Utajiri wa Dr. Dau unashtua

Utajiri wa Dr. Dau unashtua

Abrahamovic na Glazer na sasa dr Dau tena mtz..
Newcastle mpo?
 
Kesho utasikia Gazeti liombe radhi,likanushe habari hiyo kwa muktadha ule ule iliyotumia kuitangaza tunalipa wiki moja kabla ya kuchukua hatua stahiki ,Nchi yetu sijui tulikosea wapi?
 
JIBU HAYA MASWALI:-

1. Kwanini alivunja EAMWS baada ya Uhuru?

2. Kwanini kanisa kukubali siasa za ujamaa baada ya Nyerere kukutana na maaskofu waliopinga mwanzo baada ya kupata Uhuru.

3. Kwanini alifuta mahakama ya kadhi baada ya kupata Uhuru.

4. Kwanini Nyerere aliruhusu maaskofu kuingiza chakula, nguo, mabati na gari wengine wakipigwa marufuku wakati wengine wakizuiwa wakati ule wa uhujumu wa uchumi? Soma kitabu cha Padri John Sivalon.

5. Kwanini alimfukuza Tanganyika Mufti wa kwanza shehe Hassan Bin Amir?

6. Kwanini aliitenga kimaendeleo mikoa ya Pwani, Lindi, mtwara na Tabora?

7. Kwanini gazeti moja nchini Uingereza lilimtuhumu kuwa baraza la mawaziri limejaa wakatoliki? Refer speech ya mwl, alikiri kutuhumiwa ila akajibu suala zito kwa masihara kwa George Kahama.

8. Kukubali kuanzishwa ubalozi wa Vatican Tanzania huku akizuia Tanzania kujiunga OIC.

9. Kushindwa kuzuia mkataba uliosainiwa na Low asa uitwao Memorundam of understanding huku akijua Tanzania haina dini.

SOURCE: Nyerere,kanisa katoliki na muendelezo wa mfumo kristo dhidi ya Uislam Tanzania
Foolish argument, hoja yako ni nini hasa? Sikuelewi, unazungumzia tuhuma za Dau, unamzungumzia Nyerere, au unazungumzia wakristo reference yako akiwa Nyerere?

Unaizungumzia serikali ya Tanzania au? Maana hata Lowassa sidhani kama alisaini enzi za utawala wa Nyerere, hebu kwanza kanywe maji, tulia, rudisha akili zako, kunywa kahawa kama hunywi beer halafu anzisha uzi mmoja mmoja wa tuhuma zako, utawapata wa level yako tuache tujadili tuhuma za ufisadi wa Dau
 
Ownership structure ya Newcastle ipo wazi lakini unashindwa kuangalia na baadalak yake wanangalia gazeti la Dira kama reference daah! Nimecheka sana.

Napenda kujadili kwa hoja. Ndiyo maana nimesema hawa Dira wanatakiwa waeleze hizo hisa za Dau zilinunuliwa lini. Wakituambia zilinunuliwa baada ya 2007, tutajua ni uwongo. Possibility iliyopo ni ile tu kama Dau alinunua hisa hizo kabla ya 2007. Lakini kingine cha msingi hizo hisa ni za thamani gani? Maana kununua hisa kwenye biashara nje ya nchi siyo kosa.

Kinachonikera kuliko vyote ni kuhusisha mambo haya na dini, kwenye hili tunakuwa wajinga kuliko wale baba zetu. Kuna wakati huko nyuma ilikuwa nadra sana kuona watu wanazungumzia udini. Watu waliokuwa karibu na Mwalimu, wanasema rafiki yake mkubwa wa Mwalimu alikuwa Rashid Kawawa, na ndiye mtu aliyewahi kuwa karibu zaidi na Mwalimu kuliko mwingine yeyote.

