Hakujawahi kuwa na Mkataba mbaya kama huu wa Bandari, tuamke

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,489
40,999
Nchi hii imewahi kuwa na mikataba mingi mibaya, lakini hakujawahi kuwa na mkataba mbaya, wa hovyo na wa kibaradhuli kama huu wa Bandari.

Mikataba mingine, japo ilikuwa mibaya, lakini angalao ilikuwa na ukomo. Maana yake ni kwamba hata kama kukiwa na makosa, angalao unajua mtaumizwa kwa muda fulani tu, kisha mtakuwa huru, mtarekebisha makosa yenu.

Mkataba wa bandari, kati ya Tanzania na DP World hauna ukomo, eti ukomo wake ni mpaka shughuli za bandari zitakapokoma. Shughuli za bandari zitakoma lini? Tuna mategemeo bahari itakauka?

Siku zote nimekuwa na matumaini makubwa na Rais Samia, lakini baada ya hili, nina uhakika kabisa, hana dhamira njema na Tanzania, hasa Tanganyika. Na hakika amenikatisha sana tamaa na kunivunja moyo, najua ni wengi, wala siyo mimi pekee.

Imenikumbusha ile kauli ya baadhi ya Wazanzibari waliyowahi kuitamka, eti ukanda wote wa pwani ya mashariki ya Tanganyika ni sehemu ya Zanzibar kwa vile maeneo hayo wakati wa utawala wa sultani yalikuwa chini ya utawala wa sultani wa Zanzibar. Na Zanzibar ni sehemu ya Oman kwa sababu yalikuwa makao makuu ya sultani wa Oman.

Labda haya ni maandalizi ya muda mrefu ili siku moja ukanda wote wa pwani ya bahari uanze kugombaniwa kati ya Tanganyika na Zanzibar. Someni historia ya Israel na Palestine, ndipo mnaweza kupata mwangaza kuwa kuna wakati hata yasiyofikiriwa kutokea huwa yanatokea.

Wizara isiyokuwa ya muungano, wizara ya uchukuzi amewekwa Mzanzibari. Katibu mkuu wa Wizara amewekwa Mzanzibari. Sidhani kama ilikuwa ni kwa bahati mbaya.

Leo, bandari na ardhi ya maeneo ya kuzunguka bandari za Tanganyika yanauzwa na Wazanzibari, kwa waarabu. Haya yameuzwa moja kwa moja kwa sababu hakuna ukomo wa mkataba. Siyo miaka 90 wala 100, ni mkataba wa milele.

Ni wakati huu wa Rais mzanzibari, Waziri wa usafirishaji mzanzibari na katibu wa wizara akiwa mzanzibari, wanakamilisha kazi ya kuuza bandari za Tanganyika kwa waarabu.

Rais Mwinyi, Mzanzibari aliuza mbuga ya wanyama ya Tanganyika kwa waarabu. Leo Samia anauza bandari za Tanzania kwa Waarabu. Kati yao hakuna aliyewahi kuuza hata fukwe tu za Zanzibar kwa Waarabu.

Wajinga zaidi ni wabunge wa Tanganyika ambao walistahili kuwa walinzi na watetezi wa rasilimali za Tanganyika, kinyume chake wanashirikiana na Wazanzibari kuuza urithi wa nchi yao.

Karume aliwahi kusema kuwa Mwungano ni koti, likikubana unalivua. Sasa hawa akina Musukuma, siku ikitokea koti limewabana wazanzibari, wakaamua kulivua, watamfanya nini mwarabu aliyeuziwa bandari zote na Wazanzibari?

Kumbukeni Zanzibar ni nchi, ina baraza lake la mawaziri, ina katiba yake, ina mipaka yake. Muungano wetu ni kwenye Urais wa Mwungano, kwenye wizara ya ulinzi, mambo ya ndani na mambo ya nje tu.

Leo Tanganyika imekuwa kama ni eneo lenye upungufu wa watu kiasi hata cha kukopeshwa watu toka Zanzibar kuja kuongoza wizara zisizo za Mwungano.

Kuanzia leo, wananchi bila ya kujali itikadi zetu, imani zetu au maeneo tutokayo, tutamke kuwa wabunge waliopo huko Bungeni ni maadui wa Taifa, ni wauaji wa Taifa, wasiostahili heshima yoyote ya umma.

Tutamke kuwa tuna Serikali ambayo haipo kwa maslahi ya nchi, bila shaka ni serikali kibaraka. Tukiendelea kulala, mengi ya ajabu yatakuja. Wananchi tuchukue hatua za muda mfupi na mrefu kuhakikisha rasilimali zetu za bandari za Tanganyika, hata kama siyo leo au kesho, lazima zirudi kwenye nchi yetu.

Babu zetu waliuzwa utumwani kwa waarabu baada ya kupewa shanga na sahani za udongo, leo tunauzwa kwa dola 50,000 na V8!!

