Kiranga, Hoja zako dhaifu sana ndugu, nimekuuliza jambo moja je vipaumbele vya nchi vinavyotakiwa ni vipi kwa Sasa ukiachana na kuhamia Dodoma ila haujanijibu?
Tatizo nikikujibu popote, una uwezo wa kuliona jibu? Utaelewa ninachoandika?
Sijakujibu na kukuambia serikali itangulize vitu vyenye Return On Investment kabla ya kufanya straight up expenditures kama kuhamisha mji?
Unaelewa hilo maana yake nini? Unaelewa Return On Investment ni nini?
Kama huelewi, kwa nini huulizi ueleweshe? Kama unaelewa, kwa nini unaandika sijakujibu?
Umeanza kuongelea Capital Development Authority - CDA ambayo siyo msingi wa Hoja na pia ilishavunjwa hiyo mamlaka.
CDA inakosaje kuwa sehemu ya msingi wa hoja wakati ni mamlaka iliyoanzishwa kuhamisha mji kwenda Dodoma, ikashindwa? Inakosaje kuwa sehemu ya msingi wa hoja wakati inaonesha incompetency ya serikali?
Unasemaje si msingi wa hoja?
Pia umesema nchi zinazoendelea zinatakiwa kuwa uchaguzi mzuri wa vipaumbele ili zianze na Miradi inayozalisha kwanza, je vipaumbele vipi vinavyotakiwa kufanywa na nchi Sasa ukiachana na jambo la kuhamia Dodoma?
Sasa unataka niweke laundry list ya miradi badala ya kuongelea main ideas hapa? Nimeongelea ujinga wa serikali kuingilia biashara ya korosho, saidia wakulima waweze ku add value kwenye korosho waongeze exports na revenue. Tumia hela chache kuwatengenezea miundombinu na kuwezesha wafanyabiashara wajenge viwanda vya kubangua korosho, tu export finished products badala ya raw materials. This is a basic example of how the government has wrong priorities.
Una export raw korosho, huna kiwanda cha kubangua korosho cha kueleweka, halafu unahamisha mji mkuu.
Ni kama vile watoto wanakufa kwa njaa hawana chakula, baba unaenda bar kulewa!
Umesema unaongelea idea nzima ya kuhamia Dodoma tangu Enzi za nyerere ilikuwa ujinga mtupu, nafikiri wewe umetembea nchi kadhaa,
je unafahamu kwamba nchi zifuatazo zilibadilisha miji mikuu iliyorithi kutoka kwa wakoloni na lengo ilikuwa kurahisisha Utawala wa nchi, ulinzi , kuweka uwiano wa maendeleo ya maeneo ya nchi n.k.
nchi hizo ni Nigeria: Lagos to Abuja, Misri: Cairo to new Cairo, Brazil: Rio de Janeiro to Brasilia n.k
Unafananisha chumi za Nigeria, Misri na Brazil na uchumi wa Tanzania? Umeangalia hata GDPs tu za hizo nchi?
Nchi zote ulizozitaja hazipo katika level ya GDP ya Tanzania. Umasikini wetu hauturuhusu kufanya mradi wa luxury kama kuhamisha mji mkuu. Nigeria wametumia petrodollars kuhamisha mji mku. Walivyotaka kuhamisha walikuja kuchukua uzoefu kwetu. Matokeo yake, waliokuja kujifunza kwetu wamemaliza kuhamisha mji mkuu, sisi hatujamaliza. Kwa sababu hatuna hela, hatuna commitments.
Kuhamisha mji mkuu ni expenditure. Nchi masikini zina demands nyingi sana kwenye forex zake. Zinatakiwa kuwa makini kutumia forex kwenye miradi yenye
Unasema serikali imeamua kushindanisha dodoma na dar es salaam mji ulioibuka naturally, kwa kifupi hii Hoja yako Haina ukweli.
Hapa unaonesha uvivu wa kujenga hoja tu, unasema kitu, halafu unashindwa kukitetea.
Nimeeleza kwa kifupi ili turudi kwenye msingi wa Hoja, ni kwamba jambo la kuhamia Dodoma serikali iko sahihi na faida zake ni nyingi sana kama nchi na sio kwa kuangalia mawazo ya wafanyakazi wachache wa serikali wasio taka kuhama dar es salaam sababu ya Mazoea.
Faida ya kuhamia Dodoma ni ipi ambayo isingeweza kupatikana kama mji mkuu usingehamishiwa Dodoma?
Again, unaonesha uvivu wa kujenga hoja. Nilitegemea uorodheshe faida ni hii na hii na hii.
Hujaorodhesha. Hata wewe mwenyewe unazijua hizo faida au unasema zipo bila kuzijua tu?
Halafu kama bado una Hoja Jaribu kufata mtiririko wa Hoja sio kuruka ruka na maneno Bila mpangilio Mara CDA, Korosho, export za agriculture, exploit agriculture potential, social benefits na mengine kama hayo uliyoongea ambayo sio msingi wa Hoja ambavyo jibu la hayo yote ni kwamba serikali haiwezi kufanya mambo yote kwa wakati mmoja.
Hoja ukiiona utaijua? CDA mismanangement itakosaje kuwa hoja katika mjadala wa kuhamia Dodoma? Serikali isiyo na mkakati kwenye biashara ya korosho lakini inayoweka kipaumbele kuhamia Dodoma itakosaje kuwa hoja?
Kuanguka kwa exports za agriculture kwa sababu serikali haina mkakati wa ku add value kwenye agricultural products wakati serikali ina prioritize kuhamisha mji mkuu kutakosaje kuwa hoja?Nchi yenye watu wasio na social benefits za kueleweka, halafu manakimbilia kuhamisha mji mkuu itakosaje kuwa hoja kuonesha misplaced priorities?
Msingi wa hoja ni nini? Unaweza ku define msingi wa hoja?
Hoja ni kwamba kuhamia Dodoma Unasema ni gharama na Unasema serikali ifanye vipaumbele vingine,
Je gharama hizo za serikali kuhamia Dodoma ni zipi na je vipaumbele vingine ambavyo serikali inatakiwa kufanya ukiachana na kuhamia Dodoma ni vipi?
Sent using
Jamii Forums mobile app
Hilo Bunge limejengwa kwa hewa? Ofisi za serikali? Nyumba za wafanyakazi wa serikali? Mafuta ya kupeleka watu Dodoma na kurudi Dar
Soma wataalam wameandika hapa "Poverty stricken Tanzania, unlike Nigeria, cannot throw hundreds of millions of pounds at the scheme and it will take some time to develop".
Bado unasema hakuna gharama?
Africa is a continent gripped by civil wars and widespread famine. The causes of many of the continent's problems are deep rooted and can be traced to Africa's colonial past, when European powers divided the spoils of the continent into separate sovereign states.The African Inheritance examines...
books.google.de