chinekeeee
JF-Expert Member
- Mar 26, 2015
- 1,787
- 2,896
Tatizo mmekubali kuhama bila kupandishiwa mshahara
Naongelea ideas tu. Kwangu mimi Dodoma na Dar es salam kote vumbi na kutapisha vyoo wakati wa mvua tu.
na ukweli ni huu, DODOMA inabadilika kwa kasi ,tatizo ni kuwa ukiingalia kwa jicho la Dar,Mwanza au Mbeya haya mabadiliko hutayaona ...tunaijua Dodoma Ya kabla ya UDOM,na maamuzi ya JPM ya Mwaka 2017 Dodoma inakua kwa kasi!Hili ndilo kosa ambalo watu wengi wanalifanya. Ukweli naona watu hapa wanajaribu kuilinganisha Dom na Dar, lakini wanasahau kwamba ili Dom ije ifananishwe na Dar inatakiwa juhudi zifanyike kwa walau miaka mingi kidogo mbeleni.
By the way, hata Dar mpaka inafikia hapo ilipo kwanza ilijengwa kwa miaka mingi na vivyo hivyo itakavyo kuwa Dodoma in ten years to come
Sent using Jamii Forums mobile app
wanachakaa vp bhn iyo hali ya hewa watazoea mbona sisi tunaishi miaka yote huku hatuchakaiWatapanga vyote ila hali ya hewa itabaki kuwa ile ile ya kuumiza mionekano ya watu ,dodoma watumishi wanachakaa jamani lol
Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji6]wanachakaa vp bhn iyo hali ya hewa watazoea mbona sisi tunaishi miaka yote huku hatuchakai
Sent using Jamii Forums mobile app
Tunashauri Kuwe Basi hata na political move na uhamasishaji wa upandaji miti kila mwaka .... hasa kipindi hiki ambapo angalau mvua zinanyesha. Niliona Kilimanjaro walikuwa na activity ya upandaji miti million 3 katika kukabiliana na kuyeyuka kwa barafu ya mlima Kilimanjaro. Kwa Dodoma Kama Makao Makuu ..... wananchi tupo tayari kushiriki iwapo kutakuwa na movement Kama hii. Ni kwa manufaa yetu na vizazi vijavyo. Karibuni sana Idodomya😀Wajapan walianzisha nursery pale maili mbili, SNV ilianzisha kitengo cha miti huko huko maili mbili na kupanda miti Dodoma nzima kwenye mradi wa DOVAP. hivyo vyote vilitoweka sababu ya siasa zetu za kuchagua kipi kwanza. Wafadhili walipoondoka wakaondoka na kila kitu sis tupo tu. Dodoma inahitaji kupandwa miti nyingi na itasaidia hata mvua kuongezeka. Mimi kama mwenyeji wa Dodoma nimejitahidi kupanda miti ya kidumu kibao na nina kisima ambacho natumia kumwagllia maji. Karibuni Idodomya jamani.
Jirani.... Huyo amehadithiwa Dodoma ya zamani sio ya sasa. Maji yapo..... sikumbuki Ni lini nimehangaika kununua maji kuwa maji hayatoki bombani. Mambo ya Makao Makuu haya.... Yamenoga.😀Jirani, huyu jamaa nimegundua haijui Dodoma zaidi ya kusimuliwa na kufuata mkumbo.
Maana kama maji yapo hadi Ndachi, iweje mji mkongwe kama Nkuhungu ukose maji..!!??
Sent using Jamii Forums mobile app
Iiigweeeee!!!!!..[emoji23][emoji23][emoji23]Kuna jamaa walijidanganya wakapeleka tipa za mchanga huko, walipigika na maisha hadi wakaamua kurudi, Dodoma kuna michongo kweli kwa sasa lakini sio kama inavyosimuliwa mitandaoni. Kiufupi ni overrated
Mkuu hii comment ni nzuri sana ila uki idrop apa kwa Dodoma nayo inakua overrated..Maneno ya watu wa Dar wakija mikoani ndio hayo. Ooh hakuna mzunguko wa pesa.. hivi na hivyo! Halafu unamkuta hata kiwanja kashindwa kununua..kwa pesa anazopata huko penye mzunguko
Haya jirani, basi natuanze kupanda miti ili kuifanya Dodoma ya kijani.Jirani.... Huyo amehadithiwa Dodoma ya zamani sio ya sasa. Maji yapo..... sikumbuki Ni lini nimehangaika kununua maji kuwa maji hayatoki bombani. Mambo ya Makao Makuu haya.... Yamenoga.[emoji3]
Kijana nimeishi Dodoma zaidi yako ... Wewe kuwa na miaka miwili Dom usituone wengine ni washamba wa Dom.Mkuu, kwa Dodoma mjini hakuna eneo ambalo halipati maji kwasababu chanzo cha maji tunayo yapata Dodoma nzima hatujaweza kuyatumia hata kwa asilimia hamsini.
