MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,223
- 22,299
Leo ninaandika nikiwa na mawazo mengi sana mchanganyiko. Kwanza nimeshtushwa na hili ongezeko la watu wanaoniita Anko/Mjomba badala ya kaka. Hii inaashiria nini kwa mimi kijana mdogo wa CCM mwenye miaka 38? Wakati nikitafakari hilo nikashtuka kuona mvi kwenye ndevu nilipojitazama kwenye kioo.
Ninaandika huu uzi kuwakumbusha wanaJF wote kuwa hakuna bahati mbaya siasani. Hii ni baada ya watu kupaniki kwa kuona sheria mpya imepitishwa kuwapa mafao wake za viongozi.
Kiukweli hata mimi ninatafakari ni sababu gani ya msingi sana iliyosababisha watu kukaa chini kuamua kuwaneemesha zaidi hizi familia tajiri ambazo hakuna wanachokosa maishani?
Kwenye ilani ya CCM kulikuwa na hizi ahadi kwamba tukichaguliwa tutahakikisha wake za viongozi wanapata ulaji? Mimi bado natafakari na kujipa muda kujifunza kama kuna tija yoyote katika hili.
Haya mambo huwa yanaanzaga katika hali kama ya masikhara hivi kumbe nyuma ya pazia tayari kila kitu kimeshapangwa. Mke wa Rais mstaafu hakuwa anabahatisha kwenye kauli yake.
Kwa wale wafuasi wa Mbowe mtakuwa mmejifunza pia. Viongozi wenu wamekuwa wakitoa kauli zisizoeleweka ila kwa ubishi wenu mmekuwa mstari wa mbele kutetea.
Ninaandika huu uzi kuwakumbusha wanaJF wote kuwa hakuna bahati mbaya siasani. Hii ni baada ya watu kupaniki kwa kuona sheria mpya imepitishwa kuwapa mafao wake za viongozi.
Kiukweli hata mimi ninatafakari ni sababu gani ya msingi sana iliyosababisha watu kukaa chini kuamua kuwaneemesha zaidi hizi familia tajiri ambazo hakuna wanachokosa maishani?
Kwenye ilani ya CCM kulikuwa na hizi ahadi kwamba tukichaguliwa tutahakikisha wake za viongozi wanapata ulaji? Mimi bado natafakari na kujipa muda kujifunza kama kuna tija yoyote katika hili.
Haya mambo huwa yanaanzaga katika hali kama ya masikhara hivi kumbe nyuma ya pazia tayari kila kitu kimeshapangwa. Mke wa Rais mstaafu hakuwa anabahatisha kwenye kauli yake.
Kwa wale wafuasi wa Mbowe mtakuwa mmejifunza pia. Viongozi wenu wamekuwa wakitoa kauli zisizoeleweka ila kwa ubishi wenu mmekuwa mstari wa mbele kutetea.