Uwekezaji wa majengo haulipi

Uwekezaji wa majengo haulipi

Kwa kizazi kijacho hakuna shida, ila wewe uliyewekeza ni sawa na umepoteza.
Sahihi na watu wanaamini zile laki tatu tayu
Mfano nina milioni 200, itanichukua miaka mingapi kuipata hiyo milioni 200 niliyoiwekeza?
nyumba hiyo kwa mwezi unachukua 1Milioni, kwa mwaka unapata 12milioni.

Itakuchukua miaka 20 mzee, na hapo tumezingatia kila mwezi una wateja na uhalisia hauko hivyo unaweza kukata miezi hata sita unatafuta wateja au miezi mitatu.
 
Watanzania biashara au uwekezaji wetu huwa tunafikiria kwa muda mfupi, na muda wote tunataka super profit tena kwa muda mfupi iwezekanavyo. Ndiyo maana unakuta dalali anataka akiuza nyumba, ile faida anayopata akajenge nyumba yake. Ndiyo, najua shilingi yetu huteremka thamani sana, lakini duniani kote ukiwekeza kwenye nyumba huwezi kutegemea fedha ulizojengea zirudi kwa muda mfupi. Chukulia hivi. Nyumba haishuki thamani, na ile kodi unayochukuwa kila mwezi ndiyo faida yako. Yaani kama unachukuwa milioni mbili, basi hiyo ndiyo faida yako, na mtaji wako unabaki kama ulivyo. **nyumba ikijengwa kitaalam na eneo zuri inachukuwa muda kufanyiwa marekebisho makubwa. Kutoka kwenye kodi weka asilimia ndogo kila mwezi ambayo itafanya ukarabati wakati ukifika. Ila ukijenga kibongo-bongo miaka 10 tu unakuta nyumba inadai kubomolewa ijengwe nyingine.
Umefafanua vizuri mkuu
 
Kuwekeza kwenye majengo ni sawa na fedha zako kuzifukia sehemu, na kuanza kuila kidogo kidogo mpaka iishe. Na kula huko unakuwa hauli faida zaidi ya kula mtaji (fedha ulioiwekeza). Wengi ukimbilia kujenga nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k huku wakijipa matumaini majengo hayo yatawalipa na kupata faida zaidi na zaidi. kwa ujumla majengo hayo uwapa hasara, vinginevyo mmiliki hatonufaika zaidi ya kizazi chake kijacho ambacho ndio kitakuwa kinakula faida baada ya miaka kadhaa kupita. Ukitaka kuamini hili, tembelea nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k zipe miaka mitano alafu ukazitembelee tena, utazikuta zimechoka na kama hakutokuwa na hela ya ziada ya ukarabati, ndio hivyo biashara inakuwa imekufa.​
Uwekezaji ni jambo la muda mrefu, ni sawa hata usipofaidika wewe wafaidike kizazi chako. Si kama maghorofa ya kariakoo tu
 
Kuwekeza kwenye majengo ni sawa na fedha zako kuzifukia sehemu, na kuanza kuila kidogo kidogo mpaka iishe. Na kula huko unakuwa hauli faida zaidi ya kula mtaji (fedha ulioiwekeza). Wengi ukimbilia kujenga nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k huku wakijipa matumaini majengo hayo yatawalipa na kupata faida zaidi na zaidi. kwa ujumla majengo hayo uwapa hasara, vinginevyo mmiliki hatonufaika zaidi ya kizazi chake kijacho ambacho ndio kitakuwa kinakula faida baada ya miaka kadhaa kupita. Ukitaka kuamini hili, tembelea nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k zipe miaka mitano alafu ukazitembelee tena, utazikuta zimechoka na kama hakutokuwa na hela ya ziada ya ukarabati, ndio hivyo biashara inakuwa imekufa.​
Haujui chochote kuhusu uwekezaji wa majengo. Acha kupotosha watu. Kajifunze
 
Inaonekana mtoa mada hana uzoefu kwenye huo uwekezaji wa real estate

Biashara ya lodge & hotel ni uwekezaji unaolipa (speaking from my own experience), nimewekeza kiasi huko

Niliwekeza shilingi 170M hivi awali, lakini baada ya miezi 14 hivi hela yangu ilirudi kupitia hiyo hiyo biashara ya lodge

Miaka miwili mbele, nikajenga lodge ya pili kupitia lodge ya awali

Ukipata location nzuri, biashara ya lodge haiwezi kukutupa

Jambo la kuzingatia, ni kufanya maintenances za mara kwa mara, shower ikiharibika, unatakiwa ukai-replace, sijui TV hainoeshi unatakiwa ukairekebishe ili wateja wasije wakaanza kukulalamikia

Niliwahi kupata wazo la mkumbo la kwenda kuziweka hizo hela kwenye hisa/bond n.k lakini nimegundua kupitia biashara hii ya real estate unapata return nzuri kuliko kwenda kuziweka hela huko..

Ukiwa na shida ya milioni 50 ama 70 unakwenda kukopeshwa na benki bila shida yeyote huku ukipata nafasi ya kupanua wigo wa biashara yako
 
Kuwekeza kwenye majengo ni sawa na fedha zako kuzifukia sehemu, na kuanza kuila kidogo kidogo mpaka iishe.

Na kula huko unakuwa hauli faida zaidi ya kula mtaji (fedha ulioiwekeza). Wengi ukimbilia kujenga nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k huku wakijipa matumaini majengo hayo yatawalipa na kupata faida zaidi na zaidi.

Kwa ujumla majengo hayo uwapa hasara, vinginevyo mmiliki hatonufaika zaidi ya kizazi chake kijacho ambacho ndio kitakuwa kinakula faida baada ya miaka kadhaa kupita.