Sehem ambayo haina maji Dodoma ni pale tu ambapo Duwasa haija fikisha miundombinu kwaajili ya kusambaza maji
Sent using Jamii Forums mobile app
Samahani Dada, kwani kuna sehem nimekuita wewe mshamba..!!??Kijana nimeishi Dodoma zaidi yako ... Wewe kuwa na miaka miwili Dom usituone wengine ni washamba wa Dom.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ni muelezeaji mzuri ila kwenye hii mada narudia kusema hoja zako ni dhaifu sababu unaongelea mambo kwa utashi wako binafsi bila kuwa na hoja, pia unaongelea mambo mengi yasiyowiana na mada husika.Tatizo nikikujibu popote, una uwezo wa kuliona jibu? Utaelewa ninachoandika?
Sijakujibu na kukuambia serikali itangulize vitu vyenye Return On Investment kabla ya kufanya straight up expenditures kama kuhamisha mji?
Unaelewa hilo maana yake nini? Unaelewa Return On Investment ni nini?
Kama huelewi, kwa nini huulizi ueleweshe? Kama unaelewa, kwa nini unaandika sijakujibu?
CDA inakosaje kuwa sehemu ya msingi wa hoja wakati ni mamlaka iliyoanzishwa kuhamisha mji kwenda Dodoma, ikashindwa? Inakosaje kuwa sehemu ya msingi wa hoja wakati inaonesha incompetency ya serikali?
Unasemaje si msingi wa hoja?
Sasa unataka niweke laundry list ya miradi badala ya kuongelea main ideas hapa? Nimeongelea ujinga wa serikali kuingilia biashara ya korosho, saidia wakulima waweze ku add value kwenye korosho waongeze exports na revenue. Tumia hela chache kuwatengenezea miundombinu na kuwezesha wafanyabiashara wajenge viwanda vya kubangua korosho, tu export finished products badala ya raw materials. This is a basic example of how the government has wrong priorities.
Una export raw korosho, huna kiwanda cha kubangua korosho cha kueleweka, halafu unahamisha mji mkuu.
Ni kama vile watoto wanakufa kwa njaa hawana chakula, baba unaenda bar kulewa!
Unafananisha chumi za Nigeria, Misri na Brazil na uchumi wa Tanzania? Umeangalia hata GDPs tu za hizo nchi?
Nchi zote ulizozitaja hazipo katika level ya GDP ya Tanzania. Umasikini wetu hauturuhusu kufanya mradi wa luxury kama kuhamisha mji mkuu. Nigeria wametumia petrodollars kuhamisha mji mku. Walivyotaka kuhamisha walikuja kuchukua uzoefu kwetu. Matokeo yake, waliokuja kujifunza kwetu wamemaliza kuhamisha mji mkuu, sisi hatujamaliza. Kwa sababu hatuna hela, hatuna commitments.
Kuhamisha mji mkuu ni expenditure. Nchi masikini zina demands nyingi sana kwenye forex zake. Zinatakiwa kuwa makini kutumia forex kwenye miradi yenye
Hapa unaonesha uvivu wa kujenga hoja tu, unasema kitu, halafu unashindwa kukitetea.
Faida ya kuhamia Dodoma ni ipi ambayo isingeweza kupatikana kama mji mkuu usingehamishiwa Dodoma?
Again, unaonesha uvivu wa kujenga hoja. Nilitegemea uorodheshe faida ni hii na hii na hii.
Hujaorodhesha. Hata wewe mwenyewe unazijua hizo faida au unasema zipo bila kuzijua tu?
