Vifo vilivyoniumiza JF

Vifo vilivyoniumiza JF

Ukipewa uzima na siha njema mshukuru sana Mungu
Ukiamka huna miadi na tabibu mshukuru sana Mungu
Ukiamka huna kesi polisi mshukuru sana Mungu

Ukiamka una sehemu ya kwenda na ukirudi una sehemu yako mwenyewe ya kupumzisha fuvu mshukuru sana Mungu
Mengine ni changamoto za kawaida za maisha! Kamwe USIKUFURU

Hivi ndio vifo vilivyoniumiza JF
1. Mwalimu Frank.. Mtu mzima above 50 alikumbwq na changamoto za kifamilia.. Tukawa na mawasiliano ya karibu.. Lakini hatimaye akafa akiwa mpweke

2. Miguu ya kuku.. Kijana aliyekuwa na ndoto za kufanya makubwa maishani.. Akapata changamoto za kiafya zilizompelekea kupata ulemavu wa miguu.. Nilishiriki kwa karibu kwenye kutafuta tiba sahihi na suluhu ya kudumu.. Lakini hatimaye alikufa😪

3. Warumi.. Alitikisa vilivyo jukwaa la celebrity.. Akapata changamoto za figo.. Hakutamani kufa mapema.. Mawasiliano yangu ya mwisho na yeye ni wakati nimemwelekeza aende hospital ya figo Kibaha loliondo.. Hakupona alikufa

4. Valentine.. Apumzike kwa amani😪 .. Pamoja na juhudi nyingi za kuonana lakini mpaka kifo kinamchukua hatukuwahi kuonana!

5. Niah.. Huyu kwangu alikuwa Dada.. Ni mama mtu mzima aliyewahi kushika nyazfa za juu serikali ya mchonga na mzee ruksa.. Alijawa na upendo na amewasaidia wengi hata hapa JF..!

6. Gwapo Mwakatobe.. Nilimuita brother. Tulishaonana na tulikuwa na mawasiliano ya karibu. Mchambuzi mahiri wa bbc meza ya duara
Baada ya hustle za maisha akatamani akaishi maisha ya shamba kwenye utulivu.. Alifanikiwa kuhamia huko .. Lakini hakudumu.. Ajali ya boda ikamtenganisha nasi😭
Jana usiku nilijikuta nawakumbuka wote hawa.. Nikajikuta bado nina mamba zao za simu! Nimezifuta zote maana zimenikumbusha mengi

Naogopa sana maana sijui nitaona kifo cha nani tena tunayefahamiana.. Ama je itakuwa zamu yangu kwao!?🙌🏿🏃🏿😭
May All Beings Attain Enlightenment.

🙏🏾🙏🏾🙏🏾
 
Warumi.
Ni zaidi ya rafikii, zaidi ya mtu wa karibu, zaidi ya jiranii, nimekumbuka those days, alikua anakuja Main campus ananichukua ananipeleka maeneo ya kujidai, alikua ananifanya nifurahie uwepo wake kila akiwa karibu yangu, zaidi nilikua napenda mchezo wetu wa kuendesha Gari kwa kufukuzana. Toka aniache mpweke hata road ya Bagamoyo sipiti mara kwa mara tena.
Nipo na warumi huku peponi nimemuonesha comment yako kasema sio kweli. Umemsingizia.
 
Poleni wote kuguswa na Vifo vya wajumbe wenzetu hapa JF

Baadhi nimewahi ku- interact nao kwenye majukwaa kadhaa humu

Kwa kweli ni huzuni iliyoje kusikia habari za kifo cha mtu/watu unaofahamiana nao kwa namna moja ama nyingine

Lakini yapo maneno ya matumaini kwamba, Kuna siku tutakutana nao huko walipoenda
 
Mwana leo kipole, sema nikienda utaona Magnus carlsen kastaafu.
Umeona Carlsen kaandikiwa kitabu?

9781538773031_RetailCover_RetailAndCatalog.jpg
 
Nime-search username Valentina inaonyesha kweli ni RIP, huyu memba alikuwa active sana humu last seen inaonyesha sept 2nd 2025.

Kwa miaka ya nyuma kidogo kuna yule jamaa folk aliondoka kwa kansa ya kongosho,Mungu awarehemu na wote walioondoka bila kupata taarifa za vifo vyao.
 
Job 14: 1-2

[1] Man that is born of a woman is of few days, and full of trouble.
Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu.

[2] He cometh forth like a flower, and is cut down: he fleeth also as a shadow, and continueth not.
Yeye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa; Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe.
 
Back
Top Bottom