Video: Si kuibiwa ni kuzidiwa!

Video: Si kuibiwa ni kuzidiwa!

Status
Not open for further replies.
We Mwanakijiji utaishia tu kutoa "Thank you" au utachangia?
 
Kiranga... yaani leo fasihi imekutoa kapa hata maneno niliyotumia yamekukwepa... "Kuzidiwa" ni neno la makusudi nililotumia.. think about the double take..
 
Kiranga... yaani leo fasihi imekutoa kapa hata maneno niliyotumia yamekukwepa... "Kuzidiwa" ni neno la makusudi nililotumia.. think about the double take..

I don't care about spins za fasihi, hata Hitler, Stalin na Mao wauaji wakubwa wali spin mambo kwa minajili ya fasihi.

Kukaa kinyumba na mke wa mtu ni wrong and decent people should condemn that.

You did not.
 
Ha aha ha defensive my foot!

Mimi nimekuuliza maoni yako na bado nasubiria jibu lako.
Swali la nyongeza kwako, Slaa ameshitakiwa kwa kosa gani?

Slaa ametishiwa mara nyingi sana kushitakiwa na hiyo haikumfanya mvunja sheria.
Kuwa na kesi ya kujibu hakumfanyi yeye mkosaji. Kesi za madai za ajabu na kipuuzi (frivolous lawsuits) zinafika mahakamani mara nyingi sana.

Ilo swali lako la nyongeza, mbona umeshajibiwa na hizi habari hapa Daily News | Dr Slaa sued over woman companion, Dk Slaa afikishwa mahakamani, soma utaona. Mahakama ndio itakayomuhukumu... madai ya huyo mwana tumeshayasikia, sasa nasubiri utetezi wa Slaa...Naona unajaribu kumtetea bila mafanikio, subiri ajitete mwenyewe..maana unazidi kuaribu
 
I don't care about spins za fasihi, hata Hitler, Stalin na Mao wauaji wakubwa wali spin mambo kwa minajili ya fasihi.

Kukaa kinyumba na mke wa mtu ni wrong and decent people should condemn that.

You did not.

kuna vitu vingi vya kucondemn na hili kweli kabisa halijanivuta kulilaani hivyo kwani kuna kanuni nilishazisema sitozivunja na hii ni mojawapo.
 
Kiranga,
Mkuu wangu ni wapi Dr.Slaa kamtambulisha kama ni mkewe? mbona unaongeza sasa mambo hata kama.

Swala kubwa kwako ni ule unyumba ambao kimila inaonyesha jamaa alikwisha mtema mwanamke jambo ambalo kidini hakubaliwi. Hivyo alipomwacha kwa miezi sita alifikiria lile ni gari bovu atakuja kwa wakati wake kuliendesha. Mbona tunawadhalilisha wanawake kiasi hiki yaani tukikubali kesi kama hii ina maana moja tu kwamba tunatazama upande wa wanaume kulingana na matakwa yetu ya kiume. Dr.Slaa hajamuoa huyu bibie hadi sasa hivi. Na tukisema hivyo unageuza maswala kuwa ya kinyumba na mke wa mtu. Kuwepo kwa separation hutaki kusikia kwa sababu tu Dr.Slaa ni Chadema haruhusiwi kupenda mke wa mtu wakati wowote hata kama katengana na mmewe. Sasa hii tunaingia katika dini na sio sheria ya nchi. hakuna makombo hapa mkuu wangu ukiacha wengine wanachukua.
 
Wewe ni supporter wa ccm (mpondeaji mkuu wa chadema).
Eti anamlinganisha mtu aliyeleta EPA, Buzwagi, richmond, etc na mtu aliyemchumbia mwanamke aliyeseparate toka kwa mme wake

Inahusu ?? Na wewe ni supporter wa Chadema (mpondeaji mkuu wa ccm)...
 
Mimi nasubiri "Case" ianze kusikilizwa ili nifahamu UKWELI - naona bado kuna jambo halijawekwa bayana labda mpaka "Case" itakapoanza

BTW: Hii ni "Case" ya MADAI au JINAI au?
 