Ukitaka kuamini hili, tembelea nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k zipe miaka mitano alafu ukazitembelee tena, utazikuta zimechoka na kama hakutokuwa na hela ya ziada ya ukarabati, ndio hivyo biashara inakuwa imekufa.​
Sawa mkuu
 
Mfano nina milioni 200, itanichukua miaka mingapi kuipata hiyo milioni 200 niliyoiwekeza?
hiyo nyumba tayari ni mtaji kama ulitumia million 200, basi miaka 5 mbele ukitaka kuiuza utakuta imeshafika 250 au 300. kwasababu ardhi pia inapanda thamani

sasa wewe unavyosema ukusanye tena kodi hadi zifike 200 unakosea namna ya kufikiri
 
hiyo nyumba tayari ni mtaji kama ulitumia million 200, basi miaka 5 mbele ukitaka kuiuza utakuta imeshafika 250 au 300. kwasababu ardhi pia inapanda thamani

sasa wewe unavyosema ukusanye tena kodi hadi zifike 200 unakosea namna ya kufikiri
Nyumba haipandi thamani
 
Inaonekana mtoa mada hana uzoefu kwenye huo uwekezaji wa real estate

Biashara ya lodge & hotel ni uwekezaji unaolipa (speaking from my own experience), nimewekeza kiasi huko

Niliwekeza shilingi 170M hivi awali, lakini baada ya miezi 14 hivi hela yangu ilirudi kupitia hiyo hiyo biashara ya lodge

Miaka miwili mbele, nikajenga lodge ya pili kupitia lodge ya awali

Ukipata __cpLocation nzuri, biashara ya lodge haiwezi kukutupa

Jambo la kuzingatia, ni kufanya maintenances za mara kwa mara, shower ikiharibika, unatakiwa ukai-replace, sijui TV hainoeshi unatakiwa ukairekebishe ili wateja wasije wakaanza kukulalamikia

Niliwahi kupata wazo la mkumbo la kwenda kuziweka hizo hela kwenye hisa/bond n.k lakini nimegundua kupitia biashara hii ya real estate unapata return nzuri kuliko kwenda kuziweka hela huko..

Ukiwa na shida ya milioni 50 ama 70 unakwenda kukopeshwa na benki bila shida yeyote huku ukipata nafasi ya kupanua wigo wa biashara yako
Baada ya miaka 5 uje utupe mrejesho wa hayo majengo
 
Samsung ni conglomerate kubwa sana, ni chaebol kule South Korea ina biashara nyingi kubwa ikiwemo consumer electronics, inatengeneza silaha kama vifaru, inaunda meli kubwa, ina funds na securities ila bado imewekeza kwenye real estate.

Hakuna tajiri anawekeza kwenye nyumba akiwa njaa hana hela, labda mtumishi. Ukiona mtu anazika hela kwenye jengo ujue tiyari anayo hiyo biashara unayomlazimisha awekeze. Au unahisi mtu anaokota hela ndio anajenga?
Kwa nini hoteli nyingi zinachakaa wakati zinaingiza fedha?
 
Leta elimu yako ukiwa na mchanganuo wa miaka 5
Ungekuwa na nia ya kuelewa ungejifunza kwanza kabla uya kuja kuandika hapa. Hata hivyo nitakupa dondoo chache.

1. Kwanza maintenance ya nyumba inafanyika baada ya miaka 15 au zaidi. Siyo kila baada ya miaka 5. Nyumba iliyojengwa vyema miaka. 10 bado mpya kabisa. Kwenye hotel unaweza badilisha furnitures baada ya miaka 6 to 7. Lakini rangi na fittings baada ya miaka 15. Cha msingi utumie mafundi wazuri na materials zenye ubora.

2. Nyumba ni uwekezaji wa muda mrefu. Hapa tunaongelea rerurn on investment (ROI) ya miaka 8 - 15 kutegemea na matumizi ya nyumba. Hotel/Lodge zinarudisha fesha haraka zaidi.

3. Ukijenga nyumba ya kupangisha ukiwa na miaka 40, ROI ya 10 years.. Ukabahatika kuishi miaka 60, 70 tayari unakula matunda ya uwekezaji wako.
4. Nyumba inaongezeka thamani ni kweli ingawa mimi binafsi hili huwa siliweki maanani, na siyo kipambele changu.

Sasa ngoja nikupe mfano
Mfano: Nunua kiwanja 30-50m. Tufanye 50m Weka. Nyumba 3, 2 za 2-bedroom na 2 za 1 bedroom na sebule, jiko choo. Fanya simple but quality., finishing nzuri. Hizi nyumba zitagharimu kiasi cha 80m. Kwa hiyo jumla ya uwekezaji wako ni 130m. Za 2 bedroom utapanganisha kwa 250,000 na bedroom utapangisha kwa 200,000. Makusanyo kwa mwezi 900,000. Jumla ya makusanyo baada ya miaka 10 ni. Kama 108m. Ni. Kwelihaijarudisha fedha. Lakini wenzako wanacholifanya hizo fedha za kodi kidogo kidogo wanaenda ku zi invest kwenye UTT na sehemu zingine za uwekezaji. So piga hesabu kama unawekeza 900000 kila mwezi kwa miaka 10.

tena utamu wa bongo nimkwamba unapokea pesa ya miezi 6 au 3 hivyo unawekeza fedha ambayo ungeioata miezi 6 ijayo ila wewe umpeipata leo na ku invest leo.

Kaa na maujinga yako.
 
Back
Top Bottom