Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 57,321
- 90,568
Hakuna kamati ya bunge inayofuatlia utendaji/inayofanya oversight TISS?
Labda tuanzishe kampeni: freeTiss
1.TISS iwe taasisi huru isiyofungamana na upande wowote....CCM ama upinzani,
2.Pawepo na sheria kali za kuzuia political institutions ( hadi rais) kuingilia TISS,
3. Wafanyakazi wa TISS wapewe kinga ya kuepuka kuwa persecuted na politicians hasa watawala
4.Pawepo na TUME ya kibunge iliyokula kiapo ya kufuatilia utendaji wa TISS..(Hii itafanyakazi kama tuna bunge la wananchi, sio la sasa)
5.Mkurugenzi mkuu wa TISS ateuliwe na Rais lakini apitishwe na Bunge
6.TISS isiwe idara chini ya ofisi ya Raisi au Ikulu:TISS iwe agency iliyoseparate kabisa..Inapokuwa idara Ikulu ni rahisi sana Rais (Mwanasiasa) kuigeuza ifanyekazi kwa mtazamo wake.
7.TISS ipewe nguvu za kuuma: Kukamata na kuweka maabusu maalumu za kwao zinazojulikana kisheria.
8.TISS isishughurike na kulinda maslahi ya watawala na kuhakikisha wanabaki madarakani, TISS ijikite katika kulinda maslahi ya TAIFA na wananchi wake wote bila kujali itikadi za kidini, kiuchumi n.k.
9.TISS itengeneze ikague na kuhakikisha mihimili mingine ya dola inatenda haki..na wawawajibishe ipasavyo wanaoenda kinyume: Mfano Polisi,Magereza
10.Madawa ya kulevya, Rushwa, Ufisadi viwe vitengo chini ya TISS. Kwa kuwa TISS itakuwa na access ya taarifa sahihi ni rahisi kushughurika na hayo masuala ambayo yanahatarisha usalama wa wananchi na Taifa.
11.Sheria ipitishwe na iwe kosa kudisclose member wa TISS kwa namna yoyote ile: Kama unamjua kaa kimya tu..tunza kifuani.
12.Members wa TISS wale kiapo kizito sana cha utii kwa Taifa na wananchi na waape kulinda KATIBA ya nchi.. kwa akili zao zote, utashi wao wote, uwezo wao wote etc....
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app