Viongozi wa Dini na Hatma ya Tanzania

Mwl Moshi,
Nadhani hayo yakutoa shutuma za juu juu watu wanakubaliana nayo kabisa na ndio hayo hayo ya akina Mbunge Amina na blah blah zake za madawa ya kulevya. Kusema tu rushwa na madawa ya kulevya huku pesa hizo hizo haramu ndio zinazochangia ujenzi wa makanisa na misikiti ndio unafiki wenyewe. Hawa viongozi wakimwalika Richmonduli kwenye harambee zao hawawezi hata kugusia swala la Richmondi kwa sababu watamwudhi halafu ataondoka na pesa zake. Matokeo yake watamsifia kwa mwelekeo mzuri wa utawala wao lakini akishaondoka watakimbilia kwenye ibada kudai serikali imejaa rushwa, mbona wasimwambie Richmonduli mwenyewe au JK wanaoweza kukutana nao ana kwa ana?
 
Dr wHo,
Pengine swali lako ni genuine lakini ndio kusema unataka ushahidi au? Labda anza kufuatilia wachangiaji wa harambee zote zile kwenye jenzi hizo halafu majina utakayokutana nayo huko kata shauri mwenyewe kama pesa zao ni halali au vinginevyo. Hoja yangu ni kuwa viongozi hawawezi kukemea uoza huo kwa sababu wanategemea hizo pesa zinazotokana na uoza huo. Kama wanatumia kujengea makanisa, miskiti, nyumba zao wenyewe au mashule ukweli ni kuwa wachangiaji wake wengi wala rushwa na watu wa unga.
 
nakubali kabisa viongozi wa dini wananikera na katabia kao .,wanpenda kushiriki karamu na matajiri ,kuzika matajiri nk ukitazama biblia utaona kuwa Yesu alitumia muda wake kusaidia wahitaji ,wanyonge,kuponya ,kuwashibisha wenye njaa nk viongozi wetu leo wanatugawa wenye nazo na wasiokua nazo ,ikitokea kiongozi kafungisha harusi ,kabariki watoto nk ujue baada ya hapo ataenda kushiriki karamu kwenye sherehe itakayokua na vinono,tazama wanavyokataza pombe lakini angalia namana wanavyoshiriki karamu zenye pombe kwa matajiri,,jamani kwani dini ilikuja kwa masikini tu!!!!! tazama namna michango isiyokua safi inavyojenga makanisa na misikiti...tufanyeje???
 
Maaskofu, masheikh wakemea mikataba mibovu
*Wataka serikali ijibu hoja za Dk Slaa.
*Wasema kinachofanyika sasa ni kuwahadaa Watanzania
*Wataka ufisadi ukemewe kwenye nyumba za ibada
*Mtaalam akiri mikataba haiwanufaishi wazawa



Na Kizitto Noya
Mwananchi


VIONGOZI wa dini za Kikristo na Kiislam nchini, wameisihi serikali kutoa tamko linaloeleweka na la wazi kuhusu tuhuma za ufisadi zinazowakabili baadhi ya watendaji wake badala ya kuendelea kukaa kimya.

Wakizungumza jana katika warsha ya kuelimishana kuhusu faida na hasara za mikataba mbalimbali nchini, maaskofu, masista, mapadri na viongozi kutoka Baraza la Waislam Tanzania (Bakwata), walisema serikali inapaswa kujibu hoja za Mbunge wa Karatu, Dk Willibrod Slaa badala ya kumnyamazisha kwa kumtishia kumshtaki.

Askofu Dk Peter Mwamasika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Dodoma, alisema sura ya ufisadi katika baadhi ya mikataba ipo na serikali haina budi kujibu hoja hiyo kwa vielelezo badala ya kumnyamazisha Dk Slaa kwa maslahi ya kisiasa.

"Serikali itoe tamko linaloeleweka kuhusu utata wa mkataba wa mgodi wa Buzwagi, wasimtishe Dk Slaa kwa kukimbilia mahakamani maana yeye hawezi kutoa hoja za kitoto kwani ni msomi kama wao," alisema askofu Mwamasika.

