Usimkopeshe hela mtu

BARUA KUTOKA UWABATA

Habari,

Umoja wa wanaume bahili Tanzania 🇹🇿 [UWABATA] unawataka wanachama wake waache kukupesha haraka iwezekanavyo na atakae kaidi atachukuliwa hatua kali.

MAKAO MAKUU,​

UWABATA,
CHATTLE.
 
Naandika haya nikiwa na machungu sana,
Siku hizi uaminifu umepotea sana tena ni adimu kama cent 5 hasa kwenye suala la pesa.

Mwaka jana nilikopesha sana watu na asilimia kubwa ni hawa "marafiki na workmates" siyo kwamba ninafedha hapana, hapa nilipo hata uwanja tu sina.

Mtu anakuja anakueleza matatizo yake na unamwambia kwakweli saizi sina kitu, anakubembeleza weeeee mwisho unamwonea huruma unaamua kuingia kwenye account na kumpa kiasi kadhaa.

Muda wa kurejesha ukifika sasa maelezo yanaanza kuwa mengi mara ooh subiri kidogo matikiti yapo shamba wiki ijayo naenda kuvuna, baada ya wiki ukimpigia simu hapokei na ikipokelewa anapokea mkewe tena anakuambia mwenye simu hayupo

Wengine sasa... Brother naomba nivumilie kidogo mwisho wa mwezi nitarekebisha then anaingia mitini. Juzi jamaa kanipigia simu (saizi yupo chuoni) ameenda kujiendeleza na ni mwajiriwa serikalini, aliniomba nimtumie hela kwani amekwama sana nikamjibu sina then nikakata simu yake, huyo jamaa mwaka 2017 nilimkopesha laki kwa makubaliano atarudisha mwisho wa mwezi lakini akatokomea kusiko julikana na mimi niliamua tu kusamehe.

Leo nimeamka nikapiga hesaba kama watu wote wangenirudishia hela yangu ningekuwa na kiasi fulani cha pesa nikabaki nahuzunika tu nakujiona kumbe mimi mjinga sana

Saizi sitaki kabisa mchezo na pesa yangu, hela yangu watapata ndugu wa damu moja na wazazi FULL STOP.
Kuna mtu ana milioni 4.5 yangu aliniahidi kati ya mwezi atalipa siku zimepita naona kimya, mishahara imetoka napo naona kimya sasa leo iwe mbwai alipe pesa yangu ama urafiki ufe.

Mtu awapo na shida anakuwa anatia huruma kweli pindi ukimkopesha tu akatatua matatizo yake usumbufu unaanza, watu wa kariba hii sio wa kuwasaidia kabisa.

Nimejifunza.
Kopesha kwa maandishi

Usikopeshe Rafiki kizembe...urafiki utakufa na Pesa hakurudishii

Pesa ni kitu kingine man
Umenikumbusha machungu yani mana nlishaanza kuyasahau...binadamu binadamu jaman
Pesa pesa...
Huyu na ushahidi wa miamala na jumbe fupi za maneno so akijaribu kuleta janja atanitambua mimi ni nani.
Mambo yamebadilika mnooo,.
Basi tu, lakini nimejifunza sikopeshi hata iweje. Kuna taasisi za kufanya kazi hiyo
Uchoyo unawasumbueni
Ukimkopesha mtu bila dhamana unakuwa hujamkopesha bali umemfadhili.Hakuna mkopo usio na makubaliano yenye dhamana hata kama ni tsh 20000
Sikopeshi tena mtu acha tu niwe mbaya
PIGILIA MSUMARI HAKUNA KUKOPESHA PESA YAKO MPAKA UKIRIDHISHE IKIWA KWELI UTALIPWA HELA ZAKO.

Sent using Jamii Forums mobile app
Siku sio nyingi nitamfunga kaka yangu kwa sababu ya kushindwa kulipa 2m. sasa hivi hapokei simu. Nimemtumia sms nitamnyoosha na undugu ufe tu. Usikopeshe ndugu mdau
tukisema kimaandishi maana yake kuna shahidi na dhamana kama nyumba,plot nk. akishindwa kulipa unabeba kiwanja. akifa je nani atakuamini
Hii imenitokea na sasa imenip mtizamo mpya...mara nyingi nimekuwa mwepesi wa kusaidia na rafiki akinicheki kwa shida yake sijiulizi sana.

Hizi hela ndogo za kuwa nisaidie 50k, 30k hapo nitarejesha baada ya siku 2...nimezitoa na nyingi hazirejeshwi na wahusika. Anakausha kana kwamba hajui chochote vile.

