Askofu
JF-Expert Member
- Feb 14, 2009
- 1,664
- 87
mzee na wajukuu... lyrics ziko kule kwa mapenzi..
Asante babu:smile-big:
mzee na wajukuu... lyrics ziko kule kwa mapenzi..
Hivi sakata la Karamagi kupoka mke wa mtu lliliishia wapi??? Mwenye mke alienda mahakamani??
Ile habari kwenye youtube imepotea ghafla...Ni bora wangeiweka hapa watu wajionee wenyewe...
itafutwe uwekwe tena tujitahidi kuirejea kila mahala kama wanavyofanya wao ya kuanguka kikwete
Kiranga, tatizo kubwa lililopo hapa ni kwamba Slaa hajajibu mashtaka kwahiyo tunaachwa kwenye speculating side ...ni rahisi ku-miss judge. Jambo la pili ni kuwa huenda kosa la Slaa likapimwa dhidi ya uzito wa matatizo ya CCM. Wengine tunaona bora tuondoke Misri hata ikiwa ni kwa kuongozwa na Musa mwenye kosa la kuua mtu. Kosa moja tunalolifahamu dhidi ya makosa 10,000 ... ni rahisi kuchagua.Nikiondoa siasa zote na kurudi kwenye issue ya mke wa mtu kukaa na mtu mwingine, kabla ya talaka.
Hili halikubaliki, na ni kinyume cha maadili ya ndoa na ya Kiafrika. Unless mniambie huyu mwanamke alikuwa mke wa mtu akapata talaka, which does not seem to be the case here.
Yaani leo tunatetea infidelity kwa sababu aliyetenda ni Slaa ?
Slaa anazidi kujionyesha kwamba hana staha na taadhima za urais. Kama tunaangalia swala la ndoa, mimi ni bora nimchague mtu ambaye hajaoa (na hakai kunyumba na mke wa mtu) kuwa rais kuliko kumchagua mtu anayekaa na mke wa mtu kindoa, bila mke huyo wa mtu kupata talaka rasmi.
Hivi kumbe ni kweli alianguka? Aiseee!!!!!
Jamani kwenye ufunguzi wa kampeni za chadema Dr Slaa alimtambulisha Joshiphine kuwa ni Mke wake hata TBC jana kwenye taarifa ya habari wameonyesha tena
Kiranga,
Wewe ngojea tu!! Walioanzinsha hii vita ya unyumba ni CCM (CCM Strategy); ngoja naye Dr Slaa atakuja na CHADEMA Strategy; have you red a book called ART OF WAR by Sutze?? that is what is going on here; ART of WAR, that is what DR. Slaa is doing all the time! If you are reading well, between the lines you will find that Dr Slaa is a very informed and stragegist; a man who knows the ART of War; what he lacks is; the support of dumb people like you!! WE need to seize time; this is the only time we have!! Look at the big picture first, ECONOMY is our priority!
Kesi hii ipo mahakamani na ni mahakama tu ndiyo itakayosema kama Slaa kachukua mke wa mtu au laa.Kumhukumu Slaa bila hata kuanza kwa kesi hii ni uvunjaji mkubwa wa sheria zinazomuhusu binadamu hasa kipengele cha haki ya kila binadamu kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa"natural justice"!
Dr Slaa bado hajaitwa mahakamani kujitetea lkn ukifuatilia ktk maandiko mengi ya Kiranga ni kama vile tayari Dr Slaa kaisha hukumiwa ktk mahakama za kisheria;kesi iliyopo mahakamani ni ya madai dhidi ya Dr Slaa na ni mahakama tu ndiye itakayoyathibitisha kama ni kweli Dr Slaa ana hatia au la!
Kiranga unamhukumu Dr Slaa kwenye kesi iliyopo mahakamani bila kungojea hukumu halali ya mahakama? Tusubiri mahakama itaamua nini kwenye kesi hii!
Kuna mahakama mbili, mahakama ya sheria na mahakama ya public opinion. Ndiyo maana mtu anaweza kushinda kesi kwa kutumia wanasheria wazuri na mianya ya kisheria, lakini watu wakaona kwamba ana makosa.
Ninachotaka ni Slaa ajieleze kwa wapiga kura, apate kuelewa. Mahakama haipigi kura, wananchi ndio wanaopiga kura.
Wewe unakubali kila hukumu ya mahakama ?
Slaa anazidi kujionyesha kwamba hana staha na taadhima za urais. Kama tunaangalia swala la ndoa, mimi ni bora nimchague mtu ambaye hajaoa (na hakai kunyumba na mke wa mtu) kuwa rais kuliko kumchagua mtu anayekaa na mke wa mtu kindoa, bila mke huyo wa mtu kupata talaka rasmi.
Nyani,
Nitakusoma sawa nikisema kwamba unasema kwamba unafiki haukatazwi katika siasa, na kwamba wale wale waliokuwa wanampigia kelele Kikwete na uongozi wa CCM kwa unafiki na ufisadi na wao wanakamatwa with pants down kwa habari za unafiki na ufisadi ?
Kwamba Slaa aliyepiga kelele sana kuhusu ufisadi wa EPA na yeye ni fisadi tu? Tena wa kuiba mke wa mtu ?
Kwa maana nyingine,
wewe unachagua raisi ambaye kaleta EPA, Richmond, Deep Green, Meremeta, Buzwagi, IPTL, Bulyanhulu, Dowans, TICTS, kamaliza surplus yote BoT - Jakaya Kikwete.
hivi Rose Kamili anasemaje kuhusu sakata hili?
Eti hapa analinganisha ufisadi wa EPA (bilioni zaidi ya mia tatu) na kuchumbia mwanamke aliyeachika!!
Nani kasema mimi nachagua Kikwete ? Wapi ? Unaweza kunionyesha ? Hayo maneno mengine unayatoa wapi?
Eti hapa analinganisha ufisadi wa EPA (bilioni zaidi ya mia tatu) na kuchumbia mwanamke aliyeachika!!
Wanaoshindwa kuwa waaminifu katika maisha binafsi hatuwezi kuwategemea wawe waaminifu katika maisha ya umma.
Ndio maana wengine tulijua hatuwezi maisha ya umma, hata hatukutaka kuwadanganya wananchi kwamba tunaweza dhamana ya kuwaongoza, sasa inaniuma kuona mimi nina adabu angalau ya kujua kwamba sina adabu ya kutosha kuongoza watu, halafu wakati huo huo naona wahuni tu, tena ambao hawana adabu zaidi yangu (angalau mimi sijawahi kumweka mke wa mtu kinyumba) wanataka kuchukua ofisi kubwa kuliko zote nchini kwa unafiki.