Haya mambo bana haya...huwaga yana namna ya kuwaadhiri sana watu hasa wale walio mstari wa mbele kukemea dhambi au mapungufu binafsi ya wenzao...
 
I don't care about spins za fasihi, hata Hitler, Stalin na Mao wauaji wakubwa wali spin mambo kwa minajili ya fasihi.

Kukaa kinyumba na mke wa mtu ni wrong and decent people should condemn that.

You did not.

Kesi hii ipo mahakamani na ni mahakama tu ndiyo itakayosema kama Slaa kachukua mke wa mtu au laa.Kumhukumu Slaa bila hata kuanza kwa kesi hii ni uvunjaji mkubwa wa sheria zinazomuhusu binadamu hasa kipengele cha haki ya kila binadamu kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa"natural justice"!

Dr Slaa bado hajaitwa mahakamani kujitetea lkn ukifuatilia ktk maandiko mengi ya Kiranga ni kama vile tayari Dr Slaa kaisha hukumiwa ktk mahakama za kisheria;kesi iliyopo mahakamani ni ya madai dhidi ya Dr Slaa na ni mahakama tu ndiye itakayoyathibitisha kama ni kweli Dr Slaa ana hatia au la!

Kiranga unamhukumu Dr Slaa kwenye kesi iliyopo mahakamani bila kungojea hukumu halali ya mahakama? Tusubiri mahakama itaamua nini kwenye kesi hii!
 
Mapmbano,
Hivi kweli nyie haiwaingii akilini kwamba kama kuna makosa yoyote yale yamefanywa ni mke ndiye anapaswa kushtakiwa ktk kesi ya madai. Dr.Slaa angeshtakiwa tu kama kaiba huyo mke pasipo hiari yake lakini inaonyesha wazi ni mke aliyekwenda kwa Dr.Slaa na anaishi kwa mapenzi yake mwenyewe tena baada ya kuachwa miezi sita. Ndoa hakuifunga Dr.Slaa na huyo mbabaishaji wala Slaa na huyo mwanamke hivyo unamshtaki kwa makosa yapi?

Mkandara, ni kweli makosa yanaweza kuwa ya mke (First lady mtarajiwa)...but it takes two to tango..Ukweli utajulikana kesi ikisikilizwa.
 
Kesi hii ipo mahakamani na ni mahakama tu ndiyo itakayosema kama Slaa kachukua mke wa mtu au laa.Kumhukumu Slaa bila hata kuanza kwa kesi hii ni uvunjaji mkubwa wa sheria zinazomuhusu binadamu hasa kipengele cha haki ya kila binadamu kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa"natural justice"!

Dr Slaa bado hajaitwa mahakamani kujitetea lkn ukifuatilia ktk maandiko mengi ya Kiranga ni kama vile tayari Dr Slaa kaisha hukumiwa ktk mahakama za kisheria;kesi iliyopo mahakamani ni ya madai dhidi ya Dr Slaa na ni mahakama tu ndiye itakayoyathibitisha kama ni kweli Dr Slaa ana hatia au la!

Kiranga unamhukumu Dr Slaa kwenye kesi iliyopo mahakamani bila kungojea hukumu halali ya mahakama? Tusubiri mahakama itaamua nini kwenye kesi hii!
Hapana mkuu wangu wananchi wana kila haki ya kuhoji kesi hii wala sio dhambi hata kidogo. Na wanaweza kuhukumu ktk mazungumzo yao maadam hayawezi kuathiri matokeo ya hukumu.

Sisi tuendelee kuzungumza na hata kupingana kwa sababu tunatafuta majibu yetu ili kesho hukumu itakapo tolewa tutajua kaonewa au ni haki. ndivyo tulivyowamshutumu Mafisadi na tutaendelea kuwashutumu ambao tunafikira walifanya makosa.
Kama Kiranga anaona kuna makosa ni bora ayaweke wazi lakini hili la kusema ati Dr. Slaa amekaa na mke wa mtu hali hajui kwamba jamaa yake alimtema yule mwanamke siku nyingi akidhania kamweza kumbe bibie alikuwa akidai bado na mashujaa wameweka ndani kama vile imerushwa sadakallahu mwenye kupata. Dr. Kajiokotea mali kama ule wimbo wa mkulima mwema. Leo imeonekana ni dhahabu oooh ilikuwa ktk shamba langu... alaaah!
 
