Usimkopeshe hela mtu

Usimkopeshe hela mtu

Hii imenitokea na sasa imenip mtizamo mpya...mara nyingi nimekuwa mwepesi wa kusaidia na rafiki akinicheki kwa shida yake sijiulizi sana.

Hizi hela ndogo za kuwa nisaidie 50k, 30k hapo nitarejesha baada ya siku 2...nimezitoa na nyingi hazirejeshwi na wahusika. Anakausha kana kwamba hajui chochote vile.

Hawa watu wasio waaminifu wanafanya kuwasaidia watu wahitaji iwe ngumu...
Nyinyi mnaoendelea kukopesha ndo mna lea tatizo
 
Nakazia mkuu.Mwaka 2020 nimejifunza somo kubwa sana baada ya kuwakopesha watu wa karibu pesa tena kwa kujinyima.Nimeambulia kejeli.Usikopeshe kamwe akafie mbali na shida yake
 
Mimi hata iwe 20k Namuambia mtu kalete kitu chenye value ýa 20K iwe Vyombo au Radio weka apo afu sema unalipa lini hata awe ndugu nafanya ivo siku alizosema zikipita nampa wiki moja ya ziada ikisha hio bado hajalipa nauza kwa hasara kitu chake
 
Bora mpe Msaada sio Mkopo kama kakuomba Mil na unazo mpe elf 30 mwambie nakuchangia ...sina kitu kabisa...Utaokoa laki 970 na urafiki wenu pia utaendelea.
 
Kopesha kwa maandishi

Usikopeshe Rafiki kizembe...urafiki utakufa na Pesa hakurudishii

Pesa ni kitu kingine man
Hata kwa maandishi haisaidii labda akifa ndg wamlipie kama ushahidi lakini ukienda kushitaki kosa linakurudia wewe unakopa bila leseni
 
Endelea kuomba MUNGU uwe ni mwenye hali nzuri kiuchumi

la hasha kuna siku utaomba pesa mtoto mdogo akukopeshe maana mnadhani wanaokujaga kukopa wanapenda

Mkuu hivi umeshawai kukopesha mtu pesa unayoitegemea ila akakuahidi anarudisha baada ya wiki moja

Ukaona isiwe tabu ukamkopa alafu ikapita miezi hata miwili yupo kimya amekausha hata taarifa ua kuomba radhi ameshindwa kulipa ndani ya muda hakupi?

Hii kitu ikikupata utajua kwanini hii biashara ya kukopesha hailipi.
 
Wewe kama unajijua ni rafiki yangu kindakindaki nikikukopa ujue sikulipi, marafiki hatukopeshani marafiki tunasaidiana.

Labda hizi ten ten Mkuu, pesa serious aisee nitakuja attach mali zako zipigwe mnada ukijiona. Mbwai mbwai tu!.
 
Back
Top Bottom