Usimkopeshe hela mtu

Usimkopeshe hela mtu

Ndugu ndo usijaribu kabisa kumkopesha, akikuomba umkopeshe laki 1 bora umpe elf 10 mwambie hiyo laki sina chukua cha ten ikusaidie, ndugu ni wabaya sana mnaweza kuamshiana vita na ukagombana na familia
 
Kesi za madai hata mahakamani hazina tena ile hali ya ukali, mnaweza kumaliza nje ya mahakama na mtu akasepa
Mimi si mzuri sana kukopesha hua natoa ambayo iko ndani ya uwezo wangu
 
Kukopa kwa mtu? Sijawahi ila nataka kujaribu

Nishawahi kukopa branch na salary advance
Vumilia... hizo tabia zikikomaa utachafua Jina na utakosa baraka ktk kipato chako... bora kuomba kuliko kukopa halafu bila kurejesha!!
 
Naandika haya nikiwa na machungu sana,
Siku hizi uaminifu umepotea sana tena ni adimu kama cent 5 hasa kwenye suala la pesa.

Mwaka jana nilikopesha sana watu na asilimia kubwa ni hawa "marafiki na workmates" siyo kwamba ninafedha hapana, hapa nilipo hata uwanja tu sina.

Mtu anakuja anakueleza matatizo yake na unamwambia kwakweli saizi sina kitu, anakubembeleza weeeee mwisho unamwonea huruma unaamua kuingia kwenye account na kumpa kiasi kadhaa.

Muda wa kurejesha ukifika sasa maelezo yanaanza kuwa mengi mara ooh subiri kidogo matikiti yapo shamba wiki ijayo naenda kuvuna, baada ya wiki ukimpigia simu hapokei na ikipokelewa anapokea mkewe tena anakuambia mwenye simu hayupo

Wengine sasa... Brother naomba nivumilie kidogo mwisho wa mwezi nitarekebisha then anaingia mitini. Juzi jamaa kanipigia simu (saizi yupo chuoni) ameenda kujiendeleza na ni mwajiriwa serikalini, aliniomba nimtumie hela kwani amekwama sana nikamjibu sina then nikakata simu yake, huyo jamaa mwaka 2017 nilimkopesha laki kwa makubaliano atarudisha mwisho wa mwezi lakini akatokomea kusiko julikana na mimi niliamua tu kusamehe.

Leo nimeamka nikapiga hesaba kama watu wote wangenirudishia hela yangu ningekuwa na kiasi fulani cha pesa nikabaki nahuzunika tu nakujiona kumbe mimi mjinga sana

Saizi sitaki kabisa mchezo na pesa yangu, hela yangu watapata ndugu wa damu moja na wazazi FULL STOP.
Mimi huwa nafanya kama nawapa tu, hata tukiagana nakopesha.

Wasiporudisha imekula kwao. Maana kuna deal nyingine kubwa zaidi tungeweza kufanya wanakuwa wamejizibia wenyewe.

Kwa hivyo, kama unaona huna uwezo wa kuwapa hiyo hela kama sadaka, usitake kuwapa kwa minajili ya kukopesha.
 
Kuna mtu ana milioni 4.5 yangu aliniahidi kati ya mwezi atalipa siku zimepita naona kimya, mishahara imetoka napo naona kimya sasa leo iwe mbwai alipe pesa yangu ama urafiki ufe.

Mtu awapo na shida anakuwa anatia huruma kweli pindi ukimkopesha tu akatatua matatizo yake usumbufu unaanza, watu wa kariba hii sio wa kuwasaidia kabisa.

Nimejifunza.
Pasa sikulipi na urafiki uishe
 
Naandika haya nikiwa na machungu sana,
Siku hizi uaminifu umepotea sana tena ni adimu kama cent 5 hasa kwenye suala la pesa.

Mwaka jana nilikopesha sana watu na asilimia kubwa ni hawa "marafiki na workmates" siyo kwamba ninafedha hapana, hapa nilipo hata uwanja tu sina.

Mtu anakuja anakueleza matatizo yake na unamwambia kwakweli saizi sina kitu, anakubembeleza weeeee mwisho unamwonea huruma unaamua kuingia kwenye account na kumpa kiasi kadhaa.

Muda wa kurejesha ukifika sasa maelezo yanaanza kuwa mengi mara ooh subiri kidogo matikiti yapo shamba wiki ijayo naenda kuvuna, baada ya wiki ukimpigia simu hapokei na ikipokelewa anapokea mkewe tena anakuambia mwenye simu hayupo

Wengine sasa... Brother naomba nivumilie kidogo mwisho wa mwezi nitarekebisha then anaingia mitini. Juzi jamaa kanipigia simu (saizi yupo chuoni) ameenda kujiendeleza na ni mwajiriwa serikalini, aliniomba nimtumie hela kwani amekwama sana nikamjibu sina then nikakata simu yake, huyo jamaa mwaka 2017 nilimkopesha laki kwa makubaliano atarudisha mwisho wa mwezi lakini akatokomea kusiko julikana na mimi niliamua tu kusamehe.