Kesi hii ipo mahakamani na ni mahakama tu ndiyo itakayosema kama Slaa kachukua mke wa mtu au laa.Kumhukumu Slaa bila hata kuanza kwa kesi hii ni uvunjaji mkubwa wa sheria zinazomuhusu binadamu hasa kipengele cha haki ya kila binadamu kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa"natural justice"!

Dr Slaa bado hajaitwa mahakamani kujitetea lkn ukifuatilia ktk maandiko mengi ya Kiranga ni kama vile tayari Dr Slaa kaisha hukumiwa ktk mahakama za kisheria;kesi iliyopo mahakamani ni ya madai dhidi ya Dr Slaa na ni mahakama tu ndiye itakayoyathibitisha kama ni kweli Dr Slaa ana hatia au la!

Kiranga unamhukumu Dr Slaa kwenye kesi iliyopo mahakamani bila kungojea hukumu halali ya mahakama? Tusubiri mahakama itaamua nini kwenye kesi hii!


Pia huyu jamaa anayedai anahaki sawa na Slaa, kwa hiyo sio sawa kumuhukumu kuwa ni mbabaishaji,kwa upande mwingine wa shilingi
 
Mkandara, ni kweli makosa yanaweza kuwa ya mke (First lady mtarajiwa)...but it takes two to tango..Ukweli utajulikana kesi ikisikilizwa.
Bila shaka lakini kesi inamhusu Dr.Slaa otherwise hakuna kesi ikiwa hawa wawili wametango!
 
I don't care about spins za fasihi, hata Hitler, Stalin na Mao wauaji wakubwa wali spin mambo kwa minajili ya fasihi.

Japo huwezi kuona tatizo la kulinganisha nilichosema mimi na hawa kuwa ni unnecessarily reckless utatafuta namna ya kuhalalisha kwanini unafikiria nimefanya spin.

Kukaa kinyumba na mke wa mtu ni wrong and decent people should condemn that.

Hapa tunatofautiana kwa sababu dhamira ya mtu ni kuu kuliko. Kama huyo mama alijijua kuwa bado ni mke wa mtu na akaamua kumuacha mume wake na akamfuata mtu ambaye naye alikubali moyo wake wewe na mimi ni nani kucondemn kitendo ambacho kimetokana na dhamira na kiko katika suala la binafsi? Hawa ni watu wazima na wamefanya maamuzi yao wao wenyewe na it is none of your business, na wala siyo ya CCM wala mtu mwingine yoyote. Mtu mwenye hoja hapo ni mume wa huyo mama na peke yake anatakiwa kucondemn au kugombania mke wake arudi (siyo arudishwe kwani hajatekwa).
 
Pia huyu jamaa aliyedai anahaki sawa na Slaa, kwa hiyo sio sawa kumuhukumu kuwa ni mbabaishaji,kwa upande mwingine wa shilingi
Nitakupeni kesi moja ya huku majuu.
Kuna jamaa mmoja alioa mke kutoka Bongo akamleta huku. Ikatokea kwamba yule bibie alikuwa akiviwasha na roomate wake mara mume akiondoka kwenda kazini. jamaa wakamtonya mwenye mke, siku moja jamaa akaaga kama anakwenda kazini kisha akarudi ghafla na kuwakuta wajomba wanapiga zoezi la nguvu. Mjomba hakuvumilia akawa twanga wote magumi.. mara Polisi hao. Walipofika jambo la kwanza walimhoji mwanamke ambaye alisema jamaa ni abusive vibaya sana na hakika kawapiga bila makosa yoyote akidhani kwamba wao wanafanya mchezo mbaya.

