Uzuri wa mwanamke upo wapi? Ni upi?

Uzuri wa mwanamke upo wapi? Ni upi?

Dhana ya uzuri/ubaya ni pana sana: kuna uzuri/ubaya wa sura na uzuri/ubaya wa tabia. Hii ni kwa wote, wanaume na wanawake: Wapo wazuri wa sura na tabia, wazuri wa sura wabaya tabia na kinyume chake. Lakini kama walivyosema wengi, uzuri na ubaya umo katika macho na mawazo yako. Ninayemhisi mimi mzuri wa sura anaweza kuwa mbaya kwa wengine. Ninayemwona anatabia mbaya, tabia hizo hizo zinaweza kuwa nzuri au angalau kuvumilika kwa wengine. Uchaguzi ni wako, unataka nani na kwa ajili gani.
Sawa mkuu, twaenda pamoja hapo!
 
My mother's Boy friend I used to call him my Dad once told me as a man, "every woman on earth is beutiful of her own kind but a little thing to note on a woman is that her beuaty is defined with her actions and omissions, what make you feel her the way you feel is what she can make you feel in that way, she can stand unto both status a time if you want her to be so". Mke au mwanamke hata akiwa mzuri njinsi gani machoni pako, haimaanishi yu mzuri hivyo hivyo akilini kwako, atadumu kuwa mzuri iwapo atadumisha yale yanayokufanya ufikiri yeye ni mzuri kwako, akipoteza kamwe hawezi kuwa mke mzuri tena. Vionjo vyetu kwa wenzetu na ambavyo wakitufanyia ndivyo vinatupa raha na furaha ndivyo vitufanyavyo tudhani wao ni wazuri kwetu, bali wakifanya vikatutia uchungu wa shubiri kamwe hawawezi kubakia na uzuri tunaoweza kuwasifia.
Safi sana mkuu Ngoswe! Hapo ndipo nikupendapo kwa uchambuzi wako wenye facts na explanations zilizoshiba. Nimekusoma mkuu!
 
Beauty Lies in the Eyes of a Beer Holder....., Seriously though... uzuri wa mwanamke its a package (ni mambo mengi, depends na your priority).. "You don't love a woman because she is beautiful, but she is beautiful because you love her "
Hekima kama Suleiman!!! Hakika!!
 
Kama ana tabia mbovu hata awe na wowowo kama la kumimina, jicho linaloita limesheneni nyusi na kope za hali ya juu, mguu wa uhakika na sura kama ya malaika, lips zilizojaa na zinavutia sana kwa vijuisi kwa maoni yangu si mali kitu kama ana tabia mbovu ambayo haiwezi kuvumilika kabisa na yeyote yule atakayetaka kuwa karibu na dada wa mzuri kiasi hiki.
 
Hapana, Ideal yaweza kuwa the same bt explaination tofauti, hebu tilia mkazo yako bwana! Ni kweli vigezo vya kuclassify hutofautiana!
msisitizo ni kwamba hatuwezi kuweka vigezo vya mwanamke mzuri na vikafaa kwa wanaume wote. kila mtu ana mtaZamo wake tofauti na mwingine, hivyo kila couple imeingia kwenye relationship kwa vigezo tofauti sana na couple nyingine, ni wale wawili either wanakuwa na vigezo vyao vinavyofanana vya tabia, muonekano, dini , kabila, etc ndio wanaget into relationship, otherwise kama hakuna kinachomatch between them hawawezi kuwa pamoja. mimi nina mume na kabla ya kuolewa nilikuwa nimeshajiwekea vigezo vya mchumba ninaemtaka, na mwenzangu hali kadhalika, tulikuwa tunafanya kazi pamoja na tulianza kwa kuwa marafiki tu,, baadae tukagundua tunafanana kwa mambo mengi na hiyo ikawa sababu ya kuanza serious relationship na hatimae tumeona kwa miaka kibao sasa. na mpaka leo, apart from being mume and father of my kids is also rafiki yangu mkubwa.
 
Natumai hata wewe umeisha jiuliza hili swali, sasa kwa pamoja tujadili, na tuafikiane juu ya uzuri wa mwanamke. Swali hapa ni: "je uzuri wa mwanamke upo wap? Ni upi?" je ni mbele? Nyuma? Juu? Chin? Katikati? Ndani? Nje? Or? Kifupi binafsi cjaelewa. ukitaka jibu kwa ufasaha hebu make ur imaginatios kwa mke/mpenz wako, hususani penzi lako kwake!

