Eng. Zezudu
JF-Expert Member
- Aug 23, 2012
- 8,357
- 12,306
Ok nahitaji donation, Mana najua nikikopa sita lips kwa Sasa,.Sikopi bali nakopesha na mara zingine hua natoa bila kukumbuka...
Sent using Jamii Forums mobile app
Ok nahitaji donation, Mana najua nikikopa sita lips kwa Sasa,.Sikopi bali nakopesha na mara zingine hua natoa bila kukumbuka...
Nawaona wadaiwa sugu wanavyopita kimya kimyalipeni hela za watu nyau ninyi



Sio Kama wagosi.Duh jamaa yangu hata wanawake nao baadhi sio
...Mimi mfanyabiashara nimeshamua kupoteza tu uzuri madeni nayowadai hayafiki laki tatuMimi anayo yangu 4ml yani wakati ananifata aliniomba mtaji wa duka nikatoa kwa moyo mmoja kweli Mungu sio athumani rafiki yangu huyu amefungua biashara imekubali sana, na mipango ya kuikuza zaidi biashara ananishirikisha kila siku lakini kila napokumbusha hela yangu ni kalenda tu mpk sasa ni mwaka na nusu, inaumiza sanaKuna mtu ana milioni 4.5 yangu aliniahidi kati ya mwezi atalipa siku zimepita naona kimya, mishahara imetoka napo naona kimya sasa leo iwe mbwai alipe pesa yangu ama urafiki ufe.
Mtu awapo na shida anakuwa anatia huruma kweli pindi ukimkopesha tu akatatua matatizo yake usumbufu unaanza, watu wa kariba hii sio wa kuwasaidia kabisa.
Nimejifunza.
Kwakweli Binafsi nimedhukumiwa laki sita na jamaa yangu mmoja, tena yeye niilmpa kadi ya benk kabisa akachukue aliomba laki tano badae napata message kachukua laki sita tangu 2015 daah!
Ila na mimi nadaiwa na jamaa zangu wawili mmoja ananidai laki mmoja mwingine 60,000/= mmoja kanipigia sana jana sijapokea maana sina hela namwambiaje sasaila nitalipa tu.




Hahahaha mkiwa marafiki epuken sana kukopeshana
Bora umpe kama msaada lkn sio kukopeshana
Nasema ivi mtagombana, urafiki uishe
Mwanangu mmoja, siku ya Ijumaa, usikua wa saa sita, mwezi wa 1 mwaka jana , ananipigia simu..Oya Oyaaa Blood, naabika kaka, Nitumie Laki na ishirin ,jumatatu nakupa.
Nikamuuliza vipi?? Kuna usalama?? ..ananijibu yupo na Madem wanakunywa pombe
Yeye jamaa ni mnywaji wa pombe sanaaa yaan sanaaaaaa.
Basi nikamtumia 125 .
Mpaka Leo ,nawambia ivi mpaka leo hakuwahi nirudishia, urafiki ukapoteza mwelekeo.
Juzi ananitumia meseji...Kaka kaka ninaomba msaada wa elfu thelathin nimekwama hapa nilipo sijala.
Nikamwambia, Mwenyewe toka jana usiku Sijala kitu.
Akaisha kunijibu....Daaahh kudadeki ,siku ya kufa nyani
Namm nikamjibu..ndo ivo anakufa tu siku yake.
NB.. Toka ile 125 ,akawa anashindwa hata kujuliana hali, Leo hii amekamatwa ndo ananitafuta???




Wewe kama unajijua ni rafiki yangu kindakindaki nikikukopa ujue sikulipi, marafiki hatukopeshani marafiki tunasaidiana.
Mfano mimi kuna rafiki ambae akinifata hata leo akaniambia nimkopeshe laki tano, kama ninayo nampa. Najua kabisa kwamba hatairudisha, ila pia najua mimi siku nikimuotea ntamkopa zaidi ya hiyo na sitalipa!
Kuna best yangu mmoja TV yake ilipasuka kioo, akawa hana TV. Mi nilikua na TV iko idle, akanipiga saundi nimuuzie. Tukakubaliana laki 4. Jamaa akachukua akanipa 250k. Miezi imekatika mi wala sijawahi kumkumbusha. Kuna siku nikam taimu siku najua ana hela, nikamtumia sms saa 12 asubuhi "aisee kaka nimekwama, hebu nitumie 200k chapu ntakurudishia". Jamaa si akaingia mkenge? Ikawa ndio nitolee nahisi baadae aligundua ameshapigwa so wala hajawahi kunidai![]()









iyo huwa tunaita ngoma droo au bila bilaMimi anayo yangu 4ml yani wakati ananifata aliniomba mtaji wa duka nikatoa kwa moyo mmoja kweli Mungu sio athumani rafiki yangu huyu amefungua biashara imekubali sana, na mipango ya kuikuza zaidi biashara ananishirikisha kila siku lakini kila napokumbusha hela yangu ni kalenda tu mpk sasa ni mwaka na nusu, inaumiza sana
kama unamdai mtu ukampeleka Polisi ndio unapoteza kabisa, unaweza ukawa unadai milioni tano ukaishia kulipwa elfu5 kila mwezi maana lazima waangalie kipato cha mdaiwa na uwezo wake wa kulipa hilo deniKesi za madai hata mahakamani hazina tena ile hali ya ukali, mnaweza kumaliza nje ya mahakama na mtu akasepa
Mimi si mzuri sana kukopesha hua natoa ambayo iko ndani ya uwezo wangu
Haha! Kama post yako kukosa ile cc? Kulikoni?Kuna mambo yanakatisha tamaa sana...
Yote sababu ya awamu ya kusomesha watu namba watu pesa hawanaNaandika haya nikiwa na machungu sana,
Siku hizi uaminifu umepotea sana tena ni adimu kama cent 5 hasa kwenye suala la pesa.
Mwaka jana nilikopesha sana watu na asilimia kubwa ni hawa "marafiki na workmates" siyo kwamba ninafedha hapana, hapa nilipo hata uwanja tu sina.
Mtu anakuja anakueleza matatizo yake na unamwambia kwakweli saizi sina kitu, anakubembeleza weeeee mwisho unamwonea huruma unaamua kuingia kwenye account na kumpa kiasi kadhaa.
Muda wa kurejesha ukifika sasa maelezo yanaanza kuwa mengi mara ooh subiri kidogo matikiti yapo shamba wiki ijayo naenda kuvuna, baada ya wiki ukimpigia simu hapokei na ikipokelewa anapokea mkewe tena anakuambia mwenye simu hayupo
Wengine sasa... Brother naomba nivumilie kidogo mwisho wa mwezi nitarekebisha then anaingia mitini. Juzi jamaa kanipigia simu (saizi yupo chuoni) ameenda kujiendeleza na ni mwajiriwa serikalini, aliniomba nimtumie hela kwani amekwama sana nikamjibu sina then nikakata simu yake, huyo jamaa mwaka 2017 nilimkopesha laki kwa makubaliano atarudisha mwisho wa mwezi lakini akatokomea kusiko julikana na mimi niliamua tu kusamehe.
Leo nimeamka nikapiga hesaba kama watu wote wangenirudishia hela yangu ningekuwa na kiasi fulani cha pesa nikabaki nahuzunika tu nakujiona kumbe mimi mjinga sana
Saizi sitaki kabisa mchezo na pesa yangu, hela yangu watapata ndugu wa damu moja na wazazi FULL STOP.
Fanya kama umetoa msaadaHii imenitokea na sasa imenip mtizamo mpya...mara nyingi nimekuwa mwepesi wa kusaidia na rafiki akinicheki kwa shida yake sijiulizi sana.
Hizi hela ndogo za kuwa nisaidie 50k, 30k hapo nitarejesha baada ya siku 2...nimezitoa na nyingi hazirejeshwi na wahusika. Anakausha kana kwamba hajui chochote vile.
Hawa watu wasio waaminifu wanafanya kuwasaidia watu wahitaji iwe ngumu...
Mambo ya Kukopeshana hayo