Leo nimeamka nikapiga hesaba kama watu wote wangenirudishia hela yangu ningekuwa na kiasi fulani cha pesa nikabaki nahuzunika tu nakujiona kumbe mimi mjinga sana

Saizi sitaki kabisa mchezo na pesa yangu, hela yangu watapata ndugu wa damu moja na wazazi FULL STOP.
Ongeza na pisi Kali tu ndio watakao kula hela yako
 
Wewe kama unajijua ni rafiki yangu kindakindaki nikikukopa ujue sikulipi, marafiki hatukopeshani marafiki tunasaidiana.
 
Hahahaha mkiwa marafiki epuken sana kukopeshana

Bora umpe kama msaada lkn sio kukopeshana

Nasema ivi mtagombana, urafiki uishe


Mwanangu mmoja, siku ya Ijumaa, usikua wa saa sita, mwezi wa 1 mwaka jana , ananipigia simu..Oya Oyaaa Blood, naabika kaka, Nitumie Laki na ishirin ,jumatatu nakupa.


Nikamuuliza vipi?? Kuna usalama?? ..ananijibu yupo na Madem wanakunywa pombe

Yeye jamaa ni mnywaji wa pombe sanaaa yaan sanaaaaaa.



Basi nikamtumia 125 .


Mpaka Leo ,nawambia ivi mpaka leo hakuwahi nirudishia, urafiki ukapoteza mwelekeo.


Juzi ananitumia meseji...Kaka kaka ninaomba msaada wa elfu thelathin nimekwama hapa nilipo sijala.


Nikamwambia, Mwenyewe toka jana usiku Sijala kitu.


Akaisha kunijibu....Daaahh kudadeki ,siku ya kufa nyani


Namm nikamjibu..ndo ivo anakufa tu siku yake.

NB.. Toka ile 125 ,akawa anashindwa hata kujuliana hali, Leo hii amekamatwa ndo ananitafuta???
Tatizo alikuwa mlevi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naandika haya nikiwa na machungu sana,
Siku hizi uaminifu umepotea sana tena ni adimu kama cent 5 hasa kwenye suala la pesa.

Mwaka jana nilikopesha sana watu na asilimia kubwa ni hawa "marafiki na workmates" siyo kwamba ninafedha hapana, hapa nilipo hata uwanja tu sina.

Mtu anakuja anakueleza matatizo yake na unamwambia kwakweli saizi sina kitu, anakubembeleza weeeee mwisho unamwonea huruma unaamua kuingia kwenye account na kumpa kiasi kadhaa.

Muda wa kurejesha ukifika sasa maelezo yanaanza kuwa mengi mara ooh subiri kidogo matikiti yapo shamba wiki ijayo naenda kuvuna, baada ya wiki ukimpigia simu hapokei na ikipokelewa anapokea mkewe tena anakuambia mwenye simu hayupo

Wengine sasa... Brother naomba nivumilie kidogo mwisho wa mwezi nitarekebisha then anaingia mitini. Juzi jamaa kanipigia simu (saizi yupo chuoni) ameenda kujiendeleza na ni mwajiriwa serikalini, aliniomba nimtumie hela kwani amekwama sana nikamjibu sina then nikakata simu yake, huyo jamaa mwaka 2017 nilimkopesha laki kwa makubaliano atarudisha mwisho wa mwezi lakini akatokomea kusiko julikana na mimi niliamua tu kusamehe.

Leo nimeamka nikapiga hesaba kama watu wote wangenirudishia hela yangu ningekuwa na kiasi fulani cha pesa nikabaki nahuzunika tu nakujiona kumbe mimi mjinga sana

Saizi sitaki kabisa mchezo na pesa yangu, hela yangu watapata ndugu wa damu moja na wazazi FULL STOP.
Ndugu tusilaumiane uukikataza watu kukopesha tutapata wapi sapoti
 
Endelea kuomba MUNGU uwe ni mwenye hali nzuri kiuchumi

la hasha kuna siku utaomba pesa mtoto mdogo akukopeshe maana mnadhani wanaokujaga kukopa wanapenda
Kweli Yani , Mana niliowakopa walinikuta napiga kazi sehemu flani na nikawa boss wao na kuwatrain, hafu leo nawakopa baada ya kubanwa mbavu na Ela wasinitoe, wajinga sana Hawa madogo,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom