Usijiroge kununua gari isiyo brand ya Toyota kama unaishi mikoani, maji utayaita Mma !

Usijiroge kununua gari isiyo brand ya Toyota kama unaishi mikoani, maji utayaita Mma !

watu kibao

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2025
Posts
466
Reaction score
1,645
Uwe mkoani halafu uige watu wa kwenye majiji ununue mazda cx5. Range Rover, Ford, Volks-Wagen na gari nyingezo nje ya Toyota, jiandae maumivu !!

Wenzako ukiwaona wapo mikoani na wana push hizo brand mara nyingi huwa zinaenda kufanyiwa matengenezo na service Dsm na kwa mbali kidogo Mwanza na Arusha. huwezi kuzikuta garage za mikoani labda matatizo ya kawaida sana, Iga sasa uone ! tena siku hizi kuna nafuu ni DSM, nakumbuka miaka ya 2000s gari hizo matengenezo ya uhakika hadi uvuke boda uende Nairobi.

Mafundi wengi wa mikoani ni Ramli a.k.a gari pekee wanazozijua ni Toyota tena ziwe common models, nje ya hapo ni risky.
 
Matatizo yaliyo mengi kama sio yote yanamalizwa na pesa.
Ukiwa na pesa za uhakika pesa zinaambia moyo wako"unataka nini ewe moyo",moyo unajibu nataka Audi ya 2028,kisha pesa inaleta Audi ya 2028 mwaka huu wa 2025 kama moyo wako ulivyotamani.
Hizo ni level za kina Bakhresa, Gsm, n.k. ni watu wachache sana kwa Tz.

Watanzania wengi tunaponunua magari ni muhimu kujua affordability ya matengenezo,
 
Nakubaliana na mleta mada 100%..... I will die kwa toyota. Sioni haja ya kwenda na brand ingine. Ukipata hela si una upgrade to toyota... from vits labda premio to Rav 4.. to fortuner to prado to LC300... ya nini kwenda na magari ambayo roho mkononi likipata shida ukiwa safari mpaka uite fundi wa daslama?...wooiiiiiiiii... team toyota to death
 
Fundi wa kwanza wa gari ni wewe mwenyewe (siyo fundi flani) na mchawi wa kwanza wa gari ni wewe mwenyewe(siyo brand ya gari au aina ya gari). Gari zinatoka na maintenance manual na mitandaoni zimejaa tele ila watu hawasomi, wanaishia kulaumu uhaba wa mafundi au gari husika. Unapiga reverse CX5 haijasimama tayari umeshatia Drive gear, kwanini baada ya muda usiue CVT? Hata kwa toyota utaua tuu. Utofauti ni kwamba spear za toyota utazipata kwa urahisi, ila hapo tatizo siyo gari, ni wewe mwenyewe. Unaambiwa ukisha drive long safari uipe muda kidogo ifanye DPF regeneration ila wewe unafika, unapaki na kuzima hapohapo kila mara....unatarajia nini? Huoni hata madereva malorry wenyewe hawazimagi gari muda huohuo baada ya safari? Gari nyingi za kisasa na hasa za diesel zina masharti yake na hazitaki mazoea. Pia uzuri wa gari za kisasa zinakutaarifu tatizo kabla halijawa kubwa hivyo uki potezea ndipo unaishia kulaumu gari flani ni mbaya.
Subaru Forester zilianzaga kudisiwa muaka ya nyuma ila vijana wa Arusha wakakomaa nazo hivyohivyo hadi sasahivi zimekuwa kama toyota. #Drive what you love as long as you can afford it#
 
Nakubaliana na mleta mada 100%..... I will die kwa toyota. Sioni haja ya kwenda na brand ingine. Ukipata hela si una upgrade to toyota... from vits labda premio to Rav 4.. to fortuner to prado to LC300... ya nini kwenda na magari ambayo roho mkononi likipata shida ukiwa safari mpaka uite fundi wa daslama?...wooiiiiiiiii... team toyota to death
Mimi nachojua ukinunua Fortuner ni kama umenunua Ford ranger tu labda unieleweshe tofauti ila hizo ist,rav 4 na ndugu zake ni Toyota kwa maana kutatua Fortuner changamoto zake haijatofautiana na Ranger iwe kwa gharama hata parts zake pia..
 
Mimi nachojua ukinunua Fortuner ni kama umenunua Ford ranger tu labda unieleweshe tofauti ila hizo ist,rav 4 na ndugu zake ni Toyota kwa maana kutatua Fortuner changamoto zake haijatofautiana na Ranger iwe kwa gharama hata parts zake pia..
Fortuner ni almost sawa kabisa ni hilux. Hazina tofauti kubwa. Ukipata za kuanzia 2018 na kuendelea yenye engine za either 1GD au 2GD, they are quite cheap and easy to maintain ukilinganisha na ford ranger za same years.. spare za fortuner na hilux zinaingiliana kwa 90%...i am talking from experience kabisaaaaa, its very easy to maintain a fortuner compared to a ford ranger... na kingine kikubwa zaidi ni resale value... tuchukue leo fortuner uliyoiagiza 2018 say ukakaa nayo miaka 6, kisha tuuze alafu compare same scenario na ford ranger uone ipi itakua na higher market resale value compared to the purchase price uliyonunua mwanzo. Ukipata jibu utuambie mkuu.
 
