchimbaji wa mafuta na gesi, matumizi bora ya rasilimali mbali mbali za bahari pamoja na shughuli za utalii wa fukwe na michezo ya baharini. Vyote hivi vinategemea bahari, sasa swali ni kwamba kama maji haya yenye sumu yatafika huku, visiwa hivi vitafanya nini?

Mwezi Julai mwaka huu, Shirika la Umoja wa Mataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) baada ya kukaa na kujadiliana lilitoa hitimisho kuwa mpango wa Japan unaendana na viwango vya usalama vya kimataifa na hautakuwa na "athari za mionzi kwa watu na mazingira". Lakini hata hivyo wataalam wamegawanyika juu ya hatari inayotokana na umwagaji maji taka baharini wa Japan.

Wanasayansi wana wasiwasi kwamba kuzimua maji taka kunaweza kudhuru viumbe vya baharini, na pia vichafuzi vinaweza kujilimbikiza katika mfumo wa ikolojia ambao tayari ni dhaifu. Wengine wanahoji kuwa bado hakuna tafiti au takwimu za kutosha kuhusu athari za muda mrefu za kibaolojia zinazohusu “mionzi ya tritium”. Kitaalamu mionzi hii ya tritium haiwezi kuondolewa kwenye maji taka yaliyochafuliwa na vitu vya kemikali za nyuklia, hivyo wananchi wa kawaida wanaotumia bahari bila shaka watakuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wa maisha yao na afya zao.

Kwa Zanzibar kina mama wengi wanaoishi shamba zenye pwani, wanapenda kujishughulisha na kilimo cha mwani wa baharini, na kazi hii inawapatia mapato ya kuweza kujikimu kimaisha. Hivyo tatizo kama hili la kumwaga maji taka bahari linapoibuka, wamama hawa watakuwa na hofu ya kuendesha shughuli zao, achilia mbali wavuvi wanaokwenda dago kwa ajili ya shughuli zao za uvuvi.

Zoezi la umwagaji maji taka baharini linaendelea kwa siku 17, hii inaashiria kwamba maji yanayomwagwa ni mengi sana na yatafika mbali sana, hivyo mashirika ya kimataifa hayana haja ya kuionea haya Japan, ni wakati wa kuwa wawazi na wakweli juu ya suala hili, kwani hii si athari ya nchi jirani za Japan na nchi za visiwa tu, bali endapo suala hili litakuwa janga basi litakuwa ni janga la dunia.
 
Japan anajifanya mtambe asikilizi lolote hadi marafiki zake wamemkataa ni mwendo wa kumtandika sanctions ale peke yake hizo bidhaa za bahari.

Wananchi wanapinga huo upuuzi wake ndani ya nchi yake na majirani zake ila serikali yao inajizima data
 
Inasemekana hayo maji yamesafishwa kabla ya kumwagwa, isitoshe ni zoezi litakaloendelea miaka mingi ijayo maana yanamwagwa kidogo kidogo.
Mwanangu hayo maji bado sio safe maana kuna habari niliona wanasayansi wengi wa Japan wanapinga huo upuuzi wa serikali yao na Fukushima plant kurelease sasa wakati bado yanahitaji kuendelea kutibiwa.

Maana hata wananchi wa Japan, Korea, India, visiwa vidogo dogo navyo vinapinga huo uamuzi wa Japan
 
ukisikia dunia nzima wanakuwa na kansa chanzo ni huu upuuzi,kuchafua maji ni kuiangamiza dunia kwa maji ni uhai
 
Back
Top Bottom