VIDEO: Rais wa Sudan na Mwenyekiti mpya wa EAC alivyoshindwa hata kujua Marais wa Nchi nyingine

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,120
Viongozi wa Mataifa ya Afrika wana shida gani jamani? Kwanini uendelee kung'ang'ania Madarakani wakati una hali mbaya kiafya? Kazi yenyewe ya stress sana bado ukomalie kubaki hapo badala ya kulea Wajukuu.

Hapo anaonekana pamoja na kuwa na Karatasi ya Hotuba bado anashindwa kutaja majina ya Marais wa Nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
 

Waliompa huo uongozi wa Jumuiya ndio wananishangaza zaidi.

Huyu Rais amejikojolea hadharani wameona, ameenda Urusi akashindwa hata kuongea wameona. Bado wamempa uongozi wa jumuiya? Afrika ni kama ina laana.
Katiba ya EAC uongozi ni wa mzunguko nchi baada ya nchi, huwezi kupindisha hilo kwa kukataa kumpa uenyekiti maadam yuko madarakani.
 

Waliompa huo uongozi wa Jumuiya ndio wananishangaza zaidi.

Huyu Rais amejikojolea hadharani wameona, ameenda Urusi akashindwa hata kuongea wameona. Bado wamempa uongozi wa jumuiya? Afrika ni kama ina laana.
Ni rotational based leadership mkuu ambayo nchi inapewa sasa kama nchi ina kiongozi kama huyo imekula kwenu hamwezi kuiruka
 
Viongozi wa Mataifa ya Afrika wana shida gani jamani? Kwanini uendelee kung'ang'ania Madarakani wakati una hali mbaya kiafya? Kazi yenyewe ya stress sana bado ukomalie kubaki hapo badala ya kulea Wajukuu.

Hapo anaonekana pamoja na kuwa na Karatasi ya Hotuba bado anashindwa kutaja majina ya Marais wa Nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Halafu wazungu wakituita manyani watu wanajiliza tunatukanwa. Ukiachia huyo kiongozi kutokubali ukweli kuwa muda umemtupa mkono, hao viongozi wengine hawakuona kuwa hastahili kutokana na afya yake?
 
Katiba ya EAC uongozi ni wa mzunguko nchi baada ya nchi, huwezi kupindisha hilo kwa kukataa kumpa uenyekiti maadam yuko madarakani.
Asante kwa kunikumbusha. Sasa hii ni aibu kwa jumuiya nzima, kama huyu ndio kiongozi wa jumuiya ni kitu gani watajadiliana humo? Namna ya kupata viongozi inapaswa kuangaliwa upya.
 
Back
Top Bottom