Ushindi mtamu ni ushindani katika uwanja sawa, sio ule wa mezani. Magufuli, kasi yako ni ushindi wa kishindo. Ruhusu ushindani wa haki, sawa na wazi

Nchi inahitaji maendeleo ya watu ...tumejichelewesha sana kusaka kiki za demokrasia kwani ndio upuuz waliotaka tuufikirie.
Mkuu Jingalao, naunga mkono hoja, Watanzania wanachohitaji ni maendeleo na sio siasa, rais Magufuli kupitia ilani ya uchaguzi ya CCM, ameleta maendeleo ya kweli ya vitu na yanaonekana, hivyo huu ni mtaji tosha wa ushindi kwa CCM, ndio maana nimeshauri, hakuja haja ya kuogopa lolote wala chochote, wawaruhusu wote kuingia dimbani ili ushindi wa kishindo wa CCM upatikane kupitia ushindani wa haki kwa uchaguzi huru na wa haki ndani ya uwanja sawa wa siasa.
P
 
Tushakujua kuwa wewe ni ccm maana kipindi majina yamekatwa hukuongea chochote sasa umesikia tamko la jafo unajifanya kushauri
Mkuu Teja, usilete mambo ya mateja humu ila ruksa kunidhania mimi ni CCM, kwa sababu nikiamua kujiunga na chama, Tanzania hatuna any options tuna chama kimoja tuu, CCM.

Wakati majina yanakatwa mimi nilikuwa busy Dodoma na watu wa Azaki. Ushauri wa bandiko hili sio kwa Jafo ni ushauri kwa Mzee Baba mwenyewe.
P
 
Mayalla Mayalla Mayalla. Najua unaipenda sana CCM kuliko hata Tanzania!
CCM si wajinga hivyo. Wanauhakika mia kwa mia uchaguzi ukifanyika kwa halali labda wataambulia chini ya asilimia moja. Sifa mnazozitoa ni kufagilia ugali tu.
Miaka 60 madarakani CCM haiwezi kupambana kwa hoja hata na mgombea kitongoji wa upinzani ambae hakumaliza hata darasa la saba. Tumeona mpaka bungeni hakuna mbunge au waziri anayeweza jibu hoja za upinzani. Tumeona spika akitumia kamati ya maadili na madaraka ya bunge kukwepa hoja, au akihariri hotuma za wapinzani au akiwafukuza bungeni. Huku mtaani mjumbe wa kijiji anayegombea kupitia upinzani atakumbana na vioja vya VEO, WEO, polisi, usalama wa taifa, mkurugenzi, mahakama, afisa biashara, tra, bwana afya nk. nk Pascal Mayalla,
 
Sitaki kuingia ndani kwenye technicalities zilizopelekea wagombea wa upinzani kuenguliwa, bali natoa wito kwa rais Magufuli aingilie kati hali hii au yeye mwenyewe kama rais wa JMT, au kupitia kwa Waziri Jaffo wa Tamisemi, ayafute makosa yote ya wagombea wote wa vyama vyote walioenguliwa kwa sababu zozote, ziwe ni za kweli za halali au ni figisu, watoe amnesty kila aliyegombea apitishwe tuu hivyo hivyo despite all the odds ili Tanzania tuingie kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu Mwakani kwa Ushindani wa haki, uwazi na Usawa kwa vyama vyote kutendewa haki sawa, hivyo waliosusa wote warudi.
Nami sitaki kubishana na weye Paskali kwa sababu nakujua kuwa weye ni GT. Ila umesahau kuwa rafu zilianzia tangu kuchukua fomu. Wapinzani walifika wakakuta milango imefungwa na wenye fomu hawakurudi hadi machweo. Hivi, utamwambia mkulima aende ofisi ya mtendaji akashinde pale siku 3 haoni mlango ukifunguliwa?? Ndio hivyo ukaambiwa, wengine wamepita bila hata kupingwa 54% ya wagombea.
Waliopewa fomu ikawa kitendawili kuzirudisha. Waziache pale mlangoni au?? Na Mola wetu alivyo mzuri, zikanyesha mvua zisizo na mpango. Ukiziacha nje ya lmango zimelowa. Watendaji hawakuonekana hadi siku na saa zikapita.
Sasa, wale wachache zilizopokelewa ndio wakakatwa wote kuwa hawafai. Lakini leo baada ya kuwapigia mahesabu ya kweli imeonekana hata hao wakipita, hawakitingishi chama. Upooo??
Paskali, kama unasikilizwa mwambie mtani wako; Aahirishe tusikidhalilishe chama. Ushindi uwe uwanjani wa haki na wazi. Tuchukue fomu mpya, zilizoelekezwa vizuri namna ya kujazwa halafu tuombe waangalizi wapya. Hata kutoka jirani
 