Alisema sasa umefika wakati ambapo serikali inatakiwa ieleze bayana namna mgodi wa Buzwagi unavyomnufaisha Mtanzania au hata Wasukuma na Wanyamwezi wenye ardhi yao katika mgodi huo.

Alizitaka taasisi mbalimbali kusimama kidete na kutoa matamko kuikumbusha serikali wajibu wake katika kutetea maslahi ya taifa na watu wake, badala ya maslahi ya kikundi kidogo cha watu.

"Tutawezaje kuondokana na viongozi wabovu wanaowatumikisha wananchi badala ya kuwatumikia, kama si mashirika na wadau wa maendeleo kupiga kelele?" alihoji askofu huyo.

Naye Askofu Isaac Nicodemo wa Kanisa la Morovian la Tabora, alionya tabia ya watu wachache kunufaika na rasilimali za nchi huku wengine wakibaki kuwa maskini na kuipeleka nchi pabaya.

Alisema tabia hiyo sio tu inaliongezea taifa umaskini bali pia inaleta utumwa kwa taifa mbele ya mataifa mengine na isipodhibitiwa ni hatari.

Mkuu wa Shirika la Masista la Mbeya, Immaculate Mirambo, alielezea kukosekana kwa uwiano wa matumizi ya rasilimali za taifa baina ya wazawa na wageni kuwa ni sehemu ya ufisadi unaolalamikiwa na jamii.

"Mimi siyo mtaalam, nazungumza kama mtu wa kawaida kwamba kwa nini kusiwe na uwiano wa matumizi ya rasilimali za nchi kati ya wazawa na wageni?" alihoji.

Alisema kwa muda mrefu serikali imekuwa ikizuia matumizi ya baadhi ya rasilimali kwa wazawa na kuruhusu rasilimali hizo zitumike na wageni jambo ambalo limesababisha umaskini kwa mwananchi wa kawaida.

Naye Mchungaji John Magofu wa Baraza la Kikristo Tanzania (CCT), aliwataka viongozi wa dini kuwa mstari wa mbele kutetea maslahi ya taifa badala ya kuwaachia wanasiasa ambao hata kama hoja zao zina ukweli, zinapokelewa kisiasa na kupuuzwa.

Alisema hoja nzito kama za ufisadi zinatakiwa kusimamiwa na viongozi wa dini kwa kuzihubiri katika sehemu zao za ibada ambako wahusika wanaabudu ili wabadili tabia.

"Mafisadi wana imani zao na wanaabudu, viongozi wa dini wakihubiri hoja hizo huenda zikafika kwa walengwa mapema zaidi kuliko wanasiasa," alisema Mchungaji Magofu.

Alisema kuna haja kwa serikali kujichunguza na kuanza kufanya utafiti wa kina kabla ya kuingia mikataba mbalimbali kwani uzoefu unaonyesha kuwa mikataba mingi haiwanufaishi wananchi.

Akizungumza katika ibada ya ufunguzi wa warsha hiyo, Askofu Charles Salala wa Kanisa la African Inland (AICT) Dayosisi ya Pwani, alisema viongozi wa kanisa ndio dira iliyobaki na kuweza kutoa matamko yanayoheshimika katika jamii.

Alisema jamii imeanza kupoteza imani na wanasiasa badala yake inahitaji viongozi wa kiroho kuwa mstari wa mbele katika kutetea maslahi yao.

"Viongozi wa kanisa wanatakiwa kuishauri serikali na kutoa matamko ya utetezi wa wananchi badala ya kuwaachia wanasiasa,"alisema.

Akizungumza katika warsha hiyo, Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kasuto na Mshauri Mkuu wa masuala ya Uchumi na Biashara, Mikubuka Shimwela, alibainisha kuwa tafiti zilizofanywa hivi karibuni zimeonyesha kuwa asilimia 38 ya bidhaa zote zinazoingizwa nchini ni bandia.