Juzi nimeenda kwenye sala (Jumuia ndogondogo), tulipoenda kufanyia ibada ni nyumba yenye watu wenye imani mchanganyiko. Baba ni Mpemba (muislam), Mama Mkristo ndiye katibu wa Jumuia. Baba muislam ndiye aliyekuwa anawakaribisha wageni na kutupangia viti.

Nilipokuwa sekondari, nilikuwa Mwenyekiti wa YCS Mkoa, hakuna hata wakati mmoja ambapo nilikosa kualikwa kwenye sherehe za wanafunzi waislam. Wakati wa chakula, mimi na ujumbe wangu tulikuwa tunawekewa chakula mezani, wenyeji wetu wakikaa kwenye majamvi. Hata tulipofika tulipokelewa kwa upendo na furaha. Nasi pia tulikuwa tunawaalika na kuwapa nafasi ya kutoa salamu.

Juzi Papa Francis amewabeba wakimbizi wa Syria, familia sita zitakazolelewa Holy Sea. Lakini kabla ya hapo alikutana pia na viongozi wa dini ya kiislam. Kama hawa wakuu wetu wanafanya hivyo, sisi tunaojiita waumini tunapotenda tofauti, tunamfuata nani?
 
Ownership structure ya Newcastle ipo wazi lakini unashindwa kuangalia na baadalak yake wanangalia gazeti la Dira kama reference daah! Nimecheka sana.

Mbona umekomalia sana ya Newcastle tu wakati kuna kashfa nyingi tu kenye Dira. Vipi zile billion 100 ................!!?
 
Fuata Link hii uone hali ilivyo, Tatizo lipo:-

Mohamed Said: WAISLAM WA TANZANIA NA TATIZO LA UDINI KATIKA WIZARA ELIMU

WAISLAM WA TANZANIA NA TATIZO LA UDINI KATIKA WIZARA YA ELIMU
UM5d4OfKGZAOGzoyOL2k5ofU7gKUq8up-rSPW94rWq1CU0oly4DuZx0nhqPDBRsHV1Y1-QwcV7s6cEfgbDES2YV1DERqomujIb8mhJE0ThZ38ztuIb7yN3F-JAIBLHNYQ-ZS95Gsgnt3ftui-8GfkgJ1U7JyLXPmpYiUd0m7o1FtBE_QkdyKIHzyiqHeZKffKBAnnGXheHLdhvU0FaGpK9clckpP1nq9L1Q95c_d_t0X_Usrdu0FFRv3dAES0GmlBUD_sRVoUBfiJrkIzDJ1RSLnYHhm6ZJlotJWcHhOesANLUPU3pErqJRACQkqIjrU1ZeUosCWXHzwxciZB2kqvbxbC2dXxeWquDhnvP7F1hgeGqld21AEp4bFHUu-DiZeMNpIwWkW9IVkWSqXTQTW1ToO1PqqSozdgk2BBWPBZILvEmedz2-3Qi9R3Andwtl-xxxU2e9Jp4PbiVvlgJhkzzr2PH-hRg4gxEe64ogHNac_vJZbOj98n_dKdKuQVZKOsSovFVnXp18c5bGYKCwq--ISKgPCAbeQAZPbbXpGSQ4tpWL91wZOniRFzxcedUjRd6Bx=w480-h320-no

