Mwl Athumani Ramadhani
JF-Expert Member
- Sep 10, 2022
- 1,282
- 2,508
Hakuna hilo katazo Mkuu!Biblia inakataa ndoa za matala
Kilichopo ni sheria ya viwanda ya mwaka 1800 ambayo inahusiana na nuclear family pekee Kuwa rahisi kusafirishwa toka kiwanda kimoja kwenda kingine kuepusha gharama Yaani mke mmoja na watoto wawili tu!
Hakuna andiko la kibiblia linalosapoti katazo la mitara bali sheria ya kanisa pekee NDIO imechukua Hiyo ya 1800 ya industrial revolution!!
Wakati paulo anahubiri na yesu pia walikuwa mitara kama kawa ndio maana paulo anakazia Kuwa!
"Shemasi au askofu awe mume wa mke mmoja aliyelea watoto Katika kweli na naeshuhudiwa kutenda mema ""
Anasema hivyo Kwasababu mitara ilikuwepo kabla hata kristo hajaja na ilikuwepo wakati wanahubiri ndio maana ya katazo hilo kwamba ukiwa na mitara hurusiwi Kuwa shemasi wala askofu KWA mujibu wa paulo mtume!
Waroma wao wakaingiza sheria kali za mahusiano ILI kulinda uchumi wa kanisa usianguke KWA kukataza mapadri,maaskofu na masister wasioe wala kuolewa kwamba wawe mali ya kanisa na vyote wanavyomiliki!pia washirika waoe mke mmoja Moja kuepusha majukumu na uchumi uliobana!!
Hata leo ni uchumi tu unaotufanya tuwe na mke mmoja wala sio mapenzi ya Dini wala nini!
Na wenye fedha wanaoa wengi KWA mtindo wa mchepuko au mpango wa kando!!
Chunguza!
Kama mitara ingekuwa dhambi Ibrahim Baba wa imani angekataliwa na Mungu hata mfalme suleiman!!
Fuatilia hayo!