Mimi sijasoma gazeti lako lote, lakini unauliza rais amalize hiyo kesi kwa sheria ipi?! Ile kesi wote tunajua ni ya mchongo, na kosa kubwa la Mbowe siyo ugaidi! Kosa la Mbowe ni kuwa mpinzani wa kweli na kudai katiba mpya!

Pia, kama hujui kusoma between the lines, viongozi wa dini, kwa maneno mengine wanamwambia Mazaa, wanauona mchongo wote, watu wanaona kwamba yupo uchi, achutame!
Mbowe mpinzani wa kweli? Pole sana
 
Mbona mnasahau Mama alisema Mbowe hana adabu hilo ndilokosa hivyo ndio maana wenye akili wanamwomba asamehe kukosa adabu huko!!
Na hana adabu kweli, haiwezekani Magufuli hata hajazikwa akaanza kumtukana na kuandaa makusanyiko ya katiba nchi nzima! Hata kama alikuwa na madhaifu yake lakini alistahili kupewa heshima zote za maziko kama mkuu wa nchi
 
Linganisha hizi dots.
1. Rais samia akihojiwa na BBC akakiri kuwa kweli mbowe alitenda ugaidi.
2. Mbowe akakamatwa, kesi ikaanza kuunguruma.
2.Judge siyani akapokea maelezo ya Watuhumiwa kinyume na sheria, hapa ndipo kesi ilipotengenezwa, katikati ya kesi Kikaandaliwa kikao cha vyama vya siasa, moja ya ajenda ilikuwa ni mbowe asamehewe
3.. Mbowe akaambiwa aombe msamaha ili atoke gerezani lakini akagoma kuomba msamaha.
3. Judge Tiganga akatumia amri zake kupokea ushahidi akamtia mbowe na wenzake hatiani.
4. DPP akaanza kufuta kesi nyingi za ugaidi.
5. Viongozi wa dini wakaitwa ikulu, na clip iliyotolewa na ikulu ni viongozi hao wa dini wakiomba mbowe aachiwe.

Kwa hizo step huwezi kujua nini kinafanyika??? kumbuka katika uongozi wae mama Samia, doa kubwa kabisa alilonalo ni kumshitaki kiongozi wa chama kikubwa cha siasa kwa kesi ya ugaidi.
Maza hata kama atamuachia Mbowe sasa kwa kujidai kufuata mapendekezo ya Viongozi wa dini bado hatutamuelewa. Mbowe hatakiwi kusamehewa bali anatakiwa kuachiwa bila masharti yeyote yale. Hao wote wanaojidai kumuombea msamaha Mbowe hata huko Mahabusu au mahakamani hatujawahi kuwaona. Sasa hiyo huruma yao kwa Mbowe inatoka wapi? Yaani wanaona huruma tu pale wanapokutana na Maza ... This is so funny!
 
Na hana adabu kweli, haiwezekani Magufuli hata hajazikwa akaanza kumtukana na kuandaa makusanyiko ya katiba nchi nzima! Hata kama alikuwa na madhaifu yake lakini alistahili kupewa heshima zote za maziko kama mkuu wa nchi
Kumpa heshima mtu mjinga ni kuunga mkono Ujinga wake. Hata Yesu alimzuia mtu mmoja asiende kumzika baba yake kwa kumwambia waache wafu wazike wafu wao. Heshima ya mtu hutokana na matendo yake mema aliyo yatenda akiwa hai.
 
Kumpa heshima mtu mjinga ni kuunga mkono Ujinga wake. Hata Yesu alimzuia mtu mmoja asiende kumzika baba yake kwa kumwambia waache wafu wazike wafu wao. Heshima ya mtu hutokana na matendo yake mema aliyo yatenda akiwa hai.
Hakuna hiyo kitu inaitwa "Yesu", huyo mnayemwita "Yesu" alitengenezwa na waroma miaka 300 baada ya Yesu halisi kufariki ili kufanikisha malengo yao ya kisiasa, Yesu mwenyewe halisi alikuwa ni mvuvi flani hivi insignificant
 
Hakuna hiyo kitu inaitwa "Yesu", huyo mnayemwita "Yesu" alitengenezwa na waroma miaka 300 baada ya Yesu halisi kufariki ili kufanikisha malengo yao ya kisiasa, Yesu mwenyewe halisi alikuwa ni mvuvi flani hivi insignificant
Hujui lolote acha kuonesha Ujinga wako hadharani.
 
Hakuna hiyo kitu inaitwa "Yesu", huyo mnayemwita "Yesu" alitengenezwa na waroma miaka 300 baada ya Yesu halisi kufariki ili kufanikisha malengo yao ya kisiasa, Yesu mwenyewe halisi alikuwa ni mvuvi flani hivi insignificant
Mpumbavu amesema moyoni mwake, hakuna Mungu!
 
Back
Top Bottom