Maandamano ya Waislam Dhidi ya NECTA Chini ya Dr. Joyce Ndalichako
Ndugu Waziri,
Kwa muda mrefu sasa, kumekuwa na maswali mengi wakijiuliza Waislamu, moja likiwa inakuwaje katika maeneo yenye Waislamu wengi ambapo idadi ya wanafunzi Waislamu inakuwa zaidi ya asilimia 70, lakini wanapochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya watoto wa Kiislamu huporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Swali na kitendawili hiki kimekuwepo kwa muda mrefu bila kupatiwa majibu. Hata lilipofikishwa Bungeni mwaka 1999 na aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni, Mzee Kitwana Selemani Kondo, bado halikupatiwa jibu.
ar6kGfiPOg9afYE4gRWDHVHw5QlMyS5lAevP3Tkmi7yCy-T29eF24_IoxP0Vj-ydMrS2Vrlq5k_Wyc7NRkHQudZj1UesOxPrLJByxcSrdX9ES1QmAGeO54UhfCMHNH6DmYP4b5Dcfn6dgVf3LWDsVqnkEOh6kBcGo3QBm83kqvlCisa5-S8_GmCLVSYHAPrzERHoxycfe_DDkoPkmt60qF2eBLO3bu0619cOhBKHkbuwq8FQPWiDU47Ry_hUqvz6quhI0zjKM4msLGRYjVWoLcGmazH0pDfhc_j1VncF6es34y2A3lOQgfugBZzp3ZsAzqgQ-iqG-zyfdNg8bM-htQy2AVhy2i09Dcg0dPV39ZA3ff_W9Nc4anEkRh9jn-GyEW_WgNqlW3Ryc6QJoO93sIIoqw4Ue7EGy5rjK3HwK2_LqbEb0htqFT3UgJ-8HhyTVmLPJQTVd4tKVTrxDfD918g5mSkpfSS8E_tdZdvLrbyJlJBtkkNhkNeQ_pOAZ1VsH8xmiq7ZKVM0WPZmMhLdajan7JPvSuj4FVA2HfouFqttQTT5CFSUyI40Ngir413nNA2Oxw=w280-h320-no

Kitwana Selemani Kondo
Akihoji juu hali hiyo, Mzee Kitwana Kondo alitoa mfano jinsi hali ilivyokuwa katika shule ya Pembamnazi iliyokuwa na Waislamu watupu na kwa miaka mingi mfululizo kulikuwa hakuna hata mtoto mmoja aliyekuwa akichaguliwa kwenda sekondari kutoka katika shule hiyo. Aidha alisema kuwa, katika mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya watoto wa Kiislamu katika shule za msingi ilikuwa zaidi ya asilimia 70 lakini inapokuja kuchaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Waislamu iliporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Akizungumza Bungeni tarehe 2 Februari, 1999 alisema kuwa katika watoto waliofanya mtihani wa darasa la saba mwaka 1998, idadi ya Waislamu ilikuwa asilimia 71 na Wakristo 29%. Hata hivyo akasema, ilipotoka orodha ya waliochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Wakristo ikawa asilimia 79 (79%) na Waislamu 21%.

Je, hiyo ilikuwa na maana kuwa watoto wa Kiislamu kwa asili yao hawana akili? Alitaka kujua Mzee Kitwana Kondo. Lakini hakuweza kupata jibu.

Mheshimiwa Waziri,
Ni wazi kuwa Waziri wa Elimu au Waziri Mkuu ambaye ndiye msimamizi wa mambo ya serikali Bungeni asingeweza kutoa majibu ya uhakika kwa sababu swali lilihitaji kufanyika uchunguzi huru wa kina na makini kwanza.

Mheshimiwa Waziri,
Mwaka 1987 aliyekuwa Waziri wa Elimu, Profesa Kighoma Ali Malima, aliweka utaratibu mpya wa ufanyaji wa mtihani wa darasa la saba ambapo namba zilitumika toka kufanya mtihani, kusahihisha na kuchagua wanafunzi wa kwenda kidato cha kwanza. Namba zilivishwa majina baada ya taratibu zote hizo kukamilika. Mwaka huo idadi ya watoto wa Kiislamu waliokwenda kidato cha kwanza iliongezeka kwa asilimia 40 ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Hata hivyo, mara aliondolewa Waziri Malima katika wizara hiyo na utaratibu wa zamani ukarejeshwa ambapo yalikuwa yakichaguliwa majina na idadi ya Waislamu ikaporomoka na kurudi chini ya asilimia 20.

Mheshimiwa Waziri,
Hali kama hii hapana shaka inazua maswali mengi ambayo yanahitaji majibu na majibu hayo hayawezi kupatikana bila ya kufanyika uchunguzi.