Hoja ukiiona utaijua? CDA mismanangement itakosaje kuwa hoja katika mjadala wa kuhamia Dodoma? Serikali isiyo na mkakati kwenye biashara ya korosho lakini inayoweka kipaumbele kuhamia Dodoma itakosaje kuwa hoja?
Kuanguka kwa exports za agriculture kwa sababu serikali haina mkakati wa ku add value kwenye agricultural products wakati serikali ina prioritize kuhamisha mji mkuu kutakosaje kuwa hoja?Nchi yenye watu wasio na social benefits za kueleweka, halafu manakimbilia kuhamisha mji mkuu itakosaje kuwa hoja kuonesha misplaced priorities?
Msingi wa hoja ni nini? Unaweza ku define msingi wa hoja?
Hilo Bunge limejengwa kwa hewa? Ofisi za serikali? Nyumba za wafanyakazi wa serikali? Mafuta ya kupeleka watu Dodoma na kurudi Dar
Soma wataalam wameandika hapa "Poverty stricken Tanzania, unlike Nigeria, cannot throw hundreds of millions of pounds at the scheme and it will take some time to develop".
Bado unasema hakuna gharama?
![]()
The African Inheritance
Africa is a continent gripped by civil wars and widespread famine. The causes of many of the continent's problems are deep rooted and can be traced to Africa's colonial past, when European powers divided the spoils of the continent into separate sovereign states.The African Inheritance examines...books.google.de
Mbona palaini tu ongea na watu vzurDodoma sio kabisa kukame sijawahi ona Dodoma pagumu mfano hakuna
Sasa hayo mapato jiji la Dodoma linaongoza vp?Mkuu mimi nina biashara mwanza na dodoma lakin sijawahi ona mkoa wenye mzukunguko mdogo kama huu
Hebu achana na Dodoma.Naongelea ideas tu. Kwangu mimi Dodoma na Dar es salam kote vumbi na kutapisha vyoo wakati wa mvua tu.
Nipo Turks and Caicos, nitaanzaje kuonea wivu Dodoma?
Bei ni ndogo sababu hakuna makanjanja huku kila kitu serikali imedhibiti nyie jengeni milimani tu huko msituharibie jijiUkiona sehemu serikali imehamia afu bei ya viwanja ni ndogo jua hakuna ukuaji
Bei ni ndogo sababu hakuna makanjanja huku kila kitu serikali imedhibiti nyie jengeni milimani tu huko msituharibie jijiUkiona sehemu serikali imehamia afu bei ya viwanja ni ndogo jua hakuna ukuaji
Mkuu, unalalamika sana.... Ebu tuambie hapa, wapi hakuna maji Dodoma?
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ni muelezeaji mzuri ila kwenye hii mada narudia kusema hoja zako ni dhaifu sababu unaongelea mambo kwa utashi wako binafsi bila kuwa na hoja, pia unaongelea mambo mengi yasiyowiana na mada husika.
Kwanza nikusahihishe kwamba serikali haihamishi mji, bali inahamisha utendaji wa ofisi kuu za taasisi na mamlaka za serikali kutoka Dar es salaam kwenda Dodoma.
Unaongelea ROI kwamba ni muhimu kuliko kuhamia Dodoma, ila nitakujulisha Miradi michache iliyofanywa na serikali ambayo imekamilika na mingine ipo kwenye ujenzi , Miradi hiyo yote ina Economic ROI , Social ROI n.k
Miradi hiyo ni kama Train ya mwendokasi, ndege, flyover , Miradi mikubwa ya kuzalisha umeme, uboreshaji wa miundumbino kama Barabara, usafiri wa majini n.k
Serikali ina Sera yake ya Tanzania ya viwanda ambavyo ndio chachu ya maendeleo katika nchi zote, ndio maana imeamua kuboresha miundumbino ya uwekezaji kama nishati na Barabara kama njia ya kuendelea Tanzania ya viwanda huku ikiendelea kutunga Sera mbali mbali za uwekezaji utakaonufaisha nchi.
Hivyo serikali ili iweze kusimamia utekelezaji wa hivyo vyote kwa ufanisi wa Hali ya juu hasa utekelezaji na usimamiaji, ilikuwa lazima kuhamia Dodoma ili kupata muunganiko mzuri wa maendeleo ya nchi, sababu ilikuwa kila Miradi mikubwa kipindi cha nyuma ilikuwa inafanyika mikoa michache kama Dar es salaam, Arusha, Mwanza n.k
Pia kumbuka nilikuambia serikali haiwezi kufanya mambo yote kwa wakati mmoja.
Pia nimesema Capital Development Authority - CDA sio hoja ya msingi sababu ilikosa ufanisi na kujaa urasimu jambo lililopelekea kuvunjwa na serikali ya awamu ya tano
Nimekuambia kwamba acha kuruka ruka na maneno kwa kuandika vitu vingi visivyoendana na hoja husika mfano, mambo ya Korosho, export finished products nilikuambia jibu ni moja tu kwamba " serikali haiwezi kufanya mambo yote kwa wakati mmoja "
Umesema nikusaidie faida za kuhamia Dodoma
Faida za kuhamia Dodoma ni kama zifuatazo,
1. Nchi itakuwa na muunganiko mzuri wa kimaendeleo kwa mikoa yote kuliko kukalili mikoa michache kama Dar es salaam, Mwanza na Arusha, muunganiko wa nchi ni jambo litakalo shawishi wawekezaji wakubwa kuwekeza sehemu yeyote ya nchi , uwekezaji mfano hotels za kisasa, viwanda , nyumba za kuishi ( apartments ) n.k
2. Itasaidia wanachi mikoa yote kupata huduma za Kiserikali kuu kwa wakati ikizingatiwa dodoma ni kati Kati ya nchi hivyo ni rahisi wanachi wa mikoa yote kufika dodoma kwa mda mfupi
3. Itapelekea kuendelea kwa mikoa mingine ya jirani ya dodoma, mikoa kama singida, Morogoro, manyara n.k
4. Itasaidia usimamiaji na ufuatiliaji wa serikali katika Miradi mbalimbali katika mikoa yote ya nchi, Miradi kama umeme, maji, viwanda, afya n.k pia dodoma ni sehemu sahihi kwa usalama wa nchi ikizingatiwa ni kati Kati ya nchi. N.K
Hoja ya msingi kwangu ni kwamba serikali kuhamia Dodoma ni jambo zuri pia faida ni nyingi kuanzia sasa na miaka mingi ijayo, hivyo faida ni kubwa kuliko gharama iliyotumika, hivyo acha kuwa kama bendera fuata upepo kwa kuandika upotoshaji wa jambo la serikali kuhamisha utendaji wa serikali kuu kutoka dar es salaam kwenda Dodoma
Au unaweza kuelezea ni gharama gani kubwa sana iliyotumika hadi Sasa tangu serikali imehamia dodoma?
achana na hoja zako nyepesi kuelezea eti gharama ni mafuta, nyumba za wafanyakazi na wakati kitendo cha kuhama ni kama mfanyakazi wa kawaida anaamishwa mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine ambapo analipwa stahiki zake kama usafiri na makazi, na ili kupunguza gharama serikali ili wahamisha kwa train na magari ya jeshi, pia hata wakiwa dar es salaam Walikuwa wanalipwa posho za nyumba na mafuta
jambo la ofisi nimekuelezea vizuri namna Yale Majengo ya Wizara yalivyojengwa pale mji wa Kiserikali kwa gharama ndogo sana.
Kuhusu nchi kama Nigeria, India, Brazil, Misri, Mozambique n.k kuhamisha makao makuu ya miji Yao mikuu, hiyo iliwasaidia kuongeza ufanisi wa utendaji wa serikali zao sababu hizo nchi zote zilitawaliwa hivyo miji mikuu iliwekwa na wakoloni kurahisisha utendaji wa serikali za kikoloni hivyo kuhamisha makao makuu ya nchi zao ilikuwa lazima wahamishe kwenda miji mikuu mingine bila kujali gharama kubwa, pia kwa Tanzania ni hivyo hivyo.
Pia acha kukalili vitabu vilivyoandikwa na watu kama wewe, Hao ni waandishi tu na ni watu kama wewe na pia wanakosea kama wewe, hivyo hizo link za vitabu kama hazina msaada kwenye Sera ya Sasa ya serikali ya Tanzania, basi hivyo vitabu ni useless kwa Sasa ikifika mda vikihitajika na Sera ya nchi tutavitumia
Sent using Jamii Forums mobile app