Polisi walimuuliza yule mwanamke je unataka kuweka mashtaka? mwanamke akasema hapana ila anahofia usalama wake kwani jamaa anaweza kumfanyizia wakiondoka. basi wakuu zangu jamaa aliondolewa toka ktk nyumba yake mwenyewe, akapigwa marufuku ya kufika maeneo hayo kwa mita 200 kisha yule mjomba asiekuwa na mke akakabidhiwa mali kuishi nayo. Kila kitu ndani ya nyumba ni mali ya mjomba alofukuzwa yule roomate alikuja na mswaki tu. sasa kakabishiwa kila kitu pasipo kujali cheti cha ndoa wala gharama za harusi na kumleta mwali toka Bongo.

Kwa hiyo hizi sheria wakuu zangu ziogopeni na hasa huyu mjomba kwa sababu kama mwanamke aliondoka kwa sababu huyu jamaa alikuwa abusive na pia kawaacha hata watoto wake kwa miezi sita pasipo kuwajali, nadhani kesi inaweza mgeuka yeye na ndio maana hakumshitaki mkewe kwa sababu ndiye haswa anatakiwa kusimama kizimbani na sio Dr.
 
chadema wanasema wao na waumini wazuri wa siasa za nyerere na wanaamini kuwa mwalimu alikuwa mtu safi na mwenye dira


aliwalaumu sana marais waliofatia baada ya yeye kwa kulifuta azimia la arusha na kupora rsource za nchi na mengineyo kwa uoni wao


sasa mwalimu aliwahi kututolea mfano wa waziri mmoja uingereza ambae alituhumiwa tu kuwa alikuwa akitembea na mtu wa barabarani, basi ile tuhuma ikaenea na yule waziri alipoona vile akaamua kuandika barua kwa waziri mkuu kumuomba ajiuzulu, waziri mkuu hakumjibu yeye aliteua waziri mwengine kushika ile nafasi

akasisitiza tuhuma tu mtu anatakiwa ajiepushe nazo.

sasa turudi kwa huyu wetu dr Slaa, haoni kuwa anastahiki kuacha kuendelea na kampeni na kujiuzulu uongozi wa chadema kwa kufata miko ya maadili. na kuonyesha kwa kweli kuna mapungufu pahala na kutafuta suluhisho hadi hizo tuhuma zithibiti si kweli ndio arudi?



nnawalaumu sana CHADEMA mtu kama huyu kumuacha kuendelea kuzunguka kwenye kampeni maana, sasa watanzania intertionally watataka wamuone mzinzi na si mgombea urais kitu ambacho kinadestroy image ya chama na pia kinadestroy image ya mgombea wake.

mm huwa nnajiuliza tunaifunza nn jamii tunapoona kiongozi anaetaka kuiongoza nchi kama hii kusimama mbele ya watu na kukiri niliishi na mwanamke na kuzaa nae watoto wawili sijamuoa, na huyu nnaishi nae ni mchumba wangu, kwangu ni aibu nikiamini kuwa dini zote mbili zinakataza utaratibu wa kuzini na mtu kwa kuporwa au kinyume kabla ya kumuoa.

tatu jamaa kufungua kesi mahakamani si kweli kuwa imemsaidia Dr slaa kwa kuwa waandishi na vyombo vya habari watakuwa hawawezi kulizungumzia tena, na kinachobaki ni hukumu toka mahakamani. hii inamuumiza zaidi maaana hata yeye hatoweza tena kujitetea na kurejesha imani kwa watu ambayo tayari ishapotea

mwisho bila kigugumizi nasema huyu ni muhuni tu
 
Mtu wa Pwani,
sasa mwalimu aliwahi kututolea mfano wa waziri mmoja uingereza ambae alituhumiwa tu kuwa alikuwa akitembea na mtu wa barabarani, basi ile tuhuma ikaenea na yule waziri alipoona vile akaamua kuandika barua kwa waziri mkuu kumuomba ajiuzulu, waziri mkuu hakumjibu yeye aliteua waziri mwengine kushika ile nafasi akasisitiza tuhuma tu mtu anatakiwa ajiepushe nazo.
Mkuu mfano huu unamaanisha nini kwako? Dr. Slaa atajiepusha vipi na tuhuma hali kamwonyesha mpenzi wake mtarajiwa mbele ya watu kuwa ni mchumba wake.. Yule waziri angefanya hivyo ingekuwa kosa lipi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom