Uteuzi wa Askofu Malasusa ni maajabu ya Mungu!

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,330
24,214
Uteuzi wa Askofu Malasusa haukuja hivi hivi.
Ni maajabu ya mipango ya Mungu.
Wengi hawaijui historia ya familia ya Malasusa.
Alex Gehaz Malasusa ni mtoto wa pili wa mchungaji mzee Gehaz Malasusa.
Mzee Gehaz Malasusa alisomea uchungaji miaka ya mwanzoni ya 1960 hadi huko Marekani, ambako alitunukiwa shahada ya Masters katika Theology.

Aliporudi Tanzania ili kuhudumia kanisa, kwa macho ya wachungaji wenziwe alikuwa over qualified kwa wakati ule.

Viongozi wa kanisa Dayosisi ya Mashariki na Pwani(ilikuwa ina eneo kubwa hadi Morogoro miaka hiyo) kwa kuhofia nafasi zao, wakaamua kumuweka mbali sana na makao makuu.

Mzee Gehaz Malasusa akapangwa Morogoro, tena vijijini huko, karibu na Kisaki.
Mchungaji Gehaz hakukataa wito akaenda huko vijijini na Masters yake.
Huko alihubiri na kufanya maajabu.

Aliwahubiri wana vijiji kuacha mila za kizamani ambapo, walikuwa wana waua mapacha.

Familia ikizaa mapacha ilionekana ni mkosi, mapacha na walikuwa wanauwawa.

Kati ya pacha waliookolewa ni mtu mmoja ambaye akaondokea kuwa na akili nyingi zisizo za kawaida.
Huyu mtu yupo hadi leo na anaitwa John Mpapalika.

Natoa huu ushuhuda ili Mungu wacha aitwe Mungu.

John alisoma kutoka vijijini na akafaulu vizuri hadi shule za vìpaji maalum, Kibaha tulikofahamiana.

John aliendelea kupasua masomoni na baada ya high school alienda moja kwa moja hadi Uingereza ambako alisoma na alifikia kiwango cha PhD, mtoto aloyeokolewa na mchungaji mzee Gehaz Malasusa.

Kwa wanao mfahamu John Mpapalika, alikuwa Mkurugenzi pale TCRA, sasa amestaafu.

Huu ushuhuda ulitolewa siku ya misa ya kumsindikiza mchungaji mzee Gehaz Malasusa alipo fariki, pale usharika wa Mbezi Beach KKKT.

Nlipata ushuhuda vile vile wa rafiki yangu aliyeombewa na mchungaji mzee Gehaz Malasusa baada ya kuvamiwa na majambazi.
Wale majambazi walukuja kufariki, wote.

Cha ajabu kwa mzee Malasusa hakulalamikia cheo wala kugombea madaraka maisha yake yote, licha ya kuwa over qualified.
Alitumikia kanisa kama Biblia inavyosema, kuchunga kondoo wa Bwana.
Siku ya kumuaga mchungaji mzee Gehaz Malasusa, kuna maaskofu walipata taabu kujieleza kwa nini walimtupa vijijini, tena Morogoro vijini.

Hivyo kuinuliwa katika uongozi wa juu mtoto wake Alex umekuja si kwa mshangao tu, bali inaonekana kama mipango ya Mungu kumuinua mtoto wa mtumishi wake aliye mtumikia Mungu bila malalamiko yoyote, licha ya kudharauliwa na kuonewa.

Hongera Baba Askofu Alex Gehaz Malasusa, umechaguliwa kwa mpango wa Mungu.
 
Hi Ni kichekesho Cha karne

Mwaka fln gazeti la mwanahalisi limeandika makala kumuhusu huyu askofu wako malasusa alihusishwa kumtorosha mke wa mtu

Hata hvyo katiba ya kkkt Ni mbovu Kama ilivyo katiba ya Tanzania

Inawezekana VIP mtu aliekwisha kutumika miaka yake nane arudi Tena kugombea nafasi hyo hyo aliyo kwisha kuhudumu

Rc wako very systematic kweny kumteua askofu
Kkkt tunakwama mno


Malasusa Ni mpasua kanisa
 
Ukishatoka rohoni na kulazimisha ya mwilini ni vigumu kuelewa mpango na maongozi ya Mungu.