Habari njema zimeanza, Waziri katangaza wagombea wote walioenguliwa kwa kujaza fomu vibaya warudishwe.
Huu sio mwanzo mbaya, sasa tunawasubiri Mbowe na Zitto kutangaza kuruhusu timu zao kuingia dimbani.
P
Mkuu Pascal wazo lako ni zuri naomba nitangulize shukrani Kwa kuwa mzalendo na nchi yetu , Sema kurudisha tiny uwanjani si sahihi Kwa sasa kila kitu kinatokea Kwa sababu, na hizi figisu zilitokea Kwa sababu maalumu na mapenzi ya mungu Kwa Taifa letu la Tanzania. Kwa hiyo nachokuomba Rudi tena Kwa mkuu WA nchi, Raisi wetu mpendwa umuombe Kwa niaba ya watanzania wote wapenda Haki na usawa,kuwa imefika wakati WA kupata #TUMEHURUYAUCHAGUZI ndipo timu zirudi uwanjani kwenye mechi narudia mwambie watanzania wanaomba uchaguzi huu WA 24 November 2019 ufutwe uanze mchakato mpya WA #Tumehuruyauchaguzi. Asante ni Mimi mpendwa Haki mwenzio
 
Pascal Mayalla , huyo nduguyo si umweleze kwa Kisukuma ndio atakuelewa, hii lugha adhimu kwake naona siyo rafiki sana, anaiona nayo Ni ngumu kama ile lugha nyingine inayomfanya asishiriki mikutano ya kimataifa.
Uzalendo halisi na wa ni kuzungumza kwa kutumia lugha yetu adhimu ya Kiswahili.
Sababu za kutosafiri nje ni uzalendo uliotukuka wa kubana matumizi, na sio issue za lugha, kama ni lugha ya Malikia, inapanda sana, ameitumia hadi kwenye Ph.D thesis yake.
P
 
Kama wana vigezo vyote majina yao yatabandikwa. Ni utaratibu na kanuni za uchaguzi. Wao hawafuati porojo za vyama kujitoa ingawaje wenye majina yatakayobandikwa wana hiari ya kufanya kampeni au la. Kimbembe kitakuwa endapo watashinda, Chadema itawatambua? Itawafukuza? Tunasubiria!
Mkuu Sweet tablet hili ni swali la msingi sana na tunanalisubiria.
P
 
Pascal Mayalla,

PASCAL MAYALLA , NABII WA BWANA UMTABIRIA MFALME KITOKACHO KWA BWANA . LAKINI MANABII WA UONGO ( masilahi ) UTABIRIA UONGO MFALME. Kwa tahaluma yako na weredi wako, unatakiwa kuandika kile unachojua kuwa ni ukweli. Wafanyakazi wanalia, wavuvi, wakulima,mamatilie, wafanyabiashara na hata wanafunzi. Hivi CCM washinde kwa kura zipi ?. Nakusii usome biblia. SOMA Wafalme 22:1-28,34-37

[1]Wakakaa miaka mitatu pasipo vita kati ya Shamu na Israeli.

[2]Ikawa, mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme Wa Yuda akamshukia mfalme wa Israeli.

[3]Mfalme wa Israeli akawaambia watumishi wake, Je! Hamjui ya kuwa Ramoth-Gileadi ni yetu? Nasi tumenyamaza tusiitwae mkononi mwa mfalme wa Shamu?