Hata hivyo, alisema kuwa serikali imefanya jitihada za makusudi kudhibiti tatizo hilo kwa kupeleka bungeni muswada unaotaka kuipa nguvu za kisheria Tume ya Ushindani wa Biashara nchini kukamata na kuwafikisha watuhumiwa wa bidhaa bandia mahakamani.

Alisema baada ya kujadiliwa katika Bunge la Bajeti mwezi Juni, Muswada huo utapitishwa katika Bunge la Mwezi Novemba mwaka huu.

Akizungumza katika warsha hiyo Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mtaalam wa masuala ya mikataba ya biashara za Kimataifa, Profesa Francis Matambalya, alisema ni ukweli usiopingika kwamba mikataba mingi nchini haiwanufaishi wananchi.

Alisema tofauti na nchi za Magharibi nchini mikataba mingi inawanufaisha wageni badala ya wazawa jambo ambalo linaathiri uchumi wa nchi na kusababisha umaskini kwa wananchi wake.

Kwa mujibu wa Profesa Matambalya, mbali na ubovu wa mikataba, woga wa watendaji katika kusimamia ukweli na tabia yao ya kujikomba kwa serikali na kusahau maslahi ya wananchi pamoja na maamuzi ya kushitukiza ni baadhi ya mambo yanayoleta umaskini nchini.

Alisema watendaji wengi wanatumikia matakwa ya serikali badala ya wananchi na hawana uchungu wa kutetea maslahi ya nchi, zaidi ya kujilimbikizia mali na kutafuta madaraka.

"Inakuwaje nchi ina polisi, usalama wa taifa, Takukuru, wataalam na viongozi wa ngazi zote ishindwe kudhibiti ufisadi kama siyo kutokuwa na moyo wa kizalendo?" alihoji.

Alisema umasikini nchini hautakoma endapo viongozi wa dini hawataingilia kati suala hilo na kuwasemea wananchi kwani hii ni sehemu ya kazi yao waliyopewa na Mungu.

Kauli za viongozi hao zimekuja baada ya Dk Willibrod Slaa kuibua tuhuma za ufisadi dhidi ya baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali.

Tayari maaskofu wa Kanisa Katoliki ambao ni sehemu ya washiriki katika warsha hiyo wameonya kuhusu ufisadi kwamba ni hatari kwa taifa.

Viongozi hao wa dini leo wanatarajia kutoa tamko la pamoja kuhusu mjadala wa mikataba mbalimbali ikiwapo nafasi ya Tanzania katika mkataba wa Contonou.
 
Strong Points!

1. serikali kutoa tamko linaloeleweka na la wazi kuhusu tuhuma za ufisadi zinazowakabili baadhi ya watendaji wake badala ya kuendelea kukaa kimya. serikali inapaswa kujibu hoja za Mbunge wa Karatu, Dk Willibrod Slaa badala ya kumnyamazisha kwa kumtishia kumshtaki.

2. "Serikali itoe tamko linaloeleweka kuhusu utata wa mkataba wa mgodi wa Buzwagi, wasimtishe Dk Slaa kwa kukimbilia mahakamani maana yeye hawezi kutoa hoja za kitoto kwani ni msomi kama wao,"

3. serikali inatakiwa ieleze bayana namna mgodi wa Buzwagi unavyomnufaisha Mtanzania au hata Wasukuma na Wanyamwezi wenye ardhi yao katika mgodi huo.

4. taasisi mbalimbali kusimama kidete na kutoa matamko kuikumbusha serikali wajibu wake katika kutetea maslahi ya taifa na watu wake, badala ya maslahi ya kikundi kidogo cha watu.

5. "Tutawezaje kuondokana na viongozi wabovu wanaowatumikisha wananchi badala ya kuwatumikia, kama si mashirika na wadau wa maendeleo kupiga kelele?"