Niseme hayo kwa sasa
 
Hi Ni kichekesho Cha karne

Mwaka fln gazeti la mwanahalisi limeandika makala kumuhusu huyu askofu wako malasusa alihusishwa kumtorosha mke wa mtu

Hata hvyo katiba ya kkkt Ni mbovu Kama ilivyo katiba ya Tanzania

Inawezekana VIP mtu aliekwisha kutumika miaka yake nane arudi Tena kugombea nafasi hyo hyo aliyo kwisha kuhudumu

Rc wako very systematic kweny kumteua askofu
Kkkt tunakwama mno


Malasusa Ni mpasua kanisa
Si uhame tu, uende huko RC. Sijui kama huko KKKT bado mnamuamini Kristo au mnafata watu, maana he is just going to be a bishop, sio kuwa Mungu.
 
We jamaa kaa kimya tu. Acha kutumika huyajui yaliyo gizani

Hivi unamjua Malasusa wewe vizuri? Au unamjua kwa kumsikia tu baba yake aliyejifia pale kijichi?

Unamjua huyo Alex akiwaga kwa demu wake kale kabinti kalikokuwa kanasoma Tumaini University tawi la Dar alikokapagishia upande wa ghorofa la gavana 'aliyekufa' marekani kimchongo lililopo Tegeta nyuma ya msikiti kule masaiti? Anavyoropoka vitu?

Hakuna uchaguzi mle kkkt ndugu. Umafia tu
 
We jamaa kaa kimya tu. Acha kutumika huyajui yaliyo gizani

Hivi unamjua Malasusa wewe vizuri? Au unamjua kwa kumsikia tu baba yake aliyejifia pale kijichi?

Unamjua huyo Alex akiwaga kwa demu wake kale kabinti kalikokuwa kanasoma Tumaini University tawi la Dar alikokapagishia upande wa ghorofa la gavana 'aliyekufa' marekani kimchongo lililopo Tegeta nyuma ya msikiti kule masaiti? Anavyoropoka vitu?

Hakuna uchaguzi mle kkkt ndugu. Umafia tu
Ya kuambiwa changanya na za kwako.
 
Umesema umesomea kipaji kibaha na huyo mtoto wa mchungaji lakini sion dhamira hasa hujabarikiwa kubainisha dhamira yako hasa funga fanya maombi ili unachokiandika watu wakielewe
 
We jamaa kaa kimya tu. Acha kutumika huyajui yaliyo gizani

Hivi unamjua Malasusa wewe vizuri? Au unamjua kwa kumsikia tu baba yake aliyejifia pale kijichi?

Unamjua huyo Alex akiwaga kwa demu wake kale kabinti kalikokuwa kanasoma Tumaini University tawi la Dar alikokapagishia upande wa ghorofa la gavana 'aliyekufa' marekani kimchongo lililopo Tegeta nyuma ya msikiti kule masaiti? Anavyoropoka vitu?

Hakuna uchaguzi mle kkkt ndugu. Umafia tu
Kademu si kazuri au unasemaje
 
Umesema umesomea kipaji kibaha na huyo mtoto wa mchungaji lakini sion dhamira hasa hujabarikiwa kubainisha dhamira yako hasa funga fanya maombi ili unachokiandika watu wakielewe
Mkuu rudia tena kusoma vizuri ili uelewe, hakuna mtu ana somea kipaji.
 
Hi Ni kichekesho Cha karne

Mwaka fln gazeti la mwanahalisi limeandika makala kumuhusu huyu askofu wako malasusa alihusishwa kumtorosha mke wa mtu

Hata hvyo katiba ya kkkt Ni mbovu Kama ilivyo katiba ya Tanzania

Inawezekana VIP mtu aliekwisha kutumika miaka yake nane arudi Tena kugombea nafasi hyo hyo aliyo kwisha kuhudumu

Rc wako very systematic kweny kumteua askofu
Kkkt tunakwama mno


Malasusa Ni mpasua kanisa
Kwa mujibu wa Mzee johnthebaptist, Malasusa amechaguliwa kimkakati zaidi.
 