Hawa watu wasio waaminifu wanafanya kuwasaidia watu wahitaji iwe ngumu...
Ukipata marafiki madoni hamna upuuz kama huo.
Kama Tala na branch walidhulumiwa , wewe je?
Take care
Kati ya vitu sipendi ni kudai au kuanza kuulizia mtu ile hela vip, asee inakera.. lkn ndio hamna namna, tuishi humo!
Acha kabisa mazoeaa ya pesa na mtu mweusi ambae lugha yake ya kwanza n kiswahili.
We ndo tapeli mwenyewe.
Wenye maduka na biashara ya m-pesa n shida kila kukicha wateja wanakopa.
Kumbe wahanga ni wengi hongera mleta mada nimejifunza kitu
Mm kuna rafik yangu alinikopa 5,000/=mpaka leo anitafuti tena.
“Usitoe kile ambacho haupo tayari kukipoteza”
Mimi nimepoteza ndugu watatu. Mmoja Ni mtoto wa mjomba, kanikopa kwa shida zake mwaka wa tatu huu. Juzi nikikuambia asinijue na nisimjue na namba zake nikazifutilia mbali. Wengine wawili Ni watoto wa baba yangu, nao vivyo hivyo hata tulikutana popote kila mtu na hamsini zake. Ni Bora kua na marafiki WACHACHE kuliko utitiri wa ndugu mbwa.
Nikopeshe..najua wewe siyo mchoyo,
Rafiki yangu nilimkopesha pesa mwaka jana, siku zimeenda kafilisika kibiashara na sioni dalili ya. Kupata hiyo pesa yangu, roho yaniuma sana
Mtuvumilie ndugu, muendelee kutukopesha Mwenyezi Mungu atawajazia mnapotoa.
Siku hizi nakopesha wanawake tu maana huwa hawana longo longo
Njoo tukope hapa

Yna2
Kwakweli Binafsi nimedhukumiwa laki sita na jamaa yangu mmoja, tena yeye niilmpa kadi ya benk kabisa akachukue aliomba laki tano badae napata message kachukua laki sita tangu 2015 daah!

Ila na mimi nadaiwa na jamaa zangu wawili mmoja ananidai laki mmoja mwingine 60,000/= mmoja kanipigia sana jana sijapokea maana sina hela namwambiaje sasa ila nitalipa tu.
Mmmh.. wee mkopaji sana... na hurejeshi kitu!!
Fanya hivyo mkuu maana hapa mimi kuna watu wananidai ila nawazungusha kishenzi. Siyo makusudi lakini.
Kukopa kwa mtu? Sijawahi ila nataka kujaribu

Nishawahi kukopa branch na salary advance
Pole sana mkuu. Kaka yangu mmoja alinieleza "siku ukimkopesha rafiki yako, ni mwanzo wa urafiki kufa" Sikumuelewa mpaka siku yaliponikuta ya kunikuta. Unamkopesha mtu na hana hata aibu ya kusema alipe deni.
Branch walikuacha salama?
Yes
Nakopa nalipa, ila ukichelewesha wana zile msg zao ni noma
Nawaona wadaiwa sugu wanavyopita kimya kimya lipeni hela za watu nyau ninyi

BARUA KUTOKA UWABATA

Habari,

Umoja wa wanaume bahili Tanzania [UWABATA] unawataka wanachama wake waache kukupesha haraka iwezekanavyo na atakae kaidi atachukuliwa hatua kali.

MAKAO MAKUU,​

UWABATA,
CHATTLE.
Nahitaji nipate laki na 50 ,ili niache kukopa kopa Ela zenu, nichangieni Basi kwa hiari , na sio lazima, PM, Mana nipo kwenye Great depression x 4

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila kuna watu wana moyo jamani.. kuna siku nilikua napiga stori na jamaa yangu analalamika eti kamkopesha mtu milioni 6! Jamaa anadai alikopa 15m sasa wakati anawaza cha kufanya ndio mshkaji akamuwahi kumlilia shida eti jamaa nae akaingia line. Nilimcheka sana.. Mimi ata 50,000 sijakukopesha bado.
 
Ndio maana mi sijionyeshagi..nikiwa nazo au nisipokua nazo huwez jua yan..tena zaid zaid nikiw nazo fasta nawapigia cm kuomba waniazimishe pesa woote wanaopendaga kukopa kopa..hiyo ndio defensive mechanism mana nawa alert kuwa sina kitu so wanani tenga mbali (kama ilivyo kawaida ya wabongo, mkono mtupu haulamwi)..nabaki stress free...