6. tabia ya watu wachache kunufaika na rasilimali za nchi huku wengine wakibaki kuwa maskini na kuipeleka nchi pabaya. tabia hiyo sio tu inaliongezea taifa umaskini bali pia inaleta utumwa kwa taifa mbele ya mataifa mengine na isipodhibitiwa ni hatari.
kwa nini kusiwe na uwiano wa matumizi ya rasilimali za nchi kati ya wazawa na wageni?"

7. hoja nzito kama za ufisadi zinatakiwa kusimamiwa na viongozi wa dini kwa kuzihubiri katika sehemu zao za ibada ambako wahusika wanaabudu ili wabadili tabia. "Mafisadi wana imani zao na wanaabudu, viongozi wa dini wakihubiri hoja hizo huenda zikafika kwa walengwa mapema zaidi kuliko wanasiasa,"

8. tafiti zilizofanywa hivi karibuni zimeonyesha kuwa asilimia 38 ya bidhaa zote zinazoingizwa nchini ni bandia.


9. ni ukweli usiopingika kwamba mikataba mingi nchini haiwanufaishi wananchi. mbali na ubovu wa mikataba, woga wa watendaji katika kusimamia ukweli na tabia yao ya kujikomba kwa serikali na kusahau maslahi ya wananchi pamoja na maamuzi ya kushitukiza ni baadhi ya mambo yanayoleta umaskini nchini. watendaji wengi wanatumikia matakwa ya serikali badala ya wananchi na hawana uchungu wa kutetea maslahi ya nchi, zaidi ya kujilimbikizia mali na kutafuta madaraka.

10. "Inakuwaje nchi ina polisi, usalama wa taifa, Takukuru, wataalam na viongozi wa ngazi zote ishindwe kudhibiti ufisadi kama siyo kutokuwa na moyo wa kizalendo?"
 
Naam kila siku mambo yanazidi kuwa mambo!!!
Naona sasa Muungwana anazidi kubanwa kila kona,yeye na wasaidizi wake kina Kingunge,Warioba na Khatib wana kazi kweli ya kujibu.hapa mi namsikitikia Mzee Warioba,nadhani kwa kusoma ujumbe huu wa watu wa dini ni vema akakaa chini na kutafakari kwa nini alisema kauli zile,vinginevyo ni mnafiki sana huyo Mzee.Pili cha muhimu zaidi hapa ni kuwa wakati wa kampeni mwaka 2005 ni hawa hawa viongozi wa dini waliosema Muungwana ni chaguo la Mungu (sijui Mungu gani) na kufikia hatua ya kumpigia chapuo kwa kumualika kwenye uzinduzi wa makanisa yao kabla hata ya Uchaguzi.Kwa mnaokumbuka nadhani mliwasikia kina Lipumba na Mrema walivyolalamikia faulo hizi za wazi za viongozi wa dini.Sasa kama na wao wameanza kuongelea ufisadi...sijui muungwana atatokea wapi...
 
Strong Points!

1. serikali kutoa tamko linaloeleweka na la wazi kuhusu tuhuma za ufisadi zinazowakabili baadhi ya watendaji wake badala ya kuendelea kukaa kimya. serikali inapaswa kujibu hoja za Mbunge wa Karatu, Dk Willibrod Slaa badala ya kumnyamazisha kwa kumtishia kumshtaki.

2. "Serikali itoe tamko linaloeleweka kuhusu utata wa mkataba wa mgodi wa Buzwagi, wasimtishe Dk Slaa kwa kukimbilia mahakamani maana yeye hawezi kutoa hoja za kitoto kwani ni msomi kama wao,"

3. serikali inatakiwa ieleze bayana namna mgodi wa Buzwagi unavyomnufaisha Mtanzania au hata Wasukuma na Wanyamwezi wenye ardhi yao katika mgodi huo.

4. taasisi mbalimbali kusimama kidete na kutoa matamko kuikumbusha serikali wajibu wake katika kutetea maslahi ya taifa na watu wake, badala ya maslahi ya kikundi kidogo cha watu.

