Habari wadau.
Ukweli mchungu najiona nina tatizo la kisaikolojia.
Binafsi chuo nilisoma Mzumbe enzi zile za division one tupu ndio wanapata admission.
Nikiwa chuo nilipata marafiki wengi sana ila hawa watatu wameniathiri kisaikolojia. Mmoja aliitwa Nelson mwingine Frank na mwingine Abdul.
Nelson alikuwa anasomea uhasibu kozi yake ilikuwa maarufu sana kwa vichwa wanaita BAF, Nelson ndie alikuwa best students wa masomo ya biashara kidato cha sita. Alipewa zawadi kwa kuongoza nchi nzima masomo hayo.
Frank alikuwa anasoma Law na yeye alikuwa kichwa sana.
Na Abdul nae alikuwa anasoma BAF na yeye alikuwa vizuri sana darasani.
Baada ya kumaliza chuo nelson alipata kazi kampuni maarufu za uhasibu wanaziita big four.. then akahamia TRA.
Frank alipata kazi baada ya chuo kama mkufunzi ama lecture wa chuo kimoja cha uma maarufu
Abdul na yeye alipata kazi Big four nyingine.. tofauti na ile alienda nelson.
Mimi pia nilipata kazi bank moja maarufu siitaji jina.
Baada ya chuo maisha yalikuwa bata sana maana marafiki wote tulikuwa jijini dar es salaam. Kila siku tunakutana tunakula bata sana siku za weekend.. maana tulipanga nyumba maeneo jirani.
Kwa ufupi marafiki zangu wote walifariki vifo vilivyofuatana.. ndani ya miaka mitano wakaondoka wote na kuniacha mpweke.
Alianza nelson alifariki kwa ini kufeli baada ya kupata hepatitis B
Akaja abdul na yeye alifariki kwa TB ambayo ilisababisha na HIV
Wa mwisho kabisa akawa Frank na yeye alifariki kwa bacteria kwenye ubongo waliosabishwa na HIV complications.
Nje ya hao Pia nilikuwa na rafiki yangu mwingine mwalimu nilijuana nae wakati ananifundisha Physics A level anaitwa Elias Na yeye na yeye akaja kufariki kwa sababu zinazosemekana ni HIV complications.
Ukweli vifo hivyo vya jamaa zangu vimeniathiri sana kisaikolojia.
Nimekuwa na huzuni sana na uoga mkubwa sana. Najiona Naogopa madem sana mpaka napitiliza.
Ukweli mchungu najiona nina tatizo la kisaikolojia.
Binafsi chuo nilisoma Mzumbe enzi zile za division one tupu ndio wanapata admission.
Nikiwa chuo nilipata marafiki wengi sana ila hawa watatu wameniathiri kisaikolojia. Mmoja aliitwa Nelson mwingine Frank na mwingine Abdul.
Nelson alikuwa anasomea uhasibu kozi yake ilikuwa maarufu sana kwa vichwa wanaita BAF, Nelson ndie alikuwa best students wa masomo ya biashara kidato cha sita. Alipewa zawadi kwa kuongoza nchi nzima masomo hayo.
Frank alikuwa anasoma Law na yeye alikuwa kichwa sana.
Na Abdul nae alikuwa anasoma BAF na yeye alikuwa vizuri sana darasani.
Baada ya kumaliza chuo nelson alipata kazi kampuni maarufu za uhasibu wanaziita big four.. then akahamia TRA.
Frank alipata kazi baada ya chuo kama mkufunzi ama lecture wa chuo kimoja cha uma maarufu
Abdul na yeye alipata kazi Big four nyingine.. tofauti na ile alienda nelson.
Mimi pia nilipata kazi bank moja maarufu siitaji jina.
Baada ya chuo maisha yalikuwa bata sana maana marafiki wote tulikuwa jijini dar es salaam. Kila siku tunakutana tunakula bata sana siku za weekend.. maana tulipanga nyumba maeneo jirani.
Kwa ufupi marafiki zangu wote walifariki vifo vilivyofuatana.. ndani ya miaka mitano wakaondoka wote na kuniacha mpweke.
Alianza nelson alifariki kwa ini kufeli baada ya kupata hepatitis B
Akaja abdul na yeye alifariki kwa TB ambayo ilisababisha na HIV
Wa mwisho kabisa akawa Frank na yeye alifariki kwa bacteria kwenye ubongo waliosabishwa na HIV complications.
Nje ya hao Pia nilikuwa na rafiki yangu mwingine mwalimu nilijuana nae wakati ananifundisha Physics A level anaitwa Elias Na yeye na yeye akaja kufariki kwa sababu zinazosemekana ni HIV complications.
Ukweli vifo hivyo vya jamaa zangu vimeniathiri sana kisaikolojia.
Nimekuwa na huzuni sana na uoga mkubwa sana. Najiona Naogopa madem sana mpaka napitiliza.