Labda tuongeze mifano ili kuliweka wazi zaidi jambo hili. Mwaka 1983 mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Kopa Abdallah akisoma katika shule ya msingi Kichangani, Kilosa, alikosa kuchaguliwa kwenda sekondari. Yeye binafsi, wazazi wake na hata walimu wake hawakuamini matokeo yale kutokana na alivyokuwa akifanya vizuri kuliko wanafunzi wote. Baadae ilikuja kugundulika kuwa nafasi yake alipewa mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Antoni Samirani ambaye alikuwa na uwezo mdogo sana ikilinganiswa na Abdallah. Kilichofanyika ni kuwa jina la Abdallah lilifichwa na baadae Antoni akapewa jina hilo kimya kimya na kwenda kusoma sekondari akitumia jina Abdallah wakati yeye ni Antoni.

Taarifa zinasema kuwa Kopa Abdallah alipogundua hakuweza kufanya kitu akaishia kuwa dereva.

Hali kama hiyo ilimkuta pia Adam Ramadhani aliyekuwa akisoma shule ya msingi Rutihinda jijini Dar es Salaam na kumaliza darasa la saba mwaka 1999. Yalipotoka matokeo ya mtihani wa darasa la saba na kuonekana kuwa Adam hakuchaguliwa, baba yake hakuamini kuwa mtoto wake anaweza kufeli kutokana na uwezo aliokuwa nao na zaidi akitizama walivyochaguliwa watoto ambao Adam alikuwa mwalimu wao shuleni na mitaani.

Katika kufuatilia suala hilo wizarani, ilikuwa aibu kwa wizara baada ya kuonekana kuwa walichaguliwa watoto wa Kikristo wenye alama za chini kabisa huku akiachwa Adam Ramadhani aliyekuwa na alama za juu kuliko wote.

Mheshimiwa Waziri,
Mifano kama hii ni mingi mno na ipo katika ngazi zote kwa maana kutoka elimu ya msingi kwenda sekondari, kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano na kutoka kidato cha sita kwenda Chuo Kikuu. Kwamba hata kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano, wapo watu waliopata kushuhudia majina ya wanafunzi wa Kiislamu yakiwekwa pembeni japo walikuwa na sifa za kuchaguliwa.

Mheshimiwa Waziri,
Ukiacha hujuma katika kuwaacha wanafunzi Waislamu wenye sifa kuendelea na masomo, matatizo huanzia kwenye kuamua nani amefaulu na nani kafeli. Tuhuma zilizopo ni kuwa wapo wanafunzi wanapewa madaraja ya juu wakati alama zao ni za chini na wapo wanaopewa madaraja ya chini wakati alama zao ni za juu. Na hii ni kwa masomo yote.

Mheshimiwa Waziri,
Kumekuwa na utamaduni katika nchi hii wa kukataa ukweli. Kufuatia uchunguzi uliofanywa na Kamati za Bunge, tumeshuhudia wizi na ufisadi wa kutisha ukifichuliwa Bungeni hivi karibuni hali iliyopelekea mpaka Mheshimiwa Rais kubadili Baraza lake la Mawaziri.

Sasa baada ya kuyasema yote hayo, tunasema kuwa Baraza la Mitihani la Tanzania, limekuwa likilalamikiwa kwa zaidi ya miaka 30, lakini malalamiko hayo yamekuwa yakipokewa kwa sikio la uziwi. Imefikia mahali tunasema kuwa hatuna tena imani na Baraza hilo.

Mheshimiwa Waziri,
Ilikupata ukweli wa malalamiko na shutuma hizi, na ili kujibu lile swali juu ya watoto wa Kiislamu ambalo halikupata jibu Bungeni, tunaitaka serikali kufanya yafuatayo:
  1. Tume huru iundwe kuchunguza Baraza la Mitihani la Tanzania na utendaji wake kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.
  2. Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (NECTA) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaani na Baraza la Mitihani. Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa Kumputa ya Baraza la Mitihani nao wawajibishwe mara moja.
  3. Hatua za kisheria na kibinadamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa Baraza la Mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.
  4. Muundo wa Baraza la Mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea Baraza la Mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha Makatibu Wakuu Watendaji na Manaibu Katibu Wakuu wamekuwa Wakristo na Wenyeviti wa Baraza hilo ni Wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.
Mheshimiwa Waziri,
Tunaomba ieleweke kuwa tunachotaka ni kupatikana haki na kufanyika uadilifu kwa watu wote. Hatudai wala hatutaki upendeleo kwa Waislamu na wala hatutaki kuona mtu yeyote anaonewa au kuporwa haki yake, awe Mwislamu au mtu wa dini nyingine.

Tunachoamini ni kuwa kama Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haina cha kuficha, basi itaunda Tume hiyo kwa haraka na kuhakikisha kuwa ni Tume ya kuaminika itakayofanya kazi yake kwa umakini, kwa kina na kwa uadilifu wa hali ya juu kabisa.

Lakini kama Wizara yako itaona kuwa haiwezi kuunda Tume ya uchunguzi, tunacho kuhakikishia ni kuwa sisi tutafanya kila liwezekanalo na kwa namna yoyote kuhakikisha kuwa Tume hiyo inaundwa. Na ikigundulika kuwa kuna hujuma zinafanyika katika utendaji wa Baraza, basi itabidi uwajibikaji uanze kwenye Wizara kabla ya kuwawajibisha watendaji wa Baraza la Mitihani.

Ni imani yetu kuwa utayapokea madai ya Waislamu na kuyafanyia kazi kwa umakini na kwa haraka ili kujenga mustakbali mwema wa nchi hii na watu wake.

Tunaomba kuwasilisha,


Mwenyekiti
Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu
Sina la kukusaidia pole sana, unahitaji ukombozi wa fikra, labda utuambie relationship ya hilo bandiko lako na mfano wa tuhuma za kununua kiwanja cha sh milioni 4.5 kwa shilingi million 800 kulikofanywa na NSSF chini ya uongozi wa dk Dau
 
Daaa basi vyombo vya uchunguzi wamalizane na hizo tetesi za ufisadi mkubwa namna hiyo, tumalizane na Dr Dau na pia kama uongo asafishwe!
 
UWONGO MWENGINE HATA AKILINI HAUNGII, NEW CASTLE NI ILE TIMU YA KUTOKA KWENU MWANZA SAWA.
OHHHHHH KKKKKK DARAJA LA KIGAMBONIII LIMEFUNGULIWA NA MUHESHIMIWA BALOZ DAU NDIE STAA WA SHOW HIYO NDIO HABARI YA MJINI.
Mkuu inaelekea umejiunga ili uwahi kupost bandiko la kusifia ufunguliwaji wa daraja la Kigamboni? Hongera sana
 
Alikuwa na kazi maalumu yakupiga mtonyo wa taifa chini ya.........
 
Mzito Kabwela na wagalatia wote wenye husda na Dr.Dau.

Newcastle inamilikiwa na Mike Ashley kwa asilimia 100.
Pia haiko kwenye stock exchange baada ya Ashley kununua share zote na iliondolewa kutoka London stock exchange tarehe 18 July 2007.
Haya waaambie wagalatia siri moja tu ya kununua kiwanja pale Kigamboni chenye thamani ya sh 4.5 million kwa sh 800 millioni kulikofanywa na uongozi wa dk Dau pale NSSF
 
Sisikii kama Kabwe anapigwa vita kwa sababu ya dini yake. Wala sijasikia Kitilya, prof. Mahalu, William Mhando, Mramba au Yona walipelekwa mahakamani kwa sababu ya dini zao. Ila Dau tu ndiyo anaandamwa kwa dini yake.

Kweli pesa ina uwezo mkubwa, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kununua utu, mioyo hata akili za watu!
Mkuu siyo akili za watu, bali za wajinga
 
Back
Top Bottom