[4]Akamwambia Yehoshafati, Je! Utakwenda nami tupigane na Ramoth-gileadi? Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Mimi ni kama wewe, na watu wangu ni kama watu wako na farasi zangu ni kama farasi zako.

[5]Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Uulize leo, nakusihi, kwa neno la BWANA.

[6]Ndipo mfalme wa Israeli akawakusanya pamoja manabii, kama watu mia nne. Akawaambia Je! Niende juu ya Ramoth-Gileadi kuupiga vita, au ninyamaze? Wakasema Kwea; kwa kuwa BWANA atautia mkononi mwa mfalme.

[7]Lakini Yehoshafati akasema, Je! Hayupo hapa nabii wa BWANA tena, ili tumwulize yeye?

[8]Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Yupo mtu mmoja, ambaye tungeweza kumwuliza BWANA kwa yeye, yaani Mikaya mwana wa Imla; lakini namchukia; kwa sababu hanibashirii mema, ila mabaya. Yehoshafati akasema, La! Mfalme asiseme hivi.

[9]Ndipo mfalme wa Israeli akamwita akida, akamwambia, mlete hima Mikaya mwana wa Imla.

[10]Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wakikaa kila mtu katika kiti chake cha enzi, wamevaa mavazi yao, katika sakafu langoni pa Samaria; na manabii wote wakafanya unabii mbele yao.

[11]Na Zedekia mwana wa Kenaana akajifanyia pembe za chuma, akasema, BWANA asema hivi, Kwa hizo utawasukuma Washami, hata waharibike.

[12]Na manabii wote wakasema hivyo kwa unabii, wakisema, Kwea Ramoth-Gileadi, ukafanikiwe; kwa kuwa BWANA atautia mkononi mwa mfalme.

[13]Na yule mjumbe, aliyekwenda kumwita Mikaya, akamwambia, akasema, Angalia sasa, maneno ya manabii kwa kinywa kimoja husema mema kwa mfalme; neno lako na liwe, nakusihi, kama neno la mmojawapo wao, ukaseme mema.

[14]Mikaya akasema, Kama BWANA aishivyo, neno lile BWANA aniambialo, ndilo nitakalolinena.

[15]Na alipokuja kwa mfalme, mfalme alimwambia, Je! Mikaya, tuende Ramoth-Gileadi kupiga vita, au tunyamaze? Akamwambia, Kwea, ufanikiwe; kwa kuwa BWANA atautia mkononi mwa mfalme.

[16]Mfalme akamwambia, Mara ngapi nikuapishe usiniambie neno ila yaliyo kweli, kwa jina la BWANA?

[17]Akasema, Naliwaona Waisraeli wote wametawanyika milimani, kama kondoo wasio na mchungaji. BWANA akasema, Hawa hawana bwana; na warudi kila mtu nyumbani kwake kwa amani.

[18]Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Je! Sikukuambia, hatanibashiria mema, ila mabaya?

[19]Mikaya akasema, Sikia basi neno la BWANA; Nalimwona BWANA ameketi katika kiti chake cha enzi, na jeshi lote la mbinguni wamesimama upande wa mkono wake wa kuume na wa kushoto.

[20]BWANA akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili akwee Ramoth-Gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi.

[21]Akatoka pepo, akasimama mbele za BWANA, akasema, Mimi nitamdanganya.

[22]BWANA akamwambia, Jinsi gani? Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo kinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka ukafanye hivyo.

[23]Basi angalia, BWANA ametia pepo wa uongo kinywani mwa manabii wako hawa wote; naye BWANA amenena mabaya juu yako.

[24]Ndipo akakaribia Zedekia, mwana wa Kenaana, akampiga Mikaya kofi la shavu, akasema, Roho ya BWANA alitokaje kwangu ili aseme na wewe?

[25]Mikaya akamwambia, Angalia, utaona siku ile utakapoingia katika chumba cha ndani ili ujifiche.

[26]Mfalme wa Israeli akasema, Mchukueni Mikaya, mkamrudishe kwa Amoni mkuu wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme;

[27]mkaseme, Mfalme asema hivi, Mtieni mtu huyu gerezani, mkamlishe kwa chakula cha shida, na maji ya shida, hata nitakaporudi kwa amani.

