Utahamia lini kijijini?

Utahamia lini kijijini?

Hongera sana mkuu sema naona kila ulichofuga ni kwaajili ya nyama hapo home sijaona ulichosema umefuga kwaajili ya biashara 😃
Kitimoto 50 kwaajili ya nyama, kuku wa kienyeji 200 kwaajili ya nyama mayai, ng'ombe 5 kwaajili ya maziwa na mbuzi 50 kwaajili ya kubadilisha mboga.

Familia yako ni kubwa kiasi gani?
Kabadili picha sasa hivi
 
Safi mkuu Bora nmekupata nisaidie mambo yafuataayo.
1. Najihusisha na kuuza MIKOBA ya WADADA. Mabegi ya shule nk JE soko lipo huko.
2. Ardhi bei zake Zina unafuu MANA NAPENDA nikuishi sehemu nijenge.
3. PESA IPO.
4. NAPENDA kujiburudisha weekend JE MAeneO ya Bata mziki nk YAPO? Yamechanganya . MANA kipimo cha WATU kua na HELA sehemu huendana na muamuko WA SEHEM za starehe.
5. Usafiri WA maji ni WA uhakika.

Asante mkuu NMEMPATA RAFIKI WA kudumu


Kwishaaaaaaaaa
Karibu sana kijijini, ila tu usitubadilishie mazingira ya kijijini kuwa ya kimjini.
 
Samahani nikisafirisha punda WAWILI kuwaleta huko kwa AJILI ya kubeba mizigo kama mchanga TU vitu kiasi Ina RUKSA au hawaruhusu


Kwishaaaaaaaa
Ukipeleka farasi itakuwa bora zaidi
 
Tangu nilipoondoka mjini na kukimbilia huku kijijini, nimekuwa na maisha ya amani na utulivu mkubwa sana.

Nilifanikiwa kupata shamba la ekari nne, ambapo nilijenga kibanda changu cha kujipumzikia pamoja na mama chanja wangu, pia nikachimba na kisima.

Nikaweka uzio wa mimea kuzunguka hilo eneo lote la shamba, ili mifugo yangu isiweze kutoroka hapa na pale.

Nililigawa eneo kwa makundi (A,B,C,D,E) ili kuweka mifugo mabali mbali.

A. niliweka banda la ng’ombe 5 kwa ajili ya kunipa maziwa kila siku

B. niliweka banda la mbuzi 50 kwa ajili ya kubadilisha mboga

C. niliweka banda la kuku wa kienyeji 200 kwa jili ya mayai na nyama

D. nimeweka banda la kitimoto 50 kwa ajili ya nyama

E. bustani ya mboga mboga, nyanya, vitunguu, mchicha n.k

Pia nikaotesha miti ya matunda kama michungwa, papai, parachichi, migomba, miwa n.k

Mabaki/uchafu unaotoka kwenye mifugo, unakuwa unaenda maeneo ya shambani/bustanini na kuboresha uoto wa mimea.

Kwa ujumla, mazingira haya yameniwezesha kuwa na utulivu wa akili, uchumi, na afya bora; magonjwa ya akaili hayatanipata.

Rafiki yangu mmoja, alikuja kunitembelea huku kijijini kwangu; alipofika tu na kusikia miluzi mbalimbali ya ndege ikipiga pambio, akaniambia, ‘’Equation x na mimi sirudi tena mjini.’’

Nikamuuliza kwa nini? akanijibu, ‘’tangu nimekuja huku, akili yangu imetulia kabisa, naokota matunda nakula, mayai nakula nitakavyo, kachumbari najitengenezea, nyama nachoma nitakavyo, Napata hewa safi, ndege wanakuja na kuniimbia nyimbo mbalimbali; kusema kweli naenda kuuza mali zangu zote mjini na mimi nakuja kuhamia huku kijijini.’’

Nikabaki nacheka tu.

Je, wewe, utahamia lini kijijini?
View attachment 3418535
Nimebakisha miaka minne tu mjini hapa
Life lililobakia naenda malizia kijijini
 
Kijiji gani mkuu nikufuate, maana kuna vijiji vingine bora ufie mjini
Kijiji hiki kitakupendeza zaidi
wy.jpg
 
Back
Top Bottom