Ombi kwa Rais Samia, kama waarabu wana dhamira njema kwa kuchukua umiliki wa milele huku bara, hiyo neema wapelekee Zanzibar. Waifanye kuwa bandari huru. Wape na fukwe zote za Zanzibar waziendeleze kwaajili ya utalii. Tanganyika hatuitaki hiyo neema.

Kwa mikataba ya kijinga kama hii, anahitajika kiongozi jasiri asiyejali, anayeweza kusema kuwa huo mkataba ni wa kijinga, naufuta kuanzia leo. Kama kuna sijui damages au compensation wakawadai waliosaini, na hao waliowahonga pesa na magari.
 
Itoshe tu kusema unaongea kitu ambacho hujakiona Wala kukielewa. Watu wanachukua mstari mmoja wa document, wanakimbia nao kama kuku aliyekatwa kichwa.

Tafuta hiyo document, isome taratibu. Uelewe.
Katika Sheria vifungu Huwa ni complimentary.

Itoshe kusema, Mkataba Kati ya Serikali ya Tanzania na Seriakali ya Ufalme wa Dubai, inaridhiwa Leo na bunge. Sasa tusubiri Mkataba au Mikataba ya DP-WORLD na TPA
 
Itoshe tu kusema unaongea kitu ambacho hujakiona Wala kukielewa. Watu wanachukua mstari mmoja wa document, wanakimbia nao kama kuku aliyekatwa kichwa.

Tafuta hiyo document, isome taratibu. Uelewe.
Katika Sheria vifungu Huwa ni complimentary.

Itoshe kusema, Mkataba Kati ya Serikali ya Tanzania na Seriakali ya Ufalme wa Dubai, inaridhiwa Leo na bunge. Sasa tusubiri Mkataba au Mikataba ya DP-WORLD na TPA
Jinga wewe!
 
Mwanamke ni mwanamke tu, ukimsifia kidogo tu atakupa vyooote.

Screenshot_20220612-124436_Chrome.jpg
 
Nimekuelewa kwenye jambo moja tu kuwa Zanzibar wana Serikali yao,Bunge lao na Mahakama yao na iwapo Bandari na hasa hasa Dar es Salaam, Bagamoyo, Kilwa na Mtwara zitakuwa chini ya umiliki wa Waarabu ambao ni ndugu hasa na Mheshimiwa Rais basi hapo mbeleni Zanzibar wanaweza jitenga na huu Muungano feki na kuchukua hayo maeneo kama vyanzo vya mapato kwenye Serikali yao.Asante sana kwa elimu nzuri.
 
Itoshe tu kusema unaongea kitu ambacho hujakiona Wala kukielewa. Watu wanachukua mstari mmoja wa document, wanakimbia nao kama kuku aliyekatwa kichwa.

Tafuta hiyo document, isome taratibu. Uelewe.
Katika Sheria vifungu Huwa ni complimentary.

Itoshe kusema, Mkataba Kati ya Serikali ya Tanzania na Seriakali ya Ufalme wa Dubai, inaridhiwa Leo na bunge. Sasa tusubiri Mkataba au Mikataba ya DP-WORLD na TPA
Ngorongoro iko wapi?
 
Mlionewa sana, sasa mnapumua!

Alipofariki yule mtu mlikunywa bia sana, mkisema sasa mko huru.

Kiufupi haya yanayotokea mliyataka.
Pumbavu zako bila yeye tungeongelea hii mikataba mibovu?Si yeye aliaandaa hivyo alipotaka kuifanya Chato iwe Jamhuri.Unafikiri bila akili mbovu za Magufuri Wazanzibar wangekuwa na nguvu hii unayoiona leo?Kila tukiongea wasema mbona kwa mwendazake hamkuongea kila kitu alipendelea kwao.Na mbaya zaidi alijitapa kuwa Wapinzani walichelewesha sana maendeleo na akatunga sheria za ajabu ili kuwaondoa kwenye utawala wake na alipofanikiwa Mungu si Abdallah wala John akamchukua kiulaini sasa nchi imebaki mikononi mwa mashetani halisi ambao hawana huruma na nchi hii.
 
Pumbavu zako bila yeye tungeongelea hii mikataba mibovu?Si yeye aliaandaa hivyo alipotaka kuifanya Chato iwe Jamhuri.Unafikiri bila akili mbovu za Magufuri Wazanzibar wangekuwa na nguvu hii unayoiona leo?Kila tukiongea wasema mbona kwa mwendazake hamkuongea kila kitu alipendelea kwao.Na mbaya zaidi alijitapa kuwa Wapinzani walichelewesha sana maendeleo na akatunga sheria za ajabu ili kuwaondoa kwenye utawala wake na alipofanikiwa Mungu si Abdallah wala John akamchukua kiulaini sasa nchi imebaki mikononi mwa mashetani halisi ambao hawana huruma na nchi hii.
Una harisha au unakunya?

Subirini mama abinafsishe nchi kwa ndugu zake waarabu!

Si mnapumua baada ya kuonewa sana nyie?

Na bado vyupi hivyo mbona mtavaa kichwani!
 
Back
Top Bottom