5. "Tutawezaje kuondokana na viongozi wabovu wanaowatumikisha wananchi badala ya kuwatumikia, kama si mashirika na wadau wa maendeleo kupiga kelele?"

6. tabia ya watu wachache kunufaika na rasilimali za nchi huku wengine wakibaki kuwa maskini na kuipeleka nchi pabaya. tabia hiyo sio tu inaliongezea taifa umaskini bali pia inaleta utumwa kwa taifa mbele ya mataifa mengine na isipodhibitiwa ni hatari.
kwa nini kusiwe na uwiano wa matumizi ya rasilimali za nchi kati ya wazawa na wageni?"

7. hoja nzito kama za ufisadi zinatakiwa kusimamiwa na viongozi wa dini kwa kuzihubiri katika sehemu zao za ibada ambako wahusika wanaabudu ili wabadili tabia. "Mafisadi wana imani zao na wanaabudu, viongozi wa dini wakihubiri hoja hizo huenda zikafika kwa walengwa mapema zaidi kuliko wanasiasa,"

8. tafiti zilizofanywa hivi karibuni zimeonyesha kuwa asilimia 38 ya bidhaa zote zinazoingizwa nchini ni bandia.


9. ni ukweli usiopingika kwamba mikataba mingi nchini haiwanufaishi wananchi. mbali na ubovu wa mikataba, woga wa watendaji katika kusimamia ukweli na tabia yao ya kujikomba kwa serikali na kusahau maslahi ya wananchi pamoja na maamuzi ya kushitukiza ni baadhi ya mambo yanayoleta umaskini nchini. watendaji wengi wanatumikia matakwa ya serikali badala ya wananchi na hawana uchungu wa kutetea maslahi ya nchi, zaidi ya kujilimbikizia mali na kutafuta madaraka.

10. "Inakuwaje nchi ina polisi, usalama wa taifa, Takukuru, wataalam na viongozi wa ngazi zote ishindwe kudhibiti ufisadi kama siyo kutokuwa na moyo wa kizalendo?"

Good observation!

Kinachonisikitisha, ni kwamba, I personnally know some guys TAKUKURU, UWT na Polisi ambao ni Makini sana i.e. wazalendo, nina hakika kama leo hiii ukipata nafasi ya kupitia ambacho huwa wanaishauri serikali UTASHANGAA kwanini leo hii tunapigiana kelele na akina KARA

Hivi vyombo wanasiasa wamevifanya kama BLANKET to us all ili tulalae usingizi mnono, kama ambavyo imekuwa miaka yote. I think the Guys are operating clandestinely kuonyesha kuwa they are FED UP na mambo ya baadhi ya wanasiasa wanavyo-behave, kwa sababu at the end of the day ni wao (The Blankets) ndio wanaoonekana HAWAFANYI KAZI YAO IPASAVYO.

lets wait to see more to come...................
 
Kinachonisikitisha, ni kwamba, I personnally know some guys TAKUKURU, UWT na Polisi ambao ni Makini sana i.e. wazalendo,
wazalendo??hii si zarau..ni rafiki zako katika shida na raha zako,hawa ndio walioutetea ufisadi wa Mkapa asichunguzwe kisa JK kakataa,huu ndio uzalendo unaousema??mbona githongo yule wa Kenya likaataa kuendeshwa na sisa akawamwaga viongozi wakuu wa kenya wanaohuiks ana Rushwa??
labda sijui maana ya uzalendo?kwanini wamekuwa bubu??
sitaki kusika PCCB inayoongozwa na watu waoga,apewe tindu lissu
 
Hawa wamechelewa, tena kujikomba kwao kwa wananchi kumekuja katika kiza cha usiku!! Katika mapambano ya haki za watu, usawa, na haki za kiraia, vyombo vya imani haviji mwisho! vinakuwa mbele tena, mstari wa mbele!! Yaani wao wamesubiri wengine wafanye kazi wao waje na matamko ya ajabu ajabu!!