Ukinunua gari za Europe kwa hapa Tanzania ni sawa na kuoa wasanii wa Bongo awe mwanamziki au bongo movie, utajutia..!!
 
Fortuner ni almost sawa kabisa ni hilux. Hazina tofauti kubwa. Ukipata za kuanzia 2018 na kuendelea yenye engine za either 1GD au 2GD, they are quite cheap and easy to maintain ukilinganisha na ford ranger za same years.. spare za fortuner na hilux zinaingiliana kwa 90%...i am talking from experience kabisaaaaa, its very easy to maintain a fortuner compared to a ford ranger... na kingine kikubwa zaidi ni resale value... tuchukue leo fortuner uliyoiagiza 2018 say ukakaa nayo miaka 6, kisha tuuze alafu compare same scenario na ford ranger uone ipi itakua na higher market resale value compared to the purchase price uliyonunua mwanzo. Ukipata jibu utuambie mkuu.
Parts za Fortuner na Ford nakonunua mimi ili nije kuuza hazijatofautina bei na pia kuuza magari watu wananunua gari zote nimekuja na Fortuner na Ford ranger zote nimeuza gari zimejaa hapa Daslm unazungumzia mambo ya kuuza miaka hii mkuu..
Watu wana Land Rover E Face au F series ambazo kwa SA tu wanazo wachache ila Wabongo wanazo na hata hawawazi..
Niliwa kuleta Honda balade auto mwaka 2002 nilipata maneno kama yako leo hii 2025 ukirudia sishangai kumbuka kipindi hicho gari zilikua manual ile auto ya ballade waliita ya kike zilivyoanza kuletwa kibao wakaitamani ile tena..
 
Changamoto mafundi wetu ni wale waliofeli shule na wamekaririshwa gari ni toyota mtoa mada naungana na wewe maana jamaa yangu kanunua BMW X3 kahamishwa kaenda BIHARAMULO imekufa haijavuka hata mwaka
 
Bado unaishi karne ya 19 kijana!

Tembelea Kahama ujionee hizo Mazda,Audi,Range,VW,BMW,Nissan,Subaru etc zinatengenezwa hapo hapo!

Kuna garage kubwa zilizopo Dar&Mwanza na zina office Kahama,mafundi ni hao hao wana-rotate kuligana na uhitaji.

NB: Kahama kuna HAWK MOTORS LTD hao jamaa hata chopper ukipeleka wanapiga kazi.😁

images.jpeg
 
Kukariri maisha nacho ni kitu kibaya au kukaa mkoa mmoja na kutembea kuna faida nyingi sana Spare za VW kahama zinaweza kuwa Rahisi kuliko hata Dsm Kahama anaweza kuagiza Rwanda Arusha Spare zinaweza kuwa rahisi kuliko Dar kuna watu wana magari Dar spare zinatoka kahama au Arusha
TEMBEA JOMBAAA !!!
 
Parts za Fortuner na Ford nakonunua mimi ili nije kuuza hazijatofautina bei na pia kuuza magari watu wananunua gari zote nimekuja na Fortuner na Ford ranger zote nimeuza gari zimejaa hapa Daslm unazungumzia mambo ya kuuza miaka hii mkuu..
Watu wana Land Rover E Face au F series ambazo kwa SA tu wanazo wachache ila Wabongo wanazo na hata hawawazi..
Niliwa kuleta Honda balade auto mwaka 2002 nilipata maneno kama yako leo hii 2025 ukirudia sishangai kumbuka kipindi hicho gari zilikua manual ile auto ya ballade waliita ya kike zilivyoanza kuletwa kibao wakaitamani ile tena..
Umeelewa maana ya resale value???... namaamisha kuiuza after kukaa nayo hapa bongo kwa miaka kadhaa.. not straight after importation....
twende mbele turudi nyuma kumaintain fortuner ni rahisi zaidi kulinganisha na ford ranger kwasababu ya uwingi wa mafundi wanaozielewa toyota.. spare parts huko nje might be the same price sikatai, but locally kwasababu za toyota ni fast moving business people lazma wataweka faida kidogo kuliganisha na za ford, huo ndo ukweli mchungu....TOYOTA ITABAKI KUWA TOYOTA
 
wabongo bado waoga sana, mi nimesafiri na mazda axela dar-Mbeya, Mbeya-Songea then Songea-Dar(Via lindi), sijakutana na Axela hata moja, kichwani nikawa nawaza hivi gari ikipata changamoto huku si nimekwisha!
 
Back
Top Bottom