Uteuzi wa Askofu Malasusa haukuja hivi hivi.
Ni maajabu ya mipango ya Mungu.
Wengi hawaijui historia ya familia ya Malasusa.
Alex Gehaz Malasusa ni mtoto wa pili wa mchungaji mzee Gehaz Malasusa.
Mzee Gehaz Malasusa alisomea uchungaji miaka ya mwanzoni ya 1960 hadi huko Marekani, ambako alitunukiwa shahada ya Masters katika Theology.

Aliporudi Tanzania ili kuhudumia kanisa, kwa macho ya wachungaji wenziwe alikuwa over qualified kwa wakati ule.

Viongozi wa kanisa Dayosisi ya Mashariki na Pwani(ilikuwa ina eneo kubwa hadi Morogoro miaka hiyo) kwa kuhofia nafasi zao, wakaamua kumuweka mbali sana na makao makuu.

Mzee Gehaz Malasusa akapangwa Morogoro, tena vijijini huko, karibu na Kisaki.
Mchungaji Gehaz hakukataa wito akaenda huko vijijini na Masters yake.
Huko alihubiri na kufanya maajabu.

Aliwahubiri wana vijiji kuacha mila za kizamani ambapo, walikuwa wana waua mapacha.

Familia ikizaa mapacha ilionekana ni mkosi, mapacha na walikuwa wanauwawa.

Kati ya pacha waliookolewa ni mtu mmoja ambaye akaondokea kuwa na akili nyingi zisizo za kawaida.
Huyu mtu yupo hadi leo na anaitwa John Mpapalika.

Natoa huu ushuhuda ili Mungu wacha aitwe Mungu.

John alisoma kutoka vijijini na akafaulu vizuri hadi shule za vìpaji maalum, Kibaha tulikofahamiana.

John aliendelea kupasua masomoni na baada ya high school alienda moja kwa moja hadi Uingereza ambako alisoma na alifikia kiwango cha PhD, mtoto aloyeokolewa na mchungaji mzee Gehaz Malasusa.

Kwa wanao mfahamu John Mpapalika, alikuwa Mkurugenzi pale TCRA, sasa amestaafu.

Huu ushuhuda ulitolewa siku ya misa ya kumsindikiza mchungaji mzee Gehaz Malasusa alipo fariki, pale usharika wa Mbezi Beach KKKT.

Nlipata ushuhuda vile vile wa rafiki yangu aliyeombewa na mchungaji mzee Gehaz Malasusa baada ya kuvamiwa na majambazi.
Wale majambazi walukuja kufariki, wote.

Cha ajabu kwa mzee Malasusa hakulalamikia cheo wala kugombea madaraka maisha yake yote, licha ya kuwa over qualified.
Alitumikia kanisa kama Biblia inavyosema, kuchunga kondoo wa Bwana.
Siku ya kumuaga mchungaji mzee Gehaz Malasusa, kuna maaskofu walipata taabu kujieleza kwa nini walimtupa vijijini, tena Morogoro.

Hivyo kuinuliwa katika uongozi wa juu mtoto wake Alex umekuja si kwa mshangao tu, bali inaonekana kama mipango ya Mungu kumuinua mtoto wa mtumishi wake aliye mtumikia Mungu bila malalamiko yoyote, licha ya kudharauliwa na kuonewa.

Hongera Baba Askofu Alex Gehaz Malasusa, umechaguliwa kwa mpango wa Mungu.
Wewe ni kati ya wale waumini wasiojua nini maana ya utumishi ndugu, huwezi kusema kuwa Alex Malasusa kwamba avae utumishi wa baba yake ni kitu kigumu na hakiwezekani daima.

Kama ingekuwa huduma inayorithishwa basi watoto wa mzee kulola wangebeba huduma ya baba yake lakini ona akina Daniel wanaishia kujisifu na hakuna walichofanya kasome kitabu cha 2Samwel Sura zote unaweza kupata majibu ya hichi ulichokiandika na mada mfu
 
Wenye wako zao wanalalamika, sasa sijui kuoa wake zao haukuwa Mpango wa Mungu wakaushe jaranga liendelee au la.
 
Back
Top Bottom