[28]Mikaya akasema, Ukirudi kabisa kwa amani, BWANA hakusema kwa mimi. Akasema, Sikieni, enyi watu wote.

[34]Mtu mmoja akavuta upinde kwa kubahatisha, akampiga mfalme wa Israeli mahali pa kuungana mavazi yake ya chuma; kwa hiyo akamwambia mwendesha gari lake, Geuza mkono wako, unichukue kutoka katika majeshi; kwa kuwa nimejeruhiwa sana.

[35]Pigano likazidi siku ile; mfalme akategemezwa garini mwake, kinyume cha Washami, hata jioni akafa; damu ikatoka katika jeraha yake ndani ya gari.

[36]Ikapigwa mbiu jeshini, jua likichwa, kusema, Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake.

[37]Hivyo akafa mfalme, akachukuliwa Samaria, wakamzika mfalme huko Samaria.
 
Mkuu Sweet tablet hili ni swali la msingi sana na tunanalisubiria.
P
Kwa kutumia kanuni zipi, wakiwa kama Nani? Wagombea binafsi au? Kwa kuwa mdhamini ameshajitoa au ndo muendelezo wa uvunjwaji wa kanuni na Sheria za nchi? Hapo hamna uhalali wa uchaguzi labda watangazwe CCM wameshinda asililmia Mia tutawaelewa inshort waendelee na uchaguzi huku dunia ikiwa inashuhudia otherwise ni,. #tumehuruyauchaguzi
 
Pascal Mayalla,

Naunga mkono mwelekeo wa kuwapa wapinzani nafasi ya kurekebisha makosa yaliyokosewa kama yapo ili ushindani uwe wa kweli na huru zaidi.

Hili la kushikilia sana makosa madogo au walao yanayoweza kuvumilika,kurekebishika au hata kuelekezana ni suala la uzalendo na utu pia,kwani,twaelewa hali ya watanzania wengi ilivyo.Kutafuta vimakosa ili vitumike kwao kama vigezo,nadhani tutalazimika kuangalia na waliopo katika uongozi ngazi mbalimbali kwa sasa huku kwa hao,lugha ya kiswahili au kingereza kuwa tatizo zito,kubwa na la kushutusha hasa kwa viwango vya elimu vya wahusika (licha ya kutumia lugha,mfano ya kingereza kwa miaka mingi vyuoni na kabla ya hapo,level za juu na hata wengine kuishi nje labda wakitumia lugha hiyo katika kuendeleza elimu zao lakini bado kuna walakini katika hiyo lugha kila fursa itokekapo ama ilazimikapo kutumia hiyo lugha ya kingereza).

Isifike mahala tukahukumiana sana kwa vimakosa ambavyo vilihitaji zaidi kueleweshana,kurekebishana na kukubaliana.Kushikilia tu kuwa,uongozi wahitaji umakini,usahihi,umahiri na mambo kama hayo,tutakamatana wengi kwa 'fyongo' na 'ukilaza' kwenye mambo ya msingi yahusuyo hizo hizo lugha, umakini na mambo sambambsa na hayo.

Tuvumiliane,kuelewana,kueleweshana,kuelimishana na kustahimiliana na ikilazimika sana,walao basi, pawekwe malengo katika hilo kwa uwazi na kwa wote,na sio kushtukizana ama kuwashtukiza wengine kipindi nyeti kama hichi.Hatujui labda wengine walishajiandaaje katika hilo kungali mapema!
 
Magufuli lengo lake nchi ilirudi kwenye utawala wa chama kimoja, na kwa mwaka 2020 Hakuna mbunge wa upinzani atakae rudi bungeni labda Mbatia sababu ni mtu wa syteam, mi naona tuache iwe ivyo kama anavyotaka muheshimiwa rais na praise team kina Mzee Mwanakijiji.

Labda tukirudi mfumo wa chama kimoja na fikra zinazolingana nchi yetu itakuwa kama ulaya kimaendeleo
Not Mbatia, Kilimanjaro yote inarudi CCM, atakae rudi labda ZZK.
P
 
Back
Top Bottom