Uwekezaji wa majengo haulipi

Uwekezaji wa majengo haulipi

Biashara hii inategemea na wapi umewekeza, jengo la aina ile ile ubora ule ule, kodi inatofautiana sehemu na sehemu, location ndio jambo kubwa zaidi kwenye biashara nyingi.
na ubora wa ujenzi ulioufanya.. miaka mi5 ukarabati tena mkubwa hayo ni maajabu mkuu.

Nimefanya sehemu kwa udogo, naona faida yake, ningekuwa na uwezo ningefanya kwa ukubwa zaidi, ni biashara nzuri, haina stress na inalipa vizuri.

Mfano mie nijenge frem za biashara 5 kwa milioni 30, kodi ni laki 2 kwa mwezi,hapo nakuwa nakunja milioni kila mwezi, kodi ya miezi 6 ni milioni 6.. nakunja hiyo pesa wakati jengo(milioni 30) lipo, yaani hizo milioni kila mwezi ni faida.
Issue ni location mkuu. Kuna maeneo mengine hizo frame hazina wateja kabisa
 
Issue ni location mkuu. Kuna maeneo mengine hizo frame hazina wateja kabisa
Sahihi mkuu, komenti yangu ilisisitiza hapo kwenye location, biashara nyingi location ndio jambo la msingi mnoo, fremu ile ile, chumba kile kile, nyumba ile ile lakini kodi inatofautiana kutegemea iko wapi
 
Je marek

Je marekebisho yake hayo ni sawa na kujenga jengo upya? Marekebisho yanachukua hata 25%? Jibu hapana.
Kwa mimi kama itafika hiyo miaka 10, bado nitakuwa na faida kubwa sana mkuu, mie ujenzi ukijumlisha na utoto wa mjini, fundi huyu mnajuana, huyu mnapozana, ni ile miaka mi3 tu ya mwanzo pesa ilikuwa isharudi, hapa nakula faida, hii miaka miwili ni ya faida mwaka mmoja pesa yake kama ulivyosema niliitumia tumia, ila mwaka huu nimeanza kuiwekeza, hivyo ndani ya hii miaka 5 iliyobaki kabla sijaamza kufanya ukarabati, tayari nitakuwa na faida si chini ya milioni 50(sijui kama nitaiona, ama kuishika yote kwa pamoja, lakini hayo ndio mahesabu ambayo yapo) na jengo lipo likiwa limepanda thamani
Unahisi ni kwa nini hoteli zilizokuwa tishio huko nyuma, kwa sasa zinachakaa?
 
Kuwekeza kwenye majengo ni sawa na fedha zako kuzifukia sehemu, na kuanza kuila kidogo kidogo mpaka iishe.

Na kula huko unakuwa hauli faida zaidi ya kula mtaji (fedha ulioiwekeza). Wengi ukimbilia kujenga nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k huku wakijipa matumaini majengo hayo yatawalipa na kupata faida zaidi na zaidi.

Kwa ujumla majengo hayo uwapa hasara, vinginevyo mmiliki hatonufaika zaidi ya kizazi chake kijacho ambacho ndio kitakuwa kinakula faida baada ya miaka kadhaa kupita.

Ukitaka kuamini hili, tembelea nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k zipe miaka mitano alafu ukazitembelee tena, utazikuta zimechoka na kama hakutokuwa na hela ya ziada ya ukarabati, ndio hivyo biashara inakuwa imekufa.​
Ila cha ajabu, ni ngumu kukuta watu waliowekeza kwenye majengo wamefilisika kabisa.
 
Risk free.
Mtu hata awe mwizi kiasi gani hawezi kuiba nyumba na kukimbia nayo ila biashara zingine msaidizi wako akiamua tu siku moja anabeba mzigo wote na kupotea nao kisha unakuwa maskini tena.
Mkuu usijidanganye sana Kuna wengi wameibiwa nyumba mkuu, sio risk free ni low risk
 
Unahisi ni kwa nini hoteli zilizokuwa tishio huko nyuma, kwa sasa zinachakaa?

Mkuu usijidanganye sana Kuna wengi wameibiwa nyumba mkuu, sio risk free ni low risk
Hawajaiba sema wameforge nyaraka mwisho wa siku mwenye nyumba akipambana kisheria bado nyumba yake anaikuta palepale tofauti na ukiibiwa gari leo Dar kesho iko Mwanza kisha wanaichinja na kuuza spea biashara inaishia hapo.
 
Hizo hotel kuchoka



Hawajaiba sema wameforge nyaraka mwisho wa siku mwenye nyumba akipambana kisheria bado nyumba yake anaikuta palepale tofauti na ukiibiwa gari leo Dar kesho iko Mwanza kisha wanaichinja na kuuza spea biashara inaishia hapo.
Mkuu Nina ushaidi Kuna watu wamepigwa nyumba mpaka Leo hawajaipata
 
Kuwekeza kwenye majengo ni sawa na fedha zako kuzifukia sehemu, na kuanza kuila kidogo kidogo mpaka iishe.

Na kula huko unakuwa hauli faida zaidi ya kula mtaji (fedha ulioiwekeza). Wengi ukimbilia kujenga nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k huku wakijipa matumaini majengo hayo yatawalipa na kupata faida zaidi na zaidi.

Kwa ujumla majengo hayo uwapa hasara, vinginevyo mmiliki hatonufaika zaidi ya kizazi chake kijacho ambacho ndio kitakuwa kinakula faida baada ya miaka kadhaa kupita.

Ukitaka kuamini hili, tembelea nyumba za kupanga, 'apartment', hoteli, nyumba za kulala wageni n.k zipe miaka mitano alafu ukazitembelee tena, utazikuta zimechoka na kama hakutokuwa na hela ya ziada ya ukarabati, ndio hivyo biashara inakuwa imekufa.​
MTAZAMO
 
Kwa haraka haraka utaona inalipa, baada ya miaka michache jengo likianza kula hela za ukarabati, pesa inakuwa inapotea, hivo hivyo ata kwenye vyombo vya usafiri mfano mabasi n.k​
Mkuu ukiona biashara inaongezeka jua inalipa watu si wajinga
 
Ni waoga kuwekeza maeneo mengine yanayolipa kwa haraka zaidi kutokana na heka heka za hapa na pale.
Mkuu kwahio hujui kuwa wengi wanaowekeza kwenye majengo ni watu wana biashara nyingine ila wameamua kuweka fedha zao kwenye ardhi au nyumba?
 
Back
Top Bottom