Nakumbuka kipindi nasoma high school shule moja maarufu Sana tabora tulimiliki simu karibia wanafunzi wote wa darasani kwangu, miaka iyo form 5 nilifanikiwa kupata pisi Kali ya chuo furani pale tbr..
ikawa inakuja kunitembelea kila day na nilikuwa najitapa Sana kumiliki chombo Kali wajuba wa class wakawa Wana nisoma tu daily kumbe Wana mindi chini kwa chini.
Tulianzisha discussion za usiku kuhusu kujipanga na pepaz za nencta.Muda huo siku zote nilikua naongea na simu na kuchat na pisi yangu daily.
Siku na siku wadau walichoka, wakaniundia mpango mkakati wa kunikomesha... Ile nimemaliza kuongea na pisi yangu dk zikaniishia bana narudi class wazee wakanichek kwa simu yangu.
"Mambo baby mbona umekata simu", dah aisee nikajua ni yeyeeee pisi yangu iyo nawaza kumbe washenzi wale class mates wangu wananichezea mchezo mchafu.
Aisee tulichat almost masaa 2 na huyo jamaa aliye act demu wangu mpaka nikajikuta nasahau na kusoma, nashangaa jamaa zangu wanacheka Sana huku wakiambiana kwa utani text nazomtumia.
Nakuja kuelewa ujinga wanaoufanya too late jamaa walipanda mbele kuandika ubaoni upumbavu wote niliochat haikutosha Waka aanza tuma kwenye group la WhatsApp la darasani.
Niliiaibika mtu mzima, hamu ya msuli ikafa nikaenda kulala class sikwenda week nzima!
Lile darasa hapana aisee,popote mlipo respect kwenu nalikumbuka la washenzi Sana

.
Sent using
Jamii Forums mobile app