Kitanda kinazaa haram, sheria ya kupima DNA iangaliwe upya

Sean Paul

JF-Expert Member
Jun 16, 2013
807
2,106
Habari wana nzengo,

Sheria ya kupata kipimo cha vinasaba (DNA) hapa Tanzania ina mchakato mgumu kidogo. Ni kwamba ni ofisi maalum zinaweza kuomba kupata vipimo hivyo tu, katika kutekeleza majukumu yake. Either ni mahakama katika kutatua mgogoro, polisi katika uchunguzi, ofisi ya ustawi wa Jamii katika kutekeleza majukumu yake, mkuu wa wilaya n.k. Sheria inasema ili upate kipimo hicho ni lazima uende na barua kutoka moja ya vyombo hivyo. Si mtu tu binafsi ajiamulie kwenda. Wataalam wa sheria mnaweza kutusaidia vifungu.

Sababu kubwa inayosemwa serikali inazua kupima privately DNA ni kulinda maslahi ya mtoto kijamii.

Inasemekana hata ukienda kudai kipimo kujua mtoto ni wako au si wako....wengi huambiwa mtoto ni wako ili tu kumkinga mtoto yule na janga la kutokuwa na baba. Sawa, tunamlinda mtoto na malezi apate ya baba; je tunamtendea haki huyu mwanaume? Nonetheless, mbona mtu akimpa mwanafunzi mimba anafungwa miaka 30 jela? Huyu mtoto ambaye baba yake anakuwa jela kwa miaka hiyo mbona anakosa malezi ya baba? Na tuna uhakika mzazi huyu akitoka jela atakuwa na upendo na mtoto huyo?

Kwa maoni yangu hii sheria haitufai kwa hali ya sasa ya kimazingira. Tunaishi katika dunia yenye harakati haramu nyingi sana. Full of chaos, crazy world. Watu wamekuwa matapeli katika siasa, dini, ndoa, mahusiano, yaani kila mahali. Hakuna mahali binadamu upo comfortable, lolote linaweza kutokea popote usipopatarajia. Tunaishi kimachale machale mno.

Kitanda hakizai haramu. Kauli hii zamani ilikua na nguvu kwa sababu mkeo alikua na uwezo kupata mimba isiyo yako lakini akakata kabisa mawasiliano na huyo baba wa mtoto. Mnaishi kwa furaha na amani bila kelele. Zamani ilikua fahari kuwa na watoto wengi, mkeo akizaa mtoto ni wako tu unalea. Wazee waliweza kwenda sehemu wakaa miaka kadhaa, akirudi akakuta mke ana mtoto analea tu. Kwa dunia ya sasa hii ni liability isiyo na manufaa.

We umejivika upofu kitanda hakizai haramu, mkeo ana wasiliana vizuri kabisa na baba mtoto wake. Na kwa dunia hii ya generantion z upo uwezekano baadae mtoto akajua we siyo baba yake na akakukana mchana kweupe subject to hali yako ya baadae au ya huyo baba yake kibaiolojia. Mtoto yupo boarding, mama akienda kumuona anakwenda na mzazi mwenzie. Zawadi na pesa au hata ada jamaa anatoa vile vile. We umekwama mkeo akakudanganya amekopa kazini kumbe kachukua pesa kwa mzazi mwenzie.

Wanaume tuamke tulinde maslahi yetu. Amani na furaha ya moyo ni zawadi hakuna wa kukupa isipokuwa wewe mwenyewe. Sheria iweke mazingira mazuri ya kipimo hiki kiwe ruksa vile mtu atakavyo bila kumuathiri yeyote emotionally and physically.

Sean.
 
Na kubali Sana kiongozi, ila ili kulinda mtoto, kipimo hiki kiwe lazima kama kipimo Cha ukimwi wakati wa ujauzito, mama na baba wakapime DNA ili mtoto atakapo kuja aidha ajikute ktk familia kamili au awe na mama yake.
Hii itasaidia wamama na wababa kuwa waaminifu ila pia kufanya maamuzi mapema ya kutengana kabla mtoto hajazaliwa...
Maana mtoto akijatengwa na mzazi wakati keshajua na kupenda ni maumivu Sana ya hisia... Bora tu akute hayupo ktk Maisha yake!
Nawasilisha🙏
 
sawa sikatai, na mwanamme malaya jeeeee?
Hakuna mwanamme Malaya. Ni necha. Mwanamme hata ampende mke wake vipi, hata Kama anakwenda chumvini kwa mkewe, hata awe muchungaji, hata awe na wake wawili, piga ua garagaza and take it from me. lazima awe na mchepuko au Kama Hana hela hata kwa dada poa wa buku atakwenda.
Umri tu ndio utamfanya mwanaume aache wanawake wa nje lakini kutamani akiona pisi Kali kuko pale pale.
 
Hakuna mwanamme Malaya. Ni necha. Mwanamme hata ampende mke wake vipi, hata Kama anakwenda chumvini kwa mkewe, hata awe muchungaji, hata awe na wake wawili, piga ua garagaza and take it from me. lazima awe na mchepuko au Kama Hana hela hata kwa dada poa wa buku atakwenda.
Umri tu ndio utamfanya mwanaume aache wanawake wa nje lakini kutamani akiona pisi Kali kuko pale pale.

Kuna rafiki yangu tangu mkewe ana mimba alijua c ya kwake kwa sababu alikuta msg wanawasiliana mpaka anajifungua wiki ya kwanza bado wanawasiliana mwisho wa siku mwanamke kamfungukia jamaa mtoto c wake na akamuomba msamaha jamaa katulia anaendelea kulea mtoto hii imekaaje wadau?
 
Upo sahihi sheria ya DNA inapaswa kuchunguzwa upya.
Nihaki ya Mwanaume kujua kama mtoto niwake kweli.
Kaka angu ilishawahi kumkuta hii alioa mwanamke wakazaa mtoto wa kike baada ya mika 16 mkewe akamuambia mtoto wa wakwanaza ukweli kuwa huyu sio baba yako baba yako mzazi ni flani aisee broo ilimuma sanaa ila baadae akasamehe.
 
Habari wana nzengo,

Sheria ya kupata kipimo cha vinasaba (DNA) hapa Tanzania ina mchakato mgumu kidogo. Ni kwamba ni ofisi maalum zinaweza kuomba kupata vipimo hivyo tu, katika kutekeleza majukumu yake. Either ni mahakama katika kutatua mgogoro, polisi katika uchunguzi, ofisi ya ustawi wa Jamii katika kutekeleza majukumu yake, mkuu wa wilaya n.k. Sheria inasema ili upate kipimo hicho ni lazima uende na barua kutoka moja ya vyombo hivyo. Si mtu tu binafsi ajiamulie kwenda. Wataalam wa sheria mnaweza kutusaidia vifungu.

Sababu kubwa inayosemwa serikali inazua kupima privately DNA ni kulinda maslahi ya mtoto kijamii.

Inasemekana hata ukienda kudai kipimo kujua mtoto ni wako au si wako....wengi huambiwa mtoto ni wako ili tu kumkinga mtoto yule na janga la kutokuwa na baba. Sawa, tunamlinda mtoto na malezi apate ya baba; je tunamtendea haki huyu mwanaume? Nonetheless, mbona mtu akimpa mwanafunzi mimba anafungwa miaka 30 jela? Huyu mtoto ambaye baba yake anakuwa jela kwa miaka hiyo mbona anakosa malezi ya baba? Na tuna uhakika mzazi huyu akitoka jela atakuwa na upendo na mtoto huyo?

Kwa maoni yangu hii sheria haitufai kwa hali ya sasa ya kimazingira. Tunaishi katika dunia yenye harakati haramu nyingi sana. Full of chaos, crazy world. Watu wamekuwa matapeli katika siasa, dini, ndoa, mahusiano, yaani kila mahali. Hakuna mahali binadamu upo comfortable, lolote linaweza kutokea popote usipopatarajia. Tunaishi kimachale machale mno.

Kitanda hakizai haramu. Kauli hii zamani ilikua na nguvu kwa sababu mkeo alikua na uwezo kupata mimba isiyo yako lakini akakata kabisa mawasiliano na huyo baba wa mtoto. Mnaishi kwa furaha na amani bila kelele. Zamani ilikua fahari kuwa na watoto wengi, mkeo akizaa mtoto ni wako tu unalea. Wazee waliweza kwenda sehemu wakaa miaka kadhaa, akirudi akakuta mke ana mtoto analea tu. Kwa dunia ya sasa hii ni liability isiyo na manufaa.

We umejivika upofu kitanda hakizai haramu, mkeo ana wasiliana vizuri kabisa na baba mtoto wake. Na kwa dunia hii ya generantion z upo uwezekano baadae mtoto akajua we siyo baba yake na akakukana mchana kweupe subject to hali yako ya baadae au ya huyo baba yake kibaiolojia. Mtoto yupo boarding, mama akienda kumuona anakwenda na mzazi mwenzie. Zawadi na pesa au hata ada jamaa anatoa vile vile. We umekwama mkeo akakudanganya amekopa kazini kumbe kachukua pesa kwa mzazi mwenzie.

Wanaume tuamke tulinde maslahi yetu. Amani na furaha ya moyo ni zawadi hakuna wa kukupa isipokuwa wewe mwenyewe. Sheria iweke mazingira mazuri ya kipimo hiki kiwe ruksa vile mtu atakavyo bila kumuathiri yeyote emotionally and physically.

Sean.
Sio vinasaba tu, sheria zote zinazohusu masuala ya mahusiano na ndoa zinatakiwa kupitiwa upya kwa sababu zinamkandamiza mwanaume, na wanawake washaona izo loopholes kwaiyo wanayatumia mahusiano kimkakati.
 
Kuna rafiki yangu tangu mkewe ana mimba alijua c ya kwake kwa sababu alikuta msg wanawasiliana mpaka anajifungua wiki ya kwanza bado wanawasiliana mwisho wa siku mwanamke kamfungukia jamaa mtoto c wake na akamuomba msamaha jamaa katulia anaendelea kulea mtoto hii imekaaje wadau?
Koyemeshili unawezaje kuwa na rafiki bwege kiasi hicho? Hata Kama Ni limbwata, Hilo limepitiliza.
 
Back
Top Bottom