Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Raha ya mapenzi kupendana, na kupendana kunahusu kupeana raha. Kupeana raha kunahusu pesa kwa kiwango kikubwa.

Refer uzi wa Mbu kuhusu mapumziko.

yes..hapo ndo raha ya mapenzi ilipo. Unaweza kupata raha bila ya kuwa na 'pesa'. Isipokuwa mleta mada alikuwa anajaribu kuamsha mjadala kama ni sahihi kuwaponda wale wanaoangukia kwenye mapenzi kwa misingi ya pesa, je ni sahihi kuwaponda??

Ila inaonesha pesa ni kivutio kama vile mtu anavyovutiwa na sura, umbo, tabia, n.k.. mchanganyiko ukiwa sahihi (kulingana na mtu binafsi) , hapo ndo kunapelekea 'mapenzi'>?????

Kuna wengine wanapata raha kwa kuona tu uzuri wa wapenzi wao, wengine raha kwa kupiga stori tu, ili mradi kila mtu ana ladha yake....kwa hiyo kupeana raha sio lazima kuwe na pesa kwa kiwango kikubwa
 
Umeshuhudia dame akinyang'anywa kila kitu ndani ya nyumba na yule mwenye pochi kwa kuwa penzi limechujuka? Usipime aibu yake! unaweza kutamani kujiua! maana huna pakuuweka uso wako kwa aibu tele na jinsi ulivyoshuka daraja toka kule juu ulikokuwa kwa kuwa na kila kitu ndani ya nyumba sasa umeachwa mtupu! hata kiti cha kukalia huna! Penzi la pesa si penzi! mara nyingi huishia pabaya

Hayo ni bongo tu, nchi za nje hana uwezo wa kuondoka na vitu hivyo. Heck zawadi tu anazokununulia haruhusiwi kuondoka navyo pia seuze vitu kama mlifunga ndoa.

Kama jamaa alikuwa na pesa akamuonyesha kumjali na bibie aka-fall kwa jamaa kutokana na anavyoonyeshwa maraha, ni sawa na yule alopenda mtu kwa kuwa anajua kusema maneno matamu. Akiamua kukutosa anakutosa tu. Wala mwanamme kuwa hana pesa haimaanishi kuwa ndo atakuwa nawe forever.

Pesa ni sawa na mengineyo tu.
 
Kweli ila sio wote wanaobahatika kuendelea kua na hizo pesa....post yangu ya kwanza nilielezea aliekimbia familia ukaipotezea...changanya na hii uone kwanini inajalisha na vipi ni muhimu mtu akupende wa sababu nyingine zaidi ya pesa zako!!

Ofcourse ni muhimu mtu akupende kwa sababu zaidi ya pesa..., (lakini suala la pesa kuisha ni kitu gani ambacho hakitakwisha??)..., I can argue kwamba kinachowafanya watu wasikimbiwe na kuendelea kuishi pamoja ni uvumilivu... and not because of true au untrue love
 
yes..hapo ndo raha ya mapenzi ilipo. Unaweza kupata raha bila ya kuwa na 'pesa'. Isipokuwa mleta mada alikuwa anajaribu kuamsha mjadala kama ni sahihi kuwaponda wale wanaoangukia kwenye mapenzi kwa misingi ya pesa, je ni sahihi kuwaponda??

Ila inaonesha pesa ni kivutio kama vile mtu anavyovutiwa na sura, umbo, tabia, n.k.. mchanganyiko ukiwa sahihi (kulingana na mtu binafsi) , hapo ndo kunapelekea 'mapenzi'>?????

Kuna wengine wanapata raha kwa kuona tu uzuri wa wapenzi wao, wengine raha kwa kupiga stori tu, ili mradi kila mtu ana ladha yake....kwa hiyo kupeana raha sio lazima kuwe na pesa kwa kiwango kikubwa

Hebu mkuu tutajie hizo raha unazoweza pata bila ya pesa tulinganishe na raha unazoweza pata kwa pesa 😀
 
wamaume watakaosoma hii thread
halafu waamini kuwa kwenye love huitaji pesa
watalia na kusaga meno.......
 
wanawake wote ni chamelions when it comes to what they want...

bora uwe na pesa akukatae kwa mengine

kuliko ukataliwe kwa kuwa huna kitu
very painfull
 
mapenzi as a feeling should have some reasons, why not?? hata mie nakubali kabisa sababu iwe yoyote muhimu kwangu wenngine mtaishangaa, lakini kwangu ni muhimu, mfano macho, miguu, sura, tabia nk!!
Sababu yangu ya mapenzi kwa mtu fulani sio lazima ifanane na ya mtu mwingine yoyote.

ILA

Kuamua kuishi na mtu, kwa sababu ya mapenzi hayo ndio mie naona tatizo.
kwa mtazamo wangu tunatakiwa tuamue kuishi kindoa na watu ambao tunadhani kwa wakati huo, values zao na zetu, zitapikika chungu kimoja.
mfano regarles ya vivutio vile alivyokuwa navyo kama pesa, sura, tabia nk,

je

mitazamo yetu katika kuchukulia mambo muhimu kwangu kama dini? ndugu? kabila? pesa? watoto? makazi? ajira? itaweza kukaaa nyumba moja?
Mfano: Je wakati tunaongelea swala la pesa tutaongea kichina na kihaya? au tutaongea tuweze kufika conclusion? je nitaweza kukubaliana na mitazamo yake, just in case we have to choose?

VERY TRUE.....ndo maana mie ninaona WISDOM (hekima) inabidi itumike unapofikia mahali kwa kuamua kuishi pamoja. na sababu ulizozitoa kwa upande wangu naona zinajenga hoja vizuri
 
halafu lizzy u r missing the point here...hazungumzii watu wenye pesa but abusiveau ma snobs hivi.....tunazungumzia mtu ana pesa na still ana quality zingine
Hajasema habari ya quality nyingine...kasema watu kupendwa kwa pesa zao bila kuonyesha zimepatikana vipi na wapi au ni watu wa aina gani!!Au labda kma naona dabo dabo leo mnisamehe!
 
Hebu mkuu tutajie hizo raha unazoweza pata bila ya pesa tulinganishe na raha unazoweza pata kwa pesa 😀
Kaazi kweli kweli....unless hapa tunaongelea pesa ya kutosha kuendeleza maisha na sio mamilioni ya kutosha kupelekana vacation Zanzibar basi naweza kusema bibi yangu na hakuwahi kupata raha hapa duniani!!‘
 
Mapenzi ya pesa yana ubaya pale unapomuacha aliyekuwa na pesa kisa kfilisika/kaishiwa!..No money, no love!!
I can argue mapenzi ya sura na uzuri yanakuwa mabaya pale ikitokea ajali na sura kuharibika pale unapomuacha mtu sababu sio mzuri tena
 
Kaazi kweli kweli....unless hapa tunaongelea pesa ya kutosha kuendeleza maisha na sio mamilioni ya kutosha kupelekana vacation Zanzibar basi naweza kusema bibi yangu na hakuwahi kupata raha hapa duniani!!'

Si ututajie tu hizo raha alizofaidi bibi yako kwa faida ya wale ambao wanaona pesa inatoa raha zaidi? ( hakuna iliposemwa kuwa hakuna raha kabisa bila ya pesa ila tunataka kulinganisha tu)
 
Hebu mkuu tutajie hizo raha unazoweza pata bila ya pesa tulinganishe na raha unazoweza pata kwa pesa 😀

Raha ni mtazamo binafsi...ingawa inaweza kuendana na watu wengine. lakini ni purely personal.

nimetoa mfano hapo kwamba

- mnaweza kukaa chini na kupiga stori
-ukimuona mwenzio unasikia raha.
-kutembea pamoja, kama vile kwenda beach, n.k
-kulala au kula pamoja.

Ikumbukwe kuwa Pesa ni 'relative'...ninaweza kuwa napata mshahara wa milioni 10 nikajiona sina pesa nikijilinganisha na anayepata mshahara wa milioni 20.

Mwingine kipato chake cha laki 3, kinamtosha kwenda na mpenzi wake maeneo wanayotaka kwa kadiri ya uwezo wao.. Pia unaweza kuwa na ZERO income, na bado ukaenjoy mapenzi kama mwenzio anakuunga mkono katika hilo.. ni mtazamo tu.

Ila mada inajaribu kuangalia ni kwa jinsi gani tuwanyanyapae au tusiwanyanyapae waleo wana-fall in love katika misingi ya pesa, tofauti na uzuri, sauti, miguu, au umbo, n.k
 
Aiseee...kumbe ehhhh!Kwahiyo hata wale waliochiwa vijisenti bila kuvifanyia kazi nao unaweza kusema ni successul?!Labda kwenye kupokea na kuandika cheque tu na sio kwenye kusaka hizo pesa.Binafsi i would rather be with a “hard working guy“ who hasn‘t got his break yet than a snob from a rich family that doesn‘t even know how to brush his shoes because he is “SUCCESSFUL“ by your definition.
What if because of mishaps, and so many dissapointments the hard working guy turns to be a lazy snob..., will that change your mind??
 
Mi nadhani tunachanganya upendo wa kweli na pesa kitu ambacho si sahihi
tutazame familia
1.Wanasikilizana,wanaheshimiana kila jambo wanalolifanya lazima liwe kitu kimoja,hakuna anayefanya maamuzi banafsi na mengine mengi lakini familia hii ina kipato cha kubangaiza.........na mapenzi/upendo wao unaonekana wazi.

2.familia ya pili pesa ya kutosha
............dharau,kutosikilizana,vurugu zote,siku baba/mama akijisikia kutulia nyumbani ndo utasikia twende tukajipendelee kama Mbu alivotueleza kule

sasa hapa tutasema upendo unachochea mapenzi? hapo kuna upendo/mapenzi ya kweli? au ni mmoja anajionea bora kapata hata kibahati chakukumbukwa wakati huo akijipumzikie lakini moyoni ni fully majonzi.
 
Mi nadhani tunachanganya upendo wa kweli na pesa kitu ambacho si sahihi
tutazame familia
1.Wanasikilizana,wanaheshimiana kila jambo wanalolifanya lazima liwe kitu kimoja,hakuna anayefanya maamuzi banafsi na mengine mengi lakini familia hii ina kipato cha kubangaiza.........na mapenzi/upendo wao unaonekana wazi.

2.familia ya pili pesa ya kutosha
............dharau,kutosikilizana,vurugu zote,siku baba/mama akijisikia kutulia nyumbani ndo utasikia twende tukajipendelee kama Mbu alivotueleza kule

sasa hapa tutasema upendo unachochea mapenzi? hapo kuna upendo/mapenzi ya kweli? au ni mmoja anajionea bora kapata hata kibahati chakukumbukwa wakati huo akijipumzikie lakini moyoni ni fully majonzi.

Kwani lazima familia yenye pesa iwe na kasoro? Haiwezi kuwa na pesa kisha wakasikilizana?
 
Raha ni mtazamo binafsi...ingawa inaweza kuendana na watu wengine. lakini ni purely personal.

nimetoa mfano hapo kwamba

- mnaweza kukaa chini na kupiga stori
-ukimuona mwenzio unasikia raha.
-kutembea pamoja, kama vile kwenda beach, n.k
-kulala au kula pamoja.

Ikumbukwe kuwa Pesa ni 'relative'...ninaweza kuwa napata mshahara wa milioni 10 nikajiona sina pesa nikijilinganisha na anayepata mshahara wa milioni 20.

Mwingine kipato chake cha laki 3, kinamtosha kwenda na mpenzi wake maeneo wanayotaka kwa kadiri ya uwezo wao.. Pia unaweza kuwa na ZERO income, na bado ukaenjoy mapenzi kama mwenzio anakuunga mkono katika hilo.. ni mtazamo tu.

Ila mada inajaribu kuangalia ni kwa jinsi gani tuwanyanyapae au tusiwanyanyapae waleo wana-fall in love katika misingi ya pesa, tofauti na uzuri, sauti, miguu, au umbo, n.k

Kaka mpendwa hizo raha za watu wasopesa zinaweza kupatikana kwa wale wenye pesa pia lakini kuna raha za wenye pesa, wasopesa hawana (au nakosea?)

Anae fall in love kwa channel ya pesa hana kosa, muhimu awe amekuwa in-love kweli tu na sio kuwa anapenda pesa peke yake bila ya mwenye pesa yule
 
Si ututajie tu hizo raha alizofaidi bibi yako kwa faida ya wale ambao wanaona pesa inatoa raha zaidi? ( hakuna iliposemwa kuwa hakuna raha kabisa bila ya pesa ila tunataka kulinganisha tu)
Angekuwepo ningemuuliza...bahati mbaya nimebaki na kumbukumbu tu za yeye kua mwenye furaha muda wote bila kujua kwanini wakati mumewe hakua na pesa nyingi tofauti na mashemeji zake!!!
 
Mi nadhani tunachanganya upendo wa kweli na pesa kitu ambacho si sahihi
tutazame familia
1.Wanasikilizana,wanaheshimiana kila jambo wanalolifanya lazima liwe kitu kimoja,hakuna anayefanya maamuzi banafsi na mengine mengi lakini familia hii ina kipato cha kubangaiza.........na mapenzi/upendo wao unaonekana wazi.

2.familia ya pili pesa ya kutosha
............dharau,kutosikilizana,vurugu zote,siku baba/mama akijisikia kutulia nyumbani ndo utasikia twende tukajipendelee kama Mbu alivotueleza kule

sasa hapa tutasema upendo unachochea mapenzi? hapo kuna upendo/mapenzi ya kweli? au ni mmoja anajionea bora kapata hata kibahati chakukumbukwa wakati huo akijipumzikie lakini moyoni ni fully majonzi.

bora wewe unayeongelea katika mtazamo wa kifamilia.

Nafikiri katika ule mchakato wa kuelekea kuishi pamoja, yaani kipindi cha kutongozana na kupeana mikakati.. hapo je, kama msichana akiamua kuangalia kigezo cha pesa alaumiwe,??

Mapenzi kwa ujumla wake hayaendeshwi na pesa peke yake, ni mchanganyiko wa mambo mengi sana.. Ila wengi tunafikiri pesa ni kivutio cha maisha bora.
Kumbuka pia pesa inaleta kiburi, dharau, majivuno, ubwana, ubinafsi. ( pia hata mtu mwenye sura nzuri anaweza kuwa na tabia hizi)...
 
Sio zote lakini nyingi nilizoziona zimejaa hayo niliyosema,na sio zote ambazo zina maisha ya kubangaiza zina furaha lakini ukiangalia kwa undani ni kukosekana kwa mapenzi ya kweli ukimpenda mtu kwa dhati hutataka kumuona anasononeka au kupata shida at any cost.


Kwani lazima familia yenye pesa iwe na kasoro? Haiwezi kuwa na pesa kisha wakasikilizana?
 
Back
Top Bottom