Upo kichawani mwake.....i mean IQ
 
Kama ana tabia mbovu hata awe na wowowo kama la kumimina, jicho linaloita limesheneni nyusi na kope za hali ya juu, mguu wa uhakika na sura kama ya malaika, lips zilizojaa na zinavutia sana kwa vijuisi kwa maoni yangu si mali kitu kama ana tabia mbovu ambayo haiwezi kuvumilika kabisa na yeyote yule atakayetaka kuwa karibu na dada wa mzuri kiasi hiki.
Tabia yahusika sana, mwanamke anatakiwa awe na tabia nzuri yenye kuendana na uzuri wake. Mwanamke anatakiwa ajiheshimu!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tabia yahusika sana, mwanamke anatakiwa awe na tabia nzuri yenye kuendana na uzuri wake. Mwanamke anatakiwa ajiheshimu!

unanikumbusha wimbo fulani wa zamaniiii ...'uzuri si hoja tabia njema ni silaha utapendwa popoteee ..." lakini haya ni kwa ajili ya mwanamke ambaye unataka kuwa nae kwenye serious relationship kama ndoa, lakini kwa wale ambao ni wakutambia tu barabarani, disko na mwishlo kuishia guestt house a.k.a nyumba za wenyeji basi sifa za makalio marefu, miguu ya bia, shingo za upanga, macho gololi n.k. ndio mahala pake.
 
unanikumbusha wimbo fulani wa zamaniiii ...'uzuri si hoja tabia njema ni silaha utapendwa popoteee ..." lakini haya ni kwa ajili ya mwanamke ambaye unataka kuwa nae kwenye serious relationship kama ndoa, lakini kwa wale ambao ni wakutambia tu barabarani, disko na mwishlo kuishia guestt house a.k.a nyumba za wenyeji basi sifa za makalio marefu, miguu ya bia, shingo za upanga, macho gololi n.k. ndio mahala pake.


huu ndo ufafanuzi ambao Gagurito alikuwa akiuhitaji.............................
 
mhadhili umeacha kunifundisha baiolojia imebidi nisome bible. Ulipotelea wapi wewe?

uliponipiga kibuti nikaamua nitimue tu bana isiwe tabu. na kuanzia kesho napotea tena mpaka ukubali ng'ombe wangu wa mahari.
 
heheheheeh looool dah! hakyababu walosema husninyo katulia basi wanapata zambi.
walosema nimetulia ndio magrt thinkers wa ukweli. Kuna tetesi umekatorosha kapaseli, naomba ukarudishe kabla hakajakuchafulia hali ya hewa huko.
 
Uzuri wa mwanamke uko kwa anaetazama pia kwenye hisia za anaetazama na kuukubali uzuri huo.Chuki...hasira hua vinafanya watu wasione uzuri wa mtu/kitu fulani...wakati mwingine hata kama uzuri unaonekana lazima mabaya yataonekana yamezidi hivyo kulemea na hata kupoteza uzuri wote.Mapenzi hua yanawafanya wengi waone mazuri zaidi ya mabaya.Mtu anaposema uzuri wa mwanamke uko kwenye tabia..sura..umbo na kadhalika ukweli unakuwepo ila vyote vinapingika.Yote inategemea na yule mtazamaji ambae anaeamua fulani ni mzuri au la...kila mmoja kwa wakati na vigezo vyake.Ndio maana unaweza kutana wapenzi ukajiuliza huyu dada/kaka kafuata nini kwa aliyenae ilhali mi namjua ana tabia mbaya sana ila umbo ni zuri....au mbona hata sura na umbo halilipi bali tabia yake inakubalika?!Yote hii inatokana na utofauti kati yetu.Na ndio maana kuna baadhi utawasikia wakisema mara sijui wanawake wazuri kwa umbo hawaolewe/oleki japo sio kweli.Wengi tu wameolewa hata wenye tabia nzuri maana wapo wanaune ambao sura na umbo ni namba moja kwao...wale unaoweza kuwaita ni wabaya nao wapo wasioolewa japo tabia zao ni nzuri sana.Kwa kumalizia nasema...uzuri wa yeyote awe mwanamke au mwanaume upo kwenye macho na hisia za mtazamaji!
 
Back
Top Bottom