Wanapowaalika watawala kufungua mashule na hospitali zao mbona hawawakemei au kuwahoji? Hivi majuzi Waziri Mkuu alipokuwa anafungua hospitali (kliniki?) kule Mwanza alitamba na kuwashukuru makanisa kuwa wanapojenga vitu hivyo wanatekeleza Ilani ya CCM, mbona wachungaji hawakupinga? Kwani makanisa yamekuwa sehemu ya CCM, na Misikiti imekuwa ni idara za CCM!?

Sipendi, tena Sitaki, viongozi wanaofuata!!
 
Ushauri wa viongozi wa dini una walakini. Ndio hawahawa mwaka 2005 waliokuwa wansema Kikwete kachaguliwa na Mungu, wakati sie tulikuwa tunasema Kikwete kachafuka kutokana na kashafa ya mtambo wa IPTL akiwa waziri wa nishati, na leo ndio hao wanasema serikali sijui imefanyaje! Mbona wanakuwa ndumilakuwili?
Walikuwa wapi kusema masuala haya hadi akina Slaa wafurumua madudu haya?
 
Ushauri wa viongozi wa dini una walakini. Ndio hawahawa mwaka 2005 waliokuwa wansema Kikwete kachaguliwa na Mungu, wakati sie tulikuwa tunasema Kikwete kachafuka kutokana na kashafa ya mtambo wa IPTL akiwa waziri wa nishati, na leo ndio hao wanasema serikali sijui imefanyaje! Mbona wanakuwa ndumilakuwili?
Walikuwa wapi kusema masuala haya hadi akina Slaa wafurumua madudu haya?

Hawa walikuwa wanapima upepo kuona unaelekea wapi pamoja na spidi yake,baada ya kuona kuwa mambo yanazidi kumuelemea Muungwana kipenzi chao ndo haoo nao wanakurupuka "kushauri" sasa, which is too late,wao ndi wanaofadika sana na hizo "sadaka" za mafisadi as if huwa hawaijui inakopatikana wakati wakiitisha harambee zao,wanapenda sana kushare proceeds za ufisadi na mafisadi at the expense of waumini ambao ndo wanaoibiwa na hao mafisadi...in maana hawajaona kazi iliyofanywa na watawa wa kibudha kule Burma?au mambo ya Cardinal wa Phillipines alipoongoza maandamano yaliyomwondoa Ferdinand Marcos?wetu ni viongozi wa dini wasanii sana,wanaokula na mafisadi huku wao pia wakiwaibia waumini kwa michango isiyokwisha...what a bunch of religious hypocrites...
 
Tusiwalaumu sana hawa, nao pia binadamu. wameona wapi walikosea sasa wanajaribu kutubu dhambi zao. dhamira zao zinawasuta hawana jinsi.
Mwanzoni walidhani ni zile zile kelele za akina mrema kwamba ninao ushahidi, then haonyeshi. Leo Slaa ameweka wazi. na mkataba wa buzwagi uko mitaani kama njugu. watamhubiria nani uongo kanisani tena? hawana jinsi kama JK asivyo na jinsi ya kutoka. ni lazima nao waimbe wimbo wa slaa. na bado kitambo kidogo hata wale waliobaki kuimba wimbo wa ccm watabadilika na kuimba wimbo wa Taifa. Bomani ameanza na Warioba inshallah atafuata.

Inafurahisha viongozi wa dini kuliona hili kwani ipo faida kubwa kwa upande mwingine. wao ndio wanamiliki sehemu kubwa ya watanzania. ni imani yangu ujumbe wa ufisadi utawafikia watanzania wengi kwa mamilioni. Viva JF
 
..wanafiki tuu hawa hawana mpango wowote,wanaangalia upepo unaelekea wapi na ndio wanarukia ndani..wamegundua wananchi sasa hawana mchezo basi nao ndio wanatoa vikauli mbuzi vyao,kama wanataka nao wakazomee ndio tutawaelewa la sivyo hatutaki opportunist hapa.
 
