Vipimo "DNA" Mtoto "Aliyefufuka", kuokotwa Porini Vyaibua Mapya

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,035
Vipimo vya vinasaba (DNA) vya mwili wa mtoto Mabirika Wilson (8), aliyefariki dunia Aprili 16 mwaka huu wilayani Magu, pamoja vya wazazi wake, vimeonesha ni mtoto wao.

Uchunguzi huo unapingana na madai ya awali kwamba mtoto huyo amekutwa akiwa hai katika wilaya nyingine ya Kwimba mkoani hapo.

Vipimo hivyo vilivyofanywa na wataalamu wa afya kutoka Kitengo cha 'Forensic' wakishirikiana na wataalamu kutoka Ofisi' ya Mkemia wa Serikali baada ya kupata kibali cha kufukua mwili na kuufanyia vipimo kutoka mahakamani, vimeonesha kuwa mtoto aliveokotwa wilayani Kwimba Aprili 27 hana uhusiano na wazazi hao, hivyo mtoto wao halisi ni yule aliyeugua na kufariki dunia Aprili 16,. mwaka huu.​

Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa, aliyesema kuwa baada ya kubaini ukweli huo, jeshi linawashikilia wazazi wa moto huyo ambao ni Wilson Bulabo (35) na Helena Robert (33) kwa kufanya udanganyifu na kuzua taharuki katika jamii, wakitaka kujipatia mtoto aliyeokotwa ilhali siyo mtoto wao.

"Haiwezekani kwa kipindi cha siku 10 tu wazazi wawe tayari wamemsahau mtoto wao ambaye wamekaa naye kwa kipindi cha miaka minane na kuanza 'kumfananisha na mtoto ambaye sio wao. "Hivyo, baada ya uchunguzi wa kina kufanyika, watafikishwa mahakamani kujibu mashtaka mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuzua taharuki katika jamii na kuaminisha watu juu ya ufufuko wa mtoto wao," alisema Kamanda Mutafungwa.

Kamanda huyo alisema kuwa baada ya mtoto huyo kuhojiwa katika hali ya utulivu, alijitambulisha kwa jina moja la Mussa, hivyo kuwataka wazazi ambao watakuwa walipotelewa na mtoto kufika kituoni huko kumtambua kwa kuwa kwa sasa anahifadhiwa katika moja ya kituo cha kulelea watoto ambacho hakuwa tayari kukiweka wazi kwa sababu za kiuchunguzi.

Mwenyekitt wa Kijiji cha Mwangika, Jeremaniuss Masala, alisema kuwa baada ya kumpata moto huyo, walitangaza ili kuwapata ndugu zake na walipotokea wazazi hao na kueleza juu ya mtoto wao kufariki dunia na kudai huyo ndiye moto aliyefariki, wakaamua kushirikisha vyombo vya sheria kuondoa utata huo ambao ungesababisha madhara kutokana na kuhusishwa na ushirikina.
 
Sayansi imekataa..
Lakini najiuliza ni kweli wazazi wamfananishe mtoto wao wa miaka 8..!!

Kwani limit/mpaka wa ushirikina ni wapi..!!? ivi ushirikina hauwezi kumanipulate majibu ya kisayansi on it's favour..!?

Ni mara ngapi tunasikia mtu huyu amepimwa (sayansi) amekutwa na ugonjwa flan, akienda kwa mganga/kuombewa anaambiwa alitupiwa jini na anapona completely, akirudi kwenye sayansi ugonjwa hauonekani.

Scenario
Mwanzoni mwa April nilienda Tanga. Mtaa niliofikia wana story za mgonjwa anaeumwa kila kitu, i mean kila kitu. Yani amepimwa sukari ipo, UTI ipo, ukimwi upo, shinikizo la damu lipo, malaria yapo, typhoid ipo, STD's zipo, yaani kila kitu (at least alichopima). Na ana tezi dume linakaribia kuburuza chini na limeoza na kuozesha mapaja upande wa ndani (samahani kama umepata kinyaa au msisimko hasi). Huyu mgonjwa namimi nilimuona

Ni mtu wa 35-38 story zinasema alianza kunusa hela akapita na vibinti sana, alifika na kwa mke wa mtu, akaonywa bila kusikia. Sasahivi kila anaeenda kumtembelea anamuomba akamuombee msamaha kwa mwenye mke.

Swali linabaki, how far can "ushirikina" go
Watu wanapaa bila engine, wanapita ukutani vipi kuhusu hayo majibu kua compromised na ushirikina? In any ways

Gravitational force inakua takataka kwa mshirikina mwenye ungo. Vipi kuhusu DNA.
 
Unaweza ukasema habari hii imekuja na funzo

Lakini utabaki mdomo wazi siku ikija taarifa tena kuwa kuna mtu alikufa akazikwa raia wamemkutwa mtaani, utashangaa kuwaona Great Thinkers wakiamini habari hiyo

Licha ya kwamba kuna records za habari kama hiyo kuwa debunked lakini wengi wataamini.
 
Sayansi imekataa..
Lakini najiuliza ni kweli wazazi wamfananishe mtoto wao wa miaka 8..!!

Kwani limit/mpaka wa ushirikina ni wapi..!!? ivi ushirikina hauwezi kumanipulate majibu ya kisayansi on it's favour..!?

Ni mara ngapi tunasikia mtu huyu amepimwa (sayansi) amekutwa na ugonjwa flan, akienda kwa mganga/kuombewa anaambiwa alitupiwa jini na anapona completely, akirudi kwenye sayansi ugonjwa hauonekani.

Scenario
Mwanzoni mwa April nilienda Tanga. Mtaa niliofikia wana story za mgonjwa anaeumwa kila kitu, i mean kila kitu. Yani amepimwa sukari ipo, UTI ipo, ukimwi upo, shinikizo la damu lipo, malaria yapo, typhoid ipo, STD's zipo, yaani kila kitu (at least alichopima). Na ana tezi dume linakaribia kuburuza chini na limeoza na kuozesha mapaja upande wa ndani (samahani kama umepata kinyaa au msisimko hasi)

Ni mtu wa 35-38 story zinasema alianza kunusa hela akapita na vibinti sana, alifika na kwa mke wa mtu, akaonywa bila kusikia. Sasahivi kila anaeenda kumtembelea anamuomba akamuombee msamaha kwa mwenye mke.

Swali linabaki, how far can "ushirikina" go
Watu wanapaa bila engine, wanapita ukutani vipi kuhusu hayo majibu kua compromised na ushirikina? In any ways

Gravitational force inakua takataka kwa mshirikina mwenye ungo. Vipi kuhusu DNA.

Hakuna anayeweza kupaa na ungo, ule ni Utapeli kama Utapeli mwingine.

Hizo Akili ni Akili za Watu wazamani Sana
 
Back
Top Bottom