Usimkopeshe hela mtu

Usimkopeshe hela mtu

Rafiki yangu nilimkopesha pesa mwaka jana, siku zimeenda kafilisika kibiashara na sioni dalili ya. Kupata hiyo pesa yangu, roho yaniuma sana
Huyu msamehe tunaongelea wasio na woga wa madeni, kama kafirisika muonee huruma.
 
Mkuu hivi umeshawai kukopesha mtu pesa unayoitegemea ila akakuahidi anarudisha baada ya wiki moja

Ukaona isiwe tabu ukamkopa alafu ikapita miezi hata miwili yupo kimya amekausha hata taarifa ua kuomba radhi ameshindwa kulipa ndani ya muda hakupi?

Hii kitu ikikupata utajua kwanini hii biashara ya kukopesha hailipi.
Kunz dada mmoja alikuwa na shida mzigo wake wa kuuza umefika hana hela ya mzigo. Kaniomba nimkopeshe 150k atanipa baada ya week 2. Nikamuomba rafiki yangu anipe hiyo hela nimtumie. Mpaka leo hajanirudishia mpaka kani bloch simu zangu. Imebidi nilipe deni mimi. Ila nimemuambia unajizibia baraka hapa duniani, shida haziishi na hujui nani atakufaa kwa wakati gani.
 
Naandika haya nikiwa na machungu sana,
Siku hizi uaminifu umepotea sana tena ni adimu kama cent 5 hasa kwenye suala la pesa.

Mwaka jana nilikopesha sana watu na asilimia kubwa ni hawa "marafiki na workmates" siyo kwamba ninafedha hapana, hapa nilipo hata uwanja tu sina.

Mtu anakuja anakueleza matatizo yake na unamwambia kwakweli saizi sina kitu, anakubembeleza weeeee mwisho unamwonea huruma unaamua kuingia kwenye account na kumpa kiasi kadhaa.

Muda wa kurejesha ukifika sasa maelezo yanaanza kuwa mengi mara ooh subiri kidogo matikiti yapo shamba wiki ijayo naenda kuvuna, baada ya wiki ukimpigia simu hapokei na ikipokelewa anapokea mkewe tena anakuambia mwenye simu hayupo

Wengine sasa... Brother naomba nivumilie kidogo mwisho wa mwezi nitarekebisha then anaingia mitini. Juzi jamaa kanipigia simu (saizi yupo chuoni) ameenda kujiendeleza na ni mwajiriwa serikalini, aliniomba nimtumie hela kwani amekwama sana nikamjibu sina then nikakata simu yake, huyo jamaa mwaka 2017 nilimkopesha laki kwa makubaliano atarudisha mwisho wa mwezi lakini akatokomea kusiko julikana na mimi niliamua tu kusamehe.

Leo nimeamka nikapiga hesaba kama watu wote wangenirudishia hela yangu ningekuwa na kiasi fulani cha pesa nikabaki nahuzunika tu nakujiona kumbe mimi mjinga sana

Saizi sitaki kabisa mchezo na pesa yangu, hela yangu watapata ndugu wa damu moja na wazazi FULL STOP.
Na wewe usikope kwa mtu..
 
tunaokopesha kibiashara huwa tuna.mikakati ya kuokoa hela zetu zisifie kwa manyang'au...

mimi mpaka sasa nina laki 8 iko nje kwa watu lakini inaniletea riba karibu 100,000 kila wiki.

wachache sana wameshindwa kuleta pesa na ndio nimewakamatia vitu vyao kama Tv, majiko ya gesi n.k.

kukopesha ni fursa ya kukupa hela usiifanye kisamaria.

Twanga watu riba sio unatoa hela kif.ala!

achukue laki alete 120,000 baada ya wiki 2.

Hii Tv mpaa leo iko kwangu na sina presha. Elfu 50,000 sijaiona hadi leo na mwenyewe kakusha tu. Kila Juma3 anatakiwa alete 10,000 kama riba, wiki ya 3 kakausha.
sundar 17" led Tv
IMG_20220423_173148_938.jpg

huyu hapa alichukua mkopo wa Tsh 20,000 akaweka bondi jiko la gesi.

Akaahidi kuleta na riba ya Tsh 2,000 jioni yake.

nilimuwahi nikachukua elfu 10 akabakiza elfu 10.

Hii ni wiki ya 5 sijaona hata mia yake na jiko liko kwangu na wala sina presha.
IMG_20220420_114152_344.jpg



Mikopo kwangu ni biashara Tosha.

nazibeba shida za watu nazigeuza faida.
 
Bora mpe Msaada sio Mkopo kama kakuomba Mil na unazo mpe elf 30 mwambie nakuchangia ...sina kitu kabisa...Utaokoa laki 970 na urafiki wenu pia utaendelea.
Hii technique ni nzuri sana, mtu akikuomba 50k unampa 5k na kumwambia sina kitu kwa sasa, hiyo nimekupa tu wala usirudishe
 
Siku sio nyingi nitamfunga kaka yangu kwa sababu ya kushindwa kulipa 2m. sasa hivi hapokei simu. Nimemtumia sms nitamnyoosha na undugu ufe tu. Usikopeshe ndugu mdau
Baada ya vitisho alilipa. Bahati nzuri akawa mstaarabu tukaombana msamaha. Tumeendelea kujaliana
 
Back
Top Bottom