Baada ya kiongozi huyu kupewa sifa za kila aina ikiwapo moja wapo kuwa nina nukuu''ndiye chango la mungu''alipe sifa hizo na viongozi wa kidini, ambao sasa wanaona kazi imekuwa kubwa kuliko uwezo wake , basi viongozi wa kidini hawana budi kuliongoza taifa la Tanzania,

Inaoneka muheshimiwa huyu alikuwa anataka madaraka na nguvu lakini akujua hiyo kazi ni nzito kiasi gani kuongoza taifa lenye watu zaidi ya miliion 35.

jamani ni vizuri kumsaidia kiongozi wetu na serikali kwa ujumla , ninashukuru sana viongozi wa dini kufanya hivyo kwasababu watanzania ni watu wamungu na wanaitaji msaada kutoka kwa viongozi wote Wakidini,Kijadi na Kiserekali.

Tunaomba pia kila mwenye uwezo wa kumsaidia Rais wetu asiogope na sehemu ya kutoa mawazo ni hapa JF kwa sababu ninaimani kuwa anasoma huku kila siku,

Pia viongozi wa kidini ni wasomaji wazuri hapa JF pia tunawakaribisha viongozi wa Kijadi kwa sababu pia walimsaidia Rais kipindi cha uchaguzi,

wanafunzi wa vyuo mbalimbali nchi, wafanyakazi,Wakulima, wafanyabiashara, wanachama wa vyama mbalimbali, bila kujali itikadi tumsaidie Rais wetu na wasaidizi wake pale tunapo ona kumekosewa.

ninarudia mahali pakusemea kero zako ni hapa JF wanapoongea kwa uwazi zaidi huu mtandao hauna mwenyewe ni wa watanzania , siyo CCM au chama chochote cha kisiasa au kikundi cha watu karibu sana hapaJF.

ASANTENI
 
Mwalimu JKN (RIP) alisema.........................mimi nimekaa Ikulu zaidi ya miaka ishirini, sijawahi kuona kuna biashara pale, watu naona wanakimbilia Ikulu KUNA BIASHARA GAANI??

nafikiri alikuwa na maana ifuatayo
..........endapo watu wamekopa pesa ya kufanyia kampeni ili waingie Ikulu.....sijui pale Ikulu watafanya biashara gani ili warudishe mikopo hiyo...............no wonder leo tunayaona haya tunayoyaona
 
Mwalimu JKN (RIP) alisema.........................mimi nimekaa Ikulu zaidi ya miaka ishirini, sijawahi kuona kuna biashara pale, watu naona wanakimbilia Ikulu KUNA BIASHARA GAANI??

nafikiri alikuwa na maana ifuatayo
..........endapo watu wamekopa pesa ya kufanyia kampeni ili waingie Ikulu.....sijui pale Ikulu watafanya biashara gani ili warudishe mikopo hiyo...............no wonder leo tunayaona haya tunayoyaona

Heshima kuu ni kweli JF itafute njia ya kumsaidia huyu mkuu wetu.
 
msaada pekee kwa JK naweza nikasema ni ushauri tu ! maana inelekea aliokuwa nao karibu wote ni wabovu, wanamshauri vibaya, ripoti mbovu ! Pia JK itakuwa vizuri kama akifanya kazi anavyoona yeye na sio kuambiwa na watu fanya hivi, fanya vile kiasi kwamba sasa washampoteza njia !
 
aisee nimesoma ile interview yake na FT......nimechoka mbaya.....nikiisoma ile interview, napata picha ya kuwa hata apate washauri kama akina Prof Lipumba..........kama hatambui matatizo yetu ni nini......basi tumeula wa chuya.

yaani barabara zetu zisubiri ziara zake JK ndio zijengwe!!!!??...........what a joke, yaani ana-justify ziara mikoani kwa kwenda kungalia na kuamrisha barabara ijengwe........i mean nafikiri wananchi tuna-deserve better than this
 
Back
Top Bottom