Wakiniona natumbua, nawambia hiz hela za mkopo ..na we si nilikupigia unikope??
 
Naandika haya nikiwa na machungu sana,
Siku hizi uaminifu umepotea sana tena ni adimu kama cent 5 hasa kwenye suala la pesa.

Mwaka jana nilikopesha sana watu na asilimia kubwa ni hawa "marafiki na workmates" siyo kwamba ninafedha hapana, hapa nilipo hata uwanja tu sina.

Mtu anakuja anakueleza matatizo yake na unamwambia kwakweli saizi sina kitu, anakubembeleza weeeee mwisho unamwonea huruma unaamua kuingia kwenye account na kumpa kiasi kadhaa.

Muda wa kurejesha ukifika sasa maelezo yanaanza kuwa mengi mara ooh subiri kidogo matikiti yapo shamba wiki ijayo naenda kuvuna, baada ya wiki ukimpigia simu hapokei na ikipokelewa anapokea mkewe tena anakuambia mwenye simu hayupo

Wengine sasa... Brother naomba nivumilie kidogo mwisho wa mwezi nitarekebisha then anaingia mitini. Juzi jamaa kanipigia simu (saizi yupo chuoni) ameenda kujiendeleza na ni mwajiriwa serikalini, aliniomba nimtumie hela kwani amekwama sana nikamjibu sina then nikakata simu yake, huyo jamaa mwaka 2017 nilimkopesha laki kwa makubaliano atarudisha mwisho wa mwezi lakini akatokomea kusiko julikana na mimi niliamua tu kusamehe.

Leo nimeamka nikapiga hesaba kama watu wote wangenirudishia hela yangu ningekuwa na kiasi fulani cha pesa nikabaki nahuzunika tu nakujiona kumbe mimi mjinga sana

Saizi sitaki kabisa mchezo na pesa yangu, hela yangu watapata ndugu wa damu moja na wazazi FULL STOP.
 
Ndio maana mi sijionyeshagi..nikiwa nazo au nisipokua nazo huwez jua yan..tena zaid zaid nikiw nazo fasta nawapigia cm kuomba waniazimishe pesa woote wanaopendaga kukopa kopa..hiyo ndio defensive mechanism mana nawa alert kuwa sina kitu so wanani tenga mbali (kama ilivyo kawaida ya wabongo, mkono mtupu haulamwi)..nabaki stress free...

Wakiniona natumbua, nawambia hiz hela za mkopo ..na we si nilikupigia unikope??
ndo dawa yao hao,Yan mtu anakukopa baada ya hapo yeye anasahau kabisa kua ana deni la watu wewe kazi yako ni kumkumbushia tuu
 
Dah sisi ambao hatuna familia(Kuoa) watu wanaamini hatuna matumizi kabisa na pesa.......katika hali ya kawaida ni ngumu sana kumnyima mtu pesa hasa pale anapoweka shida zake wazi kwako
 
Rafiki yangu nilimkopesha pesa mwaka jana, siku zimeenda kafilisika kibiashara na sioni dalili ya. Kupata hiyo pesa yangu, roho yaniuma sana
Hahahaha mkiwa marafiki epuken sana kukopeshana

Bora umpe kama msaada lkn sio kukopeshana

Nasema ivi mtagombana, urafiki uishe


Mwanangu mmoja, siku ya Ijumaa, usikua wa saa sita, mwezi wa 1 mwaka jana , ananipigia simu..Oya Oyaaa Blood, naabika kaka, Nitumie Laki na ishirin ,jumatatu nakupa.


Nikamuuliza vipi?? Kuna usalama?? ..ananijibu yupo na Madem wanakunywa pombe

Yeye jamaa ni mnywaji wa pombe sanaaa yaan sanaaaaaa.



Basi nikamtumia 125 .


Mpaka Leo ,nawambia ivi mpaka leo hakuwahi nirudishia, urafiki ukapoteza mwelekeo.


Juzi ananitumia meseji...Kaka kaka ninaomba msaada wa elfu thelathin nimekwama hapa nilipo sijala.


Nikamwambia, Mwenyewe toka jana usiku Sijala kitu.


Akaisha kunijibu....Daaahh kudadeki ,siku ya kufa nyani


Namm nikamjibu..ndo ivo anakufa tu siku yake.

NB.. Toka ile 125 ,akawa anashindwa hata kujuliana hali, Leo hii amekamatwa ndo ananitafuta???
 
Back
Top Bottom