Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,330
- 24,214
Uteuzi wa Askofu Malasusa haukuja hivi hivi.
Ni maajabu ya mipango ya Mungu.
Wengi hawaijui historia ya familia ya Malasusa.
Alex Gehaz Malasusa ni mtoto wa pili wa mchungaji mzee Gehaz Malasusa.
Mzee Gehaz Malasusa alisomea uchungaji miaka ya mwanzoni ya 1960 hadi huko Marekani, ambako alitunukiwa shahada ya Masters katika Theology.
Aliporudi Tanzania ili kuhudumia kanisa, kwa macho ya wachungaji wenziwe alikuwa over qualified kwa wakati ule.
Viongozi wa kanisa Dayosisi ya Mashariki na Pwani(ilikuwa ina eneo kubwa hadi Morogoro miaka hiyo) kwa kuhofia nafasi zao, wakaamua kumuweka mbali sana na makao makuu.
Mzee Gehaz Malasusa akapangwa Morogoro, tena vijijini huko, karibu na Kisaki.
Mchungaji Gehaz hakukataa wito akaenda huko vijijini na Masters yake.
Huko alihubiri na kufanya maajabu.
Aliwahubiri wana vijiji kuacha mila za kizamani ambapo, walikuwa wana waua mapacha.
Familia ikizaa mapacha ilionekana ni mkosi, mapacha na walikuwa wanauwawa.
Kati ya pacha waliookolewa ni mtu mmoja ambaye akaondokea kuwa na akili nyingi zisizo za kawaida.
Huyu mtu yupo hadi leo na anaitwa John Mpapalika.
Natoa huu ushuhuda ili Mungu wacha aitwe Mungu.
John alisoma kutoka vijijini na akafaulu vizuri hadi shule za vìpaji maalum, Kibaha tulikofahamiana.
John aliendelea kupasua masomoni na baada ya high school alienda moja kwa moja hadi Uingereza ambako alisoma na alifikia kiwango cha PhD, mtoto aloyeokolewa na mchungaji mzee Gehaz Malasusa.
Kwa wanao mfahamu John Mpapalika, alikuwa Mkurugenzi pale TCRA, sasa amestaafu.
Huu ushuhuda ulitolewa siku ya misa ya kumsindikiza mchungaji mzee Gehaz Malasusa alipo fariki, pale usharika wa Mbezi Beach KKKT.
Nlipata ushuhuda vile vile wa rafiki yangu aliyeombewa na mchungaji mzee Gehaz Malasusa baada ya kuvamiwa na majambazi.
Wale majambazi walukuja kufariki, wote.
Cha ajabu kwa mzee Malasusa hakulalamikia cheo wala kugombea madaraka maisha yake yote, licha ya kuwa over qualified.
Alitumikia kanisa kama Biblia inavyosema, kuchunga kondoo wa Bwana.
Siku ya kumuaga mchungaji mzee Gehaz Malasusa, kuna maaskofu walipata taabu kujieleza kwa nini walimtupa vijijini, tena Morogoro vijini.
Hivyo kuinuliwa katika uongozi wa juu mtoto wake Alex umekuja si kwa mshangao tu, bali inaonekana kama mipango ya Mungu kumuinua mtoto wa mtumishi wake aliye mtumikia Mungu bila malalamiko yoyote, licha ya kudharauliwa na kuonewa.
Hongera Baba Askofu Alex Gehaz Malasusa, umechaguliwa kwa mpango wa Mungu.
Ni maajabu ya mipango ya Mungu.
Wengi hawaijui historia ya familia ya Malasusa.
Alex Gehaz Malasusa ni mtoto wa pili wa mchungaji mzee Gehaz Malasusa.
Mzee Gehaz Malasusa alisomea uchungaji miaka ya mwanzoni ya 1960 hadi huko Marekani, ambako alitunukiwa shahada ya Masters katika Theology.
Aliporudi Tanzania ili kuhudumia kanisa, kwa macho ya wachungaji wenziwe alikuwa over qualified kwa wakati ule.
Viongozi wa kanisa Dayosisi ya Mashariki na Pwani(ilikuwa ina eneo kubwa hadi Morogoro miaka hiyo) kwa kuhofia nafasi zao, wakaamua kumuweka mbali sana na makao makuu.
Mzee Gehaz Malasusa akapangwa Morogoro, tena vijijini huko, karibu na Kisaki.
Mchungaji Gehaz hakukataa wito akaenda huko vijijini na Masters yake.
Huko alihubiri na kufanya maajabu.
Aliwahubiri wana vijiji kuacha mila za kizamani ambapo, walikuwa wana waua mapacha.
Familia ikizaa mapacha ilionekana ni mkosi, mapacha na walikuwa wanauwawa.
Kati ya pacha waliookolewa ni mtu mmoja ambaye akaondokea kuwa na akili nyingi zisizo za kawaida.
Huyu mtu yupo hadi leo na anaitwa John Mpapalika.
Natoa huu ushuhuda ili Mungu wacha aitwe Mungu.
John alisoma kutoka vijijini na akafaulu vizuri hadi shule za vìpaji maalum, Kibaha tulikofahamiana.
John aliendelea kupasua masomoni na baada ya high school alienda moja kwa moja hadi Uingereza ambako alisoma na alifikia kiwango cha PhD, mtoto aloyeokolewa na mchungaji mzee Gehaz Malasusa.
Kwa wanao mfahamu John Mpapalika, alikuwa Mkurugenzi pale TCRA, sasa amestaafu.
Huu ushuhuda ulitolewa siku ya misa ya kumsindikiza mchungaji mzee Gehaz Malasusa alipo fariki, pale usharika wa Mbezi Beach KKKT.
Nlipata ushuhuda vile vile wa rafiki yangu aliyeombewa na mchungaji mzee Gehaz Malasusa baada ya kuvamiwa na majambazi.
Wale majambazi walukuja kufariki, wote.
Cha ajabu kwa mzee Malasusa hakulalamikia cheo wala kugombea madaraka maisha yake yote, licha ya kuwa over qualified.
Alitumikia kanisa kama Biblia inavyosema, kuchunga kondoo wa Bwana.
Siku ya kumuaga mchungaji mzee Gehaz Malasusa, kuna maaskofu walipata taabu kujieleza kwa nini walimtupa vijijini, tena Morogoro vijini.
Hivyo kuinuliwa katika uongozi wa juu mtoto wake Alex umekuja si kwa mshangao tu, bali inaonekana kama mipango ya Mungu kumuinua mtoto wa mtumishi wake aliye mtumikia Mungu bila malalamiko yoyote, licha ya kudharauliwa na kuonewa.
Hongera Baba Askofu Alex Gehaz Malasusa, umechaguliwa kwa mpango wa Mungu.