Visa gani pombe ilikufanyia hutasahau?

Visa gani pombe ilikufanyia hutasahau?

Juzi juzi tu hapa nimepanda daladala sayansi kijitonyama na jamaa amelewa saa 6 mchana jua kali,
tumetoka pale tunaelekea mwenge tumefika adi mataa pale mwenge anamwambia konda amuache sayansi na wakati alipopandia gari ndo sayansi[emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mkuu nina visa lukuki, basi tu nakosa muda wa kuviweka humu. Kulala nje kwenye veranda ya nyumba, kulala kwenye gari barabarani, na kupoteza mwelekeo mara kibao. Ila kuna hii moja ilinitokea tena ughaibuni siku ya Jumamosi nimeenda open market kununua vitu second hand kwa ajili ya familia, napita sehemu naona pamezungushiwa na mahema kibao. Nafika mlangoni nulizwa ticket na mimi nikauliza kuna nini? Muhusika ananiambia ni siku ya bia na ukikata tiketi unakunywa tani yako. Safari ya open market ikaishia hapo nilikunywa bia za zaidi ya aina tatu hadi nikakaa chini kupata network. Nyumbani nilifika salama salama kwani hawakuwa na pombe kali
Duh
 
Nilipata aibu kwenye sherehe moja hv ilikua kila mziki unapopigwa lazima niende mbele kucheza,si unajua pombe inataka mziki aibu kuu niliipata baada ya kwenda mbele kwenye kikundi cha kina mama nami nikajichanganya humo humo
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nikiri na niweke wazi, pombe sio mbaya endapo ukiitumia kwa nidham, ila ikitumika kwa upuuzi ni batili kabisa, Alhamisi iliopita nimeenda kutoa mshahara wa magu nikasema wacha nichukue laki mbili tu inatosha kwa matumizi, wife alikua safarini.
Sasa nilikua na deni la miez miwili nilikunywa urabu sehem moja ninayoaminika sana 36k, nilipolipia ndio nikaanza urabu kiasi chote cha pesa mfukoni nilichokua nacho nikakimaliza kwa mda mfupi tu kwani nilijikuta nimearika marafiki kama wanne na niliwahakikishia kula na kunywa.
Kutoka apo kichwa imewaka kila mashine ATM nilioiona nilitoa hela na kuwanunulia pombe whuni, ata nisiowajua so mpka kufika jumamosi jion ninetumia 700k , kilichoniokoa ni kufuatwa na wife baada ya kifika toka safari, na kukuta siko home, alipopiga simu nilimtajia kiwanja nilichopo. Niko ndani leo siku ya tatu nimeomba ruhusa kazini kila nikijitafakari najiona sina amani ya moyo na mie kipato changu sio cha kutumia pesa hio bila kujutia. Nineweka mkakati wa kuacha pombe na ninaomba kuanzia hapa wenye nia wenzangu tuunde group la kupeana mikakati na mabadiliko ya kweli mim naiona pombe basi
Pombe haiachwi kirahisi rahisi hivyo [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Poa mkuu sema kuna mengi sijasema kwa sababu ya muda, nimetenbea sanakwenye maombi na kwa waganga ndo usiseme. Nadhani niendelee tu maadamu maisha yanaenda
Pole sana mkuu...ungekua una practice michezo ingekusaidia...kama Foot ball au Basket ball maana in lazima utachoka tu akili haiwez hitaji pombe baada ya mazoezi...pia una make nu friends ambao wako mbali na pombe au wanakunywa ila so kula siku...
Michezo itakufanya upunguze kwa kiasi kikubwa sana..pia unaeza join Jogging clubs...kifupi uchoshe mwili na mind ili ukilala usikumbuke Pombe maana Idleness huchochea ulevi hasa kama uko addicted.
 
Pole sana mkuu...ungekua una practice michezo ingekusaidia...kama Foot ball au Basket ball maana in lazima utachoka tu akili haiwez hitaji pombe baada ya mazoezi...pia una make nu friends ambao wako mbali na pombe au wanakunywa ila so kula siku...
Michezo itakufanya upunguze kwa kiasi kikubwa sana..pia unaeza join Jogging clubs...kifupi uchoshe mwili na mind ili ukilala usikumbuke Pombe maana Idleness huchochea ulevi hasa kama uko addicted.
Asante mkuu, kuna mdau ataanza kunipeleka volleyball Jumamosi hii, aliguswa na masahibu yangu
 
Back
Top Bottom