Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Basi kote muwe mnatimiza majukumu hivyo hivyo muone kama kutakuwa na tatizo, lasivyo hamtoisha kulalamika.
Nyie kwani mnakingine mnachohitaji zaidi ya pesa? Manake skuizi hata kunjunjana hampendi
 
Sasa mimi nasema kisiwe kigezo,,, sio kilamtu anastahili kushika madaraka the same kwa uchumi, maisha ni kusaidiana, sio utegemezi wa pande moja
Kama maisha ni kusaidiana basi lazima utafute mtu wa kusaidiana nae na si wa kumsaidia tu au kukusaidia tu. Kwa hiyo uwezo wa kusaidia hauwezi kuacha kuwa kigezo.
 
Kama maisha ni kusaidiana basi lazima utafute mtu wa kusaidiana nae na si wa kumsaidia tu au kukusaidia tu. Kwa hiyo uwezo wa kusaidia hauwezi kuacha kuwa kigezo.
Hapo tunakwenda sawa
 
Hapo tunakwenda sawa
Tunakwenda sawa:mwanaume au mwanamke asiye na kitu asijilengeshe kwa mwenye hela ili aponee hapo bali ajihakikishie kwanza usalama wa kifedha ndo ajiingize kwenye majukumu yanayohitaji fedha yakiwemo mahusiano. Ila hata kama mwanamke nina hela, mwanaume una wajibu wa kunihudumia na baadhi ya huduma zinahitaji hela. Sitakuomba, nitajihudumia kwa hela yangu ila usilalamike nikikuchulia poa. Kupenda ni vitendo. Huko moyoni unavyojiskia abaona Mungu tu.
 
girls wote wanitumie number zao PM niwatumie mshiko.kwa taarifa tu m ndio taiter hapa MMU.
 
Tunakwenda sawa:mwanaume au mwanamke asiye na kitu asijilengeshe kwa mwenye hela ili aponee hapo bali ajihakikishie kwanza usalama wa kifedha ndo ajiingize kwenye majukumu yanayohitaji fedha yakiwemo mahusiano. Ila hata kama mwanamke nina hela, mwanaume una wajibu wa kunihudumia na baadhi ya huduma zinahitaji hela. Sitakuomba, nitajihudumia kwa hela yangu ila usilalamike nikikuchulia poa. Kupenda ni vitendo. Huko moyoni unavyojiskia abaona Mungu tu.
Aisee Umeongea Kuntu sana... Hebu agiza miguu ya kuku nakuja kulipa
 
Sijui kwanini siku zote kuna negative perception mwanamke akimpenda ama akipendwa na mwanaume mwenye pesa...nani kasema wasio na pesa ndo wana guarantee ya mapenzi ya kweli....
Always pray,ukibahatika kumpata mwenye utu hio hela yake ni tamuuu mno mana Ina complement yale mema anayokufanyia..pata asie na hela na asie na utu u will experience hell on earth...
 
Mtu asiye na hela ana mawazo, ana huzuni, ana hasira, hajiamini.... Mtaishia kukwazana tu kila siku. Labda awe ameridhika na umaskini wake.
 
Mtu asiye na hela ana mawazo, ana huzuni, ana hasira, hajiamini.... Mtaishia kukwazana tu kila siku. Labda awe ameridhika na umaskini wake.
[emoji17] [emoji17] duuh, wanaume tusake mpunga jamani kumbe ndio mnavyo sema!!!.
 
Mwanamke anayewaza pesa ya mwanaume ni yule mwenye fikra tegemezi.
Pia huwa ni yule ambaye hajakomaa kiakili Mara nyingi huwa ni wale matenager na ambao wapo 20+. Lakini kuna kona ambapo fikra hubadilika ambapo dunia huweza kujigeuza kutoa mtazamo mmoja kuelekea mwingine.

Pia mwanaume asiyetaka kutegemewa na mwanamke ni yule ambaye ni mvivu, asiyewajibika, mwoga wa majukumu.
Mwanaume asiyejiuliza kwa nini alipewa misuli wakati mwanamke akanyimwa.
 
[emoji17] [emoji17] duuh, wanaume tusake mpunga jamani kumbe ndio mnavyo sema!!!.
Hii inahusu jinsi zote. Hela ndo inaweka chakula mezani, nguo mwilini, watoto shuleni, paa juu ya kichwa, heshima kwenye jamii n.k. Ukiona huna kitu halafu watu wanakukimbilia basi wee mganga. Si vinginevyo.
 
Mtu asiye na hela ana mawazo, ana huzuni, ana hasira, hajiamini.... Mtaishia kukwazana tu kila siku. Labda awe ameridhika na umaskini wake.

Inategemea na mazingira Mkuu.
Pesa huwa na thamani pale penye matumizi lakini Kama hakuna matumizi basi thamani ya pesa hakuna.

Wanawake wanaoishi katika majiji ndio huiona thamani ya pesa tofauti na wanaoishi vijijini au miji midogo.
Hii ni kwa sababu wanawake wa mjini hukabiliwa na changamoto nyingi za kimuingiliano, mabadiliko ya fasheni mablimbali, usafiri na masuala ya mavazi na teknolojia.
Lakini wanawake wa vijijini huhitaji mambo ya kawaida ambayo ni chakula, maji, na malazi. Jambo hili huwafanya wasiione thamani ya pesa Kama wanawake wa mjini.

Pesa haifiti maeneo mengi Sana japo wengi hufikiri ndio kila kitu.


USHAURI: Kama unatarajia kuishi mjini basi suala la pesa haliepukiki hata kwa asiye na akili. Hivyo ni wajibu wako kutafuta mwanaume/Mwanamke ambaye atakufanya uishi mjini ukiwa unaheshimiwa kuliko uishi kwa kujidhalilisha Kama kuomba omba hela wanaume za watu, kujiuza, kuvaa nguo zisizo na stara au na thamani.

Ni wajibu wenu kina Dada kujichagulia wanaume wa hadhi zenu. sio we kwenu masikini, huna elimu, huna uzuri wowote zaidi ya kujigeuza mwanasesere kwa mapambo alafu unataka wanaume tulio na hela.

Hata sisi hatutaki wanawake masikini, wasio vutia na wasio na elimu. Huwa tunawaepuka vibaya mno. Tunaona wanaweza kutuletea mikosi ndani ya familia zetu.

Pia lazima uelewe hakuna tajiri mwenye ndoto za kuwa na mwanamke masikini na wala hatuwazagi kuhusu nyie.
Ndio maana ikitokea inakuwa moja kwa matajiri 